Mimi nina masters nataka kuoa Darasa la saba

Mimi nina masters nataka kuoa Darasa la saba

Mkuu, Uzi wako umenipa nguvu ya kuoa form 4 wangu maskini, maana nilikuwa najiuliza sana juu ya chaguo langu."hivi ni kweli ndo naenda kuoa huyu mwanamke, mbona kama hatufanani?" nikimaanisha kielimu..! mie nna kadigrii kangu yeye form 4 leaver...hata kazi hana ukiondoa kumsaidia mama ake kuuza duka la vipodozi....na kinachoniumiza kichwa zaidi kuona rafiki zangu wengi wa karibu wameoa wake ambao ni wasomi wenzao..wengine tayr hao wake zao wakiwa na kazi zao na wengine bado wanapambana kutafuta ajira...but wana degree zao mkononi.

Nikimfikiria huyu wangu wakati mwengine nachoka kabisa..maana mawazo wakati mwngine yanafika mbali kbs,najiuliza kwa mfano akikutana na wake wa marafiki zangu hatojisikia vibaya? kuona wenzake wana elimu ya kutosha hlf yeye ndo hivo tena...najiuliza hata stori zao zitaendana kweli?

Ila nimeamua kuoa tu maana nishamtia tamaa sana na sio yeye tu hadi mama yake na baadhi ya ndugu zake wa karibu..nikimuacha kwa kigezo cha elimu nahisi si sababu madhubuti na Mungu anaweza hata kunipa mtihani katika maisha yangu ya ndoa kwa hao wengine.coz huyu mtoto hana shida she is cool, heshima,mapenzi na hana tamaa...sio omba omba wa hela,mpk wakati.mwengine najisikiaga aibu naamua kumgaia hata kama hajaomba...na tena anashukuru hata ukimpa buku 5 anaona nyingi...cjui huko mbele itakuaje naomba Mungu asibadilishe tabia na fikra zake.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mbona form 4 ni elimu inatosha kabisa? Kiukweli wanawake wenye elimu kubwa sana level ya Degree ni kazi sana kuwa-manage. Ingawa sio wote wengine wanajielewa na kutambua role zao kama wake wa ndoa. Ila kwa hizo elimu za chini kiukweli ndoa inakua inaheshima, na mwanaume unaona kabisa uanaume wako. Ukisema NO ni NO kweli. Kikubwa katika ndoa ni Amani ya furaha, hasa kama kuna kusikilizana. Kiukweli mie nilioa Mwalimu wa Shule ya Msingi, alinisumbua sana. Mbaya zaidi akawa anagongwa na Afisa Elimu-Michezo ikawa kila issue inayohisu semina au kusimamia mitihani huyo aliyekua mke wangu yumo. Kuna siku nilimuuliza hivi wewe umehamia hapa mkoani juzi tu, leo hii umekua maarufu mpaka kila issue lazima uwepo? Baadae nikajua kila kitu kwa kutumia uchunguzi binafsi. Kabla ya hapo alisha nisumbua sana. Sasa hivi nina amani sana katika ndoa hii, ingawa kuna changamoto chache za kiubinaadam. Katika ndoa mambo yote yanavumilika lakini sio Kutoa PAPUCHI kwa njemba nyingine mtaani. Na furaha ya ndoa iko hapo tu.
 
Kikubwa tazama kipato,kama uwezo wa kua na mke akakaa tu ndani na wewe ukatimiza mahitaji yote ya kifamilia ya sasa na ya kimaendeleo oa hata ambae hajasoma kabisa ila kama unaona uwezo wako ukioa ambae aongezi kitu basi hamsogei hapo tafuta mwenye elimu au mwenye upeo ambae unajua ukimpa business hata ya kuku au mama ntilie ataiendeleza. Usitazame tu mapenzi tazama maisha yako unataka yaje kua vipi,chaguo sahihi litakufanya usije juta kesho
 
Kuna tofauti kubwa kati ya Elimu na IQ kwanza tuanze na hilo, Ukiwa kama msomi mwenye Elimu ya kiwango cha Masters haukupaswa kujiuliza hili swali. nadhani kuna kitu Watanzania tunatakiwa kukitambua kuwa akili ya kawaida ndio huvumbua mambo mengi duniani na sio ya kufundishwa darasani. Mfano Genius wote duniani wamevumbua vitu ambavyo havimukuwepo duniani na kwa maana hiyo ili ugundue kitu ni lazima kisiwepo duniani wewe ule wa kwanza kukitambulisha ndio maana halisi ya ugunduzi. "Note" Kuwa na mwanamke ambaye amesoma au hajasoma kabisa sio kipimo mahusiano na maendeleo ya maisha au malezi ya familia.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kweli kabisa. Lakin sikukosea kuja hapa kuweka hili bandiko. Kuna kitu inaitwa UTAFITI. utafiti sio lazima utembee nyumba hadi nyumba Kupata taarifa. Nilitaka nijue Mitazamo ya watu juu ya Hili suala. Lakin kichwani na moyoni nilikua tayari nina maamuzi yangu. Ndio Maana ITV wana KIPIMA JOTO, ile ni utafiti na wanapata Data ambazo zinaweza kuja kutumiwa kufanya Maamuzi fulani.
Wanaume wengi wanaoa wanawake wasomi kwa kujua kwamba watasaidiana katika majukumu ya Famila. Kuna baadhi yao matarajiao yao yanakua tofauti baada ya ndoa Hela za wanawake zao hazionekani au hazishikiki. Pia ndio huwa sababu ya mwanzo wa mifarakano ya Ndoa hizo.
Nawashauri Vijana Oeni wanawake kwa Kuangalia Hofu zao Kwa MUNGU, Tabia na Usikivu. Unaoa Mwanamke Mfanyakazi, Huyo atatii Bosi wake kazini, Wewe Mumewe utafuata. Kuna Siku yule Muke niliyeacha aliniambia "Mume wake wa kwanza ni Kazi anayofanya"
 
Jamani wanajamvi naombeni Mawazo yenu. Kuhusiana na kichwa cha habari hapo juu, mie ni Muislam, nilioa Mwalimu wa Primary nikaachana nae baada ya kubaini anafanya Ngono na afisa Taaluma wa Jiji.
Nimepata binti aliyeishia Darasa la saba. Nipeni uzoefu haya Maisha yatakuaje kwa gepu hilo kubwa la elimu.

Nawasilisha.

sidhani kama unataka kuoa ili uishi na elimu ya huyo mwenza wako cha muhimu ni kutafuta mwenza mtaependana kwa dhati. ila vya kuangalia la 7 au shahada utaishia kuhesabu namba tu mwisho uonekane we ndo mwenye hila

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom