Mh Godbless Lema amjibu Tendwa

CDM msituletee umwagaji damu kama mlivyofanya Igunga. Amani mliyoikuta Meru iacheni.

Inaonekana mmeanza kutapatapa, ... na bado....jimbo la ARUMERU mtalisikia redioni kama ilivyokuwa kwa majimbo mengine ya Igunga na Uzini.

Ama kweli, CDM ni full shari.
 
CDM msituletee umwagaji damu kama mlivyofanya Igunga. Amani mliyoikuta Meru iacheni.

Inaonekana mmeanza kutapatapa, ... na bado....jimbo la ARUMERU mtalisikia redioni kama ilivyokuwa kwa majimbo mengine ya Igunga na Uzini.

Ama kweli, CDM ni full shari.
Kila mara huwa nafikiri kwamba huwa unapitiwa, kumbe kichwani hakuna ubongo, ni kasha tu!!
 
Kila chaguzi CCM wanaingia na WRONG tactics ambazo huacha makovu makubwa sana kwa wananchi baada ya uchaguzi. Tendwa katumwa na CCM lakini anajikuta akiwagawa wana Arumeru... Ndio madhara ya kuwa na viongozi legelege
 
  • Thanks
Reactions: FJM
CDM msituletee umwagaji damu kama mlivyofanya Igunga. Amani mliyoikuta Meru iacheni.

Inaonekana mmeanza kutapatapa, ... na bado....jimbo la ARUMERU mtalisikia redioni kama ilivyokuwa kwa majimbo mengine ya Igunga na Uzini.

Ama kweli, CDM ni full shari.

Acha kutoa coment bila kufikilia,nani kaanza kutoa vitisho kama sio CCM?kila siku nyie ndio mnakuwa wa kwanza kuyaanzisha,alafu baada ya hapo mnawatupia lawama CDM mbinu zenu chafu lazima ziwatokee puani.
 
Hapo bado hajaja boiler mchemsaji WASIRA hawa wazee wameifanya hii nchi kama changu doa wanaiinamisha wanavotaka, sasa hapo mgombani hawana bahati wakizidi majabali yanawahusu
 
MSAJILI wa Vyama vya Siasa, John Tendwa amemshauri Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema kuwaomba radhi wazee wa kimila wa kabila la Wameru ‘Washiri’ vinginevyo hali ni mbaya kwake na kundi lake.

Tendwa alisema hayo jana kwa waandishi wa habari wakati akizungumzia mambo ya uchaguzi mdogo wa Jimbo la Arumeru Mashariki.

Alisema utovu wa nidhamu alioonesha Lema siku ya maziko ya aliyekuwa mbunge wa jimbo
hilo, Jeremiah Sumari, kiliwakera Washiri na kumtaka asikanyage jimbo hilo wakati wa kampeni.

Alisema yeye alikwenda katika jimbo hilo kuonanana wakuu wa Serikali na taasisi zake kupanga mkakati wa uchaguzi, lakini ghafla alikutana na wazee hao waliosema mbele yake, kuwa Mbunge huyo wa Arusha Mjini, hawataki kumwona katika kampeni, vingivevyo damu inaweza kumwagika juu yake.

‘’Washiri wamesema hawataki kumwona Lema katika kipindi cha kampeni kwani alileta dharau kubwa na utovu wa nidhamu siku ya maziko ya Sumari, hatua ambayo iliwakera wazee hao … ni busara tu, Lema kwenda kuwaomba radhi wazee hao kama anataka kufanya kampeni ya mgombea wa chama chake- Chadema,” alisema Tendwa. Pia Tendwa amesema Lema asipowaomba radhi huenda damu ikamwagika.

Msajili alivitaka vyama vya siasa kuheshimu mila na desturi za makabila, ili kuepuka umwagaji damu na kushauri kuwa ni vema vyama vya siasa katika kampeni kuzingatia hilo.

