Mitandao ya simu za viganjani hii haijakaa sawa

NostradamusEstrademe

JF-Expert Member
Jul 1, 2017
3,032
4,028
Inakuwaje mtu umechukua line ya mtandao fulani ukawa unatumia lakini kuna uwezekano kibinadamu kuna sababu mbalimbali kiuchumi hali ngumu au ukaugua muda mrefu kiasi kwamba huwezi hata kutumia simu kwa maana ya kununua hata vocha. Sasa baada ya siku au miezi kadhaa unaambiwa namba yako amepewa mtu mwingine?

Kumbukeni hizi namba ndio zimesajiliwa NIDA kwa maana hiyo kwa mawazo yangu kiusalama hii haijakaa sawa kabisa.

Nilikuwa na wazo mtu akisajiliwa namba yake hata kama hataitumia asipewe mtu mwingine kama mtiririko wa namba za magari ambapo haurudi nyuma hata kama gari limepata ajali halifai tena au umeamua ulipaki lisitembee.

Kumbukeni namba huwa hazina mwisho.Hakuna mwisho wa kuhesabu aslani kuna ubaya gani mkaendeleza namba kwenda mbele?

Waziri mhusika mhe naomba chunguza hili kwa mapana yake na ulifanyie kazi linahatarisha usalama na kuvuruga taratibu za taarifa za watanzania kwenye mifumo ya utambuzi kiserikali.
 
Unatakiwa ukatoe ripoti ya unachokipitia ambacho kinasababisha ushindwe kununua vocha. Hawana namna ya kujua kuwa umepatwa na janga. Watakutofautishaje na yule aliyeamua kuitupa line na kuiondoa kwenye NIDA yake kisa madeni? Kuna wanaokwenda nje ya nchi ambako hakuna ROAMING. Usisahau nao wanalipia hizo frequency wanazotumia na huku wewe mtumiaji huingizi chochote kwao.
 
Unatakiwa ukatoe ripoti ya unachokipitia ambacho kinasababisha ushindwe kununua vocha. Hawana namna ya kujua kuwa umepatwa na janga. Watakutofautishaje na yule aliyeamua kuitupa line na kuiondoa kwenye N8DA yake kisa madeni?
Nadhani umesoma mada bila kuelewa ninachongelea sio vocha ni kufungiwa line halafu anapewa mtu mwingine
 
Nadhani umesoma mada bila kuelewa ninachongelea sio vocha ni kufungiwa line halafu anapewa mtu mwingine
Kufungwa line na kupewa mtu mwingine, ni kwa sababu huitumii line hiyo kwa kipindi fulani (nadhani ni miezi mitatu mfululizo). Kutokutumia maana yake huweki vocha, hupigi simu, hutumi wala kupokea pesa kwa simu etc. Vocha hapo ni mfano tu!
 
Ukilifikiria sana hili jambo unaona kabisa hichi kinachoitwa kusajili namba ya simu ni upuuzi mtupu.

Hili jambo linakera sana.mtu unasafiri kidogo uko nje ukirudi unakutana na visa vya namba yako kutumiwa na mtu mwingine.

Bora wangekua wanazifanya zinakua dormant ukiihitaji unaifufua unaendelea nayo ukifa nayo inakufa au wangeweka muda mrefu zaidi ila sio hivi wanavyoifungia nakuirudisha sokoni.

Niliwai kusajili line mpya nikaja kupigiwa simu na dada mmoja akaanza kuniporomoshea matusi kua nilimpa mimba tukakubaliana aitoe alivyoanza kutoka damu nyingi nikamzimia simu.Ilinichukua muda sana kumueleza yule dada kua sio mimi.

Sasa kungekua na uhalifu umeripotiwa mahali siajabu ningetiwa matatani kwa jambo ambalo silifahamu.
 
Kufungwa line na kupewa mtu mwingine, ni kwa sababu huitumii line hiyo kwa kipindi fulani (nadhani ni miezi mitatu mfululizo). Kutokutumia maana yake huweki vocha, hupigi simu, hutumi wala kupokea pesa kwa simu..!! etc. Vocha hapo ni mfano tu!
Nimekuelewa mkuu sasa huoni kuwa sio sahihi kabisa.Mtu anaweza nyang'anywa namba ya gari yake kisa tu haendeshi limepaki? je huoni hata hiyo miezi mitatu ni muda mfupi tu? na utamnyang'anyaje mtu line yake umpe mwingine bila ridhaaa yake? huoni kuwa ni kosa kisheria maana line na namba hiyo hiyo ndio ina taarifa zake hadi NIDA?

nikupe mfano siku moja nilikuwa nalipia fine gari langu nilipoingiza tu namba ya simu namba yangu ya gari ikajiandika yenyewe.

