Mikoa ya kuanzia maisha

Mikoa ya kuanzia maisha

mkoa wowote uliopo pembezoni bado kun fulsa nyingi sana kuliko mijini. lakini usiende mikoa kama Kilimanjaro, Arusha, lakini waweza kwenda Manyara kule bado kunaendelea. Mikoa kama ruvuma, Lindi na Mtwara nk. mimi kwa sasa nipo Ruvuma.
 
Mdau kauliza kispoti kwa sababu hapa ni kijiweni, sio kwamba hawezi kulicomplicate swali. Amechochea mjadala tu.
Kimsingi inategemeana na nini umesoma au nini unataka kufanya. Kuna vitu ili ufanikiweinabidi uwe kwenye majiji makubwa kama Dizim, Mwanza, Arusha etc. kwa mfano kama wewe ni advocate unayeanza ukienda Katavi utafulia sana wakati Dizima utapata dili za kuanzia maisha kirahisi. Ukiwa mwalimu au mtumishi wa daraja la kati serikalini ukienda Katavi una uwezekano wa kupanda vyeo kirahisi na kumudu maisha kirahisi. Kwa hiyo mpira ulingoni akili kichwani...
 
Sijaelewa kitu kumoja, umesomea ualimu, Kituo cha kazi unachagua wewe au unapangiwa?
Kama unataka kufanya kitu kingine tofauti na kingine, hicho ndio kitaamua utakifanyia wapi.

Tukikwambia nenda morogoro, ukapangiwa kazi lindi utaacha kwenda kwa sababu tumekushauri hivyo?

Dar, Singida, Morogoro, Mbeya, Mwanza in short mikoa yote kuna watu wameendelea na kuna masikini wa hali ya juu.
Kwa hiyo suala sio mkoa, inaanza na wewe na unataka kufanya nini.
 
what about Dar City? ukiishi chanika ama charambe si kama uko mkoa
 
Habari wanajamii. Mimi ni mhitimu wa chuo kukuu ktk kitivo cha elimu, naomba mnipe ushauri kuhusu mikoa ya Tanzania ambayo mtu anaweza kuanzia kufanya kazi na kufanikiwa kimaisha. Asanteni sana na mungu awabariki, naombeni ushauri wa kunijenga tafadharini sana ndugu zangu!

kumbe ndo mana ulisoma ualimu. We ni kilaza.
 
Mdau kauliza kispoti
kwa sababu hapa ni kijiweni, sio kwamba hawezi kulicomplicate swali.
Amechochea mjadala tu.
Kimsingi inategemeana na nini umesoma au nini unataka kufanya. Kuna vitu
ili ufanikiweinabidi uwe kwenye majiji makubwa kama Dizim, Mwanza,
Arusha etc. kwa mfano kama wewe ni advocate unayeanza ukienda Katavi
utafulia sana wakati Dizima utapata dili za kuanzia maisha kirahisi.
Ukiwa mwalimu au mtumishi wa daraja la kati serikalini ukienda Katavi
una uwezekano wa kupanda vyeo kirahisi na kumudu maisha kirahisi. Kwa
hiyo mpira ulingoni akili kichwani...

Zea yu aRE Sir.,BIG LIKE
 
Kama ni ushauri, nadhani umeishaupata mwingi tu, ila mwisho wa ck wewe ndo mwamuzi na mtekelezaji. Kwa ujumla "Maisha ni popote" Songa mbele wewe ni graduate! :confused2:
 
Seriously?..mhitimu?how can you ask this(no offense)!

Popote pale mtu anaweza kuanzia maisha, inategemeana na
-bidii katika shughuli/kazi yako,
-uchangamkiaji wa Fursa/nafasi mbalimbali(kutosubiri kuambiwa kuna nafasi fulani unaweza fanya kazi hii).
-Upatikanaji wa huduma za kijamii.
-n.k

Nasema hivi kwa sababu unaweza kwenda mikoa idhaniwayo kuwa gharama ya maisha iko chini mf. Mbeya, Singida, mikoa ya Kanda ya ziwa n.k lakini "kubweteka" na kutozingatia vitu kadhaa nilivyotaja juu(pamoja na mengine kukafanya usifanikiwe. na pia mikoa inayoogopwa kwa gharama za kimaisha mf. hapa Dar es salaam, Arusha n.k ukaiogopa lakini kwa kujua utaishie/kuchangamkia fursa zaidi kukaffanya upanue wigo wa kimaisha na kimaendeleo pia.

Swali la msingi ni unataka kujishughulisha na nini, kwa ushauri wangu bidii ya kazi(na hasa kazi zaidi ya moja) matters hapa.
Swali alilouliza Ni la msingi, nisingemshauri aanzie maisha kilimanjaro kama anataka kutoka fasta! Unaweza jikuta unafanyia kazi Kula pekeake! Hata hivyo sidhani kama utakuwa na option ikiwa unafanya kazi ya kuajiriwa!
 
Unaweza kuzungukwa na fursa 100 na usiweze kuzitumia na ukaenda panapodhaniwa hapana fursa na wewe ndio ukawa wa kwanza kuziona na kuzitumia. Maisha popote coz kokote utakapoenda utawakuta watu. La msingi ni juhudi kwa kila unachoamua kufanya.
 
Nenda Kigoma wilaya ya Kasulu pale kuna fursa nyingi kule Kegerankanda, makere, mvugwe na nyamidaho. Pia utaweza kulima kahawa kule heru juu. Pamoja xana mimi ni mkulima wa mahindi na kambaranga kasulu; nina uwezo wa kula vizuri kwa elfu 50 kwa mwezi, maziwa lita 5 sh.1500, ndizi, viazi, maharage nk. Kama hujaajiriwa nenda kalime.
 
Habari wanajamii. Mimi ni mhitimu wa chuo kukuu ktk kitivo cha elimu, naomba mnipe ushauri kuhusu mikoa ya Tanzania ambayo mtu anaweza kuanzia kufanya kazi na kufanikiwa kimaisha. Asanteni sana na mungu awabariki, naombeni ushauri wa kunijenga tafadharini sana ndugu zangu!
chuo kukuu!!!tafadharini???
 
Back
Top Bottom