Mgogoro wa Zanzibar watinga Ikulu ya Marekani

Mgogoro wa Zanzibar watinga Ikulu ya Marekani

Mfano wako uko vizuri ila haujatake into consideration sababu (interest zake) za rafiki yako kutoa huo msaada.....Je alitoa huo msaada kwa sababu ya kukusaidia wewe rafiki yake tu au anawaonea huruma watoto na mke wako kwamba wanapata shida kutokana na ukata wako wewe.......Kama hana interest yeyote then hicho unachosema kitakuwa hakina sababu ya kutokea....

Lakini assume kama interest yake au msukumo wake ni uchungu alionao juu ya watoto na mke wa rafiki yake wanaopata taabu na lets say na mke wako wewe anajua kabisa huo ndio msukumo wa rafiki yako......sasa kama ugomvi utakuwa umetokea ambapo kwa namna moja au nyingine unahusiana na wewe kufanya maamuzi ambayo kwa namna moja au nyingine bado yanaendelea kuipa taabu familia yako.....kwa mananeo mengine lengo la rafiki yako halitimii....na wewe unatumia ubabe wako wa mamlaka yako katika familia kumkandamiza mama watoto wako, hauoni itakuwa natural kwa baadhi ya watu (na kwa mfano huu mama watoto wako) kuamua kwenda kwa rafiki yako kulalamika ili kuongeza pressure kwa matumaini kwamba atapata haki yake na watoto wake ?

Misaada mingi tunapewa na hawa watu wa Magharibi kwa sababu wanaamini sisi tunaheshimu utawala wa sheria na tunafuata misingi ya kidomkrasia na ndio maana sio nchi zote zinazopewa misaada na hawa watu na viongozi wetu wamekuwa wanatamba kabisa kwamba wao wanakubalika kwa sababu nchi yetu inaongozwa kwa misingi ya kidemokrasia......Sasa wengine wanapokandamizwa na kunyimwa haki zao za kidemokrasia, huoni kwamba ni natural tu baadhi yao watakimbilia kwa hao wafadhali na kulalamika kwamba hawa viongozi wetu hawafuati misingi ya kidemokrasia ili kuongeza pressure ? Mbona hiyo ni common sense tu ?. Wewe unaweza usifanye hivyo (hata mimi ningekuwa huko nisingeandamana), lakini ninakushangaa kuwashangaa hao waliamua kufanya hivyo......ni haki yao kudai haki yao kwa kuongeza pressure kutoka upande huo..............

Daaah. Hii shida sana.

Labda Mfano Utasaidia:
Tuchukulie mfano kuwa wewe ni rafiki yangu na kila ninapokwama unanisaidia kifedha kujikimu mimi na familia yangu. Itokee mimi na mama watoto wangu tuna mfarakano wa kawaida nyumbani kwetu.

  • Hivi unategemea kuwa lazima tuje mlangoni kwako tukufahamishe kuwa tuna ugomvi?
  • Kama wazee wetu wakiwa wanaendelea kutusuluhisha, bado unadhani ni busara tupite kwa wahisani wetu wote tukilalamika kuwa tunagombana?

Kitendo hiki ndicho ninachokiona kinatudhalilisha sana sisi waTanzania lakini pia waAfrika wote kwa ujumla wetu. Hatujiamini kama tunaweza kutatua matatizo yetu sisi wenyewe. Kila likitokea tatizo tunakimbilia mataifa ya magharibi.

Kwa mwendo huu tusishangae wanapotudharau ingawaje sisi ni mataajiri wakubwa sana wa rasilmali.

Eee Mwenyezi Mungu tusaidie.
 
Eti unasema nisidanganye watu, sasa uongo gani niliosema hapo ? Search kwenye google uone kama baadaye haikuwa proved kwamba Bush alishinda Florida ! kwa kukusaidia fuatilia link mojawapo hii

Who really won Bush-Gore election? - CNNPolitics.com

Nchi zinazoheshimu taratibu walizojiwekea zinatawaliwa kwa sheria....na mahakama inapotoa uamuzi wanauheshimu.....uamuzi sio lazima umridhishe kila mtu na kama kuna pande zinapingana uamuzi wowote ule lazima utamfurahisha mmoja na kumsononesha mwingine....hiyo ndio reality. Lakini lazima kuwepo na mtu au chombo ambacho watu wote wanakubaliana kwamba kina mamlaka ya kutoa haki na maamuzi yake yataheshimiwa na wote....

Rais wa Marekani aliyekuwa anaondoka madarakani ni Clinton na makamu wake ni Algore na walikaa kwa kipindi cha miaka nane na katika kipindi na kwa utaratibu wao nao walishiriki kuweka baadhi ya majaji....sasa inakuwaje sasa tena wewe unasema eti majaji wote ni Republicans wakati Clinton hata bado hajakabidhi madaraka kwa Bush ?. Kwa Marekani, majaji wengi watu wanawaangalia kwa misimamo yao kwenye issues na sio vyama, na ndio maana ukikuta issue inayotaka kuamuliwa kwa mfano inahusiana na abortion utakuta watu wanadiscuss na kusema jaji fulani, yeye historia yake kwenye issues inaonyesha ni pro-life or otherwise na si yeye ni pro-Rebulican or Democtrat. Kwa kiwango kikubwa majaji wa huko hawaegemei kwenye siasa za vyama bali issues..

