Misa ya Mkapa: Nimeona tofauti kubwa kati ya maaskofu wa Katoliki na wale wa makanisa kama la Gwajima!

We unataka tukubali ujinga? Warumi ndo wapingaji wa kanisa la Kristo, warumi ndo waliuwa mitume wa Kristo, warumi ndo walipotoa mafundisho ya biblia wakatunga ya kwao, warumi ndo waliingiza sherehe za kirumi na kuzipa utukufu wa kristo ili zikubalike. Wapi umeona neno KRISMAS? Andiko gani?


Mmh!
 
Ewe mpotevu uliyeacha mafundisho ya Kristu utatangatanga mpaka lini? Au ni dhambi ya kuasi na kujaribu kulishinda kanisa la Kristu ndiyo inakutesa? Kanisa ni Moja,Kanisa ni takatifu,Kanisa ni katoliki(limeenea ulimwenguni) Kanisa ni la mitume.

KANISA NI MOJA TU LILILOANZISHWA NA KRISTU

Kuna wakati ni vizuri tukaelezana ukweli bila kujali nani atakubaliana nao. Nataka nieleze kidogo jinsi Yesu alivyoanzisha Ukristo(kwasasa nitumie neno hili) na baadhi ya alama zinazotambua kazi hii ya Kristo na tuone kama alianzisha Kanisa au Makanisa.

1) UTEUZI WA MITUME 12

Yesu aliteua mitume 12 ambao walikuwa wakimwita Mwalimu (rabi) na kwenye maandiko mengi wakiitwa wanafunzi wake. Hawa walimfuata kote alikokwenda na kusikia kila alichofundisha. Kulikuwa na makundi makubwa ya watu kote alikokwenda lakini kwa miaka yote aliyohubiri alikuwa na wanafunzi wake.

Wakati Yesu akiteua Mitume tunaona jinsi alivyokuwa akiteua kila mmoja kwa sifa zake huku akiongozwa na Roho. Mfano uteuzi wa Petro tunaona Yesu alikwishajua huyo ndiye atakayekuja kuwa kiongozi wa Mitume yeye akiondoka duniani ndio maana alimtambua alipomwana na kumbadili jina ambalo baadae anakuja kufafanua wakati akimsimika Petro kama mkuu wa Kanisa Mathayo 1;42 Andrea akampeleka Simoni kwa Yesu. Yesu akamtazama, akasema, ``Wewe ni Simoni mwana wa Yohana; sasa utaitwa Kefa(tafsiri yake Petro au Jiwe).''

Uteuzi wa mitume 12 ni kusimika utawala ambapo tunaona kabla ya kuondoka akiwapa maagizo ya kufanya na kuwapa mamlaka kamili ili walijenge Kanisa lake. Tunaona kwenye matendo ya Mitume kuwa mitume walipiga kura kuchagua mtu wa kuziba nafasi ya Yuda ili idadi ile iliyokusudiwa na Kristo kama msingi wa Kanisa iwe pale pale.

2) KUMTEUA PETRO KUWA KIONGOZI WA MITUME

Hapa ni moja ya sehemu tunapotofautiana wakristo wengi. Yesu alimteua Petro kuwa askofu wa kwanza wa kanisa. Tunaona toka Yesu alipomwona tu Petro alimbadili jina na kumuita Kefa yaani Jiwe alafu baadae Yesu anakuja kutamka hili kwa Petro (si Mitume wote bali specifically Petro) Mathayo 16;18-19 “Nami nakuambia, wewe ni Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu ambalo hata nguvu za kuzimu haziwezi kulishinda. 19 Nitakupa funguo za Ufalme wa mbinguni na lo lo te utakalolifunga duniani litakuwa limefungwa mbinguni na lo lote utakalofungua duniani litakuwa limefunguliwa mbinguni.”

