Miaka 50: Tumethubutu, Tumeweza na Tunasonga Mbele...

Miaka 50: Tumethubutu, Tumeweza na Tunasonga Mbele...

leo nipo kwenye daladala kuna kijana kavaa shati limeandikwa maneno haya TUMEDHUBUTI ,TUMEWEZA ,NA TUNASONGA MBELE sasa wadau mimi najiulia kama kijana anayejua mateso wanayopata watanzania kw sasa kama wamedhubutu mbona ufisadi upo magamba hawayavui kwa vitendo ,kama wameweza mbona tatizo la umeme lipo kubwa sasa sukari inafanyiwa ufisadi ,kwahiyo wataendelea kutuibia raslimali zetu kama kawaida au kweli wadau inaniuma sana hawafanyi maamuzi magumu kisa kulindana
nawakilisha poleni kwa kusoma muda mrefu
 
Hiyo statement yao inanikera mno....Ni kweli tulithubutu enzi ya Kambarage tulijenga viwanda,tulisomesha watoto wetu(bure),tulikuwa na makampuni ya uchukuzi kila mkoa,tulijenga reli(tazara),usafiri reli ya kati ulikuwepo,nidhamu na uwajibikaji serikalini...baada yake TUMEWEZA kuua kila kitu na sasa TUNASONGA kurudi nyuma...!
 
Kaulimbiu nyingine ni za kukatisha tamaa badala ya kuhamasisha kam hiyo kauli mbiu
 
Inategemea huyo aliyeandika hayo maandishi alikuwa anamaanisha nini. Tukifanya tafsiri sisisi itatusumbua sana.
 
Ni kauli mbiu iloyobiniwa ili kuzima kubezwa kukulikiwa kunashika kasi na wapinzani. Ukichunguza kwa makini utagundua kuwa hata miaka 50 ya uhuru nayo ipo kwa manyiki hiyo hiyo ya kuipa ahueni serikali baada ya kuwa imechafuka kwa ufasadi, umemr n.k
 
ya shule za nyumbani.jpg

naunga mkono hoja

Rufaa_meta.jpg
 
leo nipo kwenye daladala kuna kijana kavaa shati limeandikwa maneno haya tumedhubuti ,tumeweza ,na tunasonga mbele sasa wadau mimi najiulia kama kijana anayejua mateso wanayopata watanzania kw sasa kama wamedhubutu mbona ufisadi upo magamba hawayavui kwa vitendo ,kama wameweza mbona tatizo la umeme lipo kubwa sasa sukari inafanyiwa ufisadi ,kwahiyo wataendelea kutuibia raslimali zetu kama kawaida au kweli wadau inaniuma sana hawafanyi maamuzi magumu kisa kulindana
nawakilisha poleni kwa kusoma muda mrefu

tumethubutu, tumeweza, na tunasonga mbele kudumisha umaskini wa tz
 
Wapenzi wa Jf. Jana tarehe 20 /10/11 nilikuwa naangalia kipindi cha malumbano ya hoja kinachorushwa na kituo cha ITV . Hoja ilikuwa "Utaratibu wa ukusanyaji kodi nchini, Je unakidhi haja katika kuleta maendeleo nchini? Jibu langu mimi ni kuwa haukidhi kwa sababu mifumo takribani yote ya ukusunyaji kodi imetawaliwa na Viongozi wachache ingawa sio wote wanaopenda rushwa, ambayo baadaye ikawa takrima na pengine siku hizi inaitwa 10% hali hii pengine ndio imepelekea Tanzania yetu kuwa na watu wanaosifika kwa ufisadi, Mikataba mibovu ilinayopelekea Tanzania kuingia gharama za kulipa mabilioni ya fedha kwa kushitakiwa mifano tunaijua mwenye macho haambiwi Tazama na mengineyo mengi mtajazia.

