.......Je ni kweli Jaji ali-alter constitution badala ya Kuitafsiri....
Ogah,
Kwamba Mahakama Kuu ilitengua katiba hilo hata hawabishani. Majaji walitegua kipengele vitatu:
KATIBA YA JAMHURI
39. (1) (c) Mtu hatastahili kuchaguliwa kushika kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano isipokuwa tu kama: ni mwanachama, na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa;
67. ( 1) ( b) Mtu yeyote atakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge endapo ni mwanachama na ni mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa;
21. (1) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 39 ya 47 na ya 67 ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchagua na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na nanchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.
Na, jaji Masati, akiandika kwa niaba ya jopo wala hakuficha kwamba, naam, sasa tunatengua katiba:
MAHAKAMA KUU, 2006
``The issue therefore is whether the amendments to Articles 21(1) and Articles 39 and 67 of the Constitution is ConstitutionalIt may of course sound odd to the ordinary mind to imagine that the provisions of a constitution may be challenged for being unconstitutional
So this Court may indeed declare some provisions of the Constitution, unconstitutional.
We thus proceed to declare that the said amendments to Articles 21(1), 39(1)(c) and 67(10)(b) are unconstitutional.``
Vipengele vilivyotenguliwa na mahakama vilichomekwa kinazi kwenye Katiba katikati ya kesi ya kwanza, mwaka 1993, wiki moja kabla ya hukumu ya hayati jaji Lukakingira alipokubali pingamizi la Mtikila dhidi ya sheria inayotakataza ugombea binafsi. Hivyo, hukumu dhidi ya serikali, kwamba sheria ya uchaguzi ni kinyume cha Katiba, ikawa haina nguvu kwa vile serikali ilishajiwahi kuburuza muswada wa kubadili Katiba ili hiyo sheria ya uchaguzi ikubalike.
Mtikila aliporudi safari ya pili akadai kwamba marekebisho ya Katiba yaliyopitishwa kumzuia asigombee binafsi ni batili. Athari ya mabadiliko hayo, akasema, ni kumlazimisha kuingia kwenye chama wakati Katiba ilikuwa inapiga marufuku kulazimishana hivyo, isitoshe Katiba inaruhusu yeyote kushiriki utawala wa nchi ``moja kwa moja.``
KATIBA YA JAMHURI
20 (2)ni marufuku kwa mtu yeyote kulazimishwa kujiunga na chama chochote.
20(4) Itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kulazimishwa kujiunga na chama chochote au shirika lolote au kwa chama chochote cha siasa kukataliwa kusajiliwa kwa sababu tu ya itikadi au falsafa ya chama hicho.
21(1) Kila raia wa Jamhuri wa Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja, au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wanacnhi kwa hiari yao kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.
Mahakama Kuu ikakubaliana nae kwamba serikali haina nguvu kuchomeka mabadiliko ya Katiba yanayoondoa haki za msingi zilizokuwepo awali. Hivyo mwaka 2006 majaji wakafuta vipengele vipya vilivyochomekwa kwenye Katiba, kwamba ni unconstitutional. Mtikila akawa two for two, kashitaki mara mbili kashinda mara mbili.
Sasa serikali inakwenda Mahakama ya Rufaa kupinga kitendo cha Mahakama Kuu kubadili Katiba. Serikali inadai 1) walipochomeka kipengele cha katiba kuzuia mgombea binafsi walikuwa ndani ya mipaka yao kwa mujibu wa Katiba, 2 ) Bunge ndio lina nguvu ya kubadilisha Katiba, sio Mahakama.
KATIBA YA JAMHURI
98. (1) Bunge laweza kutunga Sheria kwa ajili ya kubadilisha masharti yoyote ya Katiba hii kwa kufuata kanuni [ifuatayo]: itaungwa mkono kwa kura za Wabunge ambao idadi yao haipungui theluthi mbili ya Wabunge wote;
(2) Kwa madhumuni ya ufafanuzi wa masharti ya ibara ndogo ya 98 (1) kubadilisha masharti ya Katiba hii au masharti ya sheria maana yake ifahamike kuwa ni pamoja na kurekebisha au kusahihisha masharti haya au kufuta na kuweka masharti mengine badala yake au kusisitiza au kubadilisha matumizi ya masharti hayo.
Swali ni, jee, Mahakama ina nguvu kutengua katiba? Kama inayo, serikali inasema mwishowe majaji wanaweza kukadilisha Katiba nzima. (Kumbuka hawabishani kama ilitengua au haikutengua.)
Kawaida Katiba ni ya watu, inatoka kwa watu, kwa ajili ya watu. Kupitia wawakilishi. Inawezekana Mahakama ya Rufaa ikakubaliana na serikali kwamba wao, majaji, hawana nguvu kutangua Katiba.