Mh Godbless Lema amjibu Tendwa

Mh Godbless Lema amjibu Tendwa

Napata wasiwasi na uwezo wako wakuchambua mambo, ni mdogo mno kuzidi hata punje ya mchanga !


Wewe sio Genius brain bali ni" Brain washed Genius" wacha watu makini wachambue hoja makini.

Jiulize maswali yafuatayo tafadhali,.
* Hivi wazee wa kimila wanakubalika katika kifungu gani cha katiba ya nchi yetu,ambacho kinawapa mamlaka ya kisheria kuingilia mchakato wa uchaguzi nchini na kuzuia watu kupiga kampeni?.
* Je kitendo walichokifanya, "tishio la kuua".inakuwaje wameendelea kuwa huru,tena wakisaidiwa na watendaji waandamizi kama Tendwa badala ya kuwa Mahabusu wakisubiri mashtaka yao? .
* Je wazee hawa ambao bila shaka ni wa ccm,wana uhakika gani kwamba wanawakilisha wameru wote na si wana ccm peke yao?
Naiomba serikali ichukuwe hatua mapema kuwakamata hao INTERAHAMWE wa kimeru,na wawajibishwe kabla ya madhara kutokea.

Kama ccm ni chama cha kistaarabu ni vema mkachukuwa hatua sasa ya kuikemea kauli hii,kama hili halikufanyika basi tutajuwa kuwa hii ndio mpango mzima wa ccm kumuuwa lema ili mumrudishe mbunge wa ccm jimboni Arusha mjini.
 
Hii ni sawa kushangilia goli la moja ya timu kwenye mechi anayochezesha.

MH.TUNDU A LISU NINAOMBA UCHAMBUE KIFUNGU CHA KATIBA YA JMT KUHUSU UKABILA NA MAHUSIANO YA MILA NA CHAGUZI MBALIMBALI ILI KUKOMESHA WATU WENYE VIHEREHERE NA PESA HARAMU.MBONA MILA ZIPO NYINGI TU TZ.Halafu mbona watu wana roho za kutu?
 
Jamani kwa propaganda hii ya tendwa inaonesha kabisa ni msaidizi wa nape na wanafanya kazi moja au nyie mnaonaje?
 
Ni naibu wake siyo kaimu. Alikuwa underground sasa katokea kumsaidia bosi wake.
 
Maji yakizidi unga lazima utumie silaha za msaada! inaonekana Tendwa sasa kaanza kutumika!
 
Hivi huyu Yohana Tendwa siku hizi 'kazaliwa upya' na kugeuka kuwa ndiye Campaign Manager wa CCM mkoani sio?

Ngoja vijana waende kumuonyesha maana halisi ya Nguvu ya Umma ni nini pale AruMeru Mashariki kwao na akina Marehemu Nkoo ndio atajua somo kutochanganya siasa na shughuli za ki-serikali siku nyingine.

Vijana wenzetu hapo AruMeru;
KULA KWA CCM lakini KURA KWA CHADEMA Nguvu ya Umma na chama kitetezi cha maslahi ya wanyonge Tanzania.
 
Wana JF kitendo cha Msajili wa vyama vya siasa Jonn Tendwa kazungumza na Waandishi wa habari na kusema kuwa katika tathimini yake katika uchaguzi wa Arumeru Wazee wa kimila wamemwambia kuwa wanamwonya Lema asiende kwenye kampeni eti watamuuwa kauli hii imenisikitisha kama si kunishangaza kuwa Tanzania kuna tatizo gani?.

Hii bila kumumunya maneneo ni makakati wa ndani wa CCM wa kuandaa mazingira ya vurugu ili ikionekena CCM inashindwa waanzishe vurugu katika kampeni ili watu waumizwe waogope kwenda kupiga kura.

Hili naomba CHADEMA wajiandae mapema . Haingii akilini mtu wa heshima kama msajili wa vyama kuongelea vitu vya vurugu kutoka kwa watu wa kimila waabudu mizimu na wasiomjua Mungu. Nasema hakika haya mnayofanya laana ya Mungu na damu zitakazo mwagika bila hatia itakuwa juu yako na familia yako na vizazi vyako.

Mimi nadhani wazee hawa ilikuwa ni wakati wa kujenga Tanzania yenye amani zaidi kwa kuweka mazingiza ya watu kushindana kwa hoja na kwa amani ili ichi yetu ambayo imepata heshima kubwa iendelee kuwa nchi ya amani.

