NOT FOUND
Senior Member
- Mar 14, 2011
- 158
- 59
Habari zenu wana J.F
Wiki iliyopita nilikuwa Bumbuli jimboni kwa ndg Makamba, kwa kweli niliyoyakuta huko ni mambo ya ajabu.
Bumbuli ni sehemu ambayo naifahamu vilivyo kutokana na kuishi huko miaka kadhaa wakati nikisomea Medical Assistant pale COTC na Baadae kufanya kazi Bumbuli Hospital.
cha kwanza barabara ya kufika huko ni mbaya huwezi ukaamini, yaani wakati wa mvua huwa gari zinaishia umbali wa kilometa 30, kutoka bumbuli stend katika eneo la Soni.
Pia kuna shida ya maji utadhani ni jangwani, jimbo hili lina mito na chem chem kila kona lakini sasa hivi chem chem zote zimekufa kutokana na ukataji wa miti uliokithiri, na hata mto mkubwa uliopo haujafanyika utaratibu wowote wa kuvuna maji ya kuwasaidia wananchi.
Baada ya kukupa hiyo intro fupi, sasa twende upande wa pili wa niliyoyakuta kuhusu ndugu Januari.
Kwanza kabisa huyu jamaa mara baada ya kupitishwa (HAKUPIGIWA KURA KWA KUWA ALIKUWA PEKE YAKE) kuwa Mbunge, alihamisha ofisi ya mbunge kutoka Bumbuli na Kuipeleka Soni, tafsiri ya wengi hapa ni kwamba amekimbia kukaa na wananchi wake kwani Bumbuli ni katikati ya Mgwashi na Soni tarafa ambazo pia ni sehemu ya Jimbo hili.
ikumbukwe kwamba tangu kuanzishwa kwa jimbo la Bumbuli miaka zaidi ya 15 iliyopita, ofisi ya Mbunge ilikuwa pale pale Bumbuli, lakini ndg Januari alipochukua ubunge akaamua kuihamisha na kuipeleka sehemu ambapo access na wananchi wake ni ndogo sana.
Suala la pili ambalo nimelipata kutoka kwa vijana wengi waliokuwa wakimpigia debe Januari wakati wa kura za maoni, ni kwamba Ndg Januari ameanza kujivuna kupita maelezo, kiasi kwamba wale vijana ambao alikuwa nao bega kwa bega usiku kucha katika kuhakikisha kwamba mzee Shelukindo anang'oka, aliwatupilia mbali.
Katika kulithibitisha hili, Ndg Januari alitembelea vijiji vilivyoko maeneo ya jirani na pale wanapotoka (Mahezangulu), wakati anaondoka, alipopita Bumbuli, alijidai kasinzia kwenye gari ili asiweze kusalimiana na wananchi ambao kipindi cha nyuma alikuwa na mazoea kusalimiana nao.
Zaidi ya hayo jamaa hana mikakati yoyote ya Maendeleo kwa jimbo lake, vijana wengi wameponda utaratibu alioanzisha wa kuwasiliana na wananchi wake kwa namba ya simu hizi za kutuma ujumbe kwenda 15***, pamoja na kuwasiliana nao kwa kupitia website kwa kuwa sehemu kubwa ya wananchi wake ni masikini ambao hawana hata umeme na hata mtandao wa simu kupatikana ni kwa shida.
Pia imedaiwa kwamba ndg Januari amekuwa akitembelea shule zilizopo ndani ndani na kuishia kukagua madaftari ya wanafunzi badala ya kuhakikisha anaanzisha utaratibu wa upatikanaji wa vitabu na walimu.
Pia kubwa lingine ambalo wananchi wamemponda na kuanza kumchoka ni kwamba, baada ya kuapishwa kuwa mbunge, hajawai hata kujitokeza kuwashukuru wananchi wake kwa kuamua kumuunga mkono, jambo hili limewakera vijana na wazee wengi wa jimbo la Bumbuli kiasi cha kusema kama ataendelea hivi hivi asahau kuchaguliwa tena mwaka 2015.
