True, Koffie Annan aliingia kwa gia ya wamarekani lakini alikuwa na uwezo wa kuwaambia mambo hata kama hawakutaka kusikia. Kama ulifuatilia public enquiry - Bratain, kuhusu vita ya Iraq ndio utaona ni jinsi gani wakubwa walipata tabu ku-deal na na Koffie Annan.
Ile issue ya Rwanda, yes, ilikuwa kwenye dawati la Koffie lakini boss wake alikuwa Boutrous. The buck stops with the master hivyo aliweza kuuma uma mdomo na kitu kinamsumbua sana. Boutrous alikuwa na idea zake kuhusu UN ambazo ziliwachefua wamarekani ndio maana hakupata nafasi ya kufanya term ya pili. Koffie alileta some reforms, lakini hasa alikuwa na ideas (creative ideas) ambazo zinatekelezeka na zenye manufaa kwa nchi maskini kama Tanzania.
Kuhusu Mama Migiro, I think mud-slinging ya UN imemkumba no doubt, hivyo ndivyo mashirika haya yalivyo -ni kufa kufaana na mwenzio akiona upungufu wako mahali anaku-fix bila huruma. Nahisi huyu mama hakuzielewa politics za UN au aliona ni bora to keep her distance. Unfortunately, UN bila mtandao utakwenda na maji. West African wanajua sana kuhimili mikikimikiki na kama sisi tunataka kupata nafasi huko inabidi kujifunza mchezo mzima.
Lingine ambalo nadhani linaweza kuwa limedhoofisha chances zake, ni kwamba kama hakuleta idea - a concret idea yenye ku-add value UN basi hapo unakuwa umetoa mwanya wa watu kukufanyia majungu. Kuhudhuria vikao au makongamano na kutoa report sio IDEA. Na bado sijasikia Ban akisema kitu concrete kuhusu huyu mama badala ya genereal statements.
Kwa Tanzania, anaweza kutoa mchango sehemu fulani fulani lakini kwa jinsi tuko kwenye mkorogo wa matatizo sidhani kama anaweza kuwa na nguvu ya kutatua hayo matatizo. Tanzania tuko kwenye transition period na kama hatukupata kiongozi aina ya Kagame, tunaweza kujikuta tuko kama DRC.