TimeOut
JF-Expert Member
- Sep 20, 2022
- 3,897
- 8,333
Msiba usikie nyumba ya jirani mkuu. Hayo maneno yanaumiza kwa wafiwa
Binafsi nina hofu ya Mungu kuna tutusa moja nalo liliharibu kazi ya pesa ndefu na kazi tulikua tunafanya watu wa tatu tu! Aisee mgao ulikua mkubwa sana kwa kipindi hicho kuondoka na laki7 au 1m per dei ilikua ni kawaida kabisa, ikitokea mmekosa kabisa hela hiyo siku ni kama hamjafanya kazi basi ni laki3 au 4, niliamini kuna watu wameumbwa masikini kabisa kutoka rohoni na kila siku nilikua namuhubiria, " ukichimba shimo la uzandiki, usichimbe shimo kubwa kwani hujui atangulia nani! " Alikuja kutangulia yeye baada ya miezi miwili mimi na huyo mwingine tukapewa option ya kuendelea kufanya kazi ila c kama waajiriwa yani tujitegemee
Kuna visa viingi sana, hata hapa nilipo sasa kuna bwana mdogo mbali na kutofuga hata kuku bado hajiwezi hata yeye mwenyewe, na kazini nikama kawekwa tu kwa kujuana juana na undugulism, huku na huku nikaja kudumbukizwa section yake
wakati napambana na hizo habari He
Nikamsukumia jumba hakuamini macho yake
" wewe unashangaza sana yani huyu mtu unae msifia na kumpamba ndio mtu yuleyule alietaka kukuharibia CV alafu wewe unampambania mbona kama ni maajabu na haijawahi tokea mtu kumuongelea dogo hivi unavyo muongelea tangu na tangu ni wewe ndio unanipa habari hii mbali na wewe kufahamu alicho kufanyia, sikutegemea kupata habari zile kukuhusu wewe "
" kwanza kila mtu ana roho yake, pili kila mtu ana maono yake, binafsi sihitaji mtu anione kama ninavyotaka mimi anione au anichukulie kama ninavyotaka mimi, wewe ukiniona nakufaha tunaenda wote kama sikufai pia si lazima twende wote, hata niwe na ufanisi vipi au uwe na uvanisi, pia sirithi adui wa mtu, wewe umeshafanya mambo mengi na kazi nyingi mpaka kufika hapa, na mimi nimesha fanya kazi nyingi na mambo mengi, na pia siishii hapa, na hapa kwako mimi napita tu, ila huyu dogo kwa umri wake na elimu yake sidhani kama kuna mahala popote hapa duniani ambapo amesha wahi fanya kazi zaidi ya hapa, hivyo bado ana vitu vingi vya kujifunza apart na haya anayo endelea nayo, hivyo kwa muda mfupi nilio kaa nae nimemjua vizuri na hata hii tabia yake ni kwasababu anaishi kwa mashaka na hofu, kua baada ya hapa hajui anaenda wapi na itakuaje, pia anahisi kudharaulika muda wote
huyo mzee alistaajabu sana, nikajua yameishia hapo, tukaendelea na bla bla bla zingine, siku kama nne mbele akawa anatuzungukia akiangalia tunafanyaje kazi na tunaelekezana vipi siku ya siku baada ya kumaliza kazi tukawa tuna bla bla bla stoy naye boss akaja akaunga tela kwenye story zilizokua zinaendelea tukizimix na story za kazi, HE!
" alafu wewe kuna taharifa zako nimezipata kutoka kwa huyu mwenzako hapa, ni taharifa njema na mimi nimefurahi kusikia hayo kwa mara ya kwanza, ila kwakua yeye ndio alie sibitisha habari hizo basi kuanzia leo yeye ndio mdhamini wako mpaka atakapo kukabidhi alipo kupendekeza, nawapa miezi 6
dogo mpaka dk hii ni mwezi sasa ana adabu 12 na kanyooka kama rula ya mwalimu wa hesabu