Vijana wengi ambao walimpachika jina la Obama wa Bumbuli, sasa hivi wameanza kumpa majina mengi kama Shalo Baro, Brazamen, Bishoo n.k, kutokana na kitendo chake cha "kuwapotezea" na "kujidai"
KUFUATIA MAMBO HAYA YALIYOJITOKEZA, KUBWA LIKIWA LA KUHAMISHA OFISI, KUWACHUNIA WANANCHI, NA KUTOKWENDA KUTOA SHUKRANI, LIMEIBUKA KUNDI KUBWA LA VIJANA AMBAO WAPO KWENYE MCHAKATO WA KUMWANDIKIA BARUA MWENYEKITI WA CHADEMA MH. MBOWE PAMOJA NA KATIBU MKUU DR. SLAA, ILI WAWAPE SUPPORT YA KUFUNGUA TAWI LA CHADEMA BUMBULI, VIJANA WENGI WALISIKIKA WAKISEMA "TATIZO SIO SHELUKINDO, TATIZO SIO JANUARI, TATIZO NI CCM"
MY TAKE:
INGAWA MIMI SIO MZALIWA WA BUMBULI, LAKINI KWA KUWA BUMBULI NI SEHEMU AMBAPO NIMEISHI NA KUFANYA KAZI, NIMEKERWA NA KITENDO CHA NDUGU JANUARI KUWASUSA WANANCHI WAKE, HUKU AKISIKIKA KWENYE VYOMBO VYA HABARI KUHUSIANA NA SUALA LA DOWANS NA TANESCO, PAMOJA NA LILE LA KUHAMISHA OFISI ILI ASIWEZE KUSIKILIZA MATATIZO YA WANANCHI WA BUMBULI.
NAWAPA SUPPORT VIJANA WALIOAMUA KUANZISHA MCHAKATO WA KUFUNGUA TAWI LA CHADEMA BUMBULI, KWA KUWA NDUGU JANUARI AMESHAONA YA KWAMBA UWAKILISHI WAKE KWA WANA BUMBULI, HAUNA UPINZANI KWANI HATA KUSIMAMA KWENYE UBUNGE ALIKUWA MGOMBEA PEKEE ALIYEPITA BILA KUPINGWA.
Wiki iliyopita nilikuwa Bumbuli jimboni kwa ndg Makamba, kwa kweli niliyoyakuta huko ni mambo ya ajabu.
Bumbuli ni sehemu ambayo naifahamu vilivyo kutokana na kuishi huko miaka kadhaa wakati nikisomea Medical Assistant pale COTC na Baadae kufanya kazi Bumbuli Hospital.
cha kwanza barabara ya kufika huko ni mbaya huwezi ukaamini, yaani wakati wa mvua huwa gari zinaishia umbali wa kilometa 30, kutoka bumbuli stend katika eneo la Soni.
Pia kuna shida ya maji utadhani ni jangwani, jimbo hili lina mito na chem chem kila kona lakini sasa hivi chem chem zote zimekufa kutokana na ukataji wa miti uliokithiri, na hata mto mkubwa uliopo haujafanyika utaratibu wowote wa kuvuna maji ya kuwasaidia wananchi.
Baada ya kukupa hiyo intro fupi, sasa twende upande wa pili wa niliyoyakuta kuhusu ndugu Januari.
Kwanza kabisa huyu jamaa mara baada ya kupitishwa (HAKUPIGIWA KURA KWA KUWA ALIKUWA PEKE YAKE) kuwa Mbunge, alihamisha ofisi ya mbunge kutoka Bumbuli na Kuipeleka Soni, tafsiri ya wengi hapa ni kwamba amekimbia kukaa na wananchi wake kwani Bumbuli ni katikati ya Mgwashi na Soni tarafa ambazo pia ni sehemu ya Jimbo hili.
ikumbukwe kwamba tangu kuanzishwa kwa jimbo la Bumbuli miaka zaidi ya 15 iliyopita, ofisi ya Mbunge ilikuwa pale pale Bumbuli, lakini ndg Januari alipochukua ubunge akaamua kuihamisha na kuipeleka sehemu ambapo access na wananchi wake ni ndogo sana.
