Mhando amkana mkewe mahakamani

Mhando amkana mkewe mahakamani

[
Code:
[QUOTE]USIJIFANYE MJUAJI WA KILA KITU?KWANI WEWE NDIE NJAGU ULIOCHUNUZA SUALA HILI?YAELEKEA UNA MAFRASRESHENI YAKO[[/QUOTE]/CODE]

QUOTE=tpaul;9803541]Aliyekuwa mkurugenzi mkuu wa TANESCO, William Mhando, amemkana mkewe Eva Mhando mahakamani kwa kukataa kwamba Eva sio mke wake. Mkurugenzi huyo amefunguliwa kesi ya ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka na moja ya mashtaka yanayomkabili ni kula njama za kufanya ufisadi akishirikiana na mkewe, Eva, anayedaiwa kupewa zabuni ya mabilioni ya walipakodi kinyemela.

Source: Raia Tanzania.

MAONI YANGU
Naona wakili wa mhando ameamua kufanya hii kesi iwe complicated na kuchukua muda mrefu huku fisadi Mhando akizidi kutafuna fedha za umma alizojichotea. Haya ndio matatizo ya mawakili 'waganga njaa' tuliokuwa nao ktk nchi hii. Mawakili kama hawa hawana hata chembe ya uzalendo.

Mpaka vyeti vya ndoa vije vipatikane ili kuthibitisha uanandoa kati ya Mhando na Eva, kesi itakuwa imemaliza karne kabla ya kuamuliwa. Hivi nchi hii tumerogwa na nani?[/QUOTE][/QUOTE]

Mkuu, rudia kusoma mada kabla hujatoa mchango wako. Tatizo lako umekurupuka kuchangia kabla ya kusoma uzi.
 
Safi sana wakili! Tayari serikali ya magamba imeshalizwa hapo! Ooh mbona wanaishi nyumba moja? Mhando anasema alikuwa mpangaji wangu! Magamba kwishney!!

Hapa ndipo mhando atakapopigia kona na kujichomoa kutoka kwenye kesi hii. Huyu wakili amemfundisha jambo ambalo litamsaidia kuepuka 'kutundikwa msalabani'.
 
...bonge la trick,kwani definition ya ndoa/mke ni nini ? Kama walikuwa wakiishi pamoja kwa zaidi ya miaka miwili tayari ni mke na mume...
Kama hakuna matatizo, Hata mkiishi miaka 20 sheria inawatambua nyie ni mahawara, sheria inakuja kufanya kazi pale anapotokea tatizo ndio wanakaa chini na kuanza kufuatilia. Kama unaishi na mtu ni vizuri kuhalalisha ndio mamlaka halali za serikali zinatambua hiyo ni ndoa halali ila kama ikitokea mmojawapo amekufa ndipo watu wanakaa na kuangalia sheria inasemaje hapa au endapo mmoja akamfukuza mwenzake
 
Iwapo mke atakubali kuwa Mhando sio mume wake issue itàkuwa imekwisha. Waendesha mashtaka hawataleta vyeti, Mhando ataleta cheti cha kuonyesha mke ni mtu mwingine kabisa.

Hata kama Mhando akisema ni bachelor, anayebisha atapata wapi vyeti vya kuithibitishia mahakama kwamba ameoa? Mkuu, hii kesi imeisha mimi nakuambia.
 
Kwi kwii Mke alisemaje pale alipokanwa hadharani mahakamani? Kama Eve naye amekubali/atakubari kirahisi, hiyo ina implication kubwa, baadaye katika mgawanyo wa mali in case of anything. Eve anaweza huko usoni asipate kitu kwenye mali za Mhando kama ataachia hili liende hivi hivi na mahakama iamue kwamba Eve kweli sio Mke wa Mhando. Hii inanikumbusha kesi ya jamaa mmoja aliyefunga ndoa "fake" na mwalimu mmoja kwa kusudi la kumsaidia ahamie shule za mjini. Bahati mbaya yule bwana akafariki, yule mwalimu aliyefunga ndoa "fake" na huyo jamaa akajitokeza baada ya kifo akidai mgawanyo wa mali, kwamba na yeye ni mke halali wa ndoa wa marehemu kwa kuonesha marriage certificate!

mhando na mke wake wamekubaliana , trick ya kesi hii
 
Kuishi pamoja inaweza kuwa na maana pana. Vipi kama hawakuwa wakilala chumba kimoja...


Yaleyaleee!! watasema wanaweza kulala chumba kimoja lakini kuthibitisha kama walikuwa wanalala kitanda kimoja au wana... ni kazi kubwa

Kila kuchapo Tz ni vuta nikuvute
 
Mahakamani unatakiwa ushahidi mzuri usiotia shaka..."kuishi naye kwa miaka kadhaa" unaweza kukuthibitishaje mahakamani? Mahakama wanataka cheti halali cha ndoa (official document)kilichotolewa na mamlaka inayotambulika kisheria. Hapa ndipo penye ugumu. Usidhani kwamba wakili aliyemfundisha kumkana mkewe amekurupuka. Atakuwa amefanya legal analysis ya kutosha akaona kwamba Mhando akijitetea hivyo anaweza kuchomoka kwenye kesi hii. Sio kwamba ninatetea uhuni huu ila kwa mahakama zetu jinsi zilivyo ni vigumu sana kupokea ushahidi wa maneno/kusikia.