Kwa dunia ya sasa hakuna advantage ya kujua kitu fulani eti kwa sababu unakaa eneo fulani na mwingine asiyekaa eneo hilo basi atakuwa hajui habari za hilo eneo kama wewe......hayo mambo ni ya zamani sana.....leo uelewa wako wa siasa au hata issues nyingine za nchi yeyote duniani hazihusiani na wewe kuwa eneo fulani....zinahusiana na uamuzi wako binafsi na interest zako na muda wako.....basi !. Siku za leo mtu anaweza akawa anaishi marekani na akajua siasa za Tz kuliko yule anayeishi kariakoo !. Kwa mfano, miaka ya mwishoni mwa 90 mpaka miaka ya mwanzoni ya 2000 (around 1998 - 2004), nilikuwa nafuatilia sana siasa za Israel, mpaka wakati fulani nilipokuwa nafanya majadiliano na muarabu mmoja na muyahudi mmoja niliokuwa nasoma nao huko Sweden (around 2003) wakashangaa inakuwaje ninayajua mambo yao kuliko wao wenyewe.....ni issue ya interest tu, kwani kila kitu kipo kwenye mtandao !

Issue ya Zanzibar iko wazi, na kama tunaheshimu sheria na wananchi, Maalimu Seif angekuwa Rais sasa hivi......Jecha kama Jecha hana uwezo wa kufuta uchaguzi.....uwezo wa tume kufuta uchaguzi unaweza kubishaniwa.....lakini Jecha binafsi kufuta uchaguzi, hilo liko wazi !. Kafuta huu uchaguzi yeye mwenyewe, wakati kikatiba uamuzi wa ZEC utafikiwa ikiwa mwenyekiti (kwa sasa Jecha) au makamu mwenyekiti atakapoungwa mkono na wajumbe wanne !. Hivyo kwa kufuata sheria uamuzi wa Jecha ni batili !

By the way hakuna wanataaluma wanaojadiliana kwa sababu hakuna chochote cha kujadiliwa kitaaluma..........ninachojua mimi wanaojadiliana ni Maalimu Seif, Dr. Shein, na Marais wastaafu......hao ni wana siasa sio wanataaluma......

Usidanganye watu wewe.

Mimi nimeishi hapa marekani miaka nenda miaka rudi na nilikuwepo kipindi kile cha mgogoro wa uchaguzi. In fact ulikuwa ni mgogoro mkubwa/mbaya sana na wa hatari kwa demokrasia ya Marekani kuliko huu wa Zanzibar.

Kwa mara ya kwanza katika chaguzi za rais za Marekani, Bush alipewa uraisi bila ya kuwa na wingi wa kura. (Alipata wingi wa electoral vote kwa ajili ya madudu yaliotokea Florida). Ilikuwa ni busara tu ya Al Gore kusema basi yaishe.

Mahakama (supreme court) ya Marekani ilioamua (5-4 votes) ilijaa Republicans (chama cha Bush). Kwa Tanzania ni sawa na kuwaambia CCM watoe mahakimu ambao ni makada wao ili waamue kama Maalim ameshinda au la.

Tatizo la Zanzibar linatatulika.

Kuna wanasheria wazalendo waliobobea Zanzibar na wakitaka wanaweza kuleta wasuluhishi kutoka nchi nyingine za kiAfrika wakasaidia. Mazungumzo bado yanaendelea na hatujasikia kuwa yameshindikana. Kwa nini hatuna imani na wataalam wetu wenyewe wa kisheria, hasa waliopo Zanzibar kutatua matizo yetu? Marekani walitumia Supreme Court yao kutoa uamuzi. Mimi sikuridhika nao lakini ilibidi watu wakubali hata kama ni kwa shingo upande.

Lakini angalia sisi. Wanataaluma wetu wanaendelea kujadiliana sisi tunakimbilia kuandamana mpaka ikulu ya Marekani - ili Marekani wafanye nini?
 
Hao wazenj hawaonekani!hawajatinga Ikulu ya Marekani bali wamekaribia kama- hiyo picha sio ya kuunganisha
 
Hao wazenj hawaonekani!hawajatinga Ikulu ya Marekani bali wamekaribia kama- hiyo picha sio ya kuunganisha

Nahisi huwajui vizur wazenji,harakati hizi hazijanza leo,ipo cku zanzibar watasimama taifa huru lenye mamlaka kamili,wadanganyika hamuwezi zuia hilo.
 
Nimemsikiliza huyu mwanasheria na nimemuelewa vizuri sana. Na watu waliobobea katika sheria na Katiba ya Zanzibar kama huyu bwana ndio walioko katika majadiliano ya kupata suluhisho la mgogoro huu. Mazungumzo haya bado yanaendelea na hatujaambiwa kuwa yameshindikana au kuna mfarakano kati yao.

Sasa hiki kitendo cha kuandamana kwenda ikulu ya Marekani faida yake ni nini?