Lakini kabla Yesu hajampa mamlaka hayo Petro tunaona akimhoji Petro mara kadhaa kama msisitizo wa jukumu jipya analotaka kumtwisha (Yohana 21;15-17) Walipokwisha kula, Yesu akamwuliza Simoni Petro, “Simoni mwana wa Yohana, unanipenda kweli kuliko hawa?” Yeye akamjibu, “Ndio Bwana, wewe unajua ya kuwa nakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha wana kondoo wangu.” 16 Kwa mara nyingine Yesu akamwul iza Simoni Petro, “Simoni, mwana wa Yohana, unanipenda?” Petro akajibu, “Ndio Bwana, wewe unajua ya kuwa nakupenda.” Akamwam bia, “Chunga kondoo wangu.” 17 Kwa mara ya tatu Yesu akamwul iza Petro, “Simoni mwana wa Yohana, unanipenda?” Petro akahuzu nika sana kwa kuwa Yesu alimwuliza mara ya tatu, ‘Unanipenda?’ Akamjibu, “Bwana, wewe unajua kila kitu. Unajua ya kuwa naku penda.” Yesu akamwambia, “Lisha kondoo wangu.

Maandiko yanathibitisha Yesu alimkabidhi Petro uongozi wa Kanisa baada yake yeye aliyekuwa kiongozi kuondoka, hii ni dhahiri aliona umuhimu wa kuchagua kabisa kiongozi miongoni mwao.

3) YESU ALIANZISHA KANISA SI MAKANISA

Tunaona Yesu alianzisha Kanisa na kuweka mitume 12 huku Petro akisimikwa kama kiongozi wao. Hii maana yake Yesu alianzisha Kanisa lenye utawala rasmi na pia kusema hata milango ya kuzimu haitalishinda, kwahiyo sifa moja muhimu ya Kanisa la Kristo lazima liwe na mtiririko wa kiutawala unaoanzia kwa Petro hadi leo maana Kristo alisema halitakufa. Lakini pia Yesu alisema atalijenga Kanisa lake na hakusema nitajenga makanisa yangu. Leo tuna makanisa mengi ingawa wote tunakiri Kristo lakini ni makanisa si Kanisa maana ili liwe Kanisa lazima liwe moja chini ya kiongozi mmoja ambaye mamlaka yake unaweza kujua jinsi alivyopata kuanzia kwa Petro hadi leo. Wengi kutafuta shortcut watasema kiongozi wao ni Kristo lakini wanasahau huyo Kristo hakuliacha Kanisa bila utawala rasmi ambao haukufa Petro alivyokufa bali upo hadi leo. Hivyo hakuna mwenye uwezo wa kuanzisha Kanisa maana kazi hiyo alishaifanya Kristo miaka 2000 iliyopita, tunachopaswa kufanya ni kujua Kanisa hilo ni lipi hadi leo?

4) YESU ALITOA MAMLAKA KWA KANISA

Tunaona Yesu akiwapa maagizo mitume kwenye mambo mengi lakini ahadi kubwa juu yao ni kuachiwa msaidizi atakaye waongoza kwenye kweli yote Yohana 14;26 “Lakini yule Msaidizi, yaani Roho Mtakatifu, ambaye Baba yangu atamtuma kwenu kwa jina langu, atawafundisha mambo yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.”

Hivyo Kristo alitupa dira ya kumtegemea Roho Mtakatifu kutuongoza katika kweli. Lakini tunaona baadae Kanisa lilivyokuwa likizidi kukua changamoto za kuibuka watu na kufundisha wanayotaka na uzushi mbalimbali zikafanya Kanisa lione umuhimu wa kukusanya maandiko matakatifu na kuyaweka pamoja na kuwa sehemu ya msingi wa Imani. Hivyo Kanisa (si makanisa) ndio msingi wa ukweli maana ukweli hufunuliwa na Kanisa kwa msaada wa Roho Mtakatifu ndio maana hiyo Biblia unayotumia ni Kanisa liliamua nyaraka zipi ziwekwe, injili zipi ziwekwe, mpangilio uweje, kutoa majina ya waandishi wa injili kupitia Council of Hippo mwaka 393 ndio tunaona kazi hii ikifanywa rasmi.

HITIMISHO,

Hivyo kwa ujumla tunaona Kristo alianzisha “visible” church na hakuanzisha Makanisa ndio maana kwa mfano hatusemi makanisa ya Katoliki bali Kanisa Katoliki. Kwa neema ya Mungu na upendo wake usio na kipimo kwa watu wake, Roho Mtakatifu anatenda kazi hata nje ya Kanisa Katoliki lakini ukweli wa Kanisa kuwa MOJA tu haufutiki na wakristo wengine ni vyema mkajua hilo.