Tunasherehekea Miaka 50 ya uhuru wa Tanzania bara kwa kauli mbiu ya
TUMETHUBUTU, TUMEWEZA NA TUNASONGA MBELE ( MIAKA 50 YA UHURU) katika kauli mbiu hii nilijiwa na mawazo ambayo pengine ndio yalinisukuma kushea nanyi ambayo kwangu ni "side effect" ya miaka hamsini kisha nikajiona kama niko katika nchi ya kusadikika au naota ndoto za Kimweri. Kisha nikajiuliza je tunafurahi moja kwa moja au inatubidi tufurahi na kusikitika? Nikajua tunachofurahia ni AMANI ambayo kwa sasa naona kama "Tembo kaanza kuitia Maji" .

Nasema Tembo kaanza kuitia maji kwa sababu wengine wanatumia Amani yetu na kuiona Tanzania ni shamba la bibi, watafanya watakavyo wataiba watakavyo na hakuna atakaye sema maana hatua hazichukuliwi kwa kukosekana au ushahidi wa kutosha au hakuna kifungu kinachoweza kumhukumu huyo mtu au ndiyo hiyo mikataba mibovu kiasi kwamba watu imekuwa ni ukitaka kula kweli lazima uliwe, ukisema pengine utaonekana ni mvunjifu wa amani. Kwa hiyo Watanzania wengi wamekuwa kama wanasemea uvunguni hakuna anayewasikia hatua ni za mwendo wa konokono pengine tutafika tuendako miaka mia ijayo; maana hamsini ndio hii tuanshereheke. Nikianza na


TUMETHUBUTU:

Katika miaka hamsini tumethubutu kweli kuua shirika letu la ndege (ATCL) na kuzidi kuinua uchumi wa nchi za wenzetu kwa kutuma vifurushi na kupanda ndege zao wakati Rwanda kwa kipindi cha miaka 17 toka mauaji ya Kimbari wamethubutu kuwa na Rwandair ambayo kwa sasa inazidi kukita mizizi.
Tumethubutu; pia kuua Reli ya kati, Tazara ikiwa inajikongoja, viwanda vya nguo kama mutex, mwatex, sunguratex, urafiki, kiwanda cha matairi, general tyre, mashirika ya usagaji National Milling, usafirishaji MV Victoria zinayumbayumba, MV bukoba imezikwa, UDA ndiyo hiyo hatusemi, huko liganga ndio mgogoro yaani hata sijui. Nilikuwa nafikiri biashara lazima izae biashara kama sio kupanua lakini sisi biashara ni kuua uchumi na visingizio kibao. Hivi nauli wanazotoa abria huwa zinakwenda wapi? Maana huwezi ukakuta behewa jipya angalau moja limeongezeka kwenye treni wakati huo huo mishara ya wafanyakazi serikali inalipa sielewi.


TUMEWEZA:


Tumeweza kuifanya nchi kuwa na matatizo ya umeme mpaka tulidiriki kuleta ‘management' kutoka Afrika ya kusini kuongoza shirika la umeme hivi uliwaka maana wazawa walionekana ndio chanzo cha matatizo pengine ni sababu ya watu wenye profession zao kuamua wote kuingia kwenye siasa ambako ndiko wanaona kuna ulaji na kuacha kutumia professional zao kuboresha na kuinua uchumi. Matokeo yake bado tunaendelea kulia na tanesco, bandari, madini ambayo pengine miaka mia ijao tutakuwa tumeachiwa mashimo tu. N.k.
Tumeweza kuzipoteza biadhaa ambazo zamani nilikuwa naziona siku hizi sizioni kama mafuta ya Tanbond, sabuni za komoa, kodrai, n.k ambazo kwa kweli zilikuwa na ubora siku hizi tumebaki kushabikia vya wenzetu sanasana ‘made in china' Hivi hawa wenzetu walikuwa na wawekezaji kutoka nje na kama ndio mikataba feki haikuwepo.

