Antar bin Shaddad
JF-Expert Member
- Oct 11, 2010
- 202
- 101
Mzee tendwa anaingilia mabo ya hawa wazee wa kimeru je hawa washiili ni chama cha siasa?Baada ya msajiri wa vyama vya siasa John Tendwa kuwasemea wale aliowaita wazee wa Arumeru, kundi jipya limeibuka na kudai Tendwa kalisemea kundi la wazee wa CCM nao wanakuja kama wazee wa UPINZANI kusema yafuatayo:-
1. Neno la kutishia kuua tayari ni kuua na hawakutarajia mtu makini kama Tendwa kuendelea kulisisitiza hadharani kama sio kuchochea vurugu.
2. Lema hakumtukana mtu hata kama alionyesha vidole viwili kwani yeye mda wote anatetea maslahi ya chama chake. Walitaka atamke kidumu chama cha mapinduzi ndo waridhike?
3. Wanadai kila mmoja anaweza kuua na wote pande zote mbili ni wakazi na wana Arumeru hawana haja ya kutishana kwani wanatumia siraha sawa na mbinu sawa.
4. Wanamwambia Lema karibu Arumeru hata leo waone nani anakuwa wa kwanza kumfunga paka kengere.
5. Mwisho wanamwambia Tendwa awe tayari kujibu mbele za watanzani juu ya madhara yoyote yatakayojitokeza kutokana na vurugu anazozichochea kwa wanameru yeye akishirikiana na CCM.
Wazee hao nao wanajipanga kuitisha mkuta na waandishi wa habari mda wowote.
Source: Dr mmoja hospitali ya Tengeru ambaye ni Mmeru mkazi wa Sing'si.