Ndugu yangu hili sio jambo jepesi unavyo lidhania NIDA ni kila kitu naomba tupige kelele tukemee jambo hili halina mashiko kabisa sikutaka kutaja makampuni ya simu wepesi kufanya jambo hili.
 
Nimekuelewa mkuu sasa huoni kuwa sio sahihi kabisa.Mtu anaweza nyang'anywa namba ya gari yake kisa tu haendeshi limepaki? je huoni hata hiyo miezi mitatu ni muda mfupi tu? na utamnyang'anyaje mtu line yake umpe mwingine bila ridhaaa yake? huoni kuwa ni kosa kisheria maana line na namba hiyo hiyo ndio ina taarifa zake hadi NIDA?

nikupe mfano siku moja nilikuwa nalipia fine gari langu nilipoingiza tu namba ya simu namba yangu ya gari ikajiandika yenyewe.

Ndugu yangu hili sio jambo jepesi unavyo lidhania NIDA ni kila kitu naomba tupige kelele tukemee jambo hili halina mashiko kabisa sikutaka kutaja makampuni ya simu wepesi kufanya jambo hili.
Nakuelewa sana. Hili si jambo la kuwalaumu makampuni ya simu, bali serikali..!! Serikali inatakiwa iweke sheria au kanuni ya namna ya kufanya kwenye jambo hili. Lakini, hatutakiwa kuangalia upande mmoja wa shilngi, tujiangalie na sisi watumiaji. Maana hatukawii kutupa line na kusajili nyingine kwa sababu zetu binafsi! Sababu ambazo zina athari kwa makampuni ya simu.
 
Ukilifikiria sana hili jambo unaona kabisa hichi kinachoitwa kusajili namba ya simu ni upuuzi mtupu.Hili jambo linakera sana.mtu unasafiri kidogo uko nje ukirudi unakutana na visa vya namba yako kutumiwa na mtu mwingine.Bora wangekua wanazifanya zinakua dormant ukiihitaji unaifufua unaendelea nayo ukifa nayo inakufa au wangeweka muda mrefu zaidi ila sio hivi wanavyoifungia nakuirudisha sokoni.Niliwai kusajili line mpya nikaja kupigiwa simu na dada mmoja akaanza kuniporomoshea matusi kua nilimpa mimba tukakubaliana aitoe alivyoanza kutoka damu nyingi nikamzimia simu.Ilinichukua muda sana kumueleza yule dada kua sio mimi.Sasa kungekua na uhalifu umeripotiwa mahali siajabu ningetiwa matatani kwa jambo ambalo silifahamu.
hongera kwa ku-escape sobibo a.k.a jumba bovu
 
Kama still unataka line yako itumike huko mbeleni andika barua kwa mtandao husika mtakubaliana nao wataitunza. Kingine kama ni mweka vocha mzuri kuna line zina kaa mpaka 4 yrs au zaidi bila kuwa deleted na system. Line ikikaa miezi 3 System automatically inazidelete. Ila Wahusika wanaweza kuiset isijifute- kumbuka pia kila line TCRA kuna kodi wanakata kila mwezi so ni mzigo kwa Telecom operator kuwa na maline chungumzima yasiyotumika wakati anazilipia TCRA kila Mwezi. Lakini pia Je kama Umekufa?😁 watajuaje ili wasiiuze tena line yako?
 
Kama still unataka line yako itumike huko mbeleni andika barua kwa mtandao husika mtakubaliana nao wataitunza. Kingine kama ni mweka vocha mzuri kuna line zina kaa mpaka 4 yrs au zaidi bila kuwa deleted na system. Line ikikaa miezi 3 System automatically inazidelete . Ila Wahusika wanaweza kuiset isijifute- kumbuka pia kila line TCRA kuna kodi wanakata kila mwezi so ni mzigo kwa Telecom operator kuwa na maline chungumzima yasiyotumika wakati anazilipia TCRA kila Mwezi. Lakini pia Je kama Umekufa???😁 watajuaje ili wasiiuze tena line yako??
mbona ukifa gari lako namba iko pale pale
 