Tuachane na mawazo mgando kuwa ni lazima nyie muendelee kutawala na kutumia mbinu hata zisizofaa jamani tuamke watu wa aina ya Tendwa ni ukoma kwa Taifa.
Huyu Tendwa kwanza muda wake wa kukitumikia CCM ulishakwisha akaongezewa, so anabwabwaja tu na kujitanua na sifa za ajabu ooh ati ana mamlaka, je, mamlaka ndo ya kuongea utumbo kama huu? Isitoshe hawa wazee ni kina nani mpaka kutishia LEMA asiende ku-kampeni ARUMERU? na je, ni idadi ya wazee wote ama group ya wahuni fulani waliopewa hongo na mafisadi ionekane ni tamko la wazee wa ARUMERU? Je, kutishia maisha ya LEMA kuwa watamuua hadharani kama hivyo, si ni kuharaisha kuwa wao ni wauaji na yeyote wasiemtaka kijijini ama wilayani ARUMERU wanamuua. Hapa nadhani jeshi la polisi (ambalo sina imani nalo) limepewa clue fulani ya kiuchunguzi, wafuatilie wazee hao na connection na mauaji ya watu hapo ARUMERU. Huenda wengi wameshauwawa na hao wazee ama vijana wao kwa kuwa hawakubaliani nao kimtazamo na hata kwa lugha za kupishana tu kama ambavyo wamnataka kufanya kwa LEMA. Isitoshe kwa taarifa hii basi JESHI la polisi ni nafasi kwao sasa kuhakikisha LEMA natimiza haki yake ya msingi kikatiba ku-kampeni ARUMERU salama salimin toka mwanzo wa kampeni hadi mwisho. Na hawa wazee wakamatwe maana wametishia kuondoa uhai wa mtu wakafundishwe adabu mahabusu. Siyo finally LEMA ndo aje akamatwe eti kalazimisha kwenda ARUMERU na alishaonywa asiende hivyo kuwa chanzo cha vurugu 9Justifications amabzo zitakuwa ni za kipuuzi.
 
Nimeamini kuwa Lema tishio. Pinda anmwogopa,Makinda naye hana hamu naye,bado RC,RPC na OCD Arusha yeye ni homa kwao. Sasa CCM nayo inataka kumdhuru kwa kisingizio cha washili maana inajua vizee vile hata vikisingiziwa haviwezi kuitisha press na kukanusha kauli ya Mzito(lakini mzigo)kama Tendwa. Kweli Lema kiboko ya watawala waovu.Hebu aguswe waone moto wake
 
Mwenyekiti wa chama,eti anasimama na kusema kitengo cha propaganda ni muhimu katika chama,dunia ya leo unasifia propaganda?hawa jamaha kweli vichekesho!
 
Kama kweli Tendwa katamka hayo this is good news kwa Lema na CDM but bad news kama kweli Lema atadhurika. Tendwa anawajua wauaji wa Lema, sasa basi pindi lema akidhurika Arumeru Tendwa ni shahidi namba moja katika hili. Sumu huwa haionjwa kwa kulambwa, tusichezee amani iliyopo kwani ni vigumu sana kurejesha amani kama ilivyo rahisi kuivunja.

Amani si watu kuishi na kwenda sokoni, Amani ni mentality ya watu. Ukiisha mjeruhi mtu kisaikolojia kwa kumuulia ndugu yake ujue jeraha lake halisahauliki mpaka nae anaingia kaburini. Sasa atafanya nini kutafuta haki ya nduguye hicho ni kitendawili kitakachotufanya wote tutembee tukiwa hatuaminiani. Tusielekee huko, uchaguzi wa mbunge usiwe ni TRIGGER ya kuwasha moto wa chuki na visasi miongoni mwa watanzania bali uwe ni nyota ya kujenga umoja na mshikamano.

Haiingii akili mtu aliyepewa dhamana ya kuongoza umma kama Tendwa kuongelea uwezekano wa kutoa uhai wa mtu hadharani ili tu aonekane kuwa ni kada mzuri wa CCM. Huu ukada wa CCM ndiyo unaofanya leo hii watu wanapigwa risasi na polisi na kuuwawa bila mtu yeyote kuwajibika. Yaani CCM limekuwa chaka la kufichia uovu wa watu. One day one day one day tutalia na kusaga meno bila kujua kuwa 'sisi tukisema amani ya nini wenzako wanasema wataipata lini'
 
Wana JF kitendo cha Msajili wa vyama vya siasa Jonn Tendwa kazungumza na Waandishi wa habari na kusema kuwa katika tathimini yake katika uchaguzi wa Arumeru Wazee wa kimila wamemwambia kuwa wanamwonya Lema asiende kwenye kampeni eti watamuuwa kauli hii imenisikitisha kama si kunishangaza kuwa Tanzania kuna tatizo gani?.

