Phillipo Bukililo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 18,488
- 13,608
Rais Mstaafu wa awamu ya pili leo anatimiza miaka 97, ni mingi kwa kuiandika na kuihisi kichwani ukifanya tafakari ya kina. Ni miongo tisa na miaka saba. Amekula magunia kwa magunia ya chumvi. Ni umri mkubwa sana kuendelea kuwepo hai, akiwaona wajukuu na watoto zao. Mzee Mwinyi kwa sisi tuliokuwepo duniani wakati anaingia na kuondoka ikulu ni heshima na baraka kumuona akiwa hai miaka 27 baada ya kuondoka Ikulu.
Wengi watajiuliza ameweza vipi kuishi miaka mingi namna hii. Wapo watakaosema hana makuu kwa maana ya kutoweka visasi moyoni, wapo watakaosema hanywi pombe akiwa ni muumini mzuri wa dini ya kiislam. Na wapo watakaokwenda mbali zaidi kwa kusema amekuwa akijitunza na siku zote akishiriki matembezi ya hiari na yeye mwenyewe kupenda kutembea. Na anayependa kutembea mazoezi ya asubuhi au kukimbia taratibu (jogging) anakwepa maradhi mengi yakiwepo yale ya moyo yenye kuua haraka na pasipo kutarajiwa.
Mzee Mwinyi ameendelea kuwepo wakati wazee wenzake karibu wote wa miaka ile ya awamu ya kwanza na ya pili wakiwa tayari wameshazikwa. Siku ya msiba wa hayati John Magufuli akasoma pasipo miwani!, na akatembea kwenda na kurudi kwenye kiti chake pasipo msaada wa kushikiliwa na mtu yoyote.
Ni kweli wote tunapita juu ya uso wa dunia, lakini kupita kwa baadhi yetu ni kule kwenye baraka. Unaweza kujiuliza inakuwaje Mzee huyu anazidi kusherehekea siku za kuzaliwa kila mwaka wakati wanasiasa vijana tu wakiaga dunia. Vijana waliozaliwa akiwa tayari ni mwanasiasa wanakufa na kumuacha yeye akiendelea kuishi kwa upole bila ya makuu pale kwake mbele kidogo ya Msasani kwa Mwalimu Nyerere.
Hakuwa na makuu, hakutunza hasira wala visasi. Hakutaka kuibadili dunia (To change the world), hakuamini kuwa kila tatizo anaweza yeye kama yeye akalitatua na hivyo kuumiza walio wengi katika mchakato wa utatuzi wa hilo tatizo. Hata baada ya kukejeliwa na Mwalimu Nyerere pale Kilimanjaro Hotel Simba Grill mwezi March mwaka 1995 aliendelea kuwa mkimya mpaka ilipofika siku akaamua kujibu mapigo.
Na baada ya hapo hakutaka kujikweza au kupandisha mabega, ni kama alisamehe na kuendelea kuwa huru moyoni. Hiyo ni sifa anayotakiwa kuwa nayo kiongozi mkuu wa Taifa. Uwezo wa kunyenyekea kwa kuyaona ni madogo tu baadhi ya mambo yanakukwaza na kukukera ukiwa ofisini. Ni mtihani mgumu sana kwa viongozi wenye madaraka makubwa kwa mujibu wa katiba yetu kuweza kujishusha huku wakiwa na vyombo vyote wanavyoweza kuvitumia katika kumuangamiza mtu anayewakera.
Miaka 27 ya kuishi kama mstaafu ni mingi, wengi wakijitahidi sana wataishi miaka mitano au kumi na kuaga dunia. Amewaona wasaidizi wake watatu wakiingia ikulu na kuondoka akiendelea kula raha pale nyumbani kwake. Huyu ni mwanasiasa ambaye maisha yake ni zaidi ya kitabu alichokizindua mwaka jana. Kwamba ukiwa hai huhitaji kujijazia makorokoro mengi kichwani kwako, yataishia kukuumiza na kukumaliza siku usiyoitarajia.
Pia ni somo la ucha Mungu. Kwamba ukimtegemea Mungu siku zote hataweza kukuacha ukatetereka na kuteseka kiafya. Miaka 97 ni zaidi ya ile miaka 70 ya kwenye Biblia kwa miaka 27. Siku zote jione wa kawaida na jione hufai kitu ukiwa umepiga magoti kanisani au msikitini. Ukiwa mdogo utajifunza kujiona sehemu ya wakosaji hata kama bajeti yako ya ulinzi ni mabilioni ya shilingi kwa siku, hata kama unalindwa na mitambo imara na wanajeshi wanaotumia zana za kisasa.
Na ni hapa marais wastaafu waislam wanapokuwa ni waalimu wa uungwana unaoambatana na maisha marefu. Hawaoni sababu ya kumuonea mtu au watu. Hawaoni sababu ya kuwafanya watu wakajiona ni kwanini wamekuja duniani kupata mateso yote haya!. Wanaweza kuitwa dhaifu kwa kuwa ni watu walio 'too liberal', wakiachia uhuru mwingi wa kuongea na kuandika, lakini hiyo ni sehemu muhimu wa utoaji wa haki ambao umeandikwa katika vitabu vitakatifu. Hivyo kuona marais wastaafu wa kiislam wanaendelea kuzeeka huku nyuso zao zikiwa na tabasamu la kirafiki ni bahati inayokwenda pamoja na kuwa sababu ya tulio wengi kujifunza mambo fulani ya kimaisha.
