Mh. Membe atoa kauli nzito Bungeni kuhusu Malawi!

Malawi wanapoteza muda wanaleta usumbufu tu mkutano wa mwaka 1884 uliofanyika Berlin lazima kila nchi iheshimu mipaka iliyowekwa na wakoloni.
Mkuu Ritz, hivi katika sakata hili tunafuata legal instrument gani kuthibitisha mpaka? Mkutano wa Berlin au Heligoland Treaty?
malawi wanafuata Heligoland Treaty ambayo katika moja ya vipengele vyake inasema:
2. To the south by the line that starts on the coast of the northern border of Mozambique Province and follows the course of the Rovuma River to the point where the Messinge flows into the Rovuma. From here the line runs westward on the parallel of latitude to the shore of Lake Nyasa. Turning north, it continues along the eastern, northern, and western shores of the lake until it reaches the northern bank of the mouth of the Songwe River. It then continues up that river to its intersection point with the 33rd degree of east longitude. The line continues along the river until its closest point with the border of the geographical Congo Basin as described in Article I of the Berlin Conference and marked on the map appended to its ninth protocol. From here the line runs directly to the previously described border, follows this to the point of intersection with the 32nd degree of east longitude, turns and continues directly to the meeting point of the northern and southern branches of the Kilambo River. It follows that river until it enters Lake Tanganyika.
Nina wasi wasi kama Tanzania tuna a credible legal basis (document) to back our claims kuwa mpaka upo katikati ya Ziwa
 
Last edited by a moderator:
Waziri Benard Membe ameweka wazi kuhusu mpaka wa Tanzania na kubainisha kuwa mpaka unapita katikati ya ziwa Nyasa!

Na amebainisha kuwa mipaka hiyo iliwekwa kwakipindi hicho nyasa ikiitwa Nyasaland nahivyo wamalawi wamekuwa wakijua Nyasa ni yao na Tanzania inaishia pwani ya ziwa Nyasa!

Na amesema tatizo ni la mda mrefu tangu miaka ya 1960... Na hili tatizo lilishindikana kutatuliwa kwakuwa Kiongozi wa Malawi Kamuzu Banda Kuwa na urafiki na makaburu.. Hivyo Tanzania kwakuwa ilikuwa inaendesha harakati za ukombozi mwa afrika kusini hivyo haikuwa rahisi kwa Tanzania kukaa kitikimoja na Malawi kwakuwa Malawi iliwakumbatia Makaburu.

UPDATE:
Serikali imetoa tamko rasimi kuanzia sasa kuondoka,kuanzia sasa na serikali haitaruhusu utafiti huu kuendele mpaka makubaliano yatakapokuwamepatiwa muafaka....Na serikali iko tayari kulinda mipaka kwa gharama yoyote ile na imeitahadharisha serikali ya malawi kuondoka mara moja na kusitisha shughuli zozote zile za utafiti ndani ya Ziwa Nyasa.


Suluhisho la amani linawezekana. Hata Malawi wanataka hivyo
Malawi says lake row with Tanzania to be resolved amicably | Malawi news, Malawi - NyasaTimes breaking online news source from Malawi
 
dawa ya yao hii


ORD_AIM-120_SLAMRAAM_CLAWS_Launch_from_Hummer_lg.jpg
 
Kuipiga Malawi hakuna hata kuiambia dunia kuwa tuna vita na wamalawi.
Hivi nyie mnaodhani malawi "itapigika kirahisi" mnadhani kinachopigana vita ni ukubwa wa ardhi...au ni watu wakitumia utaalamu pamoja na vifaa!?

Ingekuwa ukubwa wa ardhi ndo kigezo cha kushinda vita basi tz ina uwezo wa kuzishinda nchi nyingi sana za ulaya ikiwemo wingereza!

Tujiulize kwanza, ni kwa nini wamalawi wamejiamini sana!?
 
Lazima Kujua makampuni hayo yanatoka nchi gani..........Yule mama ni darling wa Mabeberu,
Tutafikiri tunazichapa na Malawi kumbe tunazichapa na UK au Canada ....tutapigwaje??
 
Nina wasi wasi na uwezo wa nchi yetu na jeshi letu kwa ujumla!
Maana naona blah blah nyingi je kama bado wanaendelea na utafiti mtafanyaje?maana ata speed boat za kusua sua
Wewe unaijua nchi inayoitwa Tanzania? Brabra zipo uraiani na kwenye majukwaa ya kisiasa siyo JWTZ.
 
Hivi nyie mnaodhani malawi "itapigika kirahisi" mnadhani kinachopigana vita ni ukubwa wa ardhi...au ni watu wakitumia utaalamu pamoja na vifaa!?

Ingekuwa ukubwa wa ardhi ndo kigezo cha kushinda vita basi tz ina uwezo wa kuzishinda nchi nyingi sana za ulaya ikiwemo wingereza!

Tujiulize kwanza, ni kwa nini wamalawi wamejiamini sana!?
Mkeshaji ni muhimu ukazingatia kutulinganisha na wenzetu wa nchi za kiafrika, na hapo utakubaliana nami kwamba kwa upande wa kijeshi tuko vyema sana.
Hao waingereza ama nchi nyingi za bara ulaya na amerika sio size yetu kwani hata rada wametuuzia na kutuchakachua bei.

Kwa uimara wa jeshi letu kwa maana ya wanajeshi wetu na mafunzo wanayoyapata, bado ukweli ni kwamba tunawamudu sana malawi, hawatupi shida sana.

Wamalwi wanaonyesha dalili za kujiamini kama ambavyo hata saddam alionyesha kujiamini mbele ya marekani, kwahiyo kujiamini kwao hakututishi hata kidogo kwani hata sisi tunajiamini.
 
Haka kanchi ni kabaya kwa mambo ya kiuchumi lakini siyo kwenye mambo kugombea mipaka. Kama wamalawi hawakajui, basi waendelee na chokochoko zao. Watafumuliwa na mama yao atakimbilia Afrika Kusini awaache wanalia peke yao.

mkuu tatizo hawatakuwa peke yao, watakuwa na support ya muingereza swali je sisi tutaweza kupigana na muingereza au nasi tutamuomba mchina kuja kutusaidia? au mmarekani?
 
Nani kasema ukiibiwa vitu ndani ya nyumba yako na majambazi unasusa na kuacha kununua chochote nyumbani kwako???

makosa au kasoro zinazilalamikiwa kuwa serikali haijalinda vya kutosha raslimali zetu sio msingi wa kususa ziwa Nyasa na kwaachia wamalawi ni wendawazimu.
Unajua hapa sasa magamba watatumia hii kama mtaji wakisiasa kwa kuiingiza nchi vitani na malawi kwa hapa malawi wamepatikana ole wao wakaidi agizo kalolaiti ya nape itawaishia migongoni.Pia watanzania wenzangu jueni kwamba maisha yatakua magumu na jamaa wa magharibi simnajua wameungana na malawi baada ya kuukubali ushoga nategemea watapewa kila aina ya msaada wa kijeshi na marekani na uingereza na hapo ndipo uraniumu itachimbwa bure kama mafuta kule iraq!Kwa ufupi vita imeanza kati ya Tanzania na Malawi hata kama tutapatana na malawi!
 
Good show!!!!

Uchokozi wa Malawi nauona katika jambo moja tu hata kama ziwa Nyasa ni la kwao na sisi tunasema hapana tuna sehemu yetu ...... Hawana budu kuwa waungwana kumaliza mgogoro mezani hata ikibidi kuitumia jumuia ya kimataifa kuliko kupuuza mazungumzo na kuendeleza miradi ndani ya ziwa.............. Hizi ni dharau hata kwa Rais mnayemuita ni dhaifu hawezi kuvumilia ubinafasi huu.

kama kweli malawi wana ushahidi kwa kutosha kwa nini hawakimbilii kusuluhishwa na jirani yao (Tanzania) wao wanakimbilia kuingiza makampuni ya utafiti wa mafuta ziwani?

Mbona wakivua samaki hamuwakatazi kuendelea na shughuli za uvuvi?
 
Hakuna haja ya kupiga Jaramba kwa sababu ya hisia, swala la kwamba Ziwa Nyasa kuna mafuta ndio linalowatoa viongozi wetu mapovu, kama kweli viongozi wetu wako makini katika kuhakikisha interest za Tanzania hazichezewi, waanze kutuonyesha kwa vitendo kwa kuhakikisha kwamba tunapata a reasonable share kwenye mapato ya madini, waanze kutuonyesha kwa vitendo kwamba viongozi wazembe, wala rushwa na mafisadi wanachukuliwa hatua.

Watanzania tusiwe tayari kutengenezewa maadui wengine wakati serikali hii hii imeshindwa kudhibiti Maralia kwenye makazi yetu badala yake inasubiri misaada kutoka nje.

Kama unataka kupiga Jaramba, anza kupiga Jaramba sasa kama meseji kwa CCM kwamba comes 2015 wasipokuwa tayari kuachia madaraka kwa mujibu wa matakwa ya UMA wa Tanzania basi wajiandae kwa lolote.

Acheni kusumbuana na Poor Malawi, kwanza wanamatatizo yao mengi tu ndio maana wao kupewa hadithi ya mafuta wameona kama vile uchimbaji umeanza. sisi hatuhitaji exploration, it is confirmed kwamba dhahabu, uranium,Tanzanite, Diamond etc zimejaa chini ya ardhi yetu. Kama vipi tupige Jaramba kuyalinda haya kwanza.

hivi wewe ni miongoni wa wamalawi waliolowea huku toka enzi za kanyama chiume nini?
Maana post zako ni za kuponda tu.au uko kwenye kampeni hapa ya kuinflitrate and distabilise?
 

Nina wasi wasi kama Tanzania tuna a credible legal basis (document) to back our claims kuwa mpaka upo katikati ya Ziwa
Tanzania inategemea general international law inayosema kwamba nchi mbili zinazopakana na water body zita-share hiyo body na mpaka utakuwa katikati ya water body husika. Malawi wanajibu wanasema sheria hiyo inatumika kusipokuwa na treaty, hivyo kwa Ziwa Nyasa kwa kuwa kuna hiyo treaty sheria ya kimataifa hai-apply. Sijui Tz tuna argument gani zaidi?
 
kwa hili mkuu wa nchi ache kutabasamu awe makini na afanye maamuzi yenye maslai kwa nchi kwa gharama yoyote ile. akitabasamu na kucheka na kutoa vijembe kama kawaida yake hatuna chetu.
 
Membe si mtu wa kuamini hata kidogo, sakata la wizi wa fedha alisema atatoa taarifa lakini wapi mpaka leo
 
hii ni mikwara mbuzi. mimi nataka kuona vitendo. hatuhitaji kauli za kisiasa katika mambo muhimu yahusio nchi na wananchi. Mwenye kusema hiyo kauli ni Rais au mkuu wa majeshi. je waziri wa mambo ya nje anajeshi? Tunahitaji kusikia mwenye nchi anasema nini. Juzi rais alienda kuzika na akakaa siku kadhaa malawi. je alikuwa na maongezi gani?. mia
 
Hili lingetakiwa kuwa "Jambo la dharura kwa sasa" au "Janga la taifa kwa sasa"...Jeshi liende huko mara moja, hata ikibidi na mimi niuninganishwe katika udharura huu as soon as possible, Nyasa sio Migingo
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom