Miaka 50: Tumethubutu, Tumeweza na Tunasonga Mbele...

Miaka 50: Tumethubutu, Tumeweza na Tunasonga Mbele...

tuna mengi ya kujivunia!Hatujashindwa ila Tunachangamoto!Tusikate Tamaa!
 
TUMETHUBUTI
  • Kupanga miradi mikubwa ya maendeleo yenye kuleta tija kwa wananchi
TUMEWEZA
  • Kutekeleza miradi hiyo mfano:
1. Upanuzi mkubwa wa sekta ya Elimu;
  • shule za msingi zaidi ya 15,000 kuanzia uhuru hadi leo
  • shule za sekondari kutoka chini ya 200 wakati wa uhuru mpaka zaidi ya 4,000 hadi sasa
  • vyuo vikuu kutoka 0 wakati tunapata uhuru mpaka zaidi ya 40 hivi sasa
  • vyuo vya ufundi vya kumwaga
2. upanuzi mkubwa katika sekta ya Afya
  • madaktari kutoka 12 wakati tunapata uhuru mpaka zaidi ya 1500 hivi sasa
  • ujenzi wa zahanati kila kijiji umefikia kiwango kikubwa kwani vimesalia vijiji vichache mno
  • ujenzi wa vituo vya afya kila kata umefanywa pia kwa kiwango cha kuridhisha
  • zaidi ya asilimia 90 ya wilaya zetu zina hospitali za wilalya
  • hospitali za mikoa zaidi ya 18 katika kila mkoa isipokuwa michache tu
  • hospitali za rufaa KCMC, MBEYA, BUGANDO, KIBONG'OTO na Milembe zimeboreshwa
  • Upanuzi mkubwa wa Hospitali ya Taifa ya muhimbili ikijumuisha uwekaji wa vifaa vya kisasa vya upasuaji wa moyo, ubongo na uti wa mgongo pamoja na Kinywa na Meno
  • zaidi ya madaktari bingwa 28 wamepatiwa mafunzo nje ya nchi kwa ajili ya kufanya upasuaji wa moyo
3. Upanuzi mkubwa wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha Lami
  • kuongeza idadi ya ma-Engineer kutoka 2 wakati tunapata uhuru mapka zaidi ya 500 hivi sasa
  • mpaka sasa zaidi km 12,000 za barabara nchini kote zipo katika hatua mbalimbali ya kujengwa kwa kiwango cha Lami
4. Kuboresha kilimo bora nchini
  • maafisa ugani zaidi ya 4000 wameajiliwa na kusambazwa nchi nzima
  • wakulima wanawezeshwa pembejeo, matrekta na mikopo kwa ajili ya kuendeleza kilimo chao
TUNASONGAMBELE
  • kuendeleza mafanikio yaliyopatikana
  • kuendelea kubuni miradi mipya hasa kuimarisha sekta ya uchukuzi, nishati na madini
  • kuiwezesha STAMICO ili isimimamie vyema uchimbaji wa madini nchini
  • Kuiwezesha sekta binafsi ili ijuhusishe kikamilifu katika kukuza uchumi wa nchi yetu kupitia mpango wa PPP
  • Kuhakikisha kuwa ukuaji wa uchumi unaendana sanjali na kupunguza umasikini wa kipato kwa wananchi
MAMBO YOTE HAYO HAMRIDHIKI? MBONA HAMNA SHUKURANI NYIE!
Kweli kabisa mkuu watu wavivu wa kufuatilia na ndiyo maana EL alisema maisha bora hayaji kwa kushinda Vijiweni au Jamvini tuko pamoja sana
 
Tumefanikiwa
kuleta giza,mikataba fake,majengo mengi bila walimu tunayaita shule,kupigania kuilipa dowans,kula pesa za wastaafu wa EAC na kuwapiga mabomu ya machozi,ongezea
 
I am just shocked while counting all the pieces and losses.... fifty years of independency, sherehe since august all over the world while inflation, unemployment, TZS drop, and all the issues we have

as a norm, public accountability is a prime indicator kuonyesha good governance, I am hoping tutapewa honest account kuanzia idara, wizara hadi private avenue (donations, contribution, collateral and in-kinds)

IT IS MY PERSONAL RIGHT TO ASK, QUESTION, PROTEST AND PARTICIPATE IN THE PUBLIC ACCOUNTING QUERRY
 
Hizi sherehe ni mradi mwingine wa watendaji wa serikali...
Kuna haja gani kutumia mabilioni ya hela mbele ya inflation kama hii...
Wanafunzi wamenyimwa mikopo bcoz hela hamna,
Kuna mtu aliyeshika rimoti ya priority hapa bongo. Painfully ni Kikwete.
 
Ni miaka hamsini baada ya sisi wa Tanzania kujipatia Uhuru wetu, kumekua na kaulini mbali mbali kutoka kwa viongozi wetu kuhusu miaka hii, ila kubwa ambalo nataka tulijadili hapa leo ni hili la viongozi wetu kusema "Kuna watu wana kejeli serikali kwa maendeleo ilifikia kwa miaka 50 baada ya Uhuru" hakuna mtu mwenye akili timamu anaeweza kusema hakuna maendeleo yeyote yaliofikiwa kwa miaka 50 ya uhuru wetu, ila raia wanachodai ni kuwa "Laiti tusingekuwa na Rushwa iliyo kithiri, laiti tungeelendelea kuwa na uongozi madhubuti kama wa Mwl. Nyerere, Laiti tusingekua tunaingia kwenye mikataba mibovu ya kuwafaidisha wageni, Laita tungeondoa uzembe kwa watendaji serikalini, tungefikia maendeleo makubwa zaidi ya haya tulio nayo leo." Basi wakati wanasiasa hasa wa CCM mkiambia kuwa si maendeleo tunayostahili kujisifia ndani ya miaka 50, kubalini na tukae tukifikiri ni wapi tulipeleke kwa miaka hamsini ijayo ili ikifika basi watoto wetu wasitumie ma milioni ya shilingi kupiga propaganda ya maendeleo bali wayaone wenyewe, kumbuk awaswahili husema "Kizuru hujiuza na Kibaya hijitembeza"
 
