Mishahara ya Wake Zetu

mimi na shemejio tumepanga hivi:
school fees za watoto na chochote kinachohusiana na watoto ni jukumu langu, kwa mfano mavazi na mtoto akiumwa, japo tuna medical insurance hivyo situmii pesa yangu.
mwenzangu yeye chakula na mahitaji mengine yote ndani ya nyumba ni yake, luku, maji na mahanjumati yote ni juu yake. hata tukiwa na shughuli nyumbani, yeye ndio anagharamia. tulipanga, tukachakua, na mimi niliona majukumu yangu hayataki pesa ya hapo kwa hapo, najipanga, school fees najua ni lini nalipa na mavazi ya watoto napanga ni lini nanunua japo sina ratiba maalum, hii ni kama kipato kikiruhusu.
niliona nikichukua majukumu yake, kuna siku naweza kuwalaza njaa au giza au tukatiwa maji.
tumejenga, lakini hapa hakukua na kupanga. yeye alijenga mwanzo mpaka mwisho. Finishing asilimia kubwa nilifanya mimi maana sie wamama tuna taste zetu na vitu tunavyotaka.
Hivyo mkaka na wewe angalia mpange vipi.
 
We Paloma Wewe!

QUOTE=Paloma;4697832]uttoh2002 inaonekana roho inakuuma sana mpk ukawaita 'midudu'. Lakini mwenyewe si umesalimu amri! Chezea midudu weweee[/QUOTE]
 
Last edited by a moderator:

Mkuu, hako ka-neno hapo kwenye red kana-apply vipi wakati watu tumeshamuwowa..??sasa kama anachoenda kufanya kazini hakina faida kwa familia si bora akae tu home tumhudumie? manake kazini nako kuna risk za aina nyingi huko,,mara bosi anataka naye kuonja,,mara kashikwa na yule...hizi risk tunazichukulia poa tukiamini kuwa analofanya lina mchango chanya kwenye familia yetu,,ama sio?
 
Hali inayokutokea unaposhindwa kutimiza wajibu wako kama baba mwenye nyumba. Hicho kitu mzee wangu nimekiandika kwa kuwa kilinitokea mimi mwenyewe. Huna hela, ndani hakuna chochote na watoto wanalia njaa. Unajua kabisa mama ana hela lakini kwa utaratibu wake hachangii au kukusaidia wakati upo kwenye msoto kama huo.
 
Hii thread kwa kweli imenifundisha kuwa usawa uko mbali sana kwenye ndoa aisee..Unless labda tunachoandika humu hatukimaanishi. Na kitu ninachojaribu kukiona ni ile 'Dhana ya Mwanaume ni Kichwa cha Familia' kutumiwa vibaya..Binafsi bado naamini mwanamke kuchangia kwenye basket fund ya ndoa hakumuondelei baba ule ukichwa wake..Kitakachomuondolea ule ukichwa ni jinsi atakavyosimamia 'mapato na matumizi'..Anaweza kuwa hamshirikishi mke lakini bado akawa na matumizi ya hovyo tu..na yakukera pia!

Lakini jingine nadhani kabla ya yote ni muhimu mwanamke kujiuliza upo kwenye ndoa kwa ajili gani??..Lazima iwepo tofauti kati ya Mke na Housegirl..manake ninavyoona hapa mke naye anataka awe mtu wa kupewa tu....yaani anataka kujiweka kwenye position ya uhausigeli..This is not fair!!..Mwanamke aonyeshe naye ana 'stake' kwenye ujenzi wa familia yake..msiishie kunyonyesha tu watoto..jitahidini mchangie hata 'financially' kama mna vipato pia. Vinginevyo na smell harufu ya ndoa ambazo ni za 'kuviziana'..yaani mtu anawaza asije akafa akaniletea matatizo..na ukitangulia wewe??..lol!!
 

Nimesoma hii tu mkuu Kaizer. Sitasoma post nyingine na siwezi kuongeza kitu. Babu DC!!
Babu Dc umeniwahi sijui kwa nini............Nami nilitaka kusema hivyo hivyo..........Kwangu hii sredi sitachangia Kaizer amemaliza kabisa.
 
