REJESHO HURU
JF-Expert Member
- Mar 6, 2014
- 5,161
- 11,263
Afisa elimu kijiji?!hakunaga cheo kama hiki Tz na hii inamaanisha story yako ni uongo tu.
ona uyu naye kakurupuka tu anadandia gari kwa mbele utagogwa mwenzako kasema jiji wewe eti kijiji
Afisa elimu kijiji?!hakunaga cheo kama hiki Tz na hii inamaanisha story yako ni uongo tu.
mambo ni ya kawaida sana. Oanisha fikra zako na kitendo ulichofanya na unachotaka kukifanya. Unaposema"sasa nimepata kabinti kalikoishia darasa la saba". Kwa fikra zako...wew ni tembo na uanataka kushare na sismizi...uwe mwalimu na kiongozi wake kwa kila kitu. Mfunze vile unavotaka awe. Futa akilini mwako iyo dhana ya dharau uliyonayo kwake kwamba ni "kabnt kalikoishia", utafurahia maisha ya wawili.
Ninapofikiri kuwa unatabia ya dharau kwa mtu unayetaka kushare naye maisha...nakuchukia. Vingnevyo achana naye...ukamtafute utakayemzungumzia kwa mizani ya heshima. Acha dharau bro.
Asante mwanaume.
Naona Leo kumekucha vizur tuanzishe ligi la jana niniii
Mwombe Mungu akupe mke sahihi,maana bila hivo utaachana na wengi
jaman wanajamvi nipeni mawazo yenu. kuhusiana na kichwa cha habari hapo juu. mie ni muislam. nilioa primary ticha nikaachana nae baada ya kubaini anafanya ngono na afisa taaluma wa jiji. sasa nimepata kabinti kalikoishia darasa la saba. nipeni uzoefu haya maisha yatakuaje kwa gepu hilo kubwa la elimu???!!
NAWASILISHA....
Kwani via (viungo) vyenu vya uzazi vina elimu gani?
Afu huo uzi nautafuta siuoni nataka nijue ligi iliishaje mods wameutupia kapuni nini:sly:
Huyo wa la saba akikutana na mashangingi ya jiji utalia. Waendesha bodaboda wafyatua tofali wauza bucha wrote wake. Angalia tu mwanamke msomi anayejitambua.
ACHA DHARAU BRO. Huwezi kwa elimu uliyoitaja kuwa nayo, ukamuelezea binti unayetaka kushare naye maisha kama" kabinti kalikoishia darasa la saba". Maana yake wew si kiongozi mzuri...na uyo utamuacha ...source ni dharau zako.
Rekebisha mtazamo wako kwa mwanamke yeyote unayetaka kushare naye maisha...itakusaidia. Vingnevyo...usifanye hivyo sasa...subiri akili yako ipoe....UTAMUUMIZA UYO BINT KAMA HUNA BUSARA.
Umalaya ni silka ya mtu tu haijalishi amesoma au hajasoma. Na kwenye ndoa kikubwa ni kuvumiliana kwa hiyo ni juu yako kuamua ni makosa/mapungufu yapi unaweza kuyavumilia kwa mwenza wako. Unaweza oa huyo darasa la saba akawa anagawa tu na anaweza pia akawa ni mwanamke anayejiheshimu. Kimsingi kwenye mahusiano elimu sio kigezo muhimu sana kwa sababu hatuendi shule ili tuje tuwe na mahusiano mazuri kwenye ndoa, tunaenda shule ili tuwe na maisha mazuri.
Nina mifano miwili hai. Mimi ni PhD candidate na mke wangu ni darasa la saba, kuhusu uaminifu namuamini asilimia 800, lakini moto unaniwakia kwenye mambo mengine kiasi kana kwamba ndoa haiko stable kabisa.
Halafu kuna jamaa nafanya nae kazi sehemu moja (PhD candidate) alizaa na mwanamke (elimu yake darasa la saba) watoto wawili halafu akaamua kuishi na mwingine. Kabla hajaanza kuishi na huyo tulimshauri sana angeishi tu na huyo aliyezaa nae akakataa. Sababu yake ni kwamba alikuwa anataka mwanamke ambae watakuwa wakiongea lugha moja (upeo unaofanana). Kwa mfano wakiongea kuhusu escrow au katiba au anything trending wawe wanaelewana. Kwa hiyo alikuwa anataka mtu walau aliyefika form six. Akampata mwanafunzi wa chuo kikuu (sasa hivi ashamaliza) wakaanza maisha. Huo moto wake! Mpaka anataka kukimbia nyumba. Mkewe akiwepo home yeye anarudi saa sita usiku kila siku, mkewe akisafiri yeye anarudi home saa 12 jioni kila siku mpaka mkewe atakaporudi. Maana yake ni kwamba, anapenda kuwahi kurudi home lakini mwanamke ndio anamfanya asirudi mapema. Ameapa hatuji kumwona altareni eti anahalalisha hiyo ndoa. Na tayari wana mtoto mmoja!
Kimsingi kama umeridhika na tabia zake oa tu kuhusu elimu mnaweza hata kuendelezana baadae, siku hizi opportunities za kuongeza elimu ni nyingi. Cheers!!!
Hahahaaaaaa, we Viol hufai kabisa! kumtetea kote huko shy land kwa upuuzi wake leo unajifanya ulikuwa umelewa? Acha hizo mkuu!Jana nilikuwa nimelewa,
Btw kesho my birthday nitakie hata wishes kabla