Hivi MKUU lile kundi la wakimbizi kule Tanga waliopewa uraia wa mafungu lilipewa na CHADEMA na pia wale wakimbizi waliopewa Uraia kule Kigoma nao kumbe ni watu wa Kaskazini!? . Nadhani 2014 siyo mbali sana LETS NOT COUNTS THE CHICKS BEFORE THEY HATCH ..... .
Mtu yeyote akitaka kujua nguvu ya wanamageuzi basi atake kujua nguvu ya ukweli akisha ijua nguvu na asili ya Ukweli ...ataelewa ni kwanini wale wacheza ndombolo wa Bungeni walinywea kabisa na hatukuwaona wakikata mauno baada ya Maazimio ya Bunge .
Na atatambua ni kwanini wale "wabwabwajaji " wameonekana kituko kwa jamii.Kimsingi Dar es Salaam imesinzia kwasababu wengi siyo wote waliopo hapo ni opportunist na hawana jeuri ya kuzungumza kile wanacho kiamini ,kimsingi wengi wanaongozwa na tumbo katika kutafakari na kuamua mambo " VICHWA VYAO VIKO LIKIZO NA VINATUMIKA KAMA SOCKET YA KUSHIKIZIA MACHO,MDOMO,MASIKIO NA PUA.
Changamoto zinazotoka Dar es Salaam kimsingi hazishabahiani na lundo la wasomi waliopo hapo,vyombo vya habari,idadi ya wafanya biashara inashindwa na mikoa kama Kigoma ambako hata maagazeti hayafiki.Kwa maoni yangu ni vigumu sana kwa Dar es Salaam kuwa na muamko hasa kulingana na mfumo wa maisha ambao watu wake wameuweka kwasasa "SELFISHNESS" na ujuaji mwingi kwa kila jambo.
Kimsingi nadhani bado wana mfadhaiko na mhamaniko wa kile kilicho watokea mwaka 1995 ambapo kimsingi walikuwa wameigaragaza kabisa ccm ikabidi zipigwe tiktak na mabo ya mkono wa Mungu kuirudisha CCM Dar es Salaam .Nadhani wapiga kura wengi wa Dar es Salaam wanasumbuliwa na "LYATONGAMONIA" kiasi kwamba hawajiamini tena kama wanaweza kujiletea mabadiliko kupitia sanduku la Kura kwa kuchagua Viongozi kutoka vyama Tofauti.
Jambo Lingine nadhani wanadar es Salaam wanaathiriwa na vitendo vya wale mashujaa wao kugeuka geuka kama kinyonga na kutokuwa na misimamo thabiti mfano Mtikila,Hiza Tambwe,Masumbuko Lamwai,Frank Magoba,Kitwana Kondo, Hiza Tambwe na Kapten wao Augustino lyatonga Mrema hawa kwa kiasi fulani waliifanya Dar ikazizima .Kwasasa tunaona nyota Njema tena Ikiibuka kama akina J.Mnyika,Halima Mdee.
Vilevile kwa maoni yangu ni kwamba kuibuka kwa dhana ya ukabila kumesababisha wapambanaji wengi kutimka Dar es Salaam kurudi kwenye maeneo yao ya Asili ili kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kupitia vyama vya siasa.Hivyo kwa lugha nyingine ni kwamba Dar es Salaam kwa sasa imekuwa Chemichemi ya Maji kwa hiyo hii Bahari ya Mageuzi tunayo iona kwenye sehemu kubwa ya Tanzania ,chanzo chake ni Dar es Salaam...Zitto Kabwe,Freeman Mbowe,Tundu Lisu,Luhaga Mpina,David Kafulila,Hamis Kigwangala kuwataja baadhi tu hawa wengi wako Dar es Salaam .
Kwahiyo watu wa Dar es salaam wanaweza kujitetea kwamba kwa sasa wao ni incubator ya kuzalisha na kuchochea wapambanaji wanao weza kuhimili Tanuri na changamoto za Mageuzi.Hivyo wakati tukiikosoa Dar es Salaam kwa msingi huu ni vema tuipongeze kwa msingi wa pili kama kisima cha Mageuzi.Hata Tanzania tulijitutumua kusaidia nchi mbalimbali kupigania uhuru lakini kwa sasa nchi hizo zimetuacha mbali sana kimaendeleo na kiuwajibika.TUIKOSEA DAR ES SALAAM bila kusahau kuipongeza kwa mazuri yake kwani hata Wabunge wengi wanapochaguliwa hawakai huko bali wanarudi Dar es Salaam.
Ukiwa mfugaji wa Kienyeji wa Kuku na Ukiona Kila asubuhi Kuku wako wakitoka wanakimbilia kwa jirani basi jua siyo kwamba kukuwako ni wastaarabu hawataki kuchafua mazingira yako jua ni kwasababu kule kwa jirani yako kuna uhakika wa chakula.Dar es salaam nina wasiwasi wamejiwekea ka utaratibu wa Demokrasia ya kiuchumi hawa zingatii mageuzi ya kisiasa pekee kwa hili wakazi wa Dar wamepiga bao la Kisigino .