Mchungaji yeyote halali mbele za Mungu LAZIMA uzi wake, mamlaka yake tukiyafuatilia yarudi hadi kwa Mitume. Ndio maana wachungaji wa baadhi ya Makanisa mamlaka yao kichungaji yanakubalika wakiwemo Walutheri, Aglikana n.k sababu wamepokea mamlaka kutoka kwa watumishi waliokuwa wachungaji wa Kanisa Katoliki ambalo ndio pekee lenye mtiririko wa kimamlaka unaoweza kufatiliwa hadi kwa Petro na Mitume.

Si sahihi kukaa kwa mtumishi usiyejua alipakwa mafuta na nani kama sehemu ya kwanza muhimu kabla hujaangalia mengine kujua kama upo sehemu sahihi. Usifate miujiza na mafundisho yanakuvutia tu maana Yesu mwenyewe alisema watakuja walimu na manabii wa uongo na hakusema watakuja wachache alisema watakuja WENGI na kama haitoshi akasema watadanganya WENGI na si kudanganya wachache.
Ewe unayefahamu lakini kwa kusudi la kupotoa mafundisho ya Kristo na wewe unaamua kupotosha ili hali unajua na unaelewa. Inatakiwa uelewa huo sasa umgeukie Kristo, uache kujilisha upepo na mafundisho ya warumi yaliyo maagizo ya wanadamu.

Nimefurahi unajua hakika Yesu ndiye mwanzilishi wa Kanisa na ndiye mmiliki wa kanisa. Swali pekee ambalo umeshindwa kulijibu ni kanisa lipi? Badala utoe jibu sahihi unarudi kwenye upotofu wako, wa kudhani ni kanisa katoliki, ndilo kanisa aliloanzisha Kristo. Pole sana.

Yesu alisema ataanzisha kanisa na akaanzisha kanisa karne ya 1, miaka 30-33 tu. Mitume wake wale 11, jumlisha mmoja 1, walifanya kazi ndani ya karne hiyo moja, na waliuwawa kwa namna mbalimbali kwa sababu ya injili ya Kristo.

Kanisa la warumi(roman catholic) limeanza karne ya 4, miaka 300+ baada ya kanisa la Yesu kuanza na kufanya kazi. Kazi ya kulihudumia kanisa la Kristo ni mbiyo za kijiti, waliachiana kijiti nasi tunaachiana kijiti. Miaka 320 baada ya Kristo kuondoka, ndipo mfalme Augustino wa dola ya kirumi alipotangaza kulegeza mateso na unyanyasaji kwa wakristo. Naye aliikubali na kuwa mkristo.

Hata hivyo, Augustino hakukubali kubatizwa kama walivyobatizwa wakristo wengine, alikubali ukristo, lkn hakufuata kanuni za ukristo hasa ya kubatizwa. Alinyunyizwa, na ndio likawa pokeo jipya la ubatizo wa kunyunyiza. Hautopata popote kwenye biblia, ni Augustino ndo aliamua.

Hivyo, pamoja na Augustino kukubali kuwa Mkristo, ilimweya vigumu kuacha mila na desturi za kirumi. Ndipo hapo sasa walipo kaa mezani wakaanzisha taratibu rasmi za kirumi za kumwabudu Mungu. Taratibu zote hizo hutazipata kwenye biblia, ila waliamua wenyewe. Baadhi ni yafuatayo:-

1. Dini kuambatana na uongozi wa serikali.
2. Dini kuanzisha utawala na kumiliki njia za kiuchumi.
3. Tamaduni za kirumi kukopwa na kutumika kama taratibu za kanisa la Kristo. Mfano, sherehe za Krismas hutazipata popote kwenye biblia, ni mipango ya kirumi.
4. Wakaanzisha litrugia na makao makuu ya kanisa la kirumi. Kumbuka makao makuu ya kanisa la Yesu ni kule aliko Yesu, alienda kutuandalia makao.
5. Wakaanzisha sala za maria, rozari ambavyo hutaviona kwenye biblia. Wakati biblia inasema *"....mimi ndiyo njia kwelo na uzima...."* warumi wakaanzisha utaratibu wa kuomba kupitia kwa Maria.

Walipindua mengi sana, mengi mno.

Haya, ukisema ni wakatoliki wali assemble biblia, nikubaliane na wewe kisha nikuulize yafuatayo.

1. Kwa nini sasa wapingane nayo? Biblia inasema "...msiitwe baba nyie duniani, kwa kuwa baba yenu ni mmoja naye ndiye Mungu...". Kwa nini wakatoliki mnao mababa?

