Mh. Mbowe aongelea yaliyojiri Ikulu

Mh. Mbowe aongelea yaliyojiri Ikulu

Mh. Freeman Mbowe ambae ni mwenyekiti wa chama cha CHADEMA na kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani bungeni, Amesema kuwa pamoja na mambo mengi walioishauri serikali hawana mamlaka ya kumzui Rais kutosai muswada uliopo mezani kwake hivi sasa ila walimtaka atumie kifungu cha (97)2 kutokana na mapungufu mengi katika muswada huo! Pia serikali aliwaahidi kuyafanyia mabadiliko na mapendekezo yao kwenye kikao kijacho January 31, Aidha Mh. Mbowe anaweka wazi kuwa wakiyafanyia kazi mapendekezo yao hao wako tayari kushiriki katika utungwaji wa katiba mpya na wakiyapuuza hawana namna tena nikurudi kwa waamuzi wakuu wananchi.

OOK
I think kutakuwa na mabadiliko makubwa kwenye kikao kijacho cha Bunge.
Logic: Rais kama mwenyekiti wa CCM hawazi kuwageuka wabunge wake wlaiopitisha sheria, kamwe isingewezekana akubali maoni ya Chadema moja kwa Moja bali anaweza kuyakubali kwa njia ya kuzunguka. Hili halihitaji mtu kuwa na PhD kuelewa.
Hata Rais akisaini hiyo sheria inaweza kurekebishwa kwenye Bunge, hivyo yawezekana amesaini (ndio mana kafanya haraka) kuwaridhisha wabunge wa CCM then next bunge mabadiliko yakapendekezwa...na hili litakuwa TRUE (japo mabadiliko yote ya CDM yanaweza yasiwepo).

Kumbuka sheria ya Uchaguzi 2010 ilifanyiwa marekebisho baada ya kusainiwa kwa mbwembwe!
So tuwe na matumaini!
 
Ni kweli kabisa hawa watu wametusaliti wananchi tulikuwa na imani nao sana ila kwa swala ili wametuangusha sana na hatuna imani nao tena.

Siasa hizi. Leo watu wa cuf na ccm ndio mmekuwa wa kwanza kusema chadema imewasaliti. Wakati mlipokuwa mnashangilia kupitishwa kwa sheria mbovu mlikuwa namjiita wazalendo. Twendeni tukarekebishe katiba na wala sio kuandika katba mpya. Katba mpya itaandikwa baadae. Mind you, serikali yoyote hutolewa madarakani na katiba yoyote provided wenye nchi wameamua.
 
Hakuna kipindi ambacho Chadema mmewekwa kwenye kona mbaya au mmekalia kuti kavu kama kipindi hiki kwa kuwa makubaliano yenu na Rais ambae ni mwenyekiti wa CCM yanaweza kutumika kuwasambalatisha,kwa kuwa mkiwekwa sawa kuja kustuka Chadema chali na Wananchi wanapoteza imani na mvuto nanyi, na Wananchi kupoteza imani nanyi ndio duwa kuu la CCM dhidi yenu,kuna msemo unasema muombee adui yako njaa,ata sullender mwenyewe.

CCM wanaweza kutake advantage kumanipulate mchezo mzima mkajikuta chali. Kwa kuwa hoja ilikuwa ni kumshinikiza Rais asisaini mswada wa sheria ya katiba na sio otherway round,nyie mmeingia kwenye new agreement ambayo haikuwa kusudio lenu.

Kwa kuwa Wananchi waliwatuma kwa niaba yao mmwambie Rais madhara ya kusaini nyie mmekwenda kuvaa viatu vya Raiis kwa kwa vipimo vya CCM.

Nyie wajibu wenu ilikua ni kuachana na makubaliano na kuludisha jibu la waliowatuma wanachma wenu wa CDM na watanzania wanawaunga mkono.sasa hata mimi binafsi naanza kuona hamkubeba dhamana ya Wanachi bali mlibeba dhamana yenu.kwa kuwa mlitumwa na umma nanyi mngeomba muda kuja kuongeaa na watu waliowatuma kama yeye alivyoomba muda kumaliza mazungumzo nanyi siku ya pili.

Hakika Chadema kwa mchezo huu,tia maji tia maji,mnaweza kujikuta chali CCM ikaibuka kidedea,si ajabu laweza kuwa tego. Ole wenu akiteua tume [Kamati ya katiba],Chadema mtafute pa kukaa,simnajua wadau walivyomshikia Kidedea Zitto kwa kuchekacheka na kujipitisha kwa Presidar.manake kwa watu wote makini watawamwaga kwa kukosa msimamo wa Chadema na si kudandia ovyo offer pasipo kuiludisha kwa umma [People's Power-your slogan].

Mmekaa huko mkajiamulia na amkutaka kuwalejeshea maafisa wenu ambao ni Wananchi,ambao huwa mkishikwa kidogo tu mnakimbilia kulia kwao na kuomba kinga yao. Haya yetu macho!!!!!!!!!!one mistake one goal!!!!!!!!!!ukileta na kutafutiwa masoo,kila mmoja atakula kona,kuja kustuka umoja mlioingia nao ikulu umeishia kwenye kutoka kila mmoja na lwake. Tuombe mungu!!!!!!!!!isiwe ni moja ya michezo michafu,ambayo kwa CCM si jambo baya kwa kuwa wao kanuni yao ni moja "Mapinduzi Daima"

ahahahahahahahah! Haki ya Mungu.
 
Kikwete aliapa mbele ya wazee wa mkoa wa Dar es salaam kuwa lazima atausaini mswada, hivyo asingekubali kula matapishi yake!
 
Hakuna kipindi ambacho Chadema mmewekwa kwenye kona mbaya au mmekalia kuti kavu kama kipindi hiki kwa kuwa makubaliano yenu na Rais ambae ni mwenyekiti wa CCM yanaweza kutumika kuwasambalatisha,kwa kuwa mkiwekwa sawa kuja kustuka Chadema chali na Wananchi wanapoteza imani na mvuto nanyi, na Wananchi kupoteza imani nanyi ndio duwa kuu la CCM dhidi yenu,kuna msemo unasema muombee adui yako njaa,ata sullender mwenyewe.

CCM wanaweza kutake advantage kumanipulate mchezo mzima mkajikuta chali. Kwa kuwa hoja ilikuwa ni kumshinikiza Rais asisaini mswada wa sheria ya katiba na sio otherway round,nyie mmeingia kwenye new agreement ambayo haikuwa kusudio lenu.

Kwa kuwa Wananchi waliwatuma kwa niaba yao mmwambie Rais madhara ya kusaini nyie mmekwenda kuvaa viatu vya Raiis kwa kwa vipimo vya CCM.

Nyie wajibu wenu ilikua ni kuachana na makubaliano na kuludisha jibu la waliowatuma wanachma wenu wa CDM na watanzania wanawaunga mkono.sasa hata mimi binafsi naanza kuona hamkubeba dhamana ya Wanachi bali mlibeba dhamana yenu.kwa kuwa mlitumwa na umma nanyi mngeomba muda kuja kuongeaa na watu waliowatuma kama yeye alivyoomba muda kumaliza mazungumzo nanyi siku ya pili.

Hakika Chadema kwa mchezo huu,tia maji tia maji,mnaweza kujikuta chali CCM ikaibuka kidedea,si ajabu laweza kuwa tego. Ole wenu akiteua tume [Kamati ya katiba],Chadema mtafute pa kukaa,simnajua wadau walivyomshikia Kidedea Zitto kwa kuchekacheka na kujipitisha kwa Presidar.manake kwa watu wote makini watawamwaga kwa kukosa msimamo wa Chadema na si kudandia ovyo offer pasipo kuiludisha kwa umma [People's Power-your slogan].

