Miaka 50: Tumethubutu, Tumeweza na Tunasonga Mbele...

Miaka 50: Tumethubutu, Tumeweza na Tunasonga Mbele...

Jamani watanganyika wenzangu,hebu tujiulize mbona tunashindwa kuwa wakweli?tANZANIA haijatimiza miaka hamsini bali Tanganyika.Tujaribu kutofautisha Tanganyika na Tanzania.
 
kulikuwa hakuna nchi inayoitwa Tanzania 1961 jina la Tanzania liliundwa mnamo April 1964.



Zanzibar gained independece from Britain on 10 December 1963

znzcopy.jpg
 
Naona kuna upotovu kwenye hili, ninavyotambua na kuamini Tarehe 9 Desemba ni uhuru wa Tanganyika na sio Tanzania kama tuna taka Tanznaia ni tarehe 26/4/2014. Maoni yangu siku hiyo tuwe na bendera ya Tanganyika tu wananchi wabebe bendera hiyo, pili Wazanzibari wasijihusishe sana na siku hiyo HAIWAHUSU zaidi ya kupumzika tu, Kama wabara watakavyopumzika 12/1/2014 wakati wa miaka 50 yao.

Naomba haya yawekwe SAWA vinginevyo naigomea siku hiyo RASMI. Naomba mniunge mkono tusikubali kuburuzwa hivyo.
 
Jifunze kuwa unasoma post zilizopita zitakusaidia kuondokana na kurudia rudia kitu kilichokwisha jadiliwa.
Waliokwisha soma na kuchangia huko nyuma usiwalaumu wakikudharau kwa ku-copy na ku-paste hoja ya mtu na kujifanya yako.

Nimepita, sifikirii kurudi.
 
Mambo yote yaliyopo sasa duniani ni marudio tu,huwezi kuongea kitu leo ukakurupuka kusema eti lilisha ongelewa.Fahamu kuwa hata mtoto anapokua anapaswa kufundishwa mambo yaleyale.Sio lazima kujibu hoja ya mtu kwa vijembe.
 
Kauli mbiu ya maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru imetolewa leo ambayo ni 'Tumethubutu, Tumeweza na Tunasonga mbele'

Je iko relevant na Tanzania ya leo miaka 50 baada ya Uhuru?

Msemo huu 'Tumethubutu, Tumeweza na Tunasonga mbele'
naweza kusema kwamba kwa kiasi fulani wananchi wamejitahidi sana kuwa wavumilivu na "Mkoloni huyu Mwenyeji" Ninasema tunaye mkoloni mwenyeji ambaye haswa namaanisha hawa viongozi wetu ambao hatukuwatarajia kabisa kwamba wangetusaliti kiasi hiki na matokeo yake wamekuwa wabunifu wa "slogans" ili kutuhadaa Watanzania. Nasema hivi kwa sababu zifuatazo
1. Miaka 50 naweza kuthubutu kusema viongozi wenye kupenda RUSHWA na kujilimbikizia utajiri walikuwa ni asilimia 2 tano leo hii viongozi wanaopenda RUSHWA na kujilimbikizia mali ni asilimia 98 tunayaona haya kwa jinsi hali za wananchi wa kawaida ilivyo. Binafsi sioni hata faida ya sherehe za miaka 50 kama si kujidhalilisha tu. Maendeleo ya mtu binafsi tena kiongozi wa serikali ambaye amekula kiapo cha kutoiba mali ya serikali leo anaapa huku akitabasamu mbele ya Rais.
2. Wakandarasi wa miaka 50 iliyopita hawakuyajua mambo ya "Kichina" leo hii barabara inajengwa leo kesho inaanza kukarabatiwa.

Ah kwanza sitaki niendelee kujikumbusha machungu haya. Maana nilitaka kuzungumzia mfumko wa bei. Najisikia vibaya. Kwa heri!!!!
 
Kidumu chama cha mapinduzi na wazee wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam

Kikwete unadhihaki wapiga kura wako, hebu angalia huyo mzee na kofia yako!!!

348oqx3.jpg
 

Attachments

  • mkere.jpg
    mkere.jpg
    39.4 KB · Views: 48
mkuu huyo mzee hajapenda

kuvaa hilo likofia wala hayo maisha

anayoishi bali ni umaskini na

bila kujijua anajikuta amevaa laiti

angejua anateseka kwa ajili ya

huyo aliyekwenye kofia asingevaa
 
Kidumu chama cha mapinduzi na wazee wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam

Kikwete unadhihaki wapiga kura wako, hebu angalia huyo mzee na kofia yako!!!

348oqx3.jpg

- Wamethubutu - Kuiba rasilimali za Watanzania Wanyonge
- Wameweza - Kuiba rasilimali za Watanzania wanyonge kwa miaka 50 sasa
- Wanasonga mbele - Kuendelea kuiba rasilimali ya Watanzania wanyonge kwa miaka mingine 50 ijayo

 
Kweli wamethubutu na wameweza kuwanyonya watanzania.
 
