Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 4,783
- 14,975
Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Ndg. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiendelea na Kampeni ya Uchaguzi Makambako Mkoani Njombe leo tarehe 06 Septemba, 2025.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan leo Jumamosi Septemba 06, 2025 amewaahidi wananchi wa Makambako Mkoani Njombe kuwa kuanzia mwezi Oktoba 2025, Serikali ya awamu ya sita itaanza kujenga vituo vya kuuzia mahindi Mkoani humo kama sehemu ya kutoa fursa ya masoko kwa wakulima wa Mkoa huo.
Dkt. Samia ameyasema hayo wakati wa mkutano wake wa Kampeni kwenye soko kuu la Makambako akiwa njiani kuelekea Mkoani Iringa kuendelea na kampeni yake, akiahidi pia kulifanyia kazi ombi la Mgombea Ubunge wa Jimbo hilo Ndugu Godfrey Chongolo, aliyeomba pia Mji huo kujengewa bandari Kavu kutokana na umuhimu wake wa kuwa kitovu cha biashara kwa Mikoa ya kusini na nchi za Jirani.
"Niwapongeze pia kwasababu tayari chuo cha Mwalimu Nyerere wameshafanya matayarisho ya awali ya ujenzi wa chuo na niseme serikali itatoa fedha yote ili chuo hiki kianze kujengwa na kikamilike na kwa ukweli chuo hiki kipo kwenye mpango wa mabadiliko ya elimu ya juu na fedha yake ipo tayari ni kazi tu ifanyike." Amesema Mgombea Urais huyo.