Alisema eneo la Arumeru Mashariki ni tete na lenye ushindani mkubwa wa kisiasa na kutokana na hilo, aliwataka wagombea wa vyama vyote na viongozi katika kipindi cha kampeni, kufuata kanuni na sheria za maadili ya uchaguzi tofauti na hapo hali inaweza kuwa mbaya.

‘’Hatutaki uvunjifu wa amani uwepo kwa kupindisha demokrasia na maadili ya uchaguzi,
hivyo kila mgombea anapaswa kuzingatia hilo mara moja na vyama vinapaswa kukubali matokeo na si kuchukua sheria mkononi,” alisema.

Msajili alisema; ‘’ujambazi wa siasa’’ hautaruhusiwa katika kampeni za jimbo hilo kama vile
kupigana risasi na kumwagiana tindikali, kwani ofisi yake kwa kushirikiana na Polisi watakuwa mstari wa mbele kuhakikisha ulinzi na usalama unaimarishwa kwa asilimia 100.

Tendwa alisema matusi, udini, jinsia na kashfa, ni kauli zinazopaswa kuepukwa katika kampeni hizo, kwani zinaweza kuleta madhara makubwa ya umwagaji damu na ni kinyume na maadili ya uchaguzi, lakini viongozi
nao wanapaswa kuziepuka.

Source:Habari Leo

 
Husika na kichwa hapo juu..,Nimeamini kwamba chama cha mapinduzi (CCM) hawana jipya katika kufanya kampeni zao huku wakitumia silaha zao za udini,ukabila,unyanda na siasa za majitaka huku silaha yao ya mwisho ni kuchakachua kura...! kwakuwa hawana mbinu nyingine ya kuishinda CHADEMA baada ya kushindwa kutekeleza ahadi zake kwa wananchi na pia kushindwa kufanikisha maisha bora kwa kila Mtanzania kama ilani yao inavyosema!

katika kampeni za Igunga mwaka jana..,CCM wakishirikiana na mkuu wa wilaya kutengeneza kesi,waliweza kuwatumia masheikh ambao ni makada wa CCM ili kuishambulia Chadema pamoja na kujenga chuki ya waislamu dhidi ya Chadema mwisho wa siku eti Chadema washindwe kwenye uchaguzi kwa kukosa kura za Waislamu,,.bahati nzuri Waislamu sio wajinga au watu wa kupotoshwa kama walivyodhania CCM,CHADEMA walipata kura nyingi tu hadi kufikia mshindi wa pili..!
tumeona kwamba CCM ni chama cha kidini

Vile vile kwenye uchaguzi wa Arumeru ambao utafanyika hivi karibuni,..KAMADA GODBLESS LEMA anawanyima usingizi CCM na ndiyo silaha kubwa ya CHADEMA arumeru yaani (striker), wameanza kutumia UKABILA hasa kwa kuwatumia WASHIRI wazee wa kimeru kumtishia kifo GODBLESS LEMA asikanyanyage meru eti kwa kutoa kauli tata kwenye msiba wa sumari...,huku CCM kwa akili zao za kipuuzi wakiamni watakuwa wamemdhibiti LEMA pamoja na kujenga chuki ya kikabila kwa kuwatumia hao WASHIRI kujenga chuki dhidi ya CHADEMA..,Napenda niwaambie CCM, GODBLESS LEMA hatishiwi kifo hata siku moja ndio maana alikuwa tayari kwenda kulala gerezani na vile vile WAMERU sio wajinga kama mnavyozania kwamba kuwatumia washiri kwenye kampeni zenu chafu dhidi ya CHADEMA..!
na hii zana nimejidhihirisha CCM ni chama cha kikabila kwa kutumia washiri (wazee wa kimeru ) kuifanyia CCM kampeni na kuishambulia CHADEMA ambao hao WASHIRI..!
 
Naendelea kufatilia kama hiyo press conference imefanyika niwajuze zaidi wana jamvi. Kama kuna mtu kapata mpya kuhusu swala hilo tafadhari tupe latest. Nipo Tengeru naelekea Meru milimani kudadisi kinchoendelea.
 
kwa nini asitume polisi kwenda kuwakamata hao wazee waliotishia maisha ya Lema?
au kwa nini hao wazee wasisambaze hizi taarifa zao kwa waandishi wa habari wao wenyewe?imekuwaje hadi wakamtumia Tendwa hizi taarifa?
Naona hapa kuna mchezo mchafu unataka kuchezwa na cccm-wao wameshaona Lema akienda Arumeru atapata wafuasi wengi na simply cccm itakufa arumeru,sasa yeye anatumika kutoa taarifa ili incase Lema akienda huko,na ccm wakashindwa,wataanzisha vurugu na ikibidi waue waue watu as normal na lawama wazipeleke kwa Lema kuwa wazee walishatoa tamko.
Jamani hii nchi inaendeshwa na wazee wa kimila au raisi?na kazi ya polisi ni nini?

NAOMBA LEMA AENDE HUKO,PAMOJA NA VIONGOZI WENGINE WA CDM,JIMBO LIRUDI KWA CDM,
HII ZAMA SI ZAMA ZA KUISHI KWA KUONGOZWA NA PROPAGANDA ZA CCCM
 
CCM ni sawa na MFA MAJI, full kutapatapa...

Hapo silaha yao inayofuata baada ya hii maji taka ni kumwaga FFU wengi na lile gari la maji ya kuwasha. Wiki hii hii utaona hizo silaha zao zinaingia Arumeru. Thanks God kule Arumeru watu wameenda enda shule tofauti na Igunga na Uzini.
 
CCM hawana jipya tena,imebaki kuwalaghai watanzania,na kuwadhurumu mali zao,CCM wamebaki na ujambazi tu si chama cha kumkomboa mtanzania,Mh lema hakuna anayewe kumtisha yeye ana Mungu anayempigania,alizaliwa siku moja na atakufa siku moja Mungu atapopenda,wala siyo hao wazee wanaosubiri kufa tu ndiyo mana wanatumiwa na CCM vibaya kwa kupewa sh,mbili na ndiyo mana wamejikuta maskini wakutupwa kwasababu ya kuing'ang'ania CCM chama cha majambazi! Mungu mkubwa yeye yupo na Mh lema siku zote mana Mh lema anapigania haki na utu wa mwanadamu.Viva Mh lema.
 
Mi nafikiri hata elimu inavyoporomoka nchini CCM wanafurahia sana. Siamini siku watanzania watakapo soma na kuelimika, haya mambo yataendelea kuwepo!!
 
Tedwa nilimuona kwenye kipindi maalum TBC siku ule ya uchaguzi wa Igunga, ni ngumu sana kumtofautisha na mukama anajisahau kupita kiasi
Hauwezi kuwatofautisha. Wote ni WATEULE wa JMK. Kauli kama hii haina uhusiano wa mojakwamoja na kampeni na joto la uchaguzi la sasa na wala Lema sio mgombea wa CHADEMA licha ya kutokuwa msemaji wa chama hicho. Tendwa ni mzigo mwingine wa kodi zetu.
 
Source: Habari leo.Ingawa chanzo cha habari ni tata lakini ninavyowajuwa Wameru ni watu wa vurugu mtindo mmoja CCM wanaweza kutumia nafasi hiyo kupenyeza sumu ya uasi mara wakigundua maji yako shingoni.Ni vyema CDM wakamwondoa G Lema katika kampeni za Meru vinginevyo watajuta na uenda ukawa mwanzo mbaya wa CDM katika siasa za kanda ya kaskazini.

Ikumbukwe Laigwanani Elowassa atapenda kuonyesha bado ni mwanasiasa muhimu katika eneo la Arusha na Manyara ili ndoto zake za urais mwaka 2015 zizidi kung'aa.Sijui Lema alitamka maneno gani ila ninachojua ni mmoja wa wanasiasa wachovu kupindukia wasiojua ABC ya siasa ni bahati mbaya sana nilitoa taadhari mapema lakini hakuna aliyetaka kusikia au kuamini nilichosema.

