Miaka 61 ya Uhuru: Japo Tumefanikiwa sana kielimu, shule, vyuo na wasomi (Madaktari na Maprofesa kibao), mbona bado adui ujinga yupo? Tunakwama wapi?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,495
113,592
Wanabodi,
Makala ya Jumapili ya leo.
Screen Shot 2022-12-11 at 11.12.50 AM.png
Screen Shot 2022-12-11 at 11.13.09 AM.png

Juzi, Ijumaa, Tanzania tumeadhimisha miaka 61 ya Uhuru wa Tanzania, na kiukweli tumefanikiwa sana katika mambo mengi ya kisisasa, kiuchumi na kijamii, ila pia lazima tukubali, hapa tulipo, sipo mahali tungepaswa tuwe, tulipaswa kuwa mbali zaidi ya hapa tulipo!, hivyo “Kwa Maslahi ya Taifa” ya leo, inatafakari kwa juu juu, tulipaswa kuwa wapi na kujiuliza, jee tunakwama wapi?.

Tulipopata uhuru ile 1961, tulikuwa tunakabiliwa na maadui wakuu watatu wa taifa, hivyo tukatangaza vita dhidi ya adui ujinga, umasikini na maradhi. Leo miaka 61 ya uhuru, sio tuu maadui hao wangalipo, bali tumeongeza maadui wengine wawili, tumeongeza adui rushwa na ufisadi ambao hawakuwepo wakati tunapata uhuru.

Adui Ujinga.
Wakati tunapata uhuru, nchi yetu ilikuwa na majimbo, elimu ilikuwa ni ya kulipia, hivyo ni watoto wa kutoka majimbo yenye mazao ya biashara, yakiongozwa na kahawa, hivyo watu wa Bukoba, Kilimajaro, Arusha na Mbeya, ndio watoto wao walisoma kwasababu wazazi wao waliweza kulipa karo ya shule. Jimbo la Nyanza, lenye mikoa ya kanda ya ziwa, wao walikuwa na Pamba, Tanga wakasomeshwa na Katani. Mikoa isiyokuwa na mazao ya biashara kama Singida, Dodoma, Mikoa ya Kusini na Pwani, wao waliokolewa na kusomeshwa na Waseminari.

Hivyo makabila kama Wahaya, Wachagga na Wanyakyusa wengi kupata fursa za kujiendeleza kielimu na kuonekana kama makabila haya wana akili sana, kutokana na uwezo wa kulipiwa karo.

Rais wa Tanganyika, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, kwa kulijua hili, akatangaza elimu bure, kuanzia darasa la kwanza, hadi chuo kikuu, hii ikafungua fursa za elimu kwa Watanzania wote, na tuliendelea kufanya mitihani inayotungwa Cambridge, Uingereza. Hata baada ya kuanza elimu bure, bado waliopasi wengi mitihani hiyo, bado walikuwa ni watoto wa makabila yale yale.

Tukaachana na mitihani ya wazungu, tukaanzisha Baraza letu la mitihani, tukatunga wenyewe mitihani rafiki, lakini bado waliopasi wengi ni kutoka makabila yale yale!. Ili watu wa makabila yote wapate fursa sawa za kujiendeleza, serikali ya Nyerere ikaamua kuweka viwango tofauti tofauti vya ufaulu kwa baadhi ya mikoa, na kwa mikoa mingine viwango vikashushwa mpaka chini ya alama 50% ili kila Mtanzania aweze kuingia sekondari. Hii ikasaidia saidia watoto wa makabila yote kuingia sekondari.

Kwa yale makabila ya hali ya chini sana kama Wahadzabe na Wataturu, hawa hawakujua shule, hawaongee lugha ya Kiswahili na wanaishi maporini, serikali iliwakamata kwa nguvu watoto wa familia hizo, na kuwapeleka kwa nguvu shule za bweni na kusomeshwa chini ya ulinzi.

