Mgomo mkubwa wa wenye vituo vya mafuta 2011!

Kuwaondolea kodi wafanyabiashara hakumaanishi bei itapungua,haya ndiyo mambo tunayojichuuza nayo kila siku.Dawa ni kununua mafuta na kuyauza at break even point.Serikali ifanye hivyo au vyama vya ushirika.
 
The issue here ni kuwa wenye makampuni ya mafuta wana stock tayari walioigharamikia kwa sawa na bei ya sasa ili wapate faida kwa sasa kitakachofanyika watahold mafuta hawayauzi hivyo kutakuwa na uhaba, kwani UWURA watawanyang'anya leseni wale watakaouza mafuta bei ya juu na sio kuhold mafuta yaliyoloko stock, msipende kupinga kila issue fikirieni nje ya boksi kabla ya kujibu hoja...
Kwani ni kodi gani iliyopunguzwa?
Kama hiyo kodi hukatwa baada ya mauzo,kwanini wassipunguze bei?....ila kama hukatwa kabla ya mauzo,naweza kuwaelewa.
 
Godby, wewe utakuwa ama ni muuza mafuta au ni mnufaikaji wa moja kwa moja na bei kuwa juu. Jiulize, mbona kodi ya mafuta ilipopanda, bei yake ilipanda papo hapo kuanzia Julai 1, 2011 bila kusubiri stoke? Iweje leo bei za petrol/dizel ndo zisubiri stoke hata baada ya mwezi mzima wa Julai baada ya tozo kupunguzwa?! Acheni kuibia wananchi jamani!
 
The issue here ni kuwa wenye makampuni ya mafuta wana stock tayari walioigharamikia kwa sawa na bei ya sasa ili wapate faida kwa sasa kitakachofanyika watahold mafuta hawayauzi hivyo kutakuwa na uhaba, kwani UWURA watawanyang'anya leseni wale watakaouza mafuta bei ya juu na sio kuhold mafuta yaliyoloko stock, msipende kupinga kila issue fikirieni nje ya boksi kabla ya kujibu hoja...

Kwa hiyo wata hold mafuta na hawatagoma kama ulivyoashiria kwenye post yako ya mwanzo?
 
Hoyce-hapa hatugombani bali tunapeana taarifa ili wenye kufanya maamuzi wafanye.Nilichowasilisha ndiyo yanayosemwa na wadau.Kuhusu kwamba stock itaisha mpaka baada ya mwezi au la hilo si letu la kuamua ila kinachotusu hapa ni athari ambozo zinaweza kuletelezwa na maamuzi haya.Hakuna anayependa kulipa TZS 2200/ltr wakati maisha yenyewe ni tight.
 
Napenda kujua price per litre za jirani zetu malawi, rwanda na uganda kabla ya kucoment!
 
  1. Waache ujinga! bora na wao waingie hasara, mbona bei ya dunia ya mafuta huwa inapanda na kushuku huwa wanasubiri stock????
  2. Hapa kwa sasa tunaiangalia serikali kupitia vyombo vyake ili kupunguza ukali wa maisha! Bravo CCM! Bravo JK!
  3. Sema kitaalamu kitu amabacho kingeweza kufanya kazi kwa usahihi ni kuwa na excess supply ya mafuta (kama tu serikali ingekuwa mdau wa hii biashara) maana wao wangetoa stock kubwa na kusambaza nchi nzima kwa bei bwerere na hao wenye makampuni binafsi wangefyata mkia! Lakini kwa sasa tuiunge mkono serikali kwa hili na inabidi washushe tu bei kwani serikali imefanya kama imelipia kiwango fulani kwa ajili ya wananchi wake (wawe CUF, CCM, CHADEMA, NCCR, ....., eND OF tHINKING cAPACITY {etc})
 
Nimepigiwa simu na kupewa hiyo tetesi. Haina uhakika. Kwa tahadhari weka mafuta usiku huu. Ni tetesi tu.
 
Haya Jamani uhakika ni kwa jinsi gani bei zinatarajiwa kuwa kesho tafadhali soma hapo chini.

EWURA- REF: PPR/08 - 1/11
PUBLIC NOTICE ON CAP PRICES FOR PETROLEUM PRODUCTS EFFECTIVE 3RD AUGUST 2011
Following the completion of a public inquiry process that was aimed at coming up with a new price computation formula, EWURA hereby publishes bi-weekly cap prices for petroleum products in the Tanzania Mainland local market. These retail and wholesale prices are applicable effective Wednesday 3rd August 2011. Kindly take note of the following.
(a) Retail and wholesale prices for all petroleum products, in the Tanzania Mainland local market have gone down compared with the last prices publication of 1st July 2011. Retail prices for various products have decreased (per litre) as follows: Petrol TZS 202.37 (or 9.17%), Diesel TZS 173.49 (or 8.32%) and Kerosene TZS 181.37 (or 8.70%). The price decreases have been caused by a revision of the Petroleum Prices formula. The decrease would have been higher had it not been for a rise in petroleum prices in the world market prices and depreciation of the Tanzanian Shilling compared to the US dollar (the currency in which purchases of products in the international oil market are made). The wholesale prices for the same period have also decreased as follows: Petrol TZS 201.61 (or 9.43%), Diesel TZS 172.73 (or 8.57%) and Kerosene TZS 180.63 (or 8.95%).
(b) In line with the prevailing sector legislation, prices of petroleum products are governed by rules of supply and demand. EWURA shall continue to encourage competition in the sector by making available petroleum products pricing information including price cap. This information on prices is intended to enable stakeholders to make informed decisions on petroleum prices at any particular time.
(c) Oil marketing companies are free to sell their products at a price that give them competitive advantage, provided that such price does not exceed the price cap for the relevant product. The approved formula was gazetted through Government Notice No. 5 of 9th January 2009 and amendments made in July 2011.
(d) All petrol stations should publish petroleum product prices on clearly visible boards. The price boards should be clearly visible and should clearly show prices charged, discounts offered as well as any trade incentives or promotions on offer. Consumers are advised to purchase from those that sell products at the most competitive prices. It is an offence not to have prices published on boards located in clearly visible places in front of petrol stations and it will attract punitive measures from EWURA.
(e) Retailers must issue receipts with respect to all sales that they make and consumers are advised to demand and keep receipts that clearly show the name of petrol station, date on which such purchase was made as well as, the type of fuel and price per litre for every purchase they make.


Haruna Masebu
DIRECTOR GENERAL
EWURA
 
Serikali haina haki ya kupanga bei,hii ni nchi ya biashara huria? Wameshindwa kuregulate bei za unga na maharage, wataweza mabepari wa mafuta!
 
Serikali haina haki ya kupanga bei,hii ni nchi ya biashara huria? Wameshindwa kuregulate bei za unga na maharage, wataweza mabepari wa mafuta!

biashara huria sio kwa wafanyabishara kuwatungua wananchi/walaji tu

kulitakiwa kuwepo bodi ya kulinda walaji kabla ya huu ujinga wa biashara huria
 
Kila nikimkumbuka mwalim Jkn...machozi hunitoka. .....kwasababu alituacha mikononi mwa mafisi!
 
Acha wafunge! Na hata ikiwezekana umeme upotee kbs! Naona kungekuwa na heshima kwa nchi. Na ndiyo kungejulikana kunyoa ama kusuka. Hakunaga shida. NB: MAMBO NI MABAYA NDANI YA NCHI YETU KWA MTINDO HUU.
 
wenye wagome tu sijaona logic hata hilo punguzo ni ujinga huwezi punguka kwa tsh200 unasema unasaidia au unajikosha mbele ya wananchi? hili nipigo tuamkeni maana bila maandamano hakuna kitu kitakachofanyika
 
Kuna kamgomo baridi ka wauza mafuta.....leo vituo vingi vinadai ''havina mafuta'' habari ndio hiyo jazeni mfulu tenki magari yenu mkipata pa kujazia..........wanadai ''bei nzuri''
 
kama wakitaka kugoma wagome tu watajikuta ni wachache wanaogoma halafu wengine watatumia huo mwanya kuuza then utakuta wanaanza malumbano wenyewe kwa wenyewe.. watanzania bwana sijui ni lini tutakua na ule umoja wa kweli kuamua kukataa jambo.. tatizo letu tunakua tunapelekwa na uoga.. kama tungesimama kuanzia siku nyingi sana kutetea hali ya mafuta na uchumi wa nchi yetu unapoendelea,, wala tusingekua na wafanya biashara wasio na huruma kama hawa jamaa wa mafuta...! ila tumewaachia mpaka sasa tunalia wenyewe

na kama hatutakuja kuangalia mambo mengine ya msingi bado tutaendelea kulia na kuumia hivihivi kisa tunaendekeza woga.. ! ninajaribu kufanya uchunguzi wa kuhusu bei ya mafuta kwenye nchi kama za Rwanda na burundi ili nijue... nimesikia huko kunaunafuu wa bei ya mafuta wakati wanachukulia kwenye bandari yetu hapa..! ila tuwe waangalifu sana laasivyo mambo mengine yanayohusu maisha yetu ya kila siku yatakuja kua msumari mkali sana kwenye miili yetu kama hatutakkua waangalifu na kusimama na kukataa mapema

kumbuka,,,,,,"usipoziba ufa utajenga ukuta",,,,,
 
Back
Top Bottom