Tumeweza kuporomosha kiwango cha elimu hata kufikia wanafunzi kupenda kufaulu bila kujisomea na kufanya kazi ya kuiba mitihani matokeo yake ufahamu hakuna, uelewa mdogo, kiasi kwamba hata wakienda kwenda mashindano kama yale ya Zain challenge wanatoka kappa, sasa hivi kuna mapya "Guinese sport special'" yanahusu mambo ya michezo bado nimeshuhudia Wabongo wakiambulia 'Nil' hivi kumbe ni ushabiki tu ufahamu hakuna hii siyo kuonyesha Watanzania ni mbumbumbu hasha ila maneno mengi vitendo kidogo na sio watu wa kujisomea kuongeza maarifa. Matokeo yake tunapata wataalamu wengi wa mgongo wa chupa ama amefika hapo kwa kununua pepa n.k uchambuzi mdogo kweli tutaepuka kuingizwa' king' kwenye mikataba ambayo ndiyo inabeba maslahi ya nchi?



TUNASONGA MBELE .

Pengine ingekuwa tusonge mbele kwa kujirekebisha mapungufu yetu maana yake tuamke, tuwe na uzalendo na tufanye kazi kwa maana nyingine tuwe na viongozi bora na tusiiachie serikali pekee, kila mmoja awajibike kwa nafasi yake. Tukilalamika bila kuchukua hatua maana yake ndio twasonga mbele na makapi yetu.. Sasa hivi najua tuna mjadala wa katiba ingawa itabidi pia niishukuru katiba yetu pamoja na mapungufu yake lakini imewezesha watu kuachiana madaraka kwa amani na pengine kujivunia amani tuliyonayo mapaka leo maana kwa wenzetu twayaona. Pengine mazuri niyaonayo ni kuingia kwenye mfumo wa Teknolojia ya kisasa ‘digital' miundomibiu ya barabara lakini bado ujenzi usiongitia miundo mbinu! shule nyingi lakini bado hakuna walimu wa kutosha na wenye sifa, Hosipitali nyingi lakini gharama za matibabu hazibebeki, maji sisemi, umeme janga la Taifa, njaa ndio hiyo, bila kuusahau Uwanja wa Taifa tunaojivunia na inabidi tuwe wazalendo kuutunza je ni haya tu ndio tunatumia mabilioni kusherekea miaka hamsini ya uhuru au kuna mengine siyajui!!!!!!

Je wewe yako ni yapi yanayokufurahisha na kukuchukiza na ungependa mabadiliko kwa miaka hamsini ijayo?
 
mkuu Rubi tunashukuru kutuletea mambo ya msingi ili yajadiliwe hapa jamvini badala la ya 'wavamizi' wanoleta hoja za kuendelea kutupumbaza kama ilivyokuwa hiyo miaka 50 iliyopita!
Lakina tunakumbushana tu, tunaleta mada hapa na kutoa njia ya kutekeleza maana watu wanalalamika sana bila matendo na hakuna muda mwingine katika maisha zaidi ya huu tuliopo.
 
Tunakaribia Kusherekia miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika!Na Serikali yetu inajisifu sana kwa mafanikio na kutaka iwea sherehe Kubwa eti Tumeweza na Tunasonga mbele!
Sasa napenda kuhoji Ndani ya miaka 50 ya Uhuru kwaninii:
1)Ni miongoni mwa Nchi Masikini Sana Duniani
2)Rasilimali za Taifa kama madini na vito tumewapa Wazungu na wananufaika wao,wakati kabla ya Uhuru vilikuwa chini yetu ndio sababu ya kusaka uhuru
3)Nyumba serikali kwa ajili ya wafanyakazi wa Serikali viongozi wetu wamegawana
4)Kilimo kimedumaa
5)Huduma ya Afya kwa watanzania ni Duni,madawa na vifaa tiba vijijini hakuna kabisa watu wanalia na kuteseka
6) Elimu kwa Asiyenacho ni Duni kuanzia msingi hadi Sekondarini
7) Rushwa na Ubadhirifu wa Mali ya Umma umeongezeka na Hakuna dalili ya Ufumbuzi
8)Wananchi wananyanyaswa na matajiri wanaoshirikiana na Mapolisi!Tukio la Jana la Dodoma ni Mfano tosha,polisi wametumika kuhalalisha ukatili wa kubomoa nyumba za Watanzania.
9) Viongozi wanadhalilishwa na wanasiasa na wapambe wao (Kitendo alichofanyiwa mkuu wa wilaya wa Igunga Mama Kimario Sikukipenda na sitakiunga mkono) DC wa Enzi ya Mkolono anaulinzi wa Kutosha sasa wanavuliwa nguo na kuburuzwa
10)Gharama za mahitaji ya Msingi kwa Maisha ya kila siku zipo juu kuliko kipato cha Kawaida cha sisi watanzania umasikini unaongezeka!
12)Bajeti ya Taifa Bado Inategemea wahisani,Tangu tunapata uhuru hadi leo!
13) Viwanda hakuna,hadi vijiti va kuchokolea Meno tuna -Import
Sasa ndugu zanguni kwa haya machache nauliza hii miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika Tumesonga mbele au Tumeendelea kurudi nyuma!
Manake hata tunapo analyze mambo tuliosonga mbele na tuangalie pande hasa Idadi ya watu waliokuwepo na Pato la wakati huo,na twende mbali zaidi kwa kuangalia Hazina ya Rasilimali zilizokuwapo udhibiti na matumizi yake enzi hizo na sasa!
 
