SEHEMU YA 121
Walitumia siku sita nchini Cyprus mpaka kuiacha nchi hiyo na kuelekea nchini Uturuki.
Hakukuwa na umbali mkubwa, ni ndani ya siku saba tu meli ikaanza kuingia katika Bandari ya Akdeniz iliyokuwa katika Jiji la Antalya.
“Tumefika Uturuki! Utakwenda wapi sasa?” aliuliza Mzee Ahmed huku akimwangalia mwanaume huyo.
“Popote pale.”
“Kwa hiyo utaishi hapa?”
“Kwa muda!”
“Halafu?”
“Nataka kuondoka kuelekea Marekani!”
“Unataka kwenda Marekani?”
“Ndiyo!”
“Utafikaje?”
“Kivyovyote vile,” alisema Fareed.
“Hautakiwi kuhisi.
Ngoja nitafute mtu wa kukusaidia,” alisema Mzee Ahmed na kuchukua simu yake na kuwasiliana na mtu mmoja upande wa pili.
Fareed akashukuru Mungu, hakuamini kama angepata urahisi wa kuingia nchini Marekani kama ule aliokuwa amepewa. Alimshukuru Mzee Ahmed kwani alionekana kuwa mwanaume mwema kabisa.
Mara baada ya mzee huyo kumaliza kuzungumza na mtu huyo, akamwambia Fareed asubiri ambapo baada ya saa moja, mwanaume mmoja akafika hapo bandarini ambapo kinyemela akamchukua Fareed na kuondoka naye.
Mzee huyo akajitambulisha kwa jina la Al Fakh. Alikuwa mzee mwenye ndevu nyingi mno, aliongea kitaratibu sana, hakuwa na mapepe, alikuwa mwanaume mstaarabu sana kiasi kwamba wakati mwingine Fareed alihisi kwamba mwanaume huyo alikuwa mtumishi wa Mungu hapo Uturuki.
Walizungumza mambo mengi mno, Fareed alimdanganya mzee huyo kwamba alitaka kwenda nchini Marekani kwa kuwa alikuwa mzamiaji, alitaka kwenda kutafuta maisha nchini humo.
Mzee Al Fakh alifurahi sana, akamwambia kwamba angemsaidia kwa hali na mali pasipo gharama zozote zile.
“Kweli?”
“Ndiyo!”
“Nashukuru sana!”
Wakachukua dakika chache wakafika nyumbani kwa mzee huyo. Ilikuwa nyumba kubwa, yenye walinzi wengi na kila kitu kwa ndani. Wakaingia ndani, akakutana na familia ya mzee huyo ambaye alimkaribishwa kwa furaha tele.
Akapelekwa katika chumba ambacho alitakiwa kukaa kwa siku zote ambazo angesubiri safari ya kwenda nchini Marekani.
Moyo wa Fareed ulikuwa na furaha tele, hakuamini kama kweli alikutana na familia ya watu waliokuwa na upendo mkubwa kama watu hao.
“Jisikie huru!” alisema mzee huyo.....