Course Coordinator
JF-Expert Member
- Jul 27, 2019
- 1,682
- 3,065
Maisha haya wamejaa mambo mengi sana hasa ya utafutaji.
Je, umeshawahi kupotezana na ndugu yako wa tumbo moja, binamu yako, Baba Mkubwa au Baba Mdogo, Shangazi, Mama au Baba, Bibi au Babu, Mpwa, rafiki yako au hata jirani yako, Baba Mkwe au Mama Mkwe unawasikia sikia tu wapo mahali fulani lakini kutokana na maisha yetu haya kitanzania umeshindwa kwenda kumtafuta huko mikoani alikokimbilia.
Binafsi baba yetu huwa anatuambia anaye Kaka yake mkubwa ambae aliondoka nyumbani toka mwaka 1957 hadi sasa hajawahi kurudi ila ana watoto kama watano nao aliwaacha wakiwa wadogo. Kati yao watatu wapo Uingereza na wenyewe waliondoka mwaka 1983 na hawajai kurudi tunasikia tu story mmoja yupo Kigoma na mmoja tunamsikiaga tu TBC Taifa ila huyo wa Kigoma ndo huwa anatutembelea.
Sababu za kuondoka nyumbani tunaambiwa ni kutafuta maisha ila tulishafanya kila njia kumtangaza kupata imeshindika tumetumia radio na magazeti hatujwahi kumpata. Mtoto wake huyo anaekaa Kigoma alimsikia Baba yake kuwa yupo Singida akaanza pori kwa pori lakini wapi.
Kuna mtu akamwambia yupo Ruvuma akaanza ardhi kwa ardhi lakini wapi.
Kubwa zaidi aliondoka akiwa hajawahi kupiga hata picha ,huwa tunatamani kumuona huyo dingi lakini imeshindikana.
Hapa ina maana Baba Mdogo wetu huyu hajui hata sura ya ndugu zake, hajawahi kuhudhuria msiba wa Baba yake wala Mama yake.
Wengine huwa tunajisemea bado hai muda mwingine tunajisemea tu huyo alishachukuliwa na mbingu.
Je, una ndugu amewahi kuondoka nyumbani na hajawahi kurudi na kwa nini, sababu za kuondoka nyumbani ni nini?
Njia gani umewahi kutumia ili kumpata?
Je, ni kweli kuwa kuna dawa za kuwarudisha watu waliopotea au kuondoka nyumbani?
Unajisikiaje kusikia ndugu yako kukimbia nyumbani
Je, kuwa mlowezi ni laana?
Je, tutumie chanjo kama iliyompata Osama kwa kutafuta vinasaba?
Je, umeshawahi kupotezana na ndugu yako wa tumbo moja, binamu yako, Baba Mkubwa au Baba Mdogo, Shangazi, Mama au Baba, Bibi au Babu, Mpwa, rafiki yako au hata jirani yako, Baba Mkwe au Mama Mkwe unawasikia sikia tu wapo mahali fulani lakini kutokana na maisha yetu haya kitanzania umeshindwa kwenda kumtafuta huko mikoani alikokimbilia.
Binafsi baba yetu huwa anatuambia anaye Kaka yake mkubwa ambae aliondoka nyumbani toka mwaka 1957 hadi sasa hajawahi kurudi ila ana watoto kama watano nao aliwaacha wakiwa wadogo. Kati yao watatu wapo Uingereza na wenyewe waliondoka mwaka 1983 na hawajai kurudi tunasikia tu story mmoja yupo Kigoma na mmoja tunamsikiaga tu TBC Taifa ila huyo wa Kigoma ndo huwa anatutembelea.
Sababu za kuondoka nyumbani tunaambiwa ni kutafuta maisha ila tulishafanya kila njia kumtangaza kupata imeshindika tumetumia radio na magazeti hatujwahi kumpata. Mtoto wake huyo anaekaa Kigoma alimsikia Baba yake kuwa yupo Singida akaanza pori kwa pori lakini wapi.
Kuna mtu akamwambia yupo Ruvuma akaanza ardhi kwa ardhi lakini wapi.
Kubwa zaidi aliondoka akiwa hajawahi kupiga hata picha ,huwa tunatamani kumuona huyo dingi lakini imeshindikana.
Hapa ina maana Baba Mdogo wetu huyu hajui hata sura ya ndugu zake, hajawahi kuhudhuria msiba wa Baba yake wala Mama yake.
Wengine huwa tunajisemea bado hai muda mwingine tunajisemea tu huyo alishachukuliwa na mbingu.
Je, una ndugu amewahi kuondoka nyumbani na hajawahi kurudi na kwa nini, sababu za kuondoka nyumbani ni nini?
Njia gani umewahi kutumia ili kumpata?
Je, ni kweli kuwa kuna dawa za kuwarudisha watu waliopotea au kuondoka nyumbani?
Unajisikiaje kusikia ndugu yako kukimbia nyumbani
Je, kuwa mlowezi ni laana?
Je, tutumie chanjo kama iliyompata Osama kwa kutafuta vinasaba?