2. Kama wao ndo walitengeneza biblia, kwa nini watofautiane na 1Timoth 3ff? Ambayo inataja sifa anuawai za mtu kuwa askofu? Na nani alikuambia, kwa andiko lipi Mtume Petro aliitwa askofu? Umeona wapi? Kuna tofauti ya mtu kuwa mtume, mwalimu, mwinjilisti na kuwa askofu. Askofu ana vigezo vyake vinavyopimika.

3. Wakusanye maandiko lkn washindwe kuliishi neno la ubatizo? Petro alibatizwa kwa kuzamishwa na wanafunzi wote na Yesu mwenyewe, kwa nini warumi hamzamishi?

Jambo lingine nikukumbushe, kanisa ni moja nalo ni la Kristo. Ile kutaja la warumi maana yake limeanzishwa na kumilikiwa na warumi. Waanglican limeanzishwa na kumilikiwa na waanglicani. Sasa kulisambaza dunia nzima kanisa lao, haina maaana kuwa ndio umoja unaotajwa wa kanisa la Kristo. Wanasambaza la kwao, anglican la kwao, fpct la kwao, full gospel la kwao n.k.
 
John the baptist, nadhani tubaki na Utanzania ambao ni unatuunganisha kuliko kufuata misingi ya namna ya kuendesha ibaada.

Uaskofu ni wito wa kumhubiri Yesu Kristo ambae ni Bwana na mwokozi wa wanadamu. Namna ya kuendesha ibaada in mapokeo toka Vatcana au kwingineko. Kama umewahi kumsikia Martin Luther King mchungaji na activist, hakuna na mfumo wa kuzungumza kwa culture ya Vatcana, yet content yake kwenye injili ya Yesu au utetezi wa haki za binadamu haukuwa na "ustaarabu wa Vatcana". Kama umskikiza Jesse Jackson, huwezi kumlinganisha na Ruachi au Pengo.

Yet, wote ni watumishi na tuwaheshimu kwa mwito wao wa kuhubiri injili ya Yesu Kristo.

Tuwaacheni watumishi watumikie mwito wa Mungu maishani mwao, maadamu wapo kwenye muktadha wa kuhubiri upendo wa Kristo kwenye maisha ya watu.
Maadam wanaendeleza mila na desturi za kirumi, hawapaswi kuitwa watumishi wa Kristo bali watumishi wa Rumi. Fahamu hilo
 
Acha upotoshaji katoliki ni kanisa linaloendesha mambo yake ovyo hovyo na wala hawana utaratibu wowote mzuri kama unavyodai
 
Kanisa Katoliki ni taasisi mambo yake ni ya kitaasisi tofauti na makanisa ya hao wahuni kama Gwajima
 
Hapana.Mafundisho yanafundisha kuwa papa si mwakilishi wa Mungu duniani bali ni Khaifa wa mtume Petro.
Mathayo 8:13
Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani? 14Wakasema, Wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii. 15Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani? 16Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai. 17Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni. 18Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.

19 Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni. 20Ndipo alipowakataza sana wanafunzi wake wasimwambie mtu ye yote ya kwamba yeye ndiye Kristo.

Petro ndiye aliyekabidhiwa mamlaka hayo kutoka kwa Kristu Yesu mwenyewe ili kuliongoza kanisa lake.Petro amekabidhiwa funguo za mamlaka anaweza kufunga na kufungua jambo duniani na mbinguni ikawa hivyo.Baada ya Petro ambaye ndiye papa wa kwanza kabisa na kiongozi wa kanisa la Yesu kanisa limeendeleza utaratibu wa kiti cha Petro ili kuchunga na kulinda kondoo wa bwana.

Yn 21:15-25

Basi walipokwisha kula, Yesu akamwambia Simoni Petro, Je! Simoni wa Yohana, wewe wanipenda kuliko hawa? Akamwambia, Naam, Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, Lisha wana-kondoo wangu. Akamwambia tena mara ya pili, Simoni wa Yohana, wanipenda? Akamwambia, Ndiyo, Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, Chunga kondoo zangu. Akamwambia mara ya tatu, Simoni wa Yohana, wanipenda? Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, Wanipenda? Akamwambia, Bwana, wewe wajua yote; wewe umetambua ya kuwa nakupenda. Yesu akamwambia, Lisha kondoo zangu.