Japo wote hawakufaulu hata kiwango cha chini kabisa, bado serikali iliwaingiza sekondari kwa nguvu kwenye shule za bweni, mwanzo ilianza na Ilburu, wenzao wakawa wanawaona na kuwatorosha wote, ndipo serikali ikawapeleka Shule ya Sekondari ya Pugu, hapo walisoma mpaka kidato cha 4, japo wote hawakufaulu, lakini angalau walijua kusoma, kuandika na ustaarabu wa kuvaa nguo.

Serikali ikawarudisha kujiunga na jamaa zao, kwa kuwapa na zawadi za nguo nyingi za kuwavisha jamii nzima, wakawaacha kijijini kwao, baada ya mwezi, wakaenda kuwatembelea kukagua maendeleo yao, walishangaa, sio tuu zile nguo walizikuta pale pale walipowaacha, bali hata nguo za wale waliosomeshwa na kustaarabika, nao walizivua pale pale na kuziacha pale pale, na kuvaa mavazi yao ya asili!.

Juhudi za Awamu ya kwanza kupambana na adui ujinga ziliendelea kwa kuanzisha elimu ya watu wazi, kisomo cha ngumbaru, na kuibadili mitaala ya elimu kuwa na elimu ya kujitegemea na kuanzisha vyuo vya ufundi nchi nzima. Elimu ya mkoloni ililenga kupata makarani, baada ya uhuru tukaanzisha elimu ni kazi, elimu ya kujitegemea, ili lengo la kuelimika sio tuu ili kuajiriwa bali kujiajiri.

Kuna kipindi, nchi ya Tanzania ndio ilikuwa nchi kiongozi barani Afrika kwa literacy level ya watu wanaojua kusoma na kuandika. Hiki kiwango kwa sasa kimeshuka, sijui tunakwama wapi?

Kwa sasa karibu kila kata ina shule ya sekondari, kila mkoa kuna vyuo vya ufundi stadi. Tulipopata uhuru, tulikuwa na chuo kikuu kimoja tuu, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kwa jina maarufu UDSM, na fani ya kwanza ni sheria, sasa tuna vyuo vikuu vingi na fani nyingi, tunatoa wahitimu wengi, tuna maprofesa na madaktari wa Ph.D wa kutosha, kutoka vyuo vikuu vya kuheshimika na kueleweka hadi vyuo vikuu vya mtandaoni, ambayo vinatoa Ph.D hata kwa darasa la saba kama Ph.D ya Mhe. Joseph Kasheku Msukuma.

Na majuzi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kimemtunuku Rais Samia, shahada ya heshima ya udaktari wa Falsafa, iitwayo Honoria Causa, hivyo Rais Samia sasa ni Dr. Samia Suluhu Hassan, japo kikawaida madakitari wa Honoria Causa, hawapaswi kutumia jina la Dr, lakini kwa Tanzania, jina hilo limetumika kwa Dr. Jakaya Kikwete na Dr. Reginald Mengi, hivyo hakuna ubaya jina hilo likitumiwa na Rais Samia, kuwa sasa atambuliwe rasmi kama Rais Dr. Samia Suluhu Hassan, na nashauri lile jina la Mama Samia, sasa life, libaki ofisini kwake, nyumani kwenye familia yake na kwa watu wake wa karibu. Nami nijiunge na Watanzania wenzagu kumpongeza Rais Samia kutunukiwa Ph.D ya heshima, hongera sana Rais wetu Samia kutunukiwa udakitari wa falfasa, ni heshima kubwa kwako na kwa taifa kwa ujumla. Swali hawa ma Ph.D tulionao wa kumwaga, jee wanalisaidiaje taifa letu kusonga mbele?. tunakwama wapi?

Naomba kwa leo niishie hapa, wiki ijayo nitaangazia miaka 61 ya uhuru kwenye mapambano dhidi ya adui umasikini, kiukweli kabisa Watanzania wengi bado ni masikini, jee tunakwama wapi?

Nawatakia heri ya Uhuru na Jamhuri.

Paskali
 
Nilichogundua kwenye makala yako kwa uchache sana

1:Ubora wa elimu itolewayo ni hafifu sana,bora liende


2:Rushwa imetamalaki,maana yake tumeongeza maadui kwenye taifa letu

3: Rais Samia hastahili kuitwa Dr kwa sababu kanuni haziruhusu,japo kuna makosa yamefanyika hapo nyuma
 
Paskali kabla hujauliza wenye PhD wanalisaidiaje taifa kwa elimu yao, jiulize kwanza wewe swali hili..inakuwaje pamoja na elimu yako ya masters bado unadhani ccm inao uwezo kutatua kero za watanzania, je ilikuwa sawa kwa mtu aliyeelimika kama wewe kugombea uongozi kupitia ccm?
 
Kwa bahati mbaya sana wanaoitwa wasomi ndio wamegeuka wajinga kuliko wale ambao hawajaenda shule kabisa! Ukitaka kupima ujinga wa wasomi wetu, fuatilia mambo yanayofanywa na wanasiasa wasomi walioko ndani ya CCM. Utashangaa kuona mtu ana vyeti vya usomi na anajua wapi jina la Dr. litumike, lakini anamwita mama Samia Dr!

Kwa maneno marahisi ni ngumu kutofautisha msomi na mtu ambaye hajaenda shule kabisa. Hii ni dhahiri kuwa tuna majengo ya kutolea elimu, lakini elimu inayotolewa ina ubora hafifu sana.
 
Tena wasomi ndiyo wamekuwa wajinga kuliko wasiosoma........wanaojiita wasomi wengi ndiyo wanasiasa ila angalia wanavyojenga hoja majukwaani au Bungeni ni aibu, Angalia kwenye taasisi za umma nyingi zinajiendesha Kwa hasara wakati zilianzishwa Kwa mafanikio na watu waliokuwa na maono na wala hawakuwa na elimu. Wengi wanadhani kusifia ndiyo uzalendo ila kukosoa ni usaliti........wengi wanaojiita wasomi ni washamba na wachumia tumbo,wanawaza zaidi kunufaika kibinafsi.......wengi ni wajuaji mno........
 
Nimemkumbuka Professor wa Majalalani,Wananchi wengi wa Tanzania wamepumbazwa na Mwasisi wa Taifa,CCM.Waoga,hawajiamini.hawashindani na Mazingira na watu wa kada zao!
Wanapenda kutumia akili kidogo na kupata ridhiki,hawawazi mambo Makubwa na kuandika majina yao yakumbukwe! Wana Maneno mengi bila vitendo na unafiki mwingi.sio wakweli.
 
Wanabodi,
Makala ya Jumapili ya leo.
View attachment 2442731View attachment 2442732
Juzi, Ijumaa, Tanzania tumeadhimisha miaka 61 ya Uhuru wa Tanzania, na kiukweli tumefanikiwa sana katika mambo mengi ya kisisasa, kiuchumi na kijamii, ila pia lazima tukubali, hapa tulipo, sipo mahali tungepaswa tuwe, tulipaswa kuwa mbali zaidi ya hapa tulipo!, hivyo “Kwa Maslahi ya Taifa” ya leo, inatafakari kwa juu juu, tulipaswa kuwa wapi na kujiuliza, jee tunakwama wapi?.

Tulipopata uhuru ile 1961, tulikuwa tunakabiliwa na maadui wakuu watatu wa taifa, hivyo tukatangaza vita dhidi ya adui ujinga, umasikini na maradhi. Leo miaka 61 ya uhuru, sio tuu maadui hao wangalipo, bali tumeongeza maadui wengine wawili, tumeongeza adui rushwa na ufisadi ambao hawakuwepo wakati tunapata uhuru.

Adui Ujinga.
Wakati tunapata uhuru, nchi yetu ilikuwa na majimbo, elimu ilikuwa ni ya kulipia, hivyo ni watoto wa kutoka majimbo yenye mazao ya biashara, yakiongozwa na kahawa, hivyo watu wa Bukoba, Kilimajaro, Arusha na Mbeya, ndio watoto wao walisoma kwasababu wazazi wao waliweza kulipa karo ya shule. Jimbo la Nyanza, lenye mikoa ya kanda ya ziwa, wao walikuwa na Pamba, Tanga wakasomeshwa na Katani. Mikoa isiyokuwa na mazao ya biashara kama Singida, Dodoma, Mikoa ya Kusini na Pwani, wao waliokolewa na kusomeshwa na Waseminari.

