Mh. Membe atoa kauli nzito Bungeni kuhusu Malawi!

Tangu Lowasa ateuliwe kuwa mwenyekiti wa kamati hii hajawahi kusimama Bungeni kusoma maoni ya kamati hii.
 
by then Watz tulikuwa kuitu kimoja ...we acha tu!
Kwa nini tumefika hapa? Miaka hamsini ya uhuru bado mipaka ya nchi hii ina utata! Kweli Watanzania tunahitaji maelezo toshelevu.Kwa bahati mbaya kama Wamalawi wameshaona dalili za uhakika za uwepo wa mafuta mzozo huu utakuwa mgumu zaidi kutatua.Lakini ninaamini pia Wamalawi wanatujua vizuri sana jinsi tulivya serious katika kulinda mipaka yetu, kama wamesahau wajikumbushe yaliyompata Idd Amin.Wakituchezea tutafika hapo Lilongwe na Blantire kuwasabahi na huyo dada Joyce hatakuwa tena rais.
 
rais wa sasa alikuwa hatuuungi mkono tangu zamani wakati wa ukombozi, alikuwa na bado ni kibaraka wa mabwana wazungu
 
Kwenye maelezo yako hakuna ufafanuzi wowote , bora hata thread za watu wengine humu ndani zina maelezo ya kutosha.
Kama Waziri ndivyo alivyoeleza hivyo, basi hilo ziwa litachukuliwa na Wamalawi, na itabidi tubadili vitabu vyetu vya Jiografia haraka!

Usipende kukurupuka mbona Membe kaeleweka vizuri wewe unataka serikali ifuate mawazo yenu nyie Pro-Chadema msioitakia mema nchi yetu.

Wewe kwa akili yako unataka JWTZ waanze vita ili suala linaitaji mazungumzo mpaka hatua ya vita kufikia mpaka mahakama ya Kimataifa ya Haki (International Court of Justice-ICJ) washindwe.

Malawi wanapoteza muda wanaleta usumbufu tu mkutano wa mwaka 1884 uliofanyika Berlin lazima kila nchi iheshimu mipaka iliyowekwa na wakoloni.
 
hii wizara haina tofauti na takukuru wapo wapo tu sioni faida yake mabalozi wapo huko nje hawatusaidii hebu fikiria wabunge walikuwa wanalia na tbs magari hayakaguliwi kuna kampuni feki zipo nje lakini hakuna balozi ailehusishwa au hata kusema kuna kitu hicho mpaka waliposema bungeni

nasikia kila mara wazenji wanalalamika wanaopewa kazi ni watoto wa wakubwa huku bara
 
Kamati ya kudumu ya Bunge ya Ulinzi, usalama na Mambo ya Nje inatoa maoni yake sasa. Inahangaika zaidi na utendaji wa Membe ingawa haimtaji kwa jina. Imeponda mambo mengi utadhani maoni haya yameandikwa na kambi rasmi ya upinzani!

Acha hizo wewe upinzani ndo huwa wanajadili mtu??
hii ya usalama si ni ya mmmhh waziri mkuu aliyeacha kazi!
 
Nimelisikiliza tamko la waziri inaonekana kama tuliwaachia sana Malawi wafanye watakalo baada ya kelele nyingi serekali inakuja na tamko la kututia upofu waTanzania kwamba serekali iko makini na inajua kichoendelea wakati kila mmoja wetu anajua imewachukua wiki nzima kuandaa tamko !!!!!!!!!!!!!!!!!!.


inaonekana unapenda vita. Tanzania isingetoa tamko wakati mazunguzo yako mezani.

1. Mwalimu Nyerere na Kamuzu banda walikuwa paka na panya wasingeweza kukaa meza moja lakini kila mtu aliamua kulitumia ziwa baada ya kuona hakuna uwezekana na kuzungumza. Nyerere na Banda walikuwa wana ugomvi katika mambo matatu, mosi, mpaka wa ziwa nyasa, Kamuzu Banda (malawi) kuwa na uhusiano wa kibalozi na utawala wa kibaguzi wa Afrika kusini na Banda alimtuhumu Nyerere kwamba anawatumia wakimbizi wa Malawi waliokimbilia Tanzania kutaka kumpindua.

2. Mkapa na Muluzi ndio walioamsha upya mazungumzo baada ya kuonekana kwamba Bakili Muluzi anayo nia ya dhati ya kuzungumza. hadi Muluzi anaondoka madarakani mazungumzo yalikuwa hajaisha.