Naona kuna upotovu kwenye hili, ninavyotambua na kuamini Tarehe 9 Desemba ni uhuru wa Tanganyika na sio Tanzania kama tuna taka Tanznaia ni tarehe 26/4/2014. Maoni yangu siku hiyo tuwe na bendera ya Tanganyika tu wananchi wabebe bendera hiyo, pili Wazanzibari wasijihusishe sana na siku hiyo HAIWAHUSU zaidi ya kupumzika tu, Kama wabara watakavyopumzika 12/1/2014 wakati wa miaka 50 yao.

Naomba haya yawekwe SAWA vinginevyo naigomea siku hiyo RASMI. Naomba mniunge mkono tusikubali kuburuzwa hivyo.
Hoja yako itakuwa miaka 50 ya MUUNGANO na sio UHURU..Kifupi sikukuu hii ni ya Watanganyika nadhani umefika mwanzo wa kuitambua Tanganyika kwa madai ya Watanganyika..Hizi kamba za kutokuwa na nchi inaitwa Tanganyika, wakati Zanzibar wameitambua yao kuwa ni nchi, nadhani imefika wakati na sisi wananchi wa bara tukatae na kusema Tanganyika ipo na hai...Karibuni ktk kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika na Wazanzibar watatuunga mkono, nasi tutasherehekea nao siku ya MAPINDUZI ikifika miaka 50...
 
  • Thanks
Reactions: Nzi
- Wamethubutu - Kuiba rasilimali za Watanzania Wanyonge
- Wameweza - Kuiba rasilimali za Watanzania wanyonge kwa miaka 50 sasa
- Wanasonga mbele - Kuendelea kuiba rasilimali ya Watanzania wanyonge kwa miaka mingine 50 ijayo


Hii Propaganda ya CCM ya "Tumethubutu, Tumeweza na Tunasonga mbele" inaniudhi kwelikweli basi tu!!!
 
Kwa wenye uthubutu wa kuitaka Tanganyika yao ktk katiba Mpya, huu ndio wakati wa kuonyesha mapenzi yenu ya kuwa na serikali tatu..
 
Hiyo kaulimbiu ni ya kipumbavu sana.Mtu muelewa mwenye akili huwezi kuishangilia na kuisifia.
 
Kaulimbiu hii ni ya kipumbavu sana.Mtu mwenye akili hawezi kuisifia na kuishangilia wakati nchi hiko katika wakati mgumu wa kutokuwa na adhina .Ofisi hazina pesa za kujiendesha,kama mafuta ya magari,malipo kwa watumishi hata mishahala hawajapata.
 
Ni kauli mbiu nzuri kabisa.Tumethubutu kujitawala na tumeweza. Tumeweza kupunguza umasikini kwa hali ya juu sana na hili nalo tumeweza ingawa jitihada bado zinafanyika maana kutokomeza umasikini ni mchakato na mwisho tunasongambele katika kujiletea maendeleo na hili tumeliona chini ya serikali ya Rais Kikwete kwa kuwekeza sana katika elimu mfano Chuo Kikuu Cha Dodoma, na katika kilimo kwani ni hivi karibuni benki ya wakulima inaanzishwa ukiachilia mbali benki ya wanawake ambayo imekwisha anza kazi.

Hakika tunasonga mbele.


Inasikitisha sana kuona kuwa hata kwenye JF ambapo mtu una akili hata ya japo kuweza kutumia computer na internet, unashindwa kuelewa kuwa Tanzania imetota. Uliza kati ya miaka 50 ni shule gani tumejenga, linganisha shule hizo na alizojenga mkononi, ni barabara gani temejenga, acha za mkoloni tulizokarabati na kurefusha, ni hospitali gani ya maana tumejenga, uwanja wa ndege gani tumejenga, ni bandari gani tumejenga, umesikia aliyosema ofisa mmoja wa Chuo Kikuu cha Dodoma, sasa wanatafuta watu kutoka pakistan, Nigeria etc etc....ina maana hata wakufundisha vyuo Vikuu tumeshindwa kuwa nao.

Huko ndio kuthubutu, kuweza na kusonga mbele? My aaaaaaaaaaaaaahhh.
 
TZ@50

TUMETHUBUTU=KUWA MAFISADI NA KUDHULUMU WANYONGE
TUMEWEZA=Kutengeneza madili kama richmond, IPTL, etc
TUNASONGA MBELE= Giza tororo, masikini kuongezeka, dhuluma zitaduandamana

suluhisho=miaka 50 tulianza kwa nia moja. tukapoteza dira na kujikuta tunaadhimisha miaka 50 pasipo kujua tumefika vipi....sasa ni wakati wa kutengeneza mpango mkakati wa miaka 50 huku tukijeweka malengo ya miaka 10 kujitathmini. vinginevyo naona tukiadhimisha miaka 50 mingine (kwa watakaojaliwa) na habari kama hizi za kuishi gizani, porojo nyingi za kisiasa huku darasa moja likisomewa kama madarasa mawili. TUFIKIRI, TUJIPANGE, TUCHUKUA HATUA!
 
Back
Top Bottom