Hii bila kumumunya maneneo ni makakati wa ndani wa CCM wa kuandaa mazingira ya vurugu ili ikionekena CCM inashindwa waanzishe vurugu katika kampeni ili watu waumizwe waogope kwenda kupiga kura.

Hili naomba CHADEMA wajiandae mapema . Haingii akilini mtu wa heshima kama msajili wa vyama kuongelea vitu vya vurugu kutoka kwa watu wa kimila waabudu mizimu na wasiomjua Mungu. Nasema hakika haya mnayofanya laana ya Mungu na damu zitakazo mwagika bila hatia itakuwa juu yako na familia yako na vizazi vyako.

Mimi nadhani wazee hawa ilikuwa ni wakati wa kujenga Tanzania yenye amani zaidi kwa kuweka mazingiza ya watu kushindana kwa hoja na kwa amani ili ichi yetu ambayo imepata heshima kubwa iendelee kuwa nchi ya amani.

Tuachane na mawazo mgando kuwa ni lazima nyie muendelee kutawala na kutumia mbinu hata zisizofaa jamani tuamke watu wa aina ya Tendwa ni ukoma kwa Taifa.

Hapo peny red, hivi ni kweli au umetolea mfano tu kuwa alistahili kuwa hivyo!
 
TENDWA hajui alitendalo.Anajimwagia tindikali bila kujua,asubiri matokeo yake mda si mrefu!!
 
MAAGIZO YA VIJANA WA TANZANIA KWA KAMANDA LEMA:
KWA KUSHIRIKIANA NA
'WASHIRI-CHADEMA' NENDA ARUMERU MASHARIKI KUWAFIKISHIA SALAAM ZA KUPIGANIA KUREJESHWA KWA 'HAKI, HESHIMA NA UTU WA KILA MTANZANIA'


Hakika Vijana wote nchini Tanzania nawapeni HEKO SANAAAAAAAAAAAAAAAA kwa kumfanya kijana mwenzetu Mhe Kamanda Gobless Lema, Mbunge wa Arusha Mjini, kwa kumfanya huyu mwenzetu awe ni mtu wa kukinyima usingizi kila kiongozi wa MAGAMBA pamoja na maafisa wa serikali ma-kada kama Yohana Tendwa.

Kimsingi, huyu kijana mwezetu wala hatumheshimu kwa kitu pesa alizo nazo mfukoni maana kiukweli fedha bado hana; na wala vijana hatujachagua kumheshimu huyu kijana mwenzetu kwa kuwa na cheo tu cha ki-bunge maana wapo wengi tu wenye vyeo vikubwa zaidi ya hiyo tena wanaolipwa
Tshs 20,000,000/- na miposho zaidi juu (Kafulila et al).

Naam, nasema Machalii wote Tanzania hatujachagua kumheshimu na kumpa ufuasi uliotukuka Kamanda Lema shauri ya usomi wowote maana kama ni usomi tu tunao Ma-Profesa kibao nchini lakini wanajificha mbele ya dhuluma tunaofanyiwa wanyonge wa nchi hii huku wao wakiendelea kuvuta kuku kwa mrija hata bila ya kujali vijana wa nchi hii hali yetu ikoe.

Hakika, kuna kitu cha kipekee mno kile kinachomfanya Kamanda Lema nyota yake ang'ae mpaka kuwatikisa Ma-Washiri CCM huko AruMeru, kila alichonacho huyu kijana mwenzetu ambacho Mamilionea wenye fedha za kukwapua kama Lowassa hawana.

Ndio, nasema kuna kitu kikubwa sana chenye upekee kinachomfanya wanyonge wa nchi hii wamkubali Kamanda Lema na kumkataa Msomi kama Dokta Bana anayeonekana kuwa ni mfano hai wa wasomi wanaokubaliana na wadhulumishi wa nchi hii kwa kila kitu ilmradi tu mkono uende kinywani mwakwe.

