Mh. Mbowe aongelea yaliyojiri Ikulu

Sitachoka

JF-Expert Member
Nov 17, 2011
3,030
1,303
Mh. Freeman Mbowe ambae ni mwenyekiti wa chama cha CHADEMA na kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani bungeni, Amesema kuwa pamoja na mambo mengi walioishauri serikali hawana mamlaka ya kumzui Rais kutosai muswada uliopo mezani kwake hivi sasa ila walimtaka atumie kifungu cha (97)2 kutokana na mapungufu mengi katika muswada huo!

Pia serikali aliwaahidi kuyafanyia mabadiliko na mapendekezo yao kwenye kikao kijacho January 31, Aidha Mh. Mbowe anaweka wazi kuwa wakiyafanyia kazi mapendekezo yao hao wako tayari kushiriki katika utungwaji wa katiba mpya na wakiyapuuza hawana namna tena nikurudi kwa waamuzi wakuu wananchi.
 
mkuu mimi cjakunote,yaani unataka mbowe aongee kipi,thread yako ni kama haiko straight.heb sema kipi aongee?
 
Chadema hawana la kufanya kwa sasa inawabidi kuwa wapole tu maana makosa walifanya toka mwanzo... Sasa wakubali kupakatwa tu hawana jinsi.
 
Chadema hawana la kufanya kwa sasa inawabidi kuwa wapole tu maana makosa walifanya toka mwanzo... Sasa wakubali kupakatwa tu hawana jinsi.

Kwani aliyempakata mwenzake hapa ni nani? Kwani ktk ilani ya ccm hawakuwa na mpango wa kubadili katiba ila chadema wamelikomalia wamefanya kuibadili mpaka hapo huoni ccm wamepakatwa kimshazari?
 
Naanza kukosa imani na viongozi wa CDM, Nahisi niwasaliti wa wananchi, Tutaendelea kuishi kwa matumaini Hewa mpaka lini?
Imekuwa ni kawaida ya viongozi wa upinzani wakiingia ikulu wanarudi wamesahau kilichowapeleka, Inaumiza saana,
 
Naanza kukosa imani na viongozi wa CDM, Nahisi niwasaliti wa wananchi, Tutaendelea kuishi kwa matumaini Hewa mpaka lini?
Imekuwa ni kawaida ya viongozi wa upinzani wakiingia ikulu wanarudi wamesahau kilichowapeleka, Inaumiza saana,

asvali na wewe umelinoti hilo mkuu. maalim sefu alipotembelea kwa mia2 tu, kwishney.
akaanza kumhubiri utafikiri yeye ndo tarishi wake.
Napata picha kuwa hata wao wakiingia huko watakuwa kama wao!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

wanaharakati sasa kazi ni kwenu kuiokoa Tz. Mkishindwa nanyi, historia itawahukumu milele.
 
Mtazamo wangu naona CDM wamejitahidi kuwasilisha mapendekezo yao kwa njia nzuri nasi wananchi ni mashahidi. Chamuhimu, wananchi na wale wote watakaopewa dhamana ya kusimamia/kuendesha mchakato wa kutengeneza KATIBA MPYA wasiweke itikadi/matakwa ya upande wowote kwa upendeleo. Maoni ya wananchi/wadau ndiyo yawe msingi wa andiko hilo.
 
Watawala wa Nchı hıı nı kanyagatwende bora lıende sı tu kwa serıkalı balı hata kwenye vyama vya sıasa ndo kınachoendelea sahz.
 
Kwani aliyempakata mwenzake hapa ni nani? Kwani ktk ilani ya ccm hawakuwa na mpango wa kubadili katiba ila chadema wamelikomalia wamefanya kuibadili mpaka hapo huoni ccm wamepakatwa kimshazari?

aliyepakatwa ni chadema, japo CCM hawakuwa na ajenda ya katiba wameona umuhimu wake kutokana na hali ya kisiasa ilivyo kwa sasa nchini.

CCM wamegutuka kuwa kulikuwa kuna uwezekano ya wao kundolewa kwenye uongozi wa nchi hii na sasa wamejipa nguvu ya kuendelea kuingoza nchi hii kwa kujitengenezea katiba yao itakayo linda maslahi yao.

Chadema walikuja na hoja za maana sana ila walishindwa kuzisimamia na sasa hawana jinsi tena zaidi ya kuungana na magamba kuwasaidia kuunda katiba itakayo wasaidia magamba kutawala milele, uko ndiko kupakatwa kwao.
 
Naanza kukosa imani na viongozi wa CDM, Nahisi niwasaliti wa wananchi, Tutaendelea kuishi kwa matumaini Hewa mpaka lini?
Imekuwa ni kawaida ya viongozi wa upinzani wakiingia ikulu wanarudi wamesahau kilichowapeleka, Inaumiza saana,

Ni kweli kabisa hawa watu wametusaliti wananchi tulikuwa na imani nao sana ila kwa swala ili wametuangusha sana na hatuna imani nao tena.
 