Hivyo makabila kama Wahaya, Wachagga na Wanyakyusa wengi kupata fursa za kujiendeleza kielimu na kuonekana kama makabila haya wana akili sana, kutokana na uwezo wa kulipiwa karo.

Rais wa Tanganyika, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, kwa kulijua hili, akatangaza elimu bure, kuanzia darasa la kwanza, hadi chuo kikuu, hii ikafungua fursa za elimu kwa Watanzania wote, na tuliendelea kufanya mitihani inayotungwa Cambridge, Uingereza. Hata baada ya kuanza elimu bure, bado waliopasi wengi mitihani hiyo, bado walikuwa ni watoto wa makabila yale yale.

Tukaachana na mitihani ya wazungu, tukaanzisha Baraza letu la mitihani, tukatunga wenyewe mitihani rafiki, lakini bado waliopasi wengi ni kutoka makabila yale yale!. Ili watu wa makabila yote wapate fursa sawa za kujiendeleza, serikali ya Nyerere ikaamua kuweka viwango tofauti tofauti vya ufaulu kwa baadhi ya mikoa, na kwa mikoa mingine viwango vikashushwa mpaka chini ya alama 50% ili kila Mtanzania aweze kuingia sekondari. Hii ikasaidia saidia watoto wa makabila yote kuingia sekondari.

Kwa yale makabila ya hali ya chini sana kama Wahadzabe na Wataturu, hawa hawakujua shule, hawaongee lugha ya Kiswahili na wanaishi maporini, serikali iliwakamata kwa nguvu watoto wa familia hizo, na kuwapeleka kwa nguvu shule za bweni na kusomeshwa chini ya ulinzi.

Japo wote hawakufaulu hata kiwango cha chini kabisa, bado serikali iliwaingiza sekondari kwa nguvu kwenye shule za bweni, mwanzo ilianza na Ilburu, wenzao wakawa wanawaona na kuwatorosha wote, ndipo serikali ikawapeleka Shule ya Sekondari ya Pugu, hapo walisoma mpaka kidato cha 4, japo wote hawakufaulu, lakini angalau walijua kusoma, kuandika na ustaarabu wa kuvaa nguo.

Serikali ikawarudisha kujiunga na jamaa zao, kwa kuwapa na zawadi za nguo nyingi za kuwavisha jamii nzima, wakawaacha kijijini kwao, baada ya mwezi, wakaenda kuwatembelea kukagua maendeleo yao, walishangaa, sio tuu zile nguo walizikuta pale pale walipowaacha, bali hata nguo za wale waliosomeshwa na kustaarabika, nao walizivua pale pale na kuziacha pale pale, na kuvaa mavazi yao ya asili!.

Juhudi za Awamu ya kwanza kupambana na adui ujinga ziliendelea kwa kuanzisha elimu ya watu wazi, kisomo cha ngumbaru, na kuibadili mitaala ya elimu kuwa na elimu ya kujitegemea na kuanzisha vyuo vya ufundi nchi nzima. Elimu ya mkoloni ililenga kupata makarani, baada ya uhuru tukaanzisha elimu ni kazi, elimu ya kujitegemea, ili lengo la kuelimika sio tuu ili kuajiriwa bali kujiajiri.

Kuna kipindi, nchi ya Tanzania ndio ilikuwa nchi kiongozi barani Afrika kwa literacy level ya watu wanaojua kusoma na kuandika. Hiki kiwango kwa sasa kimeshuka, sijui tunakwama wapi?.