Suala la pili ambalo nimelipata kutoka kwa vijana wengi waliokuwa wakimpigia debe Januari wakati wa kura za maoni, ni kwamba Ndg Januari ameanza kujivuna kupita maelezo, kiasi kwamba wale vijana ambao alikuwa nao bega kwa bega usiku kucha katika kuhakikisha kwamba mzee Shelukindo anang'oka, aliwatupilia mbali.
Katika kulithibitisha hili, Ndg Januari alitembelea vijiji vilivyoko maeneo ya jirani na pale wanapotoka (Mahezangulu), wakati anaondoka, alipopita Bumbuli, alijidai kasinzia kwenye gari ili asiweze kusalimiana na wananchi ambao kipindi cha nyuma alikuwa na mazoea kusalimiana nao.
Zaidi ya hayo jamaa hana mikakati yoyote ya Maendeleo kwa jimbo lake, vijana wengi wameponda utaratibu alioanzisha wa kuwasiliana na wananchi wake kwa namba ya simu hizi za kutuma ujumbe kwenda 15***, pamoja na kuwasiliana nao kwa kupitia website kwa kuwa sehemu kubwa ya wananchi wake ni masikini ambao hawana hata umeme na hata mtandao wa simu kupatikana ni kwa shida.
Pia imedaiwa kwamba ndg Januari amekuwa akitembelea shule zilizopo ndani ndani na kuishia kukagua madaftari ya wanafunzi badala ya kuhakikisha anaanzisha utaratibu wa upatikanaji wa vitabu na walimu.
Pia kubwa lingine ambalo wananchi wamemponda na kuanza kumchoka ni kwamba, baada ya kuapishwa kuwa mbunge, hajawai hata kujitokeza kuwashukuru wananchi wake kwa kuamua kumuunga mkono, jambo hili limewakera vijana na wazee wengi wa jimbo la Bumbuli kiasi cha kusema kama ataendelea hivi hivi asahau kuchaguliwa tena mwaka 2015.
Vijana wengi ambao walimpachika jina la Obama wa Bumbuli, sasa hivi wameanza kumpa majina mengi kama Shalo Baro, Brazamen, Bishoo n.k, kutokana na kitendo chake cha "kuwapotezea" na "kujidai"
KUFUATIA MAMBO HAYA YALIYOJITOKEZA, KUBWA LIKIWA LA KUHAMISHA OFISI, KUWACHUNIA WANANCHI, NA KUTOKWENDA KUTOA SHUKRANI, LIMEIBUKA KUNDI KUBWA LA VIJANA AMBAO WAPO KWENYE MCHAKATO WA KUMWANDIKIA BARUA MWENYEKITI WA CHADEMA MH. MBOWE PAMOJA NA KATIBU MKUU DR. SLAA, ILI WAWAPE SUPPORT YA KUFUNGUA TAWI LA CHADEMA BUMBULI, VIJANA WENGI WALISIKIKA WAKISEMA "TATIZO SIO SHELUKINDO, TATIZO SIO JANUARI, TATIZO NI CCM"
MY TAKE:
INGAWA MIMI SIO MZALIWA WA BUMBULI, LAKINI KWA KUWA BUMBULI NI SEHEMU AMBAPO NIMEISHI NA KUFANYA KAZI, NIMEKERWA NA KITENDO CHA NDUGU JANUARI KUWASUSA WANANCHI WAKE, HUKU AKISIKIKA KWENYE VYOMBO VYA HABARI KUHUSIANA NA SUALA LA DOWANS NA TANESCO, PAMOJA NA LILE LA KUHAMISHA OFISI ILI ASIWEZE KUSIKILIZA MATATIZO YA WANANCHI WA BUMBULI.
NAWAPA SUPPORT VIJANA WALIOAMUA KUANZISHA MCHAKATO WA KUFUNGUA TAWI LA CHADEMA BUMBULI, KWA KUWA NDUGU JANUARI AMESHAONA YA KWAMBA UWAKILISHI WAKE KWA WANA BUMBULI, HAUNA UPINZANI KWANI HATA KUSIMAMA KWENYE UBUNGE ALIKUWA MGOMBEA PEKEE ALIYEPITA BILA KUPINGWA.