Michirizi ya Damu

Michirizi ya Damu

Sikutaka upate Hasara, vipi kama ungekuja kwa gharama zako kisha usingenikuta, maana nilipata dharula ya ghafla leo na kulazimika kuharibu weekend yangu
Sasa hotelin ningekuja kufanya nini eti
 
SEHEMU YA 67

Muda huo ulikuwa zamu ya Mzee Sadiq, alilala na Fareed usiku kucha, haikuishia siku hiyo, huo ulikuwa muda wake wa kuwa na mwanaume tata huyo. Maisha ya Fareed yaliendelea kubadilika, alikaribia kuwa milionea kwa sababu tu alijiuza kwa wanaume matajiri ambao walikuwa tayari kutoa kiasi chochote cha fedha mpaka kufanikisha kile walichokuwa wakikihitaji.

Siku ziliendelea kukatika, waliendelea kuwa pamoja. Japokuwa maisha yalikuwa mazuri, alipata kila kitu alichokuwa akikihitaji lakini hakuacha kuwasiliana na wanaume wengine, wote hao alitaka kulala naye na mwanaume ambaye alikuwa na hamu naye kwa kipindi hicho alikuwa Belleck.

Aliendelea kuwasiliana na mwanaume huyo, hakutaka kuonana naye kwa muda huo, alitaka kumuweka kiporo, alale naye katika siku za mwisho za kutaka kuondoka nchini humo.

Kwa kuwa mwanaume huyo alimuhitaji sana, alijitahidi kumtumia kiasi kikubwa cha fedha, kila shida ambayo Fareed alikuwa akiililia, alitumiwa fedha na mwanaume huyo ingawa hawakuwa wameonana.

Baada ya kukaa na Mzee Sadiq kwa siku kadhaa hatimaye akaamua kuondoka nyumbani kwa mzee huyo na kwenda kuonana na Belleck ambaye alionekana kuwa na kiasi kikubwa cha fedha.

Macho yake yalipotua kwa mwanaume huyo, moyo wake ulimlegea, alikuwa mwanaume mwenye sura nzuri, ya kitoto ambapo mwili wake ulikuwa umejazia kidogo. Alipomuona tu, moyo wake ukatokea kumpenda, alikuwa ana mvuto wa ajabu, zaidi ya wanaume wote ambao aliwahi kukutana nao.

Belleck alivalia suti iliyotengenezwa na Kampuni ya Pollo, alivalia saa nzuri, ya thamani iliyotengenezwa na Kampuni ya Solex, kwa kifupi, muonekano wake ulikuwa ni wa kitajiri.

“Fareed…” aliita Belleck huku akimwangalia mwanaume huyo.
“Nimekuja kukuona mpenzi!” alisema Fareed.

Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kuonana na mwanauume huyo, kilichofuata baada ya hapo ni kula maisha kwa kutembea sehemu mbalimbali. Fareed alijisikia amani moyoni, hakuuacha kumshukuru Mungu kwa kumuumba mwanaume.
 
SEHEMU YA 68

Alijua kwamba kuulikuwa na wanawake wengi waliotamani nafasi kama ile aliyokuwa nayo lakini hakukuwa na yeyote aliywahi kuipata. Alifarijika na muda wote alijiona kuwa mtu mpya, aliyebarikiwa na Mungu, mtu msafi ambaye hata kama angekufa basi angekwenda peponi.

“Nakupenda sana Fareed,” alisema Belleck huku wakiwa kitandani.
“Nakupenda pia!” alijibu Fareed na kumbusu shavuni.
*** Belleck Peter alikuwa miongoni mwa matajiri wakubwa waliokuwa na kampuni nyingi nchini Marekani. Alikuwa miongoni mwa watu waliojitengenezea utajiri mkubwa huku ukiendelea kuongezeka kila siku iliyoitwa leo.

Alikuwa miongoni mwa mabilionea ambao waliheshimika nchini Marekani kutokana na mchango mkubwa aliokuwa akiutoa katika jamii. Utajiri wake wa dola bilioni kumi na tano ulikuwa ukitikisa kila kona. Alikuwa mtu wa watu, bilionea asiyekuwa na sifa, bilionea ambaye siku zote alitaka kuishi katika maisha ya chini kwa ajili ya kuwafanya hata wale masikini kuona wapo sawa naye.

Japokuwa alikuwa na kampuni nyingi lakini nyuma ya pazia utajiri wa mwanaume huyo ulikuwa ukisaidiwa na biashara kubwa ya madawa ya kulevya aliyokuwa akiifanya. Hiyo ilikuwa siri kubwa, aliwaandaa vijana wake ambao walikuwa wakizunguka dunia nzima kwa ajili ya kumfanyia kazi hiyo.

Alijificha kwa kutumia kivuli cha serikali, hakukuwa na mtu aliyehisi kama mwanaume huyo alikuwa akishughulika na biashara hiyo. Alikuwa na vijana wa Kimexico ambao walikuwa na kazi kubwa ya kusambaza mizigo yake Marekani ya Kati na Kusini, alikuwa na vija abarani Afrika ambao nao alikuwa akiwatumia kumsafirishia biashara yake.

Alitisha, utajiri wake uliongezeka. Kwa kuwatumia vijana wake, akawatafuta watu wengine ambao walikuwa na kazi ya kumeza dawa hizo na kuzipeleka sehemu husika. Wanaume wengi waliogopa kumeza kwa kuwa walipata tabu muda wa kutoa madawa hayo chooni kupitia sehemu ya haja ndogo na ndiyo ikawa sababu ya kuwatafuta wanaume waliokuwa wakijihusisha na mapenzi ya jinsi moja.
 
SEHEMU YA 69

Kwenye kutafuta watu hao, aliwapata wengi, aliwatumia, hakutaka kuacha, aliendelea kujificha kwa mwamvuli wa serikali. Kwenye kuendelea kutafuta wanaume hao, ndipo akafanikiwa kumpata Fareed.

Hakumpenda mwanaume huyo, aliamua kuwa naye kwa kuwa alitaka kuona biashara yake ikiendelea kusonga mbele, alitaka kumtumia katika kusafirisha biashara zake kama walivyofanya wenzake.

Alitumia kiasi kikubwa cha fedha kumuhonga lakini alijua kwamba mwisho wa siku angepata kile alichokuwa akikihitaji. Alimuonyeshea mapenzi ya dhati, Fareed hakujua kwamba mwanaume huyo hakuwa tofauti na Keith, aliendelea kumwamini kila siku.

Aliwapanga vijana wake kama kawaida, ilikuwa ni lazima kumtumia mwanaume huyo kusafirisha madawa yake kupeleka nchini Ufaransa na baada ya kufika huko, vijana wake wangempokea na kumlazimisha kuyatoa kisha kumuua.

Hilo halikuwa tatizo, akajipanga kwa ajili ya kufanya kazi hiyo. Kabla ya kumsafirisha ilibidi kwanza amleweshe na kisha kumywesha kete za madawa ya kulevya na kisha kumlazimisha kusafiri kuelekea nchini Ufaransa.

“Ushawahi kunywa Kemikal Boom?” aliuliza Belleck huku akimwangalia mwanaume huyo.
 
Shunie mm nakuaminia sana ..najua utaimaliza!wewe ni jembe!
 
Back
Top Bottom