samahani sijaelewan unazungumzia uhuru wa tanganyika au Tanzania ,kwa historia niliyosoma na kusimuliwa Tanzania haijawahi kutawaliwa.ok tuwe wakweli kusema mambo waziwaz bila kificho
 
samahani sijaelewan unazungumzia uhuru wa Tanganyika au Tanzania ,kwa historia niliyosoma na kusimuliwa Tanzania haijawahi kutawaliwa.ok tuwe wakweli kusema mambo waziwaz bila kificho

Hapa ndipo penye tatizo, nashangaa sana kusikia wengi wakisema
eti uhuru wa Tanzania Bara...
 
Nikisikia haya maneno ya "Tusherekee Miaka 50 ya Uhuru", huwa kichwa kinaniuma sana, hadi nameza analgesics!
 
Yes, and the saddest part ni namna ambavyo tumefikia kupiga magoti kiuchumi
 
Una Point MTM..tumejisahau sana, but nani wa kuirekebisha system ilivyo? who is to blame?
Nani wa kuquerry?
Nafikiri inatakiwa hii miaka 50 tuangalie wapi tulijikwaa then tuangalie nini cha kufanya. Nafikiri hizi cellebrations zitatuzindua sana.
 
I am just shocked while counting all the pieces and losses.... fifty years of independency, sherehe since august all over the world while inflation, unemployment, TZS drop, and all the issues we have

as a norm, public accountability is a prime indicator kuonyesha good governance, I am hoping tutapewa honest account kuanzia idara, wizara hadi private avenue (donations, contribution, collateral and in-kinds)

IT IS MY PERSONAL RIGHT TO ASK, QUESTION, PROTEST AND PARTICIPATE IN THE PUBLIC ACCOUNTING QUERRY

Mkuu nakubaliana na hoja yako ila wasiwasi wangu matokeo ya hayo mahesabu kama yataleta jita kwa mwananchi wa kawaida, sababu inayopelekea mimi kusema hivyo tumezoea kuona makosa mengi kwenye mahesabu ya serikali ambayo kila wakati kamati za bunge na AUDITOR General wamekuwa wakitoa lakini hakuna hatua yoyote inayochukuliwa "Business as usual".Hata hili itakuwa hivyo hivyo matumizi ya maonyesho haya yamekuwa makubwa sana bila kuwa na tija yoyote.Maonyesho yanafanyika Dsm na wizara zote zipo Dsm........lakini maonyesho haya yanaonekana ni ya kitaifa na ukweli haya sura ya kitaifa.
 
Taarifa nilizonazo ni kuwa hadi hivi sasa sherehe hizo za mawizara zimeshatumia Sh36 billion
 
Taarifa nilizonazo ni kuwa hadi hivi sasa sherehe hizo za mawizara zimeshatumia Sh36 billion
Mimi naona tusiangalie figures, they are just numbers...tuangalie kama inastahili? Haya maadhimisho yametusaidiaje watanzania?
Kwangu mimi naona yamesaidia sana kucreate awareness..
 
Mimi naona tusiangalie figures, they are just numbers...tuangalie kama inastahili? Haya maadhimisho yametusaidiaje watanzania?
Kwangu mimi naona yamesaidia sana kucreate awareness..

Rejao mbona hueleweki? Maadhimisho yamesaidia awareness ya kitu gani?
 
Rejao mbona hueleweki? Maadhimisho yamesaidia awareness ya kitu gani?

Tanzania ina wizara mbali mbali na kila wizara ina agencies nyingi...ilikuiwa shida sana kuzifahamu kila moja na kazi zake. Maadhimisho yamefanya kufahamika kwake, majukumu yake, mafanikio yake changamoto zilizopo.
Maadhimisho yametufanya tufunguke macho..tunaona kwa 50 yrz, tumeachieve nini?
 
Mimi naona tusiangalie figures, they are just numbers...tuangalie kama inastahili? Haya maadhimisho yametusaidiaje watanzania?
Kwangu mimi naona yamesaidia sana kucreate awareness..

Awareness ya DSM tu? Wizara zote zipo Dsm maonyesho yanafanyika DSM sasa hiyo awareness watu wa tandahimba wanaipataje?
 
Mimi naona tusiangalie figures, they are just numbers...tuangalie kama inastahili? Haya maadhimisho yametusaidiaje watanzania?
Kwangu mimi naona yamesaidia sana kucreate awareness..

Kabla sijakubaliana na wewe kudismiss figures, naomba urejee na kufanya refence kwenye post ya kwanza kabisa kwenye thread hii
 
Una Point MTM..tumejisahau sana, but nani wa kuirekebisha system ilivyo? who is to blame?
Nani wa kuquerry?
Nafikiri inatakiwa hii miaka 50 tuangalie wapi tulijikwaa then tuangalie nini cha kufanya. Nafikiri hizi cellebrations zitatuzindua sana.
?????rejao masaburi yako yanatia aibu ...azima ya ff si hayupo?
 
Back
Top Bottom