Kuna ngoma afande sele ameimba(,hajarap) kwenye albamu yake ya mkuki moyoni,Majani alifanya vema sana kiukweli, ana midundo mingi sana iliyotoa hit song zaidi ya Mika Mwamba, ila kwa upande wangu Mika Mwamba alikuwa bora na sababu kubwa kwangu ni kwamba jamaa alikuwa anatayarisha midundo ya kizazi kipya pamoja na dance, na kote alifanya vizuri. Majani sijui kama alishawahi kutengeneza beat tofauti na za Bongo Flava mtanikumbusha.
Kwenye chorus anasema,
Nasikitika kunitosa bila kosa mamaaa, ingawa wazi natambua kila lenye mwanzo halikosi mwisho.
Biti ya hii ngoma alifanya majani, ina design flani hivi ya peke yake.
Au lile goma la maralia aliloimba afande sele. Majani alikuwa fundi asee