Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,152
Dakika kadhaa zilizopita nilikutana na maajabu hapa mtaani kwetu
Wamekuja wanaojiita maofisa wa kausha damu wako na mjumbe na mwenyekiti wa serikali za mitaa na polisi wawiili wakaingia kwenye nyumba moja ya mdada
Dada akagoma kufungua, wakaenda upande wa chumbani wakaita wakasogeza pazia wakamwona, mjumbe akaomba afungue asiwe na wasiwasi khaaa yaliyofuata yanasikitisha sana
Mdada alienda pembeni na mjumbe na kadhaa wakamsainisha makaraatasi, kilichofuata ni kuita vijana waliokuja nao wakaanza na tv ya 42, wakafuata na makochi meza ya mable sebuleni, wakamaliza sebule nzima wakaona haitoshi mdada analia tu jamani.
Wakaenda chumban kwake wakabeba kitanda, walitaka na godoro mjumbe akazuia, wakazoa kabati la mbao jamani aisee.
Hizi kampuni nani mmiliki na nani anawapa jeuri kama hizi jamani! dada kabaki na vyumba vyake viwili na godoro analia analia analia kama kafiwa na wazazi wote siku moja
Tuwe makini mnaopenda kukopa wapendwa, mikopo ndio mizuri mingine ina laana, mtaua wazazi wenu wakisikia mambo kama haya.
Rip mali za dada yangu.
Wamekuja wanaojiita maofisa wa kausha damu wako na mjumbe na mwenyekiti wa serikali za mitaa na polisi wawiili wakaingia kwenye nyumba moja ya mdada
Dada akagoma kufungua, wakaenda upande wa chumbani wakaita wakasogeza pazia wakamwona, mjumbe akaomba afungue asiwe na wasiwasi khaaa yaliyofuata yanasikitisha sana
Mdada alienda pembeni na mjumbe na kadhaa wakamsainisha makaraatasi, kilichofuata ni kuita vijana waliokuja nao wakaanza na tv ya 42, wakafuata na makochi meza ya mable sebuleni, wakamaliza sebule nzima wakaona haitoshi mdada analia tu jamani.
Wakaenda chumban kwake wakabeba kitanda, walitaka na godoro mjumbe akazuia, wakazoa kabati la mbao jamani aisee.
Hizi kampuni nani mmiliki na nani anawapa jeuri kama hizi jamani! dada kabaki na vyumba vyake viwili na godoro analia analia analia kama kafiwa na wazazi wote siku moja
Tuwe makini mnaopenda kukopa wapendwa, mikopo ndio mizuri mingine ina laana, mtaua wazazi wenu wakisikia mambo kama haya.
Rip mali za dada yangu.