Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,076
- 463,977
- Thread starter
- #2,601
SEHEMU YA 156
“I don’t know! Everyone wants to get the damn money bro,” (sijui! Kila mmoja anaitaka pesa kaka) alisema jamaa mwingine, walikuwa Wamarekani weusi ambao hata kwa kuwasikia jinsi Kiingereza chao walivyokuwa wakiongea, haikuwa ngumu kugundua kama walikuwa wao.
Wakati Marekani ikiendelea kusumbuka kumtafuta Fareed, katika nchi nyingine, zile zilizokuwa na uadui mkubwa na Marekani walikuwa na furaha mno.
Walifurahi kuona nchi hiyo ikiwa imeshambuliwa na watu kadhaa kuuawa.
Nchini Urusi, mpaka watu wakawa wanashangilia baa, waliwachukia majirani zao hao na muda wowote ule walitamani kuona nchi hiyo ikipotea katika uso wa dunia.
Uarabuni, katika nchi mbalimbali watu walikuwa wakifurahia, kundi la kigaidi la Al Qaida lilijitangaza hadharani kwamba wao ndiyo walikuwa wamewatuma watu kupeleka mabomu na kulipua kituo hicho, kilichowashangaza ni sababu ya mtu wao mmoja kukimbia kwani lengo lilikuwa ni kuwaua wote.
Maelezo hayo kidogo yakawafanya Wamarekani kufikiria mara mbili kwamba inawezekana mwanaume huyo hakuwa na lengo la kuulipua kituo hicho bali alishinikizwa na watu kufanya hivyo.
Walitaka kujua, kama kweli alilipua kituo hicho na kukimbia, ilikuwa ni lazima wamtafute na kumpata ili kujua ni wakina nani walikuwa wamemtuma kushambulia kituo hicho na kwa sababu gani alikuwa akikimbia.
Fareed alichukiwa lakini FBI walikuwa wakimuhitaji kwa nguvu zote. Waliendelea kutangaza dau nono kupatikana kwa mtu huyo lakini ilishindikana ila baada ya siku nne, wakapigiwa simu na kuambiwa kwamba mtu huyo alikuwa katika Hospitali ya Britania Medical Center iliyokuwa hapohapo Pennslyvania hivyo walitakiwa kwenda kumuona huko.
“Hospitali?” aliuliza ofisa mmoja wa FBI.
“Ndiyo! Tumeambiwa yupo huko, hizo ni taarifa za chini, twendeni,” alisema Thomson, mwanaume yuleyule aliyekuwa na jukumu kubwa la kumtafuta Fareed kwa tukio alilokuwa amelifanya.
“I don’t know! Everyone wants to get the damn money bro,” (sijui! Kila mmoja anaitaka pesa kaka) alisema jamaa mwingine, walikuwa Wamarekani weusi ambao hata kwa kuwasikia jinsi Kiingereza chao walivyokuwa wakiongea, haikuwa ngumu kugundua kama walikuwa wao.
Wakati Marekani ikiendelea kusumbuka kumtafuta Fareed, katika nchi nyingine, zile zilizokuwa na uadui mkubwa na Marekani walikuwa na furaha mno.
Walifurahi kuona nchi hiyo ikiwa imeshambuliwa na watu kadhaa kuuawa.
Nchini Urusi, mpaka watu wakawa wanashangilia baa, waliwachukia majirani zao hao na muda wowote ule walitamani kuona nchi hiyo ikipotea katika uso wa dunia.
Uarabuni, katika nchi mbalimbali watu walikuwa wakifurahia, kundi la kigaidi la Al Qaida lilijitangaza hadharani kwamba wao ndiyo walikuwa wamewatuma watu kupeleka mabomu na kulipua kituo hicho, kilichowashangaza ni sababu ya mtu wao mmoja kukimbia kwani lengo lilikuwa ni kuwaua wote.
Maelezo hayo kidogo yakawafanya Wamarekani kufikiria mara mbili kwamba inawezekana mwanaume huyo hakuwa na lengo la kuulipua kituo hicho bali alishinikizwa na watu kufanya hivyo.
Walitaka kujua, kama kweli alilipua kituo hicho na kukimbia, ilikuwa ni lazima wamtafute na kumpata ili kujua ni wakina nani walikuwa wamemtuma kushambulia kituo hicho na kwa sababu gani alikuwa akikimbia.
Fareed alichukiwa lakini FBI walikuwa wakimuhitaji kwa nguvu zote. Waliendelea kutangaza dau nono kupatikana kwa mtu huyo lakini ilishindikana ila baada ya siku nne, wakapigiwa simu na kuambiwa kwamba mtu huyo alikuwa katika Hospitali ya Britania Medical Center iliyokuwa hapohapo Pennslyvania hivyo walitakiwa kwenda kumuona huko.
“Hospitali?” aliuliza ofisa mmoja wa FBI.
“Ndiyo! Tumeambiwa yupo huko, hizo ni taarifa za chini, twendeni,” alisema Thomson, mwanaume yuleyule aliyekuwa na jukumu kubwa la kumtafuta Fareed kwa tukio alilokuwa amelifanya.
