Mitandao ya simu Tanzania ipo 'compromised'?

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,633
697,754
Ni wiki ya Mtandao wa Tigo Tanzania baada ya muajiriwa wake kitengo cha sheria kuwa mmoja wa mashahidi katika kesi ya ugaidi inayomkabili Freeman Mbowe mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani CHADEMA.

Kampeni zimeanza kushika kasi kila kona kususia huduma za mtandao husika.

Hili lina madhara japo si makubwa. Mwaka jana Vodacom Tanzania ilipitia katika wakati mgumu kuhusiana na kutoa siri za wateja. Wateja wote ni wanasiasa wa upinzani wa chama cha CHADEMA. Kampeni ile ya kususia bidhaa na huduma za Vodacom Tanzania ilikuwa kubwa na mbaya, lakini yalipita japo jina lake lilichafuka kwa kaisi chake, ni zamu ya Tigo sasa.

Hizi kampeni za kususia bidhaa na huduma za mitandao husika haziwezi kufanikiwa kwa asilimia 100 lakini zinapeleka ujumbe kwa sauti ya juu kwa wahusika kwamba haya mambo si sawa na si sahihi hasa linapokuja hili la kulinda siri za wateja

Mimi siilaumu hii mitandao ya simu Tanzania. Ni sahihi kabisa kwa usalama wa nchi kuwa na nyoka na mapandikizi kila mahali.. Na hii sio Tanzania tuu bali ni popote pale ulimwenguni. Usalama wana watu wao kwenye sekta binafsi na za serikali pia. Wana nyoka wao kwenye makampuni makubwa na madogo. Kila mahali wapo na kiusalama sio kosa kabisa

Haya makampuni ya simu na sekta nyingine pia kuna wafanyakazi wanaajiriwa kwa vimemo ama kwa simu moja tuu.. Wengine huajiriwa kwa mlungula kabisa kuficha uhalisia na wengine huajiriwa kwa uwezo wao. Ni kati ya hao kuna nyoka na mapandikizi na kamwe huwezi kuwajua kwakuwa sifa moja ya usalama ni kuwa invisible kama huyu wetu hapa JF

Sasa kosa liko wapi? Kosa hili hapa

Kuna ombwe ama kasoro kubwa kwenye baadhi ya watendaji kwenye mamlaka zetu. Hasa linapokuja swala la kudili na wapinzani kwenye kaliba ya mashtaka na sheria za makosa ya jinai nk

Kama nilivyosema maswala yote ya usalama huwa ni invisible. Kwahiyo hata siku moja huwezi kumkuta mwanausalama wa taifa ngazi ya nyoka au pandikizi akisimama mahakamani na kutoa ushahidi. Kazi ya usalama ni kugundua na kuonesha tatizo lilipo.. Mamalaka za kisheria ndio hutafuta njia sahihi ya kudili nalo.

Kesi ya Mbowe imeonesha madhaifu mengi toka mamlaka zetu namna ya kuwatumia mashahidi vipenyo kama mashahidi visible hii ni hatari sana. Sana, na madhara yake ni mengi kama hilo la kujulikana kuwa kumbe kuna maafisa vipenyo huko na huko na kupelekea kuharibu biashara za wengine

Kitu kingine cha kushangaza ni hili la mashahidi wa ugaidi kuwa wazi na kujulikana na kila mtu. Kwa kanuni za kesi za kigaidi mashahidi hufichwa na ni ngumu mno kujulikana wazi wazi.

Tunapowatia ndimu machoni Tigo tusisayasahau na haya mengine mengi kwakuwa hata tunaokaa nao vijiweni mitaani, vijiweni mitandaoni huku wengine wakiwa ni wasiri wetu kati yao ni nyoka, mapandikizi na maafisa vipenyo
 
Lengo la kusajili namba zetu za simu kwa kutumia kitambukisho cha Taifa ni kudhibiti vitendo vya kihalifu.

hii ni kwa mitando yote, linapo kuja suala suala la usalama na Amani ya nchi ni jukumu la kila raia mwema kutoa taarifa.

Usisahau pia TCRA wapo wanatupia jicho lao kwa lengo hilo hilo.
lengo tutumie mawasiliano kwa nia njema.
kinyume chake haupo salama.

Kimsingi kesi yoyote ile lazima iendeshwa kwa uwazi bila kificho isipokuwa kwa kesi za mauaji ya kimbali ndipo mashahidi wake wanaweza kufichwa wasitambulike.

Kwa kesi ya Mbowe sioni kama kuna ulazima wa kuwaficha mashahidi isipokuwa kwa wale ambao inabidi kufanya hivyo.
kama hakuna ulazima ni takwa la kisheria kesi ikaendeshwa kwa uwazi isipo kuwa inapo bidi.

Kesi hii ya Mbowe inaendeshwa kwa uhuru na uwazi wa kiwango cha juu ndio maana hata wafuasi wake wanashangaa sana, lkn lengo ni haki ionekane kweli imetendeka.
 
wakati hao vipenyo na nyoka wanaharibu biashara za watu kwa kujichomeka, ajabu nyingine hao nyoka na vimeo wapo kwenye nyumba za ibada, ni viongozi na waumini wa kawaida, ukijaribu kuusema uovu wa wa mamlaka utatulizwa kwa neno la mungu utii mamlaka na usiinyoshee kidole imetoka kwa mungu, ukishupaza shingo utajikuta mikononi mwa mamlaka unashitakiwa kwa uchochezi
 
Lengo la kusajili namba zetu za simu kwa kutumia kitambukisho cha Taifa ni kudhibiti vitendo vya kihalifu.

hii ni kwa mitando yote, linapo kuja suala suala la usalama na Amani ya nchi ni jukumu la kila raia mwema kutoa taarifa.

Usisahau pia TCRA wapo wanatupia jicho lao kwa lengo hilo hilo.
lengo tutumie mawasiliano kwa nia njema.
kinyume chake haupo salama.

Kimsingi kesi yoyote ile lazima iendeshwa kwa uwazi bila kificho isipokuwa kwa kesi za mauaji ya kimbali ndipo mashahidi wake wanaweza kufichwa wasitambulike.

Kwa kesi ya Mbowe sioni kama kuna ulazima wa kuwaficha mashahidi isipokuwa kwa wale ambao inabidi kufanya hivyo.
kama hakuna ulazima ni takwa la kisheria kesi ikaendeshwa kwa uwazi isipo kuwa inapo bidi.

Kesi hii ya Mbowe inaendeshwa kwa uhuru na uwazi wa kiwango cha juu ndio maana hata wafuasi wake wanashangaa sana, lkn lengo ni haki ionekane kweli imetendeka.
Ingekuwa ni kesi ya ugaidi kweli haya yasingetokea..Kumbuka hii sio kesi pekee ya ugaidi zipo nyingi tuu.. Umeshawahi kuona hata watuhumiwa wakipelekwa mahakamani? Ni full squad.. Na kesi inasomwa kabla ya saa mbili asubuhi na ulinzi kiwango wa 5G
 
Ni wewe na kundi lako lote
😂😂. Kundi au mkutano wa manyoka tu..
Mi ngoja nichomoke niende kwenye Uzi wa billgate tukamsimange maana ati hataki mwanae aolewe na maskini!,kilichobaki hivi Sasa ni kumroga tu naona anazeeka vibaya.
 
Back
Top Bottom