Au wewe unaposema Zanzibar imevamiwa na JWTZ kama si uchochezi huu ni nini?

Mpaka leo vituo kama airport na bandari vipo chini ya ulinzi wa vifaru.
 
Kifyatu

Unaweza kulinganisha kati ya Marekani na Tanzania? Ni lini USA ilishawahi kuomba misaada Tanzania? Halafu kikwete ameenda USA zaidi ya mara 20, yeye Obama alikuja mara ngapi hapa?

Hukuelewa, hoja si nani mkubwa na nani hajitoshelezi, hoja ni utamaduni wa fikra za kutawaliwa. Hata kama ni mdogo kwa hali na umbo, una jukumu la kuwa na msimamo katika huo udogo wake, kinyume cha hili ni kujidhalilisha na kufikiria kuna watu fulani wanaumia sana kwa matatizo yako. 0.5 watakucheka na 0.5 wengine watakudharau.
 
Hapo ndio tutaona usiriasi wa mmarekani na jinsi anavyo iheshimu demomrasia.

Mara nyingi tumezoea kumsikia Mmarekani akitetea haki za mashoga zaidi hadi inafikia hatua kuziwekea vikwazo baadhi ya nchi kisa zimekataa ushoga na wakati huo amesahau maswala ya msingi kama demokrasia na inabidi Obama ajue umuhimu wa demokrasia na ndio iliyomfikisha hapo alipo na kuwa mtu wa kwanza mweusi duniani kuwa rais Marekani.
Rais WA kwanza mweusi? Obama?
 
Marekani walikuwa na mgogoro wao mkubwa sana wa kiuchaguzi (Al Gore vs. George W. Bush) mwaka 1999/2000.

Hivi waMarekani waishio Tanzania waliandamana mpaka Magogoni kwa Mkapa kushinikiza Al Gore apewe ushindi?

Mbona tunauendeleza huu utumwa jamani?

Mara tumekimbilia ikulu ya Marekani, mara ikulu ya Uingereza? Si afadhali haya maandamano yangekwenda Umoja wa Mataifa New York au Geneva ningeelewa? Tumekuwa kama watoto jamani. Ukisukumwa kidogo unakimbia kwa mama kulia na kulalamika.

Ya Rabbi, tutakuja jitawala lini sisi waMatumbi?
 
Marekani walikuwa na mgogoro wao mkubwa sana wa kiuchaguzi (Al Gore vs. George W. Bush) mwaka 1999/2000.

Hivi waMarekani waishio Tanzania waliandamana mpaka Magogoni kwa Mkapa kushinikiza Al Gore apewe ushindi?

Mbona tunauendeleza huu utumwa jamani?

Mara tumekimbilia ikulu ya Marekani, mara ikulu ya Uingereza? Si afadhali haya maandamano yangekwenda Umoja wa Mataifa New York au Geneva ningeelewa? Tumekuwa kama watoto jamani. Ukisukumwa kidogo unakimbia kwa mama kulia na kulalamika.

Ya Rabbi, tutakuja jitawala lini sisi waMatumbi? Dooo!

...unajaribu kuigeuza mbili kuwa moja?! we chizi kweli.
 
Nani kawashikia waZanzibari mtutu kichwani kuwa uchaguzi ukirudiwa leo wasipige kura walivyofanya awali?

Mimi sijui sheria na KATIBA ya Zanzibar lakini nijuavyo mimi ni kuwa tume ya uchaguzi, ZEC, imesema imeona madudu kwenye uchaguzi uliopita na imetaka uchaguzi urudiwe.

Kwa sasa hivi pande zote zenye malalamiko ziko kwenye majadiliano ya usuluhishi. Hili la kuzungumzia majeshi ya kivamizi ya Tanganyika ni upuuzi mtupu. Yaani waZanzibari mnajisikia mpo karibu zaidi na Oman kuliko Tanganyika? - Eti raia wa Oman walifurahi sana!
  • Leo watu wanakwenda ikulu ya Marekani kuandamana ili Marekani iifanye nini Tanzania?
  • Je, mazungumzo ya usuluhishi yameshindikana kutatua hili tatizo?
  • Marekani ni nani katika muundo na Katiba ya serikali ya Zanzibar?
  • Ni kipi tusichoweza kukizungumza na kuelewana katika lugha yetu ya Kiswahili mpaka tuwaite waMarekani?
  • Kwa nini tusiwaite Kenya, Uganda, Afrika Kusini, Ghana badala ya Marekani na Uingereza?
  • Hiki kiherehere cha kukimbilia nchi za magharibi chanzo chake ni kipi?

Nina maswali mengi najiuliza kwa hili na nakosa majibu. Matatizo tunayo - ndio, lakini hivi hatuwezi kukaa na kupata suluhu sisi wenyewe mpaka tukimbilie kwa "mabwana" zetu huko ulaya? This is pathetic.

ha ha haaaa....wazungu walituloga vibaya.....
yaan kumekucha lkn hatuamki.
 
Mfano wako uko vizuri ila haujatake into consideration sababu (interest zake) za rafiki yako kutoa huo msaada.....Je alitoa huo msaada kