nimejitahidi mara nyingi kuwa msomaji wa vitabu,kila nikianza nasoma vizuri muda unafika najikuta nakata tamaa ya kuendelea kusoma vitabu,nafikiri maisha ya Watanzania yamejengwa kwenye kutafuta fedha na kuhangaika na maisha,ndiyo msingi haswa tulikojengwa ndiyo maana Tanzania inashindwa kutoa wataalamu wa kushindana kimataifa,Rose Migiro angekuwa amejengwa kwenye msingi wa usomaji vitabu kama Thabo Mbeki bado angekuwa ameshikilia nafasi yake ya Deputy UN Secretary,ni aibu mno kwa taifa letu kuwa na kiongozi kama Kikwete anayeshindwa kuteua mawaziri wenye uwezo wa kuongoza kwa sababu ya kutokusoma vitabu,mageuzi hayawezi kuja japo yanatamaniwa na watanzania walio wengi kwa kuwa hatuna maarifa ya kuyaleta hayo mageuzi,uwezo wetu ni mdogo sana kiasi kwamba tunadharauliwa kimataifa,japo Mwanakijiji umeeleza historia yako kwa kifupi imenifurahisha sana hasa ulipotaja kuwa umetoka Tanga,tulifikiri Tanga wanatoka watu wasiopenda maendeleo katika Elimu,nimependa wazo lako