Kheri ya kuzaliwa Mzee Ali Hassan Mwinyi.
Wengi watajiuliza ameweza vipi kuishi miaka mingi namna hii. Wapo watakaosema hana makuu kwa maana ya kutoweka visasi moyoni, wapo watakaosema hanywi pombe akiwa ni muumini mzuri wa dini ya kiislam. Na wapo watakaokwenda mbali zaidi kwa kusema amekuwa akijitunza na siku zote akishiriki matembezi ya hiari na yeye mwenyewe kupenda kutembea. Na anayependa kutembea mazoezi ya asubuhi au kukimbia taratibu (jogging) anakwepa maradhi mengi yakiwepo yale ya moyo yenye kuua haraka na pasipo kutarajiwa.
Mzee Mwinyi ameendelea kuwepo wakati wazee wenzake karibu wote wa miaka ile ya awamu ya kwanza na ya pili wakiwa tayari wameshazikwa. Siku ya msiba wa hayati John Magufuli akasoma pasipo miwani!, na akatembea kwenda na kurudi kwenye kiti chake pasipo msaada wa kushikiliwa na mtu yoyote.
Ni kweli wote tunapita juu ya uso wa dunia, lakini kupita kwa baadhi yetu ni kule kwenye baraka. Unaweza kujiuliza inakuwaje Mzee huyu anazidi kusherehekea siku za kuzaliwa kila mwaka wakati wanasiasa vijana tu wakiaga dunia. Vijana waliozaliwa akiwa tayari ni mwanasiasa wanakufa na kumuacha yeye akiendelea kuishi kwa upole bila ya makuu pale kwake mbele kidogo ya Msasani kwa Mwalimu Nyerere.
Hakuwa na makuu, hakutunza hasira wala visasi. Hakutaka kuibadili dunia (To change the world), hakuamini kuwa kila tatizo anaweza yeye kama yeye akalitatua na hivyo kuumiza walio wengi katika mchakato wa utatuzi wa hilo tatizo. Hata baada ya kukejeliwa na Mwalimu Nyerere pale Kilimanjaro Hotel Simba Grill mwezi March mwaka 1995 aliendelea kuwa mkimya mpaka ilipofika siku akaamua kujibu mapigo.
Na baada ya hapo hakutaka kujikweza au kupandisha mabega, ni kama alisamehe na kuendelea kuwa huru moyoni. Hiyo ni sifa anayotakiwa kuwa nayo kiongozi mkuu wa Taifa. Uwezo wa kunyenyekea kwa kuyaona ni madogo tu baadhi ya mambo yanakukwaza na kukukera ukiwa ofisini. Ni mtihani mgumu sana kwa viongozi wenye madaraka makubwa kwa mujibu wa katiba yetu kuweza kujishusha huku wakiwa na vyombo vyote wanavyoweza kuvitumia katika kumuangamiza mtu anayewakera.
Miaka 27 ya kuishi kama mstaafu ni mingi, wengi wakijitahidi sana wataishi miaka mitano au kumi na kuaga dunia. Amewaona wasaidizi wake watatu wakiingia ikulu na kuondoka akiendelea kula raha pale nyumbani kwake. Huyu ni mwanasiasa ambaye maisha yake ni zaidi ya kitabu alichokizindua mwaka jana. Kwamba ukiwa hai huhitaji kujijazia makorokoro mengi kichwani kwako, yataishia kukuumiza na kukumaliza siku usiyoitarajia.
Pia ni somo la ucha Mungu. Kwamba ukimtegemea Mungu siku zote hataweza kukuacha ukatetereka na kuteseka kiafya. Miaka 97 ni zaidi ya ile miaka 70 ya kwenye Biblia kwa miaka 27. Siku zote jione wa kawaida na jione hufai kitu ukiwa umepiga magoti kanisani au msikitini. Ukiwa mdogo utajifunza kujiona sehemu ya wakosaji hata kama bajeti yako ya ulinzi ni mabilioni ya shilingi kwa siku, hata kama unalindwa na mitambo imara na wanajeshi wanaotumia zana za kisasa.
Na ni hapa marais wastaafu waislam wanapokuwa ni waalimu wa uungwana unaoambatana na maisha marefu. Hawaoni sababu ya kumuonea mtu au watu. Hawaoni sababu ya kuwafanya watu wakajiona ni kwanini wamekuja duniani kupata mateso yote haya!. Wanaweza kuitwa dhaifu kwa kuwa ni watu walio 'too liberal', wakiachia uhuru mwingi wa kuongea na kuandika, lakini hiyo ni sehemu muhimu wa utoaji wa haki ambao umeandikwa katika vitabu vitakatifu. Hivyo kuona marais wastaafu wa kiislam wanaendelea kuzeeka huku nyuso zao zikiwa na tabasamu la kirafiki ni bahati inayokwenda pamoja na kuwa sababu ya tulio wengi kujifunza mambo fulani ya kimaisha.
Kheri ya kuzaliwa Mzee Ali Hassan Mwinyi.