Mmekaa huko mkajiamulia na amkutaka kuwalejeshea maafisa wenu ambao ni Wananchi,ambao huwa mkishikwa kidogo tu mnakimbilia kulia kwao na kuomba kinga yao. Haya yetu macho!!!!!!!!!!one mistake one goal!!!!!!!!!!ukileta na kutafutiwa masoo,kila mmoja atakula kona,kuja kustuka umoja mlioingia nao ikulu umeishia kwenye kutoka kila mmoja na lwake. Tuombe mungu!!!!!!!!!isiwe ni moja ya michezo michafu,ambayo kwa CCM si jambo baya kwa kuwa wao kanuni yao ni moja "Mapinduzi Daima"

Hofu yangu ni kwanini walipokunywa chai ya ikulu wote walibaki kucheka? Isije kuwa ile chai ilichanganywa na mavi ya jk
 
Waliokuwa na sera ya katiba mpya ni CUF toka awali na walishaandika wanayoipendekeza, magwanda wamerukia njiani tu, na kama uonavyo, magwanda hawana jipya, maandamani walianzisha CUF, kususa walianzisha CUF, CUF walisusa kabisa kuingi baraza la wawakilishi na walikuwa hawachukuwi posho wala mishahara. Umesaau, hawa magwanda hawana jipya, na mpaka la kuonana na Rais, CUF walianza na ikawasaidia sana, magwanda nayo hii imewasaidia sana kisiasa. Hawana jipya.
Je kama Cuf ndio waanzilishi wa yote hayo, wameisha pata walichokitaka sasa? walikuwa wanaandamana ili Seif awe Makamo na duni awe Waziri wa Afya? kama waliandamana kutaka Katiba Mpya , je wameisha ipata? mbona kafu mnaonekana kama vile kila kitu mlichokitaka kimeisha patikana? CUF Zanzibar wameipata katiba, CUF Bara je???? au CUF ni kwa ajili ya Zanzibar pekee yake ni hawa wengine wa Bara ni geresha tu na watu wa kuchuma kama masisiem?
 
mlitegemea jipya kwani, tushikamane jamani tujenge taifa, je tufanye nini ili tujikite kwenye kufanya kazi na kuwajibika ipasavyo na kuacha kabisa blabla na kusogoa maofisini?

Tufanyenini ili kuhakikisha wezi, hasa huko mawizarani wanapewa adhabu kali hata ikiwezekana iwe ya kifo kwa uwapiga mawe na kuwachoma moto kama tufanyavyo kwa vibaka; na tufanye nini ili kila mmoja wetu atii sheria na kutumia madaraka yake kwa faida ya wananchi? Tufanye nini ili kila mmoja wetu atimize wajibu wake bila kusukumwa au kukumbushwa?
tupate katiba nzuri
 
Kwa kweli mimi naona chadema walikua na hamu na juice ya ikulu, hakuna lolote au labda walitaka kukalia makochi ya ikulu.
 
Kizunguzungu............ imeshakuwa sheria afu tuendeleee kutoa maoni!!!!!!!!!!!!!!!!! sijaelewa,
 
Bibie,
Aliyerukia njiani ni Kikwete. Hii haikuwemo kwenye ilani ya CCM. Haikuwemo kwenye kampeni zake lakini ghafla ameifanya kuwa ni pendekezo lake. Wapi na wapi? Anyway, in the final analysis it was Chadema's push that made Kikwete adopt the katiba issue. It was not CUF.


Hawa walishaolewa na kuridhika na hali halisi. By the way, mwenyekiti wenu Lipumba kapotelea wapi?
I like that, alafu umempa ukweli. Hii ngoma ya katiba kikwete kadandia Treni iliyokuwa kwenye spidi kali sasa angalia kasaini katiba yenye mapungufu na pia hapa kadanganywa. Maskini Tanzania....
 
Kwa kweli mimi naona chadema walikua na hamu na juice ya ikulu, hakuna lolote au labda walitaka kukalia makochi ya ikulu.

Kwani tuklija kwako hatuwezi kukalia makochi? au ukatupatia juice au hata chai jamani? au sukari bado haijashuka bei nini mwanangu kiasi hata cha kuwapa wageni wako chai?? duu. Vitu vya kawaida sana mbona?
 
Chadema hawana la kufanya kwa sasa inawabidi kuwa wapole tu maana makosa walifanya toka mwanzo... Sasa wakubali kupakatwa tu hawana jinsi.

Kosa gani hilo Mkuu?
Kila mara tumezoea Chadema ndo wanatumia mahakama ya wananchi. Unaweza kuliweka wazi ili nao iwe zamu yao kushtakiwa kwa wananchi?
 
Naanza kukosa imani na viongozi wa CDM, Nahisi niwasaliti wa wananchi, Tutaendelea kuishi kwa matumaini Hewa mpaka lini?
Imekuwa ni kawaida ya viongozi wa upinzani wakiingia ikulu wanarudi wamesahau kilichowapeleka, Inaumiza saana,

Acha umbea, sasa wewe ulitaka wafanye nini? acha kulalamika bila kuwa na solution
 
Acheni kuona chadema ili waonekane wanafanya kazi mpaka waandamane wamefanya jambo la msingi yasipofanyiwa kazi ndo tunaweza amuua vinginevyo ushabiki wa kijinga kamwe aukubaliki big up chadema mmeanza vizuri
 
aliyepakatwa ni chadema, japo CCM hawakuwa na ajenda ya katiba wameona umuhimu wake kutokana na hali ya kisiasa ilivyo kwa sasa nchini.

CCM wamegutuka kuwa kulikuwa kuna uwezekano ya wao kundolewa kwenye uongozi wa nchi hii na sasa wamejipa nguvu ya kuendelea kuingoza nchi hii kwa kujitengenezea katiba yao itakayo linda maslahi yao.

Chadema walikuja na hoja za maana sana ila walishindwa kuzisimamia na sasa hawana jinsi tena zaidi ya kuungana na magamba kuwasaidia kuunda katiba itakayo wasaidia magamba kutawala milele, uko ndiko kupakatwa kwao.

Wewe ni raia wa nchi gani? Katiba ya tanzania siyo ya CHADEMA wala CCM, ni ya watu wote na hivyo tunategemea mtu yeyote mwenye akili timamu atatoa mchango wa kuboresha mchakato badala ya ushabiki wa kipuuzi unaoendelea hapa. Mawazo ya aina hii hayatakiwi hapa, hata kama ni mpita njia unaechangia, unatumia akili yako vibaya.
 
Kwa kweli mimi naona chadema walikua na hamu na juice ya ikulu, hakuna lolote au labda walitaka kukalia makochi ya ikulu.
Ikulu ni nyumba ya watanzania si nyumba ya Kikwete, wanawe ,wala mkewe au si ya CCM,kwa hiyo kwenda ikulu kwa maswala ya kitaifa si dhambi
 
aliyepakatwa ni chadema, japo CCM hawakuwa na ajenda ya katiba wameona umuhimu wake kutokana na hali ya kisiasa ilivyo kwa sasa nchini.

CCM wamegutuka kuwa kulikuwa kuna uwezekano ya wao kundolewa kwenye uongozi wa nchi hii na sasa wamejipa nguvu ya kuendelea kuingoza nchi hii kwa kujitengenezea katiba yao itakayo linda maslahi yao.

Chadema walikuja na hoja za maana sana ila walishindwa kuzisimamia na sasa hawana jinsi tena zaidi ya kuungana na magamba kuwasaidia kuunda katiba itakayo wasaidia magamba kutawala milele, uko ndiko kupakatwa kwao.