Correct mahakamani wanaangalia hoja si mihemko na hisia.
 
tunapopinga Ufisadi ndio mkae mkijua kua siyo zuri watu kila kona ni ufisadi ufisadi tukisema hatutaki intarahamwe ndio maana yake
 
hizi zote ni plani zao hao kuifanya kesi iwe refu - wachina ndio wanajua dawa ya mafisadi - ni Shaba au risasi tu
 
kama sheria hatuzijui tungoje wanaojua waje watufafanulie. Kukana tu mahakamani kwamba huyu si mke wangu hakukuondolei mashtaka mahakamani moja kwa moja. Pia si cheti cha ndoa tu pekee,ndio kidhibitisho mahakamani kwamba flani ni mkeo au mmeo,kuna grounds nyingi sana!.Tusubiri tuone.
 
Ngoja wanasheria waje wadadavue lakini nijuavyo Mimi conflict of interest inaenda hadi kwa ndugu, jamaa na marafiki. Anaweza kukana sio mke wake lakini mahakama ikajiridhisha kuwa ana uhusiano na huyo mwanamke na hivyo ilikuwa kosa kumpatia tends ya kufanya kazi za Tanesco. Kama amezaa naye, kakaa naye nyumba moja, ni rafiki, wanafahamiana nk,,, mote humo maadili yanambana
 
...bonge la trick,kwani definition ya ndoa/mke ni nini ? Kama walikuwa wakiishi pamoja kwa zaidi ya miaka miwili tayari ni mke na mume...

Tambua tofauti kati ya mke na mke halali. Mke halali ni mwenye cheti cha ndoa. Na kama hawakufunga ndoa kisheria kodi zetu zimeliwa hivi.
 
kama sheria hatuzijui tungoje wanaojua waje watufafanulie. Kukana tu mahakamani kwamba huyu si mke wangu hakukuondolei mashtaka mahakamani moja kwa moja. Pia si cheti cha ndoa tu pekee,ndio kidhibitisho mahakamani kwamba flani ni mkeo au mmeo,kuna grounds nyingi sana!.Tusubiri tuone.

Hii siyo ishu. Kama kesi wameiframe kama mke, itakuwa imekula kwao. Labda waifute waanze upya kama ndugu, jamaa etc
 
Hapo ndio watu wa Usalama wanatakiwa kuleta cheti cha ndoa mahakamani just 30 mins baada ya kutamka kuwa sio mkewee
 
Mhando amezusha hoja ya kufikirisha mahakama zetu. Hii hoja itafanya hata kesi ya msingi isahaulike. Na Kama mawakili wa serikali wali frame charges zao kwamba Mhando alimpendelea "MKE" wake kumpatia tenda itakuwa imekula kwao. Na kama hakuna official documents i.e marriage certificates (kwenye ofisi za vizazi na vifo) ndio itakuwa vigumu kabisa ku prove Eva ni mke wa Mhando. Kwasababu serikali itategemea ushahidi wa Mhando na Eva, ambao wao tayari wanakana sio MKE NA MME! Kweli ukishangaa ya Balali, bado ya akina Mhando.
 
Mhando amezusha hoja ya kufikirisha mahakama zetu. Hii hoja itafanya hata kesi ya msingi isahaulike. Na Kama mawakili wa serikali wali frame charges zao kwamba Mhando alimpendelea "MKE" wake kumpatia tenda itakuwa imekula kwao. Na kama hakuna official documents i.e marriage certificates (kwenye ofisi za vizazi na vifo) ndio itakuwa vigumu kabisa ku prove Eva ni mke wa Mhando. Kwasababu serikali itategemea ushahidi wa Mhando na Eva, ambao wao tayari wanakana sio MKE NA MME! Kweli ukishangaa ya Balali, bado ya akina Mhando.

Unaweza kuta hao 'mahakama' ndio wamewafundisha kukanana.
 
Iwapo mke atakubali kuwa Mhando sio mume wake issue itàkuwa imekwisha. Waendesha mashtaka hawataleta vyeti, Mhando ataleta cheti cha kuonyesha mke ni mtu mwingine kabisa.

Na siyo lazima awe na mke.
 
Mhando amezusha hoja ya kufikirisha mahakama zetu. Hii hoja itafanya hata kesi ya msingi isahaulike. Na Kama mawakili wa serikali wali frame charges zao kwamba Mhando alimpendelea "MKE" wake kumpatia tenda itakuwa imekula kwao. Na kama hakuna official documents i.e marriage certificates (kwenye ofisi za vizazi na vifo) ndio itakuwa vigumu kabisa ku prove Eva ni mke wa Mhando. Kwasababu serikali itategemea ushahidi wa Mhando na Eva, ambao wao tayari wanakana sio MKE NA MME! Kweli ukishangaa ya Balali, bado ya akina Mhando.

Huko ofisini ukute files zimeshakuwa "delete delete kabisa"
 
Back
Top Bottom