Mh. Mbilinyi (Sugu) alipuka bungeni

Mh. Mbilinyi (Sugu) alipuka bungeni

MBUNGE wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (Chadema), maarufu kwa jina la Sugu, juzi alilishambulia Baraza la Mawaziri akisema kuwa limejaa wapumbavu. Tukio hilo lilitokea juzi jioni wakati mbunge huyo akichangia hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2013/14.

Sugu, alisema Baraza lote la Mawaziri linaundwa na wapumbavu, kwa kuwa linashiriki kubomoa nchi linayoiongoza.

"Kabla sijaanza kuchangia, nataka ninukuu maandiko katika biblia yanayosema kwamba: ‘Mwanamke mpumbavu huibomoa nyumba yake kwa mikono yake mwenyewe' vilevile Serikali pumbavu inabomoa nchi yake yenyewe, yaani namaanisha Baraza la Mawaziri wapumbavu.
 

Attachments

  • SUGU.jpg
    SUGU.jpg
    125 KB · Views: 187
Sugu awashambulia Mawaziri
*Awaita wapumbavu
MBUNGE wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi
(Chadema), maarufu kwa jina la Sugu, juzi
alilishambulia Baraza la Mawaziri akisema kuwa
limejaa wapumbavu. Tukio hilo lilitokea juzi
jioni wakati mbunge huyo akichangia hotuba ya
bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa
fedha 2013/14.
Sugu, alisema Baraza lote la Mawaziri
linaundwa na wapumbavu, kwa kuwa linashiriki
kubomoa nchi linayoiongoza.
“Kabla sijaanza kuchangia, nataka ninukuu
maandiko katika biblia yanayosema kwamba:
‘Mwanamke mpumbavu huibomoa nyumba
yake kwa mikono yake mwenyewe’ vilevile
Serikali pumbavu inabomoa nchi yake yenyewe,
yaani namaanisha Baraza la Mawaziri
wapumbavu.
“Mambo mengi nchi hii hayaendi kutokana na
Serikali pumbavu, juzi hapa Mbatia (James
Mbatia, Mbunge wa Kuteuliwa kupitia NCCR-
Mageuzi) alileta hoja bungeni kuhusu mitaala ya
elimu nchini, mkatumia wingi wenu
kuinyanyapaa sasa matokeo ya form four
(kidato cha nne), yamewaumbua.
“Hatuwezi tukawa na Waziri wa Elimu boya,
mwenye elimu ya kuungaunga halafu tukafanya
vizuri katika elimu.
Sugu alikwenda mbali akisema jambo hilo
lilikuwa ni kazi ya Idara ya Usalama wa Taifa,
kufanya uchunguzi wa mawaziri wanaotarajiwa
kuteliuliwa na Rais ili kubaini uwezo wao.
Aliwashutumu Usalama wa Taifa kwa kuacha
kufanya mambo hayo ya msingi na kubaki na
kazi ya kuifuatilia Chadema na kung’oa watu
kucha.
“Mimi binafsi sijisikii kuwa sehemu ya Bunge
hili, kukaa na wabunge kama wakina Mwigulu
(Mwigulu Nchemba, Mbunge wa Iramba
Magharibi kupitia CCM), huyu naye ni
mpumbavu,” alisema Mbilinyi.
Kabla ya kuendelea na mjadala, Spika wa
Bunge, Anne Makinda, alimkatisha mbunge
huyo na kumtaka kutotumia neno pumbafu
wakati akiendelea kuchangia hoja yake.
Hata hivyo, Sugu aligoma kutotumia neno hilo
kwa kusema kuwa: “Mheshimiwa Spika, naomba
taifa lielewe upumbafu sio tusi ndio maana lipo
hata kwenye biblia, upumabavu ni ‘stupidity’,
lucky of knowledge of understanding’ ambayo
mawaziri wote wanayo,” alisema Sugu.
Mbali na Sugu Mbunge wa Kigoma Kusini, David
Kafulila (NCCR-Mageuzi), naye akichangia
mjadala huo, alisema Tanzania ni nchi tajiri ila
wanaosababisha umasikini wa Watanzania ni
viongozi.
“Kila kitu cha utajiri tunacho, nchi yetu ni nchi
ya pili kwa vivutio vya utalii duniani, lakini
mapato yetu ni chini ya asilimia 10, kwa nini
tunashindwa kuwatajirisha Watanzania,” alihoji
Kafulila.
Aliwataka pia wabunge kutokubali mkutano wa
Bunge kumalizika bila majibu ya Serikali kuhusu
taarifa za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu
za Serikali (CAG).
“Kwa sababu mnaona CAG anaikosoa Serikali
mnaleta sheria za kuifinya ripoti yake, hii
mnafanya kwa faida ya nani? Hii nchi ni yetu
sote, hamuwezi mkasema nchi ni ya amani
wakati mnakula wenyewe,” alisema.
Kafulila pia alizungumzia misafara ya viongozi
isiyo na tija ambayo inasababisha fedha nyingi
za Serikali kupotea.
Kwa upande wake, Mbunge wa Nzega, Dk.
Khamis Kigwangala (CCM) akichangia hotuba
hiyo ya bajeti yeye aliwashambulia Chadema
akisema kuwa vitendo vyao ni vya kipuuzi.
Alisema Chadema wanachezea mchakato wa
uundwaji wa Katiba mpya, kitendo alichodai
kuwa ni cha kipuuzi.
Aliishangaa Serikali kuona inawaacha watu
wachache kutaka kuharibu mchakato huo
ambao ni muhimu kwa mustakabali wa taifa.
Mbunge wa Mkanyageni, Habibu Mnyaa (CUF)
aliitaka Serikali kumaliza mgogoro wa Mtwara
ndani ya miezi minne kwa kuwa mgogoro huo
bado upo licha ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda
kusema umekwisha.
Aliyataja madai ya watu hao kuwa ni uzalishaji
wa umeme wa Megawati 300 katika Mkoa wa
Mtwara, kuunganisha mkoa huo katika gridi ya
taifa na kufungua fursa za viwanda na bandari.
Mbunge wa Bariadi Mashariki, John Cheyo
(UDP), alisema Serikali lazima ichukue
tahadhari kulinda amani na umoja wa kitaifa
nchini.
Alisema migogoro inayoendelea sasa kuhusiana
na udini, ardhi na maliasili nyingine kama vile
gesi idhibitiwe ili kuiepusha nchi katika
machafuko.
 
Hata mie nilibahatika kumsikiliza...yaani duh...Chadomo mnatisha kwa vitengo...kitengo cha utekaji..kitengo cha matusi..na kadhalika...Na mnayo bahati mko na mheshimiwa mwenye CV nzuri kweli eneo hilo na sio ajabu akaingia tena studio kurekodi albamu nyingine ya MATUSI..(nadhani mheshimiwa ana watoto, wakue waje kumsikiliza baba yao)

Na huu ndio UTAJIRI wa cd4..ups sorry chadomo...mwanasias labda ni Zito peke yake, Wengine wote ni wanaharakati (wana-hihop), Wanaotenda kwa kuongozwa na mihemuko, uwezo mdogo wa kujenga hoja, wasioweza kuchagua waseme nini na wakati gani)..kuna mmoja (nadhani aligida viroba kadhaa) alipopanda jukwaani kule NMC Arusha akaanza kuropoka siri za vikao vya ndani vya chama...tutaitenga kanda ya kaskazini..bla...bla...bla......

Any way...nasubiri albamu nyingine ya mitusi (virusi), zile nyingine nilishazisikiliza umetisha.....

Ups...nilitaka kusahau...kwa kuwa AGENDA kuu ni (nchi haitotawalika) mna utajiri wa watekelezaji...
 
Hata mie nilibahatika kumsikiliza...yaani duh...Chadomo mnatisha kwa vitengo...kitengo cha utekaji..kitengo cha matusi..na kadhalika...Na mnayo bahati mko na mheshimiwa mwenye CV nzuri kweli eneo hilo na sio ajabu akaingia tena studio kurekodi albamu nyingine ya MATUSI..(nadhani mheshimiwa ana watoto, wakue waje kumsikiliza baba yao)

Na huu ndio UTAJIRI wa cd4..ups sorry chadomo...mwanasias labda ni Zito peke yake, Wengine wote ni wanaharakati (wana-hihop), Wanaotenda kwa kuongozwa na mihemuko, uwezo mdogo wa kujenga hoja, wasioweza kuchagua waseme nini na wakati gani)..kuna mmoja (nadhani aligida viroba kadhaa) alipopanda jukwaani kule NMC Arusha akaanza kuropoka siri za vikao vya ndani vya chama...tutaitenga kanda ya kaskazini..bla...bla...bla......

Any way...nasubiri albamu nyingine ya mitusi (virusi), zile nyingine nilishazisikiliza umetisha.....

Ups...nilitaka kusahau...kwa kuwa AGENDA kuu ni (nchi haitotawalika) mna utajiri wa watekelezaji...

we gamba unataka kutudanganya mchana mchana? We subiri 2015 ndio utajua tu.
 
Hata mie nilibahatika kumsikiliza...yaani duh...Chadomo mnatisha kwa vitengo...kitengo cha utekaji..kitengo cha matusi..na kadhalika...Na mnayo bahati mko na mheshimiwa mwenye CV nzuri kweli eneo hilo na sio ajabu akaingia tena studio kurekodi albamu nyingine ya MATUSI..(nadhani mheshimiwa ana watoto, wakue waje kumsikiliza baba yao)

Na huu ndio UTAJIRI wa cd4..ups sorry chadomo...mwanasias labda ni Zito peke yake, Wengine wote ni wanaharakati (wana-hihop), Wanaotenda kwa kuongozwa na mihemuko, uwezo mdogo wa kujenga hoja, wasioweza kuchagua waseme nini na wakati gani)..kuna mmoja (nadhani aligida viroba kadhaa) alipopanda jukwaani kule NMC Arusha akaanza kuropoka siri za vikao vya ndani vya chama...tutaitenga kanda ya kaskazini..bla...bla...bla......

Any way...nasubiri albamu nyingine ya mitusi (virusi), zile nyingine nilishazisikiliza umetisha.....

Ups...nilitaka kusahau...kwa kuwa AGENDA kuu ni (nchi haitotawalika) mna utajiri wa watekelezaji...

Wewe gamba gambino acha kupiga mayowe
 
Hata mie nilibahatika kumsikiliza...yaani duh...Chadomo mnatisha kwa vitengo...kitengo cha utekaji..kitengo cha matusi..na kadhalika...Na mnayo bahati mko na mheshimiwa mwenye CV nzuri kweli eneo hilo na sio ajabu akaingia tena studio kurekodi albamu nyingine ya MATUSI..(nadhani mheshimiwa ana watoto, wakue waje kumsikiliza baba yao)

Na huu ndio UTAJIRI wa cd4..ups sorry chadomo...mwanasias labda ni Zito peke yake, Wengine wote ni wanaharakati (wana-hihop), Wanaotenda kwa kuongozwa na mihemuko, uwezo mdogo wa kujenga hoja, wasioweza kuchagua waseme nini na wakati gani)..kuna mmoja (nadhani aligida viroba kadhaa) alipopanda jukwaani kule NMC Arusha akaanza kuropoka siri za vikao vya ndani vya chama...tutaitenga kanda ya kaskazini..bla...bla...bla......

Any way...nasubiri albamu nyingine ya mitusi (virusi), zile nyingine nilishazisikiliza umetisha.....

Ups...nilitaka kusahau...kwa kuwa AGENDA kuu ni (nchi haitotawalika) mna utajiri wa watekelezaji...
upo peke yako kaka. Kuandika humu mpaka ulipwe. Huoni aibu? Mimi na wenzangu tunalipenda taifa letu. Wewe unapenda mfuko wa Mwigulu.
 
Wakati mwingine huwa najiuliza sana, " hivi kwanini Mungu Aliweka tofauti kubwa sana ya kimtazamo baina ya wanadamu? " hata hivyo, sijawahi pata jibu linalokidhi hamu yangu ya kutaka kufahamu. Binafsi, sijaona tatizo la mchango wa Mh. Mbilinyi, 'SUGU' ; hivi, kwa namna ambavyo serikali yetu inatenda, ni neno gani hasa linaistahili? Ulimtaka 'SUGU' awe mnafiki dhidi ya dhamiri yake kwa kupunguza ukali wa maneno? Hiyo ni kawaida ya wanafiki. Neno kali litatumika tu, ilimradi limtendee haki mtamkiwa.
Mr. Gideon, lazima utambue kuwa mafisadi wanalipa watu kuandika humu na kujitetea. Wao Tanzania yao ni ya "ndio mzee" bila kuuliza wala kuhoji. Hii ni kwa sababu wanafikilia kwa matumbo, sio vichwa tena. Hivyo achana nao. Taifa letu haliwezi kwenda popote tukiwa na Anna makinda bungeni au mbunge yeyote kutoka CCM na kiongozi wa Ikulu awe CCM. Dhambi zao ni kubwa mno kiasi kwamba ili kuziendesha, lazima taifa lilipe gharama sana. Mfano leo kwenye gazeti la " the guardian" linaeleza jinsi kampuni ya Urusi au Russia inavyotaka kukwepa kodi dollar mil.205 na uongozi upo umetizama kama mimi na wewe. Ila wao waishakatiwa za kuendesha uchafu wao na Mwigulu. Sasa inabidi tuwe watu wazima. Nchi zoootr zilizotuzunguka wako mbali sana. Kenya hawana rasirimali kama sisi lakini wanatuacha tukiwatizama. Ni kwa sababu waliamua kuwatoa viongozi wooote kama wa CCM. Ona Rwanda. Nchi imekuwa kwenye vita mida yote lakini sasa hivi wako mbali. Tuombe sana vituko vya Mwigulu viendelee maana mpaka mwisho, kila mtanzania atakuwa ametosheka na CCM. Tusikubali tena kanga na kofia. Wala misemo ya aina yoyote....sijui nguvu mpya na kasi mpya. Hawa watu ni wale wale. Wanapokezana vijiti tu. Mungu ibariki Tanzania.
 
Back
Top Bottom