Kwa sasa karibu kila kata ina shule ya sekondari, kila mkoa kuna vyuo vya ufundi stadi. Tulipopata uhuru, tulikuwa na chuo kikuu kimoja tuu, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kwa jina maarufu UDSM, na fani ya kwanza ni sheria, sasa tuna vyuo vikuu vingi na fani nyingi, tunatoa wahitimu wengi, tuna maprofesa na madaktari wa Ph.D wa kutosha, kutoka vyuo vikuu vya kuheshimika na kueleweka hadi vyuo vikuu vya mtandaoni, ambayo vinatoa Ph.D hata kwa darasa la saba kama Ph.D ya Mhe. Joseph Kasheku Msukuma.

Na majuzi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kimemtunuku Rais Samia, shahada ya heshima ya udaktari wa Falsafa, iitwayo Honoria Causa, hivyo Rais Samia sasa ni Dr. Samia Suluhu Hassan, japo kikawaida madakitari wa Honoria Causa, hawapaswi kutumia jina la Dr, lakini kwa Tanzania, jina hilo limetumika kwa Dr. Jakaya Kikwete na Dr. Reginald Mengi, hivyo hakuna ubaya jina hilo likitumiwa na Rais Samia, kuwa sasa atambuliwe rasmi kama Rais Dr. Samia Suluhu Hassan, na nashauri lile jina la Mama Samia, sasa life, libaki ofisini kwake, nyumani kwenye familia yake na kwa watu wake wa karibu. Nami nijiunge na Watanzania wenzagu kumpongeza Rais Samia kutunukiwa Ph.D ya heshima, hongera sana Rais wetu Samia kutunukiwa udakitari wa falfasa, ni heshima kubwa kwako na kwa taifa kwa ujumla. Swali hawa ma Ph.D tulionao wa kumwaga, jee wanalisaidiaje taifa letu kusonga mbele?. tunakwama wapi?.

Naomba kwa leo niishie hapa, wiki ijayo nitaangazia miaka 61 ya uhuru kwenye mapambano dhidi ya adui umasikini, kiukweli kabisa Watanzania wengi bado ni masikini, jee tunakwama wapi?.

Nawatakia heri ya Uhuru na Jamhuri.

Paskali
Tatizo kubwa la watanzania ni kuendekeza njaa waliyonayo. Njaa ya madaraka, njaa ya kufanikiwa haraka, njaa ya kupata upendeleo.
Mwisho wa siku hata namna ya kufikiri inaathiriwa na njaa. Wengi wanabaki kusifia sifia tu hata pasipo stahili
 
Tatizo kubwa la watanzania ni kuendekeza njaa waliyonayo. Njaa ya madaraka, njaa ya kufanikiwa haraka, njaa ya kupata upendeleo.
Mwisho wa siku hata namna ya kufikiri inaathiriwa na njaa. Wengi wanabaki kusifia sifia tu hata pasipo stahili
Ni kweli, lakini hizo njaa zinaletwa na watu kuwa watupu vichwani. Yaani watu wana phd za madesa lakini maarifa na ubunifu hakuna sasa hapo lazima wawe wazandiki na wanafiki.
Taifa lenye watu 61.7M,likiwa na umri wa miaka 61 tangu uhuru. Halina maji, umeme wala haliwezi kujilisha lenyewe huku likiwa na ardhi ambayo almost 75 % ni nzuri kwa kilimo halafu kutwa kucha wanazunguka huko na huko kuomba omba na kutafuta wawekezaji shame on them. Why can't you invest on your own people?. Hao mnao waomba wao nani kawapa?. Taifa hili kwa jinsi lilivyo maskini nadhani hata Mungu anatushangaa sana. Taifa lolote, lisilowajengea uwezo watu wake kuweza kushiriki katika ujenzi wa uchumi wake huwa maskini na watumwa milele. Kazani kuleta wawekezaji uchwara.
 
Kaongezeka adui mwingne now UCHAWA
Wanabodi,
Makala ya Jumapili ya leo.
View attachment 2442731View attachment 2442732
Juzi, Ijumaa, Tanzania tumeadhimisha miaka 61 ya Uhuru wa Tanzania, na kiukweli tumefanikiwa sana katika mambo mengi ya kisisasa, kiuchumi na kijamii, ila pia lazima tukubali, hapa tulipo, sipo mahali tungepaswa tuwe, tulipaswa kuwa mbali zaidi ya hapa tulipo!, hivyo “Kwa Maslahi ya Taifa” ya leo, inatafakari kwa juu juu, tulipaswa kuwa wapi na kujiuliza, jee tunakwama wapi?.

Tulipopata uhuru ile 1961, tulikuwa tunakabiliwa na maadui wakuu watatu wa taifa, hivyo tukatangaza vita dhidi ya adui ujinga, umasikini na maradhi. Leo miaka 61 ya uhuru, sio tuu maadui hao wangalipo, bali tumeongeza maadui wengine wawili, tumeongeza adui rushwa na ufisadi ambao hawakuwepo wakati tunapata uhuru.

Adui Ujinga.
Wakati tunapata uhuru, nchi yetu ilikuwa na majimbo, elimu ilikuwa ni ya kulipia, hivyo ni watoto wa kutoka majimbo yenye mazao ya biashara, yakiongozwa na kahawa, hivyo watu wa Bukoba, Kilimajaro, Arusha na Mbeya, ndio watoto wao walisoma kwasababu wazazi wao waliweza kulipa karo ya shule. Jimbo la Nyanza, lenye mikoa ya kanda ya ziwa, wao walikuwa na Pamba, Tanga wakasomeshwa na Katani. Mikoa isiyokuwa na mazao ya biashara kama Singida, Dodoma, Mikoa ya Kusini na Pwani, wao waliokolewa na kusomeshwa na Waseminari.

Hivyo makabila kama Wahaya, Wachagga na Wanyakyusa wengi kupata fursa za kujiendeleza kielimu na kuonekana kama makabila haya wana akili sana, kutokana na uwezo wa kulipiwa karo.

Rais wa Tanganyika, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, kwa kulijua hili, akatangaza elimu bure, kuanzia darasa la kwanza, hadi chuo kikuu, hii ikafungua fursa za elimu kwa Watanzania wote, na tuliendelea kufanya mitihani inayotungwa Cambridge, Uingereza. Hata baada ya kuanza elimu bure, bado waliopasi wengi mitihani hiyo, bado walikuwa ni watoto wa makabila yale yale.

Tukaachana na mitihani ya wazungu, tukaanzisha Baraza letu la mitihani, tukatunga wenyewe mitihani rafiki, lakini bado waliopasi wengi ni kutoka makabila yale yale!. Ili watu wa makabila yote wapate fursa sawa za kujiendeleza, serikali ya Nyerere ikaamua kuweka viwango tofauti tofauti vya ufaulu kwa baadhi ya mikoa, na kwa mikoa mingine viwango vikashushwa mpaka chini ya alama 50% ili kila Mtanzania aweze kuingia sekondari. Hii ikasaidia saidia watoto wa makabila yote kuingia sekondari.

Kwa yale makabila ya hali ya chini sana kama Wahadzabe na Wataturu, hawa hawakujua shule, hawaongee lugha ya Kiswahili na wanaishi maporini, serikali iliwakamata kwa nguvu watoto wa familia hizo, na kuwapeleka kwa nguvu shule za bweni na kusomeshwa chini ya ulinzi.

Japo wote hawakufaulu hata kiwango cha chini kabisa, bado serikali iliwaingiza sekondari kwa nguvu kwenye shule za bweni, mwanzo ilianza na Ilburu, wenzao wakawa wanawaona na kuwatorosha wote, ndipo serikali ikawapeleka Shule ya Sekondari ya Pugu, hapo walisoma mpaka kidato cha 4, japo wote hawakufaulu, lakini angalau walijua kusoma, kuandika na ustaarabu wa kuvaa nguo.

Serikali ikawarudisha kujiunga na jamaa zao, kwa kuwapa na zawadi za nguo nyingi za kuwavisha jamii nzima, wakawaacha kijijini kwao, baada ya mwezi, wakaenda kuwatembelea kukagua maendeleo yao, walishangaa, sio tuu zile nguo walizikuta pale pale walipowaacha, bali hata nguo za wale waliosomeshwa na kustaarabika, nao walizivua pale pale na kuziacha pale pale, na kuvaa mavazi yao ya asili!.