G Lema asiende Arumeru kama hawajui wameru angewauliza Rais wa awamu ya pili A H Mwinyi,A L Mrema na Askofu Dr Thomas Laiser na Askofu Dr Erasto Kweka katika mgogoro wa KKKT kanda ya kaskazini.Wameru ni rahisi sana kutumika hasa katika zama hizi ambazo vijana hawana ajira.
 
Who are those Washiris, do they have power to prohibit a prrson to get in Meru?
Tendwa ni mtu wa ajabu sana, yaani yeye anaishi Dar, Washiri Arusha, Lema Arusha. Hao Washiri wameshindwa kufikisha ujumbe Arusha hadi wamtume Tendwa !
 
Mi nafikiri hata elimu inavyoporomoka nchini CCM wanafurahia sana. Siamini siku watanzania watakapo soma na kuelimika, haya mambo yataendelea kuwepo!!

Mkuu hebu nikumbushe hii avatar yako huyu mzee asiye na elimu alikamatwaga wapi vile
 
Husika na kichwa hapo juu..,Nimeamini kwamba chama cha mapinduzi (CCM) hawana jipya katika kufanya kampeni zao huku wakitumia silaha zao za udini,ukabila,unyanda na siasa za majitaka huku silaha yao ya mwisho ni kuchakachua kura...! kwakuwa hawana mbinu nyingine ya kuishinda CHADEMA baada ya kushindwa kutekeleza ahadi zake kwa wananchi na pia kushindwa kufanikisha maisha bora kwa kila Mtanzania kama ilani yao inavyosema!

katika kampeni za Igunga mwaka jana..,CCM wakishirikiana na mkuu wa wilaya kutengeneza kesi,waliweza kuwatumia masheikh ambao ni makada wa CCM ili kuishambulia Chadema pamoja na kujenga chuki ya waislamu dhidi ya Chadema mwisho wa siku eti Chadema washindwe kwenye uchaguzi kwa kukosa kura za Waislamu,,.bahati nzuri Waislamu sio wajinga au watu wa kupotoshwa kama walivyodhania CCM,CHADEMA walipata kura nyingi tu hadi kufikia mshindi wa pili..!
tumeona kwamba CCM ni chama cha kidini

Vile vile kwenye uchaguzi wa Arumeru ambao utafanyika hivi karibuni,..KAMADA GODBLESS LEMA anawanyima usingizi CCM na ndiyo silaha kubwa ya CHADEMA arumeru yaani (striker), wameanza kutumia UKABILA hasa kwa kuwatumia WASHIRI wazee wa kimeru kumtishia kifo GODBLESS LEMA asikanyanyage meru eti kwa kutoa kauli tata kwenye msiba wa sumari...,huku CCM kwa akili zao za kipuuzi wakiamni watakuwa wamemdhibiti LEMA pamoja na kujenga chuki ya kikabila kwa kuwatumia hao WASHIRI kujenga chuki dhidi ya CHADEMA..,Napenda niwaambie CCM, GODBLESS LEMA hatishiwi kifo hata siku moja ndio maana alikuwa tayari kwenda kulala gerezani na vile vile WAMERU sio wajinga kama mnavyozania kwamba kuwatumia washiri kwenye kampeni zenu chafu dhidi ya CHADEMA..!
na hii zana nimejidhihirisha CCM ni chama cha kikabila kwa kutumia washiri (wazee wa kimeru ) kuifanyia CCM kampeni na kuishambulia CHADEMA ambao hao WASHIRI..!
"Ukiona mtu/watu wanashambulia wenzao kwa misingi ya ukabila,rangi au udini,hao watu ni walioshiwa sera kichwani,wamefilisika kichwani,ni wapumbavu,natumia neno zuri wapumbavu" - J.K.NYERERE
 
Back
Top Bottom