3. Kikwete ambaye pia alikuwa ni waziri wa mambo ya nje wakati huo alishiriki sana katika mazungumzo hayo na akajaribu kuyaendeleza lakini Rais mpya wa malawi Marehemu Bingu wa Mutahalika alikuwa hatoi ushirikiano wa kutosha kuna tetesi kwamba alikuwa muumini wa wanaoamini kwamba Ziwa Nyasa ni la Malawi.

4. Rais Joyce banda amekuwa madarakani kwa muda mfupi bado haijafahamika msimamo wake kwani makampuni ya kutafuta mafuta (Ya Uingereza) yaliyoko ziwa Nyasa yana chimbuko lake katika utawala wa Mutharika. hata hivyo, wanaojua msimamo wa huyu mama wanasema na yeye ni muumini wa wanaodai ziwa lote ni la Malawi.


Hivyo kauli ya Membe ni sawa kutoka sasa.
 
Ah! Ina maana tuliwagwaya Makaburu! Na baada ya Kaburu kuondolewa serikali ilifanya nini. Jamani "Chelewa chelewa............"
 
Mh. Membe tumekusikia tena umechelewa, hii kauli ingetoka wiki iliyopita. Laiti kama angeitoa AMIRIJESHI MKUU mwenyewe vijana tukaanza kupiga jaramba.

Mimi ningekua na mawasiliano na Malima ningeomba aniazime smg yake nikaitumie kulinda heshima ya nchi yangu.
 
Nimelisikiliza tamko la waziri inaonekana kama tuliwaachia sana Malawi wafanye watakalo baada ya kelele nyingi serekali inakuja na tamko la kututia upofu waTanzania kwamba serekali iko makini na inajua kichoendelea wakati kila mmoja wetu anajua imewachukua wiki nzima kuandaa tamko !!!!!!!!!!!!!!!!!!.
Na wka kuongezea, wakati wa kutoa matamko , kwa suala hili, ulishapita. sasa kinachotakiwa ni vitendo. Hivi kama hayo makampuni yakigoma kuacha hizo shughuli zao, Membe ameonyesha ni jinsi gani tutakabiliana nayo?
 
Usipende kukurupuka mbona Membe kaeleweka vizuri wewe unataka serikali ifuate mawazo yenu nyie Pro-Chadema msioitakia mema nchi yetu.

Wewe kwa akili yako unataka JWTZ waanze vita ili suala linaitaji mazungumzo mpaka hatua ya vita kufikia mpaka mahakama ya Kimataifa ya Haki (International Court of Justice-ICJ) washindwe.

Malawi wanapoteza muda wanaleta usumbufu tu mkutano wa mwaka 1884 uliofanyika Berlin lazima kila nchi iheshimu mipaka iliyowekwa na wakoloni.

Mkuu yaelekea Chadema imekukaa sana akilini, huwezi fanya jambo lolote bila kuitaja.
 
Mh. Membe tumekusikia tena umechelewa, hii kauli ingetoka wiki iliyopita. Laiti kama angeitoa AMIRIJESHI MKUU mwenyewe vijana tukaanza kupiga jaramba.

Hakuna haja ya kupiga Jaramba kwa sababu ya hisia, swala la kwamba Ziwa Nyasa kuna mafuta ndio linalowatoa viongozi wetu mapovu, kama kweli viongozi wetu wako makini katika kuhakikisha interest za Tanzania hazichezewi, waanze kutuonyesha kwa vitendo kwa kuhakikisha kwamba tunapata a reasonable share kwenye mapato ya madini, waanze kutuonyesha kwa vitendo kwamba viongozi wazembe, wala rushwa na mafisadi wanachukuliwa hatua.

Watanzania tusiwe tayari kutengenezewa maadui wengine wakati serikali hii hii imeshindwa kudhibiti Maralia kwenye makazi yetu badala yake inasubiri misaada kutoka nje.

Kama unataka kupiga Jaramba, anza kupiga Jaramba sasa kama meseji kwa CCM kwamba comes 2015 wasipokuwa tayari kuachia madaraka kwa mujibu wa matakwa ya UMA wa Tanzania basi wajiandae kwa lolote.

Acheni kusumbuana na Poor Malawi, kwanza wanamatatizo yao mengi tu ndio maana wao kupewa hadithi ya mafuta wameona kama vile uchimbaji umeanza. sisi hatuhitaji exploration, it is confirmed kwamba dhahabu, uranium,Tanzanite, Diamond etc zimejaa chini ya ardhi yetu. Kama vipi tupige Jaramba kuyalinda haya kwanza.
 
Ah! Ina maana tuliwagwaya Makaburu! Na baada ya Kaburu kuondolewa serikali ilifanya nini. Jamani "Chelewa chelewa............"

Kumbuka moja ya Marais waliotafutwa na Makaburu kuuwawa kwa muda mrefu ni Nyerere kutokana na harakati zake za ukombozi kusini mwa Afrika ikiwemo Afrika kusini.... Tulikuwa tunapokea wakimbilizi wa Afrika kusini hata Nelson Mandela aliwahi kufika nchini wakati wa harakati hizo ( rejea kitabu cha Long work to freedom cha Mandela). makaburu waliitumia sana Malawi kama njia ya kupitia kufika Tanzania na walitaka Nyasa iwe ya Malawi ili waweze kupenya kufika Tanzania.
 
MAMA POROJO sipendi vita ila inaonekana serekali yetu imekuwa na uvumilivu wa kupitiliza inakuwaje ndege zinaruka katika anga la Tanzania zaidi ya mara tano tunaziachia zimefika hadi kutua pwani ya ziwa Nyasa bado tunaangalia ?.Kwanini tusitungue walau ndege moja kuonyesha tuko serious hatuna masikhara linapokuja suala la mipaka ya nchi yetu.Unadhani Malawi wakigundua mafuta au gesi watataka tena mazungumzo Mama POROJO ungekuwa mke wangu pengine ungeeelwa namaanisha nini nakwambia akitokea kidume akakukonyeza vita vinaanzia hapo hapo hakuna cha mazungumzo wala mahakama na suala la ziwa Nyasa nisingekuwa na mazunguzo na malawi kitendo cha kuvuka mpaka kingekuwa sababu tosha ya kuwafunza adabu.

inaonekana unapenda vita. Tanzania isingetoa tamko wakati mazunguzo yako mezani.

1. Mwalimu Nyerere na Kamuzu banda walikuwa paka na panya wasingeweza kukaa meza moja lakini kila mtu aliamua kulitumia ziwa baada ya kuona hakuna uwezekana na kuzungumza. Nyerere na Banda walikuwa wana ugomvi katika mambo matatu, mosi, mpaka wa ziwa nyasa, Kamuzu Banda (malawi) kuwa na uhusiano wa kibalozi na utawala wa kibaguzi wa Afrika kusini na Banda alimtuhumu Nyerere kwamba anawatumia wakimbizi wa Malawi waliokimbilia Tanzania kutaka kumpindua.

2. Mkapa na Muluzi ndio walioamsha upya mazungumzo baada ya kuonekana kwamba Bakili Muluzi anayo nia ya dhati ya kuzungumza. hadi Muluzi anaondoka madarakani mazungumzo yalikuwa hajaisha.

3. Kikwete ambaye pia alikuwa ni waziri wa mambo ya nje wakati huo alishiriki sana katika mazungumzo hayo na akajaribu kuyaendeleza lakini Rais mpya wa malawi Marehemu Bingu wa Mutahalika alikuwa hatoi ushirikiano wa kutosha kuna tetesi kwamba alikuwa muumini wa wanaoamini kwamba Ziwa Nyasa ni la Malawi.

4. Rais Joyce banda amekuwa madarakani kwa muda mfupi bado haijafahamika msimamo wake kwani makampuni ya kutafuta mafuta (Ya Uingereza) yaliyoko ziwa Nyasa yana chimbuko lake katika utawala wa Mutharika. hata hivyo, wanaojua msimamo wa huyu mama wanasema na yeye ni muumini wa wanaodai ziwa lote ni la Malawi.


Hivyo kauli ya Membe ni sawa kutoka sasa.
 
Last edited by a moderator:
Hapa ndo tunaona na kushudia ukiukwaji wa sheria za kimataifa na upofu wa viongozi waew wa Tanzania au Malawi. Naona wachangiaji wengi mnapenda zipigwe lakini hayo yote yana negative impacts kwa nchi hizi mbili. Je Tanzania ikitokea ikadeclare vita dhidi ya Malawi wakati Malawi haijafanya hivyo hamuoni kuwa Tanzania itabeba lawama kati damage,destruction and injuries to the people of Malawi? Na ili ni swala linalo katazwa kwamjibu wa sheria za kimataifa.
Ushauri wangu kama mtanzania nadhani ingekuwa vizuri Tanzania kuishitaki kwa Malawi kama wamekataa dialogue na sisi watanzania.Tunaweza kuepuka ugonvi huu kwa kuitumia vizuri African Union au United Nations au SADC.
 
Back
Top Bottom