Last edited by a moderator:
Mimi nahisi tunahitaji tafsiri zaidi ya ndoa kwani watu huunganishwa na KUWA MWILI MMOJA; hiyo ina maana pana sana. Nawashauri kina mama warudi tena kwa wachungaji na Mashekhe wakaombe tafsiri ya ndoa.
Kimsingi mambo yaliyo andikwa kwenye vitabu vitakatifu (Biblia na Quran) yanahitaji uelewa mpana zaidi na sio copy paste ndio sababu watumishi kama mapadri na Maulamaa husomea kwa angalau miaka minne (baada ya kidato cha sita) ili kuwa na uwezo wa kuelewa maana halisi ya kilichokusudiwa
 
Wakuu,
Hebu na tu shee Experience zenu especialy nyie wenye wake wanaofanya Kazi namna Pato linavyokuwa Distributed Home.
Nataka ku Draw Bonge moja la Conclusion hapa Kwangu

Kwani Ustawi wa Jamii hawana Gawiwo Elekezi tutumie hilo kama KIASHIRIA?
 
bold ya kwanza kusema ukweli wala sitakubali ifike aadhirike mie straika wake nipo lakini ndo wasijisahau!
hiyo ya pili umesahau wanaume wengi wanvojipendelea kujisosomola kwenye lunch,breakfast,na moja moto moja baridi hela wanazotumia toka asubuhi mpaka muda wanarudi home usiku zinalingana na zile wanazowapa wake zao kama hela za matumizi iwe ya siku au ya mwezi?tuanze na kuwauliza wa humu jamvini?leo ndyo leo!
 
pacha bora umekuja!
mi ugomvi wangu kwa wale wanaowaachia majukumu wake zao kisa wana fanya kazi,na wala sio siri hili wanaume wanalifanya sana!sasa jamani tusipotumia pesa zenu tukatumie za nani?nyie mwageni mihela siye si ndo wadau wakuu twazitumia,zetu ni za kununulia karoti na less wig au we unaonaje pacha!af nilisahau kukusalimia!mambo?dom wazima?
 

Mie sijambo pacha wangu na dom fresh tu aisee..
Ukute mfano wewe ndo una kipato kikubwa kuliko mumeo..utasubiri adundulize ndio mnunue kibajaji alimradi zako unawapelekea wamasai..lol. Wakati mwingine inabidi mpange maisha kwa kuangalia mbele zaidi. Maisha yanaenda kasi sana aisee..
 

hapana ila nataka hata hico kidogo ukilete tukitumie sio ndo uchukulie poa tu!nunua hata sukari kilo kumi lete home,kwani mkeo si anajua mume ana kipato kidogo,shida ni pale mtu ana kapto na bado anataka muke yake ifanye mabo yote home anhhha hiyo haikubaliki!kufanya kazi sio ndo sababu ya kuwaachia majukumu kinamama,kwanza huwa mna msemo wenu wenyewe,eti we wife hela yako itumike kwa msosi na mambo mengine ya ndani mi yangu ni ya kujenga na mambo mengine makubwa makubwa!
pacha unajua matumizi ndani ni makubwa sana kuliko mnavoyatazama?hizo za less wig ni kamfano tu lakini bado mwananmke ana haki ya kuhudumiwa na mumewe hata kama anafanya kazi!tufanye joint sawa lakini nikitaka zile hela za kudeka pia nipewe sio uso wa mbuzi tu kisa nafanya kazi!
 
Hahahaha pesa za mkeo wewe mwanaume za nini?hizo ni dalili za kukwepa uwajibikaji..mambo ya kutunza mke na familia ni la kwako aisee acheni kukwepa majukumu nyie wanaume wa dot com
Kujua maendeleo ya mke wangu ni moja ya majukumu yangu kwahiyo kutofatilia mashahara wa mke wangu unafanya shughili zipi ni kukwepa majukumu pia.
 


Uposema mwanamke ahudumiwe na mke wake unamaanisha nini snowwhie?
 
Last edited by a moderator:

can you prove that? unahisi tu kwa sababu bwana wako anarudi late night bas unafkir wote tunarudi late hours. kujilipia nauli ya kwenda kazini kwake kwa mshahara wake kamwe sio zigo la financial obligation as you call it!
 
can you prove that? unahisi tu kwa sababu bwana wako anarudi late night bas unafkir wote tunarudi late hours. kujilipia nauli ya kwenda kazini kwake kwa mshahara wake kamwe sio zigo la financial obligation as you call it!

easy jamani!easy!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…