Kuna mtu aliwahi kunipa stori za maisha yake akiwa na pesa na akiwa hana.
Alinambia kua wakati yeye yuko fiti kiuchumi alikua anawashangaa wanaolalamika kwamba maisha magumu hawana chochote.
Baada ya miaka kadhaa nayeye akafulia, Sasa kwake ilikua ni hatari akawa anajiuliza kwamba hivi hata watu wengine wanaosema maisha magumu, ni kama yangu kweli? Mbona wao wanaishi tu na siku zinaenda ili hali yeye hata hata mia.
Ndicho kilichopo kwa nguruwe FC kwasasa, kipindi sisi tunahaha wao ilikua furaha tele.
Hawakujua kama balaa litawageukia, kwasasa wapowapo tu mbele hapafai nyuma hapafai.
Walikariri mwendo wakasahau kwamba mambo yanabadilikaga.
Mateso yao ya miaka mitatu utadhani muongo mmoja umepita, kumbukeni tu bado msimu ujao tabu ipo palepale ili ngoma iwe droo.
Mnashindwa kushinda kwenye peach kali kama ile ya majaliwa stadium, je kama mngepelekwa kwenye uvuvi wa isamuhyo stadium ingekuaje.
Msimsahau mna kibarua na Azam, au kwasababu mlimfunga kwenye kile kipeyu Zanzibar mnaona ni mwepesi.
#Nabado balaa lipo palepale.