Mh. January Makamba, Nakupongeza kwa hili

Mh. January Makamba, Nakupongeza kwa hili

Tuache roho mbaya kama kafanya jambo zuri ,anastahili pongezi ingawa ni mwana CCM
tuache chuki bila sababu ah
 
halow wana jf,

punde nilikuwa naangalia original comedy, nikaona masanja akimtembelea mh. J.makamba kwenye ofisi yake iliyo jengo la nssf water front. He has an excellent office there. Ni ofisi ya maendeleo ya watu wa jimbo la bumbuli.

I was so amazed kusikia alipopata ule mkopo wa gari alitafuta ofisi akaajiri vijana kwa ajili ya kutafuta fedha za maendeleo jimboni bumbuli!

Mm ni nimemkubali huyu jamaa, wachumia tumbo mjifunze hapa. Wabunge wangu wa cdm, tujifunze hapa tuige yalio mazuri.

Big up hon j. Makamba.

hata mimi niliiona na nilikusudia kuja kuanzisha uzi wa kumpongeza. Alitumia akili kubwa sana. Na kilichonivutia ni kuwemo kwa vitabu mbalimbali vya siasa, niliona mabuku makubwa ya mandela, kama kweli anayasoma kwa lengo la kujipa elimu kuwasaidia watanzania, nampongeza lakini kama ni kutumia elim hiyo kuiba pesa za serikali kama alivyofanya baba yake na dada yake mwanaisha
 
kwanini hiyo office isingejengwa kwenye jimbo husika au mkoa husika. Bado hujanishawishi niwasifie magamba. January ni kizazi cha nyoka.
 
Halow Wana JF,

Punde nilikuwa naangalia Original Comedy, nikaona Masanja akimtembelea Mh. J.Makamba kwenye ofisi yake iliyo jengo la NSSF Water Front. He has an excellent office there. Ni ofisi ya maendeleo ya watu wa jimbo la Bumbuli.

I was so amazed kusikia alipopata ule mkopo wa gari alitafuta ofisi akaajiri vijana kwa ajili ya kutafuta fedha za maendeleo jimboni Bumbuli!

Mm ni Nimemkubali huyu jamaa, wachumia tumbo mjifunze hapa. Wabunge wangu wa CDM, tujifunze hapa tuige yalio mazuri.

Big up Hon J. Makamba.

Yule ni mwizi tu, Hana jipya
 
Wananchi wa bumbuli wanaweza kuwasiliana na mbunge wao muda wowote kwa kutuma ujumbe mfupi wa simu ya mkononi bure na mbunge hujibu au kuwasiliana na mamlaka husika mara moja kwa ajili ya utatuzi. Kawaulize wana bumbuli wakwambie namna walivyonufaika na huu ubunifu sio unakoment mambo ya bumbuli ukiwa Honolulu.

wewe kweli ni zero,yaani kisa mtu kakwambia ofisi ya watu wa bumbuli na wewe mishipa inakutoka kupongeza,watu wanaanzisha hadi makanisa ili wapate mitaji kwa migongo ya waumini wewe unashangaa ofisi.hivi kwa hali ya watu wa bumbuli inaendana na mbunge wao kuwa na ofisi ya namna ile,unazifahamu gharama za uendeshaji wa jengo lile pamoja na kodi yake?.Akili kumukichwa ukizubaa unaachwa feli..................msalimie nape.
 
Mkuu ulianza vizuri ila umemaliza vibaya, lengo lako lilikuwa ni kujaribu kubeza wabunge fulani ukiwalinganisha na January. Kikubwa waangalie wengine, kabla na baada ya kupata ubunge na pia mwangalie January kabla na baada ya kupata ubunge halafu walinganishe.

Ahsanta

mkuu sikuwa na lengo la kumsema mtu yeyote, wala sina muda wa kupnteza kwenye jambo kama hilo, mbona kabla ya hapa sikusema, nilicho kisifia ni mwanzo mzuri na vision yake. Akiisimamia vizuri, akitumia facility hi kucatalyze resources atawapeleka mbali wana Bumbuli.
 
Tuache roho mbaya kama kafanya jambo zuri ,anastahili pongezi ingawa ni mwana CCM
tuache chuki bila sababu ah

ni kweli kbs mm binafsi siipendi ccm na mfumo wake wa utawala
 
wana cdm mmefikia hatua ya upofu. Kila kinachofanywa na mtu wa ccm hakina maana. Ofisi ile ya mhe. makamba ni ya kuibua miradi na kutafuta wafadhili sasa mlitaka ikae Bumbuli halafu iweje? Kwani ile mmeambiwa ni ofisi ya mbunge! Tukianza kuulizana ooh! huyo kaiba akiwa ikulu, ooh babake mwizi. Nasisi tukiuliza utajiri wa wachaga wameupata wapi na cdm yao?!
 
ofisi ya maendeleo ya bumbuli ndani ya water front Dar es salaam? kwamba huu nao ni ubunifu, acheni masihara! wazee wa kisambaa kutoka bumbuli wanaruhusiwa kweli kuingia kwenye hiyo ofisi? hizi ni mbwembwe na maonyesho ya ukwasi tu. ofisi hiyo kama ina nia hiyo kweli ilipaswa kuwa huko huko bumbuli na vijana wa kishambaa ndiyo waidhibiti ili kufanya two-flow of information i.e kutoka kwa mbunge kwenda kwa wasambaa and vice versa.
 
Bangöö, mm sio wakala wa mafisadi, ninapenda mageuzi ya kifikra na kimfumo ambayo mwisho wa siku utatuletea maendeleo.

Kijana wangu Mh Silinde kutokuwa na gari wala m 1 sio ishu hapa, kufanya kazi ikulu sijui baba yake alikuwa nani sio hoja pia. Hoja ni kuwa ameweza kuwa na strategic ofc in a strategic place kutarp in resources kwa ajili ya maendeleo jimboni kwake. Hapa mjin kuna facility mtu anazohitaji at modest level kuweza kufanya anacho taka.

Hata mkinipiga mawe lakn naona kuwa tu na hi vision ni hatua ya muhimu sana, lakn ukweli utabaki ofs hi imezalisha nin kwa ajili ya watu wa Jimbo la Bumbuli. Hi ndo hoja ambayo tunapaswa kutembea nayo, lakn ameanza vizuri na ninamsuport. Kuna wengne wanasema angeanzisha ofs kule Bumbuli, hili sina data kama kule hakun ofs, lakn fikiria awe na ofs kubwa kule Bumbuli, kuna dev partner wana tight schedules utawakalisha wapi kwa muda mfupi kuwaonyesha mambo ya kwenu ili wakupe suport bila kuwaharibia ratiba zao.Mh Makamba hi mm nakuunga mkono.

Changamoto: ofs kama ile imeshazalisha nn? Hili ndo swali tunalopaswa kuhoji mwisho wa siku. Kama hakuna kitu fo 3yr basi amekula hasara na maono yake ameshindwa kuyatimiza ingawa alianza vizuri

@ KIRESUA

Hiyo paragragh yako ya mwisho ungeifanyia kazi kwanza kabla ya kumwagia sifa hizo si unajua watoto wa mjini wanaishi kimjini mjini sasa isije ikawa ndio penye ofisi yake kwa ajili yake.


 
kipi cha maana kilichokurusha roho pale? ni zile picha za maskini wa bumbuli zinazotumika kutafuta sympathy kwa wahisani wakati wa kuomba misaada na wingi wa vitabu kwenye shelfu?

au niile view ya bahari?

Miradi na misaada kupitia january makamba ni deal binafsi hasa baada ya kufanya lile alilofanya juu ya fedha za msaada kutoka kwa yule dada wa familia ya ROCA FELA.

Since huyu jamaa kaonyesha unafiki kwenye swala la kuwawajibisha mawaziri naamini ni ni mchumia tumbo na ni kijana asiye na kifra huru milele hata kama angekuwa na ofisi mawinguni.

Ni wazi wengi waliochangia hii mada ni CDM damu halafu wafupi wa uelewa, mleta mada kaweka wazi nami nakubaliana nae kwamba alivyofanya JM ni kitu kizuri bila kuleta ushabiki wa chama yaani;
1. Kuanzisha ofisi ya maendeleo ya jimbo, ni wabunge wangapi wamefanya hivyo aidha wa CCM au CDM?
2. Kuanzisha free no ili wananchi wake waweze kumtumia kero zao bure kwa kutumia SMS wangapi wanayo hiyo?
3. Wabunge wangapi CDM au CCM wametumia hela zao za mikopo ya magari kuanzisha kitu ambacho wanatarajio kitongeza chachu ya maendeleo jimboni mwao?

Ni vema kama kina sie ambao hatujafungana upande wowote tunaangalia mambo kwa mapana zaidi kuliko kuwa kipofu wa kila kitu cha CCM au CDM hakifai sababu tu kimeanzishwa na mpinzani wako, kweli umaskini wa fikra mbaya sana.

Suala sasa kama ile ofisi ina tija ndio hoja, lakini wazo ni zuri nami pia lanipongeza ingawa hiyo shoo sikuiona.
 
Aliyekuambia wabunge wa CDM hawana taasisi wala office ni nani! Tena hizo oofice ziko majimboni kwani Mbumbuli na mtaa gani hapo Dar!
 
Tukisema kwamba ni mbunge pekee aliyetumia technolojia kujiweka mbali na wapiga kura wake itakuwaje. Think critically guy.
 
mleta mada usiwe mwepesi kudanganywa.........ile ofisi ni ya kawaida sana..

jamaa labda amepewa kitu kuja kupima upepo yeye anasifia ile ofisi hajaona nyumba anyoishi ni ya kiasi gani kuna mtandao fulani waliweka sherehe ya ufunguzi wa nyumba yao ya mabilioni ngoja niitafute halafu niwaletee
 
Ni wazi wengi waliochangia hii mada ni CDM damu halafu wafupi wa uelewa, mleta mada kaweka wazi nami nakubaliana nae kwamba alivyofanya JM ni kitu kizuri bila kuleta ushabiki wa chama yaani;
1. Kuanzisha ofisi ya maendeleo ya jimbo, ni wabunge wangapi wamefanya hivyo aidha wa CCM au CDM?
2. Kuanzisha free no ili wananchi wake waweze kumtumia kero zao bure kwa kutumia SMS wangapi wanayo hiyo?
3. Wabunge wangapi CDM au CCM wametumia hela zao za mikopo ya magari kuanzisha kitu ambacho wanatarajio kitongeza chachu ya maendeleo jimboni mwao?

Ni vema kama kina sie ambao hatujafungana upande wowote tunaangalia mambo kwa mapana zaidi kuliko kuwa kipofu wa kila kitu cha CCM au CDM hakifai sababu tu kimeanzishwa na mpinzani wako, kweli umaskini wa fikra mbaya sana.

Suala sasa kama ile ofisi ina tija ndio hoja, lakini wazo ni zuri nami pia lanipongeza ingawa hiyo shoo sikuiona.

WaMzizima
1. Nenda Hai, utakuta ofisi ya maendeleo iliyoanzishwa na Mbowe pia hapa arusha ofisi ya maendeleo imeanzishwa na lema na imejikita zaidi kusomesha zaidi ya watoto 800 wasio na uwezo na mikopo kwa kina mama wenye mazingira magumu, nenda Kigoma tagundua Zito alichofanyia kupitia mkopo uwo n.k.
2.free number kuwasiliana na wananchi ni layman solution kwani hakuwaomba kura kupitia simu, na pia angekuwa anazingatia izo sms za wapiga kura asingeonyesha chuki na dharau juu ya swala la kutokua na imani na waziri mkuu(Jambo ambalo hata JK amekiri kufurahishwa kwani anajua wananchi wanahitaji nini)
3.Kuhusu mkopo wa gari anza kufuatilia Filikonjombe alichokifanya kupitia mkopo uwo, Lema alichokifanya bila kumsahau ndesamburo alichokifanya kupitia mkopo uwo.

Juu ya swala hili sifungamani na chama chochote ila nakosa imani na mradi wowote wa January Makamba kwani alishawai kuomba msaada wa kujenga hospitali mkoani mbeya lakini akatafuna pesa hizo na mhisani mwanadada ambaye ni mwanafamilia ya Roca Fela alipokuja Tz kutazama hospital hiyo aliambulia kituko cha mwaka na alipomuuliza Makamba alimtukana matusi ya nguoni bila kutoa ufafanuzi wowote.

Point yangu ni kwamba, hata kama wazo ni zuri bado limeanzishwa na mwizi aliyekula fedha za mradi wa hospital na kuwaacha mamilioni ya waTZ wakitaabika. Ni kipi kitakachomzuia kuiba fedha za misaada ya miradi kama alivyofanya awali??????????????
 
mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Mhe kweli ana ofisi nzuri; lakini lile swala la kutumia pesa za kununulia gari kufungulia ofisi si matumizi kinyume na makusudio yake? hilo sio kosa jamani? si ndo matumizi mabaya yanaanza kidogo, kesho mkimpa hela ya kufungua kiwanda anajenga hoteli...
 
Januari makamba alipata pesa za wapora nchi wakati akijiandaa kugombea ubunge,ni kuhadi wa wawekezaji na walarushwa uku akijidai kuwa ni mzalendo mwenye uchungu na nchi yake.Muulizeni makubaliano yake na zitto kabwe uku wakitegemea wazungu ili watawale Tanzania kwa madai ya kutoa sehemu ya nchi iliyo na rasilimali kama asante kutokana na mchango wao wa kuwawezesha kuchukua dola au watu wao wakaribu kuchukua nchi
 
anasubiri ile dola 1 M aliyoombewa na dada yake mwamvita kwa shemeji yake, sijui kama ataipata maana hajaukwaa u waziri wa nishati
 
Halow Wana JF,

Punde nilikuwa naangalia Original Comedy, nikaona Masanja akimtembelea Mh. J.Makamba kwenye ofisi yake iliyo jengo la NSSF Water Front. He has an excellent office there. Ni ofisi ya maendeleo ya watu wa jimbo la Bumbuli.

I was so amazed kusikia alipopata ule mkopo wa gari alitafuta ofisi akaajiri vijana kwa ajili ya kutafuta fedha za maendeleo jimboni Bumbuli!

Mm ni Nimemkubali huyu jamaa, wachumia tumbo mjifunze hapa. Wabunge wangu wa CDM, tujifunze hapa tuige yalio mazuri.

Big up Hon J. Makamba.

Ofisi ya maendeleo ya Bumbuli kwa nini ipo Dar?????
 
Back
Top Bottom