Sidhani kama habari hii inaleta utofauti wowote given what we already know...

Ingeleta utofauti only kama kungekuwa na taarifa mpya ya yale yaliyoyojiri kunako kikao...

Otherwise nadhani ni muendelezo ule ule wa kujaribu kuwaelewesha wananchi kuwa issue imerudi bungeni.

Tofauti ni kwamba maybe sasa CDM watawaeleza wabunge wa ccm kuwa "Rais kasema mkubaliane na sisi kuhusiana na mapendekezo yetu"
 
Kwani aliyempakata mwenzake hapa ni nani? Kwani ktk ilani ya ccm hawakuwa na mpango wa kubadili katiba ila chadema wamelikomalia wamefanya kuibadili mpaka hapo huoni ccm wamepakatwa kimshazari?

Ni kweli lakini nimecheka sana.. Kimshazari!!!!!!!z!z!z
 
Mlitegemea jipya kwani, tushikamane jamani tujenge taifa, je tufanye nini ili tujikite kwenye kufanya kazi na kuwajibika ipasavyo na kuacha kabisa blabla na kusogoa maofisini?

Tufanyenini ili kuhakikisha wezi, hasa huko mawizarani wanapewa adhabu kali hata ikiwezekana iwe ya kifo kwa uwapiga mawe na kuwachoma moto kama tufanyavyo kwa vibaka; na tufanye nini ili kila mmoja wetu atii sheria na kutumia madaraka yake kwa faida ya wananchi? Tufanye nini ili kila mmoja wetu atimize wajibu wake bila kusukumwa au kukumbushwa?
 
Mlitegemea jipya kwani, tushikamane jamani tujenge taifa, je tufanye nini ili tujikite kwenye kufanya kazi na kuwajibika ipasavyo na kuacha kabisa blabla na kusogoa maofisini?

Tufanyenini ili kuhakikisha wezi, hasa huko mawizarani wanapewa adhabu kali hata ikiwezekana iwe ya kifo kwa uwapiga mawe na kuwachoma moto kama tufanyavyo kwa vibaka; na tufanye nini ili kila mmoja wetu atii sheria na kutumia madaraka yake kwa faida ya wananchi? Tufanye nini ili kila mmoja wetu atimize wajibu wake bila kusukumwa au kukumbushwa?

umemaliza kila kitu, uwajibikaji kwa kwenda mbele ndio dira
 
... Sioni Tatizo lolote na muafaka kama CDM walivyoupeleka na kukubaliwa na CCM...

Niwaambie KITU...

Mwisho wa siku CCM watakiuka kilichokubaliwa .... Repeat ... At the end of the day CCM will make a U turn!!

WHY?

CCM has not yet developed a sense of maturity to deal WISELY with NATIONAL Serious ISSUES..!! Kuweza kulitekeleza hili kwa BUSARA ni maajabu ya Miaka 50 y UHURU wa Taifa Hili. Kujua Hilo ...CDM ni kuwapa last chance ..kama walivyofanya and wait them to show the WISDOM they don't and will never have ... Wana busara gani ... Na hiyo michezo ya KUVUA gamba? Wameshindwa kuvuana gamba , ufisadi na mengi mengineyo ...Watatoa wapi UWEZO, HEKIMA na BUSARA za UTU Huru katika kusimamia kitu makini kama Katiba. Kwa namna yeyote ile KASORO yao inayojionyesha kwenye mambo kadhaa Kijamii ...Itajionesha kwenye Swala la katiba!

Lakini CCM bado ina fursa ya kubadilika na kuamka toka usingizi mzito ..Kwanza WAVUENE GAMBA ..and they can do it seriously IF THE REALLY WANT....NA ... MWANGA NA HEKIMA itakayopatikana hapo ..sasa itumike KUMULIKIA na kutegeneza Katiba mpya. NDIO wafanye Kitu kimoja kuhakikishai umma kwamba wanaona kwa macho sahihi matatizo ya kijamii ...VINGINEVYO ..Na Kweli kabisa ... Wanatoa wapi Mamlaka ya Kujihusisha na jambo zito kama la uundwaji wa katiba mpya.

Najua na ninahakika.. kabla ya Kikao kijacho cha Bunge ... CCM watakuwa wamevuana magamba na mafisadi sugu .. watapigwa chini .. na HIVYO ... Watakuwa na mamlaka na sauti ya kweli ya kusimamia Mchakato wa Katiba Mpaya! CCM wanaweza kulifanya hili na kuwa kinara wa Tanzania MPYA!!
 
Si wakati muafaka wa kumlaum mtu yeyote.kila mmoja wetu ajitokeze kushiriki ktk mchakato huu mhm kwa taifa.mbowe alifanya blanda bungeni,akajistukia,akaenda kwa Jk kusema alichonacho.mswada umeshasainiwa,kujadili eti asingesaini ni sawa na kumfanyia post moterm maiti.
 
Back
Top Bottom