Hapo namba 13 nimecheka sana, it is too surprising to be true!
bora mimi ninaeishi nyumba ya kuwezekwa na nyasi, siku mgeni anaponitembelea na kumchinjia kuku au nikienda msibani kwa jirani au ndugu au nikialikwa harusini na kula nyama sipati tabu, nanyofoa kinyasi cha kujichokolea kutoka kwenye paa la nyumba yangu wenyewe kiulaini tu lol!!!
 
Mengine Kama Kweli!
Ila Elimu na Kilimo tumeweza,Shule kila Kata na Power Tiler hadi Mashambani!
 
mkuu Rubi tunashukuru kutuletea mambo ya msingi ili yajadiliwe hapa jamvini badala la ya 'wavamizi' wanoleta hoja za kuendelea kutupumbaza kama ilivyokuwa hiyo miaka 50 iliyopita!
Lakina tunakumbushana tu, tunaleta mada hapa na kutoa njia ya kutekeleza maana watu wanalalamika sana bila matendo na hakuna muda mwingine katika maisha zaidi ya huu tuliopo.

Ni kweli ndugu Wakati ukuta, Tutaja taharuki kwenye machimbo tumeachiwa mashimo, kwenye hayo mafuta tunayoanza kuyaota nayo ikawa ni mikataba miaka 100 nyie mnalipwa 3% badala ya kufikiria miaka 50 ijayo mfano tuwe na kiwanda cha kukata, kusafisha na kuyeyusha na kutengeneza vito mbalimbali badala ya kusema miaka mia watu (wawekezaji) wawe tu wanachukua michanga kupeleka kwao kwa ajili ya ku-process sielewe hao wataalamu wetu wanasomea nadharia tu au na vitendo!
 
Kuna memba mmoja amewahi kuleta hoja hapa kuwa kauli mbiu hii ibadilike na iwe: TUMEJARIBU, TUMESHINDWA, TUJIPANGE UPYA. Kuliko hiyo ambayo haina uhalisia!
 
Kuna memba mmoja amewahi kuleta hoja hapa kuwa kauli mbiu hii ibadilike na iwe: TUMEJARIBU, TUMESHINDWA, TUJIPANGE UPYA. Kuliko hiyo ambayo haina uhalisia!


Wanajua ukweli lakini wezoea kusema uongo na hili ndilo linatumaliza
 
Wanajua ukweli lakini wezoea kusema uongo na hili ndilo linatumaliza
Ndio maana ianabidi sasa tuamke maana bila kuamka hiyo Katiba tunayoililia haitakidhi matakwa ya Watanzania bali ya vikundi fulanifulani hasa wenye uchu wa madaraka na si kujenga nchi hatimaye baada ya katiba mpya miaka mitano baadaye nayo itaonekana haifai na ina mapungufu je kila mara tutalilia kubadilii katiba yenye mapungufu? au vision 2020 ni kupaa tu angani na kujenga maghorofa mengi na yasioyokidhi viwango na kuangalia miundo mbinu?
 
Back
Top Bottom