Wala sio siri tena kwamba kwetu sisi vijana kumtii kule huyu kijana mwenzetu maneno yake na kumpuuza Waziri Ngeleja yoooote haya yanatokana na kitu kidogo sana lakini chenye upekee mno katika uhai na mustakabali mzima wa taifa letu leo na kesho.

Ni kweli, kwake huyu Kamanda Lema kwamba vijana tunatambua kitu lulu, kuaminika, kutegemeka na thamani kubwa iliomo ndani ya KILE ANACHOSIMAMIA NA KUIAMINI KWANIABA NA FAIDA YA WANYONGE kutufariji wakati wote wa shida na dhuluma zisizoisha kote nchini

Kwake yeye Kamanda Lema, bila kitu KUJIKWEZA, vijana wenzake tunatambua dhahabu ya ajabu mno katika ule ujasiri wake wa kutete Maslahi ya Umma kwa kuzingatia misingi ya ile falsafa ya KUREJESHWA KWA HESHMA, HAKI NA UTU WA MTANZANIA.

Hadi hapo sasa, Kamanda Lema, kwa maagizo yetu sisi vijana wa nchi hii tunaodhulumiwa sana, tunaoporwa sana rasilmali zetu na vile vile kila mara KUPOKONYWA HAKI ZETU ZA KUJICHAGULIA VIONGOZI TUNAOWAPENDA SISI WENYEWE, hivi sasa tunakuagiza kupitia chama chetu makini CHADEMA uongozi timu ya kukata na shoka kwenda AruMeru Mashariki kusaidiana na Wapiganaji wenzetu wakazi wa pale kuendesha kampeni ya kufa mtu, chumba hadi chumba hadi kiongozi wa kweli wa wananchi kupatikana bila rushwa!!

Kazi iendelee na utetezi wa haki za sisi wanyonge iwe mbeeeeeeeeele kama tai!!
 
'WASHIRI-CHADEMA NA SISI VIJANA SASA 'KUPIGA KURA KWA FUJO' KUMUUMBUA SHETANI YA MAGAMBA NA MBUYU WAKE UFISADI NCHINI

Kwa uwezo Mwenyezi Mungu atutiae nguvu, vijana sasa 'tunapiga kura kwa fujo' kuumbua shetani, kuandika vizuri historia AruMeru Mashariki huku tukiongozwa na kazi murua wa Kamanda Lema kwa kushirikiana kwa karibu sana na
'Washiri-CHADEMA' ili kumuumbua huyu naibu wa Nape, Ndg Yohane Tenwa.

Azma yetu hii mpya inatokana na ukweli kwamba hata siku moja 'Washiri-CCM' hawajawahi kuteuliwa na Wameru ili wawe wazungumzaji wa 'Washiri-CHADEMA' kupitia kwa Afisa Mwandamizi mpya na Kada wa chama hicho kwa cheo kipya cha Naibu Afisa wa Itikadi na Uenezi CCM, Bw Yohane Tendwa.
 
'WASHIRI-CHADEMA' NA SISI VIJANA SASA 'KUPIGA KURA KWA FUJO' KUMUUMBUA SHETANI YA MAGAMBA NA MBUYU WAKE UFISADI NCHINI

Kwa uwezo wake Mwenyezi Mungu atutiae nguvu, vijana sasa 'tunapiga kura kwa fujo' kuumbua shetani, kuandika upya na vizuri zaidi historia pale AruMeru Mashariki hivi karibuni.

Naam, vijana kote nchini tunadhamiria kufanya hivi huku tukiongozwa na kazi murua wa Kamanda Lema kwa kushirikiana kwa karibu sana na
'Washiri-CHADEMA' ili kumuumbua huyu naibu wa kujitolea wa Nape, Ndg Yohane Tenwa.

Azma yetu hii mpya inatokana na ukweli kwamba hata siku moja 'Washiri-CCM' hawajawahi kuteuliwa na Wameru ili wawe wazungumzaji wa 'Washiri-CHADEMA' kupitia kwa Afisa Mwandamizi mpya na Kada wa chama hicho kwa cheo kipya cha Naibu Afisa wa Itikadi na Uenezi CCM, Bw Yohane Tendwa.

Jamani kwa propaganda hii ya tendwa inaonesha kabisa ni msaidizi wa nape na wanafanya kazi moja au nyie mnaonaje?

Ni naibu wake siyo kaimu. Alikuwa underground sasa katokea kumsaidia bosi wake.
 
Back
Top Bottom