Juhudi za Awamu ya kwanza kupambana na adui ujinga ziliendelea kwa kuanzisha elimu ya watu wazi, kisomo cha ngumbaru, na kuibadili mitaala ya elimu kuwa na elimu ya kujitegemea na kuanzisha vyuo vya ufundi nchi nzima. Elimu ya mkoloni ililenga kupata makarani, baada ya uhuru tukaanzisha elimu ni kazi, elimu ya kujitegemea, ili lengo la kuelimika sio tuu ili kuajiriwa bali kujiajiri.

Kuna kipindi, nchi ya Tanzania ndio ilikuwa nchi kiongozi barani Afrika kwa literacy level ya watu wanaojua kusoma na kuandika. Hiki kiwango kwa sasa kimeshuka, sijui tunakwama wapi?.

Kwa sasa karibu kila kata ina shule ya sekondari, kila mkoa kuna vyuo vya ufundi stadi. Tulipopata uhuru, tulikuwa na chuo kikuu kimoja tuu, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kwa jina maarufu UDSM, na fani ya kwanza ni sheria, sasa tuna vyuo vikuu vingi na fani nyingi, tunatoa wahitimu wengi, tuna maprofesa na madaktari wa Ph.D wa kutosha, kutoka vyuo vikuu vya kuheshimika na kueleweka hadi vyuo vikuu vya mtandaoni, ambayo vinatoa Ph.D hata kwa darasa la saba kama Ph.D ya Mhe. Joseph Kasheku Msukuma.

Na majuzi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kimemtunuku Rais Samia, shahada ya heshima ya udaktari wa Falsafa, iitwayo Honoria Causa, hivyo Rais Samia sasa ni Dr. Samia Suluhu Hassan, japo kikawaida madakitari wa Honoria Causa, hawapaswi kutumia jina la Dr, lakini kwa Tanzania, jina hilo limetumika kwa Dr. Jakaya Kikwete na Dr. Reginald Mengi, hivyo hakuna ubaya jina hilo likitumiwa na Rais Samia, kuwa sasa atambuliwe rasmi kama Rais Dr. Samia Suluhu Hassan, na nashauri lile jina la Mama Samia, sasa life, libaki ofisini kwake, nyumani kwenye familia yake na kwa watu wake wa karibu. Nami nijiunge na Watanzania wenzagu kumpongeza Rais Samia kutunukiwa Ph.D ya heshima, hongera sana Rais wetu Samia kutunukiwa udakitari wa falfasa, ni heshima kubwa kwako na kwa taifa kwa ujumla. Swali hawa ma Ph.D tulionao wa kumwaga, jee wanalisaidiaje taifa letu kusonga mbele?. tunakwama wapi?.

Naomba kwa leo niishie hapa, wiki ijayo nitaangazia miaka 61 ya uhuru kwenye mapambano dhidi ya adui umasikini, kiukweli kabisa Watanzania wengi bado ni masikini, jee tunakwama wapi?.

Nawatakia heri ya Uhuru na Jamhuri.

Paskali
 
UCHAWA unaangamiza nchi hiii
Tena wasomi ndiyo wamekuwa wajinga kuliko wasiosoma........wanaojiita wasomi wengi ndiyo wanasiasa ila angalia wanavyojenga hoja majukwaani au Bungeni ni aibu, Angalia kwenye taasisi za umma nyingi zinajiendesha Kwa hasara wakati zilianzishwa Kwa mafanikio na watu waliokuwa na maono na wala hawakuwa na elimu. Wengi wanadhani kusifia ndiyo uzalendo ila kukosoa ni usaliti........wengi wanaojiita wasomi ni washamba na wachumia tumbo,wanawaza zaidi kunufaika kibinafsi.......wengi ni wajuaji mno........
 
Back
Top Bottom