Ndugu tunaweza kutumia informal terms as much as we can but we should not brand Chadema that way. I do not think CDM leaders have succumbed to CCM yet. Tuwape muda na tuwatie moyo ili tuone watakavyotuongoza ili tupate katiba mpya. CCM wanaweweza kufanya watakavyo lakini historia ishaandikwa wazo la katiba mpya ni agenda ya CDM kuanzia kwenye mikutano kabla ya uchaguzi na kwenye uchaguzi kupitia election manifesto. Sasa wazo lao limekuwa hijacked na manyangau na kukifanya lao lakini katika approach ya mvinyo wa zamani ndani ya chupa mpya lakini chafu.

Lakini lazima tuzingatie tena kwa makini kuwa Tanzania sio ya CDM na wanaharakati na NCCR kwa upande mmoja na CCM, CUF, TLP, UDP na vingine vyama vya briefcase. La hasha ni yetu sote. Sasa walioomba kukutana na rais na wakaaidiwa kuwa wasubiri kikao kijacho cha bunge wanatuambia waliyokubaliana sisi tunakataa na tunalazimisha tunayotaka kusikia ndio waseme ndio nini hii. Hivi wakitudanganya kuwa tulikubaliana hivi na hivi na kesho hakuna kilichofanyika tutasema nini. Naona cha msingi January/February sio mbali tuwe na subira ili tuone maboresho kama yatahakisi kile tunachotaka. Kama hicho hakitafanywa basi tunaweza tukasema ni nani kampakata mwingine.

Halafu tukishakubali kuwa TZ ni ya wote na sisi ambao hatuko kwenye party hierachy tujaribu kutoa mawazo chanya ni nini kifanyike. We have to articulate plans proactively and on wide spectrum. Na tupelleke mawazo yetu kwenye jukwaa husika either CDM, Wanaharakati au NCCR mageuzi au kwa wadau wengine wenye mapenzi mema na Tanzania na ambao wame take lead kuonyesha ni jinsi gani bunge limetuburuza. Na makongamano yakiitwa na maandamano tujitokeze kuonyesha tunavyounga mkono. Tukikaa tunalaumu CDM na viongozi wake wasiofika hata 100 wakati wananchi ni zaidi ya 40 millioni tukifa Mungu atatuuliza ujuzi wetu na uwezo wetu tuliutumiaje?
 
Unajua mtu anaweza akakupima mtu na akajua wewe ni nani kwa lugha unayoitumia. Akili yako yote umeielekza kwenye vyakula kuliko hata muktadha wa kile ambacho CDM walikuwa wanatafuta. Hakuna mahala popote walisema wanaenda kumlazimisha Kikwete asitie sahihi muswada. Walikwenda kama wazalendo na wamenda nchi yao kumweleza kile wanachoona muswada umepotoka na baadae kumpa mapendekezo. Uwezo wa kumlazimisha kama wangekuwa nao basi hata kwa kusema tu si rais angesikia? Hivyo basi tuweke jamvini mambo ya msingi na ambayo ni researchable sio kejeli za chai na vyakula.
 
Chadema kwa hili mlilolitenda hamna tofauti na Mkulima mmoja wa maeneo ya uko kwetu usukumani ambako jamaa alikuwa na shughuri ya kilimo kuamkia siku ya pili kwa maana ya kesho,tunaita kilimo hicho chake ni aina hiyo NGESE yani kilimo cha shamba kubwa kinachoitaji nguvu kubwa.Hivyo jamaa huyo alikuwa hana ngombe na jembe la kulimia ngesse hiyo hivyo ikambidi aaende kuazima kwa jirani yake.Jamaa jioni mdogo mdogo akasogea kwa jirani yake mwenye vifaa hvvyo vya ngesee yani kilimo.

Jamaa alipofika akakuta weneyeji wake wanakula Ugali na mboga ya mzubo [Juice na Chai] wakamkaribisha jamaa karibu mgeni alivyokuwa hamnazo akaweka masaburi yake chini na kuanza kufakamia ugali na mzubo.Kwenye hatua za kuendelea kuumanga huku akiendelea kupiga soga nyingine kabisa tofauti na shida yake kwa wenyeji wake,story zenyewe na wenyeji wake mara oooh mara eeehh.Kidogo wanasikika hodi kuna mgeni mwingine mlangoni, wenyeji wakampa karibu mpaka ndani na karibu ya mwisho kwa mgeni ni kuambiwa karibu mkekani ujiunge nasi kwenye chakula ugali na mboga ya mzuboa [AKA JUICE NA CHAI].