Kama still unataka line yako itumike huko mbeleni andika barua kwa mtandao husika mtakubaliana nao wataitunza. Kingine kama ni mweka vocha mzuri kuna line zina kaa mpaka 4 yrs au zaidi bila kuwa deleted na system. Line ikikaa miezi 3 System automatically inazidelete . Ila Wahusika wanaweza kuiset isijifute- kumbuka pia kila line TCRA kuna kodi wanakata kila mwezi so ni mzigo kwa Telecom operator kuwa na maline chungumzima yasiyotumika wakati anazilipia TCRA kila Mwezi. Lakini pia Je kama Umekufa???😁 watajuaje ili wasiiuze tena line yako?
Bro kinacholipiwa kodi sio idadi ya namba za simu walizonazo watu na ndio maana ukienda kununua kitu dukani unalipa VAT pale pale bila wewe kujua kutokana bei ya bidhaa unayonunuahuwezi kukaa nyumbani kwako ukaambiwa ulipe kodi ya bidhaa ambayo hujanunua take it from me. Tunadanganyana hapa wengine wanao comment humu nimegundua wanatetea hii kitu sababu wanafanya kazi makampuni ya simu.
 
Mimi mwenyewe nimelazwa hospitali kitandani miezi sita sikuwa naweza tumia simu.Ndani ya miezi kadhaa nilijaribu kutumia simbanking kutoa hela yangu imeshindikana. Siwezi muamini mtu kumpa kadi yangu ya bank akanitolee hela zangu isitoshe kuna wakati nilikuwa sina fahamu kabisa nimerudi sasa uraiani nakutana na kituko hiki familia yangu iliteseka sana.

Mambo ya familia huwezi jua yana mambo yake sio kila mtu unamuamini unaweza ukawa na watoto wasio sawa au hata mke asiye sawa akaenda kukomba hela zako zote akidhani utakufa sasa nimerudi uraiani mungu akili timamu kaninusuru nakutana na kigingi kingine. Au basi angalau waweke programm maalum baada ya miezi kadhaa unatumiwa alert automatic angalia line yako itafungwa lakini isiwe miezi mitatu.Kumfungia mtu bila ridhaa yake ni unyama sana.
 
Usipoitumia line miezi 3 uwa wanai block one way.yaani huwezi kupiga simu ila watu wanaweza kukupigia.hapo ukipiga simu customer care wanakufungulia.ukiongeza mwezi mweingine yaani miezi 4.wanai block 2 ways hapo itakupasa uende shop zao wakakufungulie.ukiongeza mwezi mwingine yaani miezi 5 hapo wana delete kabisa registration.na inarudishwa sokoni
 
Inakuwaje mtu umechukua line ya mtandao fulani ukawa unatumia lakini kuna uwezekano kibinadamu kuna sababu mbalimbali kiuchumi hali ngumu au ukaugua muda mrefu kiasi kwamba huwezi hata kutumia simu kwa maana ya kununua hata vocha. Sasa baada ya siku au miezi kadhaa unaambiwa namba yako amepewa mtu mwingine?

Kumbukeni hizi namba ndio zimesajiliwa NIDA kwa maana hiyo kwa mawazo yangu kiusalama hii haijakaa sawa kabisa.

Nilikuwa na wazo mtu akisajiliwa namba yake hata kama hataitumia asipewe mtu mwingine kama mtiririko wa namba za magari ambapo haurudi nyuma hata kama gari limepata ajali halifai tena au umeamua ulipaki lisitembee.

Kumbukeni namba huwa hazina mwisho.Hakuna mwisho wa kuhesabu aslani kuna ubaya gani mkaendeleza namba kwenda mbele?

Waziri mhusika mhe naomba chunguza hili kwa mapana yake na ulifanyie kazi linahatarisha usalama na kuvuruga taratibu za taarifa za watanzania kwenye mifumo ya utambuzi kiserikali.
Hoja Ina Mashiko...
 
Kufungwa line na kupewa mtu mwingine, ni kwa sababu huitumii line hiyo kwa kipindi fulani (nadhani ni miezi mitatu mfululizo). Kutokutumia maana yake huweki vocha, hupigi simu, hutumi wala kupokea pesa kwa simu..!! etc. Vocha hapo ni mfano tu..!!
Ina maana ukisafiri Nje ya Nchi kwa miezi sita tu tayari unakuwa Disqualified kuitumia line yako ambayo pengine umeitumia zaidi ya Miaka Kumi?

Hii siyo haki.
 
Ina maana ukisafiri Nje ya Nchi kwa miezi sita tu tayari unakuwa Disqualified kuitumia line yako ambayo pengine umeitumia zaidi ya Miaka Kumi?

Hii siyo haki.
Yes, lakini wao watajuaje kwamba umesafiri au umeitupa line? Unatakiwa ukatoe taarifa kabla ya kusafiri
 
Back
Top Bottom