Sote tu mashahidi juu ya kazi kubwa ya kitume inayofanywa na papa dunia nzima katika kumtangaza Kristu na kuhubiri ujumbe wake.Mfano Papa Yohane Paulo II alizunguka nchi nyingi sana duniani na kote alipofika alitangaza na kuhubiri ujumbe wa Yesu kuhusu amani.Papa ni mpatanishi na msuluhishi wa migogoro mingi iliyo na inayotokea duniani.Kazi hizi ni ishara wazi kuwa yeye amekabidhiwa mamlaka na msalaba kama alivyokabidhiwa Petro katika kuendelea kuchunga kondoo wa Bwana.
Nani kakudanganya kuwa Petro alikuwa papa wakwanza? Huo ni uongo na hakuna andiko linalosema hivyo.
 
Maadam wanaendeleza mila na desturi za kirumi, hawapaswi kuitwa watumishi wa Kristo bali watumishi wa Rumi. Fahamu hilo
Sina la kusema mkuu. Anaewaita ni Mungu alie juu, kwa kumtumikia kwa kufuata desturi za Vatcana au kwingineko,sina la kusema kabisa.
Ila itoshe tu kuwaheshimu kwa wao kuitikia wito wa "Alie juu"
 
Sina la kusema mkuu. Anaewaita ni Mungu alie juu, kwa kumtumikia kwa kufuata desturi za Vatcana au kwingineko,sina la kusema kabisa.
Ila itoshe tu kuwaheshimu kwa wao kuitikia wito wa "Alie juu"
Juu wapi mkuu? Vatcan ni juu? Asilimia 90 ya wanaylyafanya ni maagizo ya Vatican siyo juu. Hebu sona 1Timo 3, uone sifa za wanaoyafanya ya aliye juu
 
Ukiwakuta wana sali unaweza sema wanafukuza mwizi,kuna wengine haitoshi wao kabla ya kuombea wanaomba kipaza sauti,sasa sijajua shetani anaogopa kipaza sauti,yaani unaya treat maswala ya kiroho kwa kutumia njia za kimwili.

Yesu alikemea lakini si kwa style yao fujo tupu.
 
Na wewe nionyeshe andiko lisilosema hivyo
Andiko linalosemaje? Wewe ndo ulete andiko la Petro kuitwa papa. Halipo, ila lipo linalokataza ujinga huo wa kuitana baba mtakatifu.

Soma Mathayo 23:9 Wala msimwite mtu baba duniani; maana Baba yenu ni mmoja, aliye mbinguni. Wala msiitwe viongozi; maana kiongozi wenu ni mmoja naye ndiye Kristo.

Na kwa andiko hili ni uthibitisho wa hekaya zenu kuwa warumi ndio waliounganisha biblia, ilikuwaje wakakiuka andiko hilo?
 
Imani ya makanisa ya Kikatoliki, na makanisa yote ya kiprotestanti k.v Lutheran, Anglikana, Moravian, Menonite, nk ni makanisa yanayomwabudu Mungu kwa kuishia kwenye nafsi. Nafsi ya mwanadamu imeundwa na components kuu tatu UTASHI, AKILI, na HISIA. Ibada zao zote huwa hazivuki hapa na kuingia rohoni.

Ibada zao zimekaa kiakili-akili, na kihekima-hekima tu,,. Ndio maana utakuta mtu anaitwa askofu mkuu ila hawezi kukemea viumbe vya rohoni kama mapepo/majini, ... kwa sababu roho hizi chafu hukemewa kwa namna ya rohoni.

Ninapoyasema haya sio kwamba ninamsapoti Gwajima, ila lipo Kanisa la kweli (sio Gwajima, na sio Katoliki). Ukitaka kulijua nitafute.

Jesus is Lord .
Ndivyo mnavyojidanya mdogo wangu nilimwachia ziwa alitolewa pepo na padri bila hayo makelele yenu,kamshika kichwa kamwombea,kamwagia maji na alikuwa peke yake sisi tukiwa pembeni.

Mungi haitaji mbwembwe.
 
Hapana.Mafundisho yanafundisha kuwa papa si mwakilishi wa Mungu duniani bali ni Khaifa wa mtume Petro.
Mathayo 8:13
Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani? 14Wakasema, Wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii. 15Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani? 16Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai. 17Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni. 18Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.

19 Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni. 20Ndipo alipowakataza sana wanafunzi wake wasimwambie mtu ye yote ya kwamba yeye ndiye Kristo.

Petro ndiye aliyekabidhiwa mamlaka hayo kutoka kwa Kristu Yesu mwenyewe ili kuliongoza kanisa lake.Petro amekabidhiwa funguo za mamlaka anaweza kufunga na kufungua jambo duniani na mbinguni ikawa hivyo.Baada ya Petro ambaye ndiye papa wa kwanza kabisa na kiongozi wa kanisa la Yesu kanisa limeendeleza utaratibu wa kiti cha Petro ili kuchunga na kulinda kondoo wa bwana.

Yn 21:15-25

Basi walipokwisha kula, Yesu akamwambia Simoni Petro, Je! Simoni wa Yohana, wewe wanipenda kuliko hawa? Akamwambia, Naam, Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, Lisha wana-kondoo wangu. Akamwambia tena mara ya pili, Simoni wa Yohana, wanipenda? Akamwambia, Ndiyo, Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, Chunga kondoo zangu. Akamwambia mara ya tatu, Simoni wa Yohana, wanipenda? Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, Wanipenda? Akamwambia, Bwana, wewe wajua yote; wewe umetambua ya kuwa nakupenda. Yesu akamwambia, Lisha kondoo zangu.

Sote tu mashahidi juu ya kazi kubwa ya kitume inayofanywa na papa dunia nzima katika kumtangaza Kristu na kuhubiri ujumbe wake.Mfano Papa Yohane Paulo II alizunguka nchi nyingi sana duniani na kote alipofika alitangaza na kuhubiri ujumbe wa Yesu kuhusu amani.Papa ni mpatanishi na msuluhishi wa migogoro mingi iliyo na inayotokea duniani.Kazi hizi ni ishara wazi kuwa yeye amekabidhiwa mamlaka na msalaba kama alivyokabidhiwa Petro katika kuendelea kuchunga kondoo wa Bwana.
Uache utapeli wako mkuu. Wapi imeandikwa Peter ni Papa wa Kwanza? Wapi Petro alikabidhi huduma mtu mmoja na kumpa uongozi? Hivi nyie mnasoma biblia kweli?

Hebu soma Mathayo 23:9-12 halafu njoo tujadiliane tufute ujinga huo kwa pamoja

Screenshot_20200728-125750.jpg
 
Juu wapi mkuu? Vatcan ni juu? Asilimia 90 ya wanaylyafanya ni maagizo ya Vatican siyo juu. Hebu sona 1Timo 3, uone sifa za wanaoyafanya ya aliye juu
Kwa misingi ya biblia, kuna mengi mazuri wanayofanya japo kwa kupungukiwa sifa ya kuwa wanandoa naomba nisitie neno hapa.
Ila itoshe kusema, "Yule mama aliekamatwa na mafarisayo akizini wakitaka apigwe mawe, Yesu hakumtia hukumuni japo alijua ametenda dhambi.

Principle aliyoitoa ni nenda usitende dhambi tena.

Kwa kuwa wajua wana nakisi ya kukidhi utimilifu wa maandiko, nikushauri uwatafute na kuwasaidie waijue kweli yote kibiblia na sio kufuata maelekezo ya Vatcana pekee.
 
Kwa misingi ya biblia, kuna mengi mazuri wanayofanya japo kwa kupungukiwa sifa ya kuwa wanandoa naomba nisitie neno hapa.
Ila itoshe kusema, "Yule mama aliekamatwa na mafarisayo akizini wakitaka apigwe mawe, Yesu hakumtia hukumuni japo alijua ametenda dhambi.

Principle aliyoitoa ni nenda usitende dhambi tena.

Kwa kuwa wajua wana nakisi ya kukidhi utimilifu wa maandiko, nikushauri uwatafute na kuwasaidie waijue kweli yote kibiblia na sio kufuata maelekezo ya Vatcana pekee.
Waliohoji maamuzi ya Vatican, siyo watawa tena. Mfanl Fr Nkwera hata huyu mwandishi Privatus Karugendo. Alihoji anakuwaje Padre ilo hali hana ndoa, leo anaendelea na ndoa yake japo ukatoliki bado umemzingira. Askofu Slaa aligundua hilo akajisalimisha kwa Mshumbusi lkn ukatoliki wa kufuata maagizo ya Vatican bado umemzinga.

Biblia iko wazi sana, haijatuficha jambo lolote ni sisi tu kukubali na kutii
 
Back
Top Bottom