Mkaribishwaji akaibuka na yake moyoni kwa kuwaambia wenyeji wake jamani sahamaanini sana kama nitawakwaza yani mguu huu hapa kwenu kabla ya yote kilichonileta ni Jembe na Ngombe kesho nina bonge ya NGESE jamani hivyo nijuzeni haraka kama nitapata au la manake vinginevyo mimi huu mguu na njia mpaka nipate kutimiza shida yangu.

Wenyeji kwa kusikia ujumbe wake huo wakamwambia kisukuma NDOO SHIDA,IGESHAGE TOLYE WAPANDEKAGA [yani kaa tule wewe umeshapata /timiziwa shida yako ndugu] basi mgeni huyu akaweka masaburi yake na kunawa kisha kuanza kusukumiza ugali wa kisukumio cha mzubo na maziwa kwa raha mstarehe.

MJINGA wa kwanza kufika kusikia mwenzie kaomba akatangaza shibe yake [Yeeh wajameni na mimi nilikuwa ninaitaji Jembe na Ngombe ndio vilinileta hapa kwenu nilikuwa nasubili tumalize kula niwaambie,wakamwambia ndio hivyo tena aliekuja kwa nia ya shida hiyo kesha chukua'[Yani kwa kisukuma walimwambia PUMBAAAAAAAAAAAAAAAAAFFFFFFUUUUUUUUUUUU!!!!!!!!!!!!!.[Yani tamka kama vile anavyotamka mcheza sinema wa kizazi kipya Nchini Ray Kigosi-Manake huyu uitamka Pumbavu kwa kisukuma na kwa sauti sahiii].

Hakika Chadema isijekuwa ni huyu mami wa kwanza aliejali kula ugali na mzubo [JUICE YA PASSION NA CHAI] basi mwenye Jembe na Ngombe [Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania] uenda anasubilia mwenye shida genuine ya kweli apewe JEMBE NA NGOMBE kwa kuwa wa kwanza alikuwa CUF na si ajabu CDM nao wakaingia kwenye mchezo ule ule wa kukaa na kufakamia Juice na Chai na kusahau kuonyesha kuwa mguu ule ikulu serious ni mpaka niambie JEMBE NA NGOMBE VIPO NDIO NAKAA KULA vinginevyo kisukuma tunasema YAYA [YANI HAPANA].


Inaonyesha ni jinsi gani unavyohusudu kula kuliko kitu kingine. Yaani wewe unafikiri vichwa vile vya watu makini walienda Ikulu kunywa chai kwa muda wa siku mbili basi. Unataka kuuaminisha umma kuwa watu hawa hawana pesa ya kununua chai? Na wala huwezi kujitetea kuwa umetumia lugha ya picha bali ni kejeli isiyojenga. Mkutano wowote huwa una agenda short of which hauna sifa ya kuitwa mkutano. Mkutano wa CDM na Rais ulikuwa na agenda. Na zilikuwa zinaongelewa moja baada ya nyingine na zaidi kabrasha la kurasa 17 Rais alikabidhiwa likiwa limeandikwa kwa ufasaha kabisa. Kazi yao wamefanya kama walivyotumwa na ilikuwa ni kazi ya serikali kutekeleza au kukataa. Moja rais amekataa amesaini muswada. Sasa tusubiri bunge la February kama hamna kilichofanyika na CDM ikakaa kimya au ikawa kama CUF na TLP hapo unaweza kuisakama upendavyo. Kwa sasa ni mapema mno kuwahukumu wakati wametumia nafasi iliyopo kuwakiklisha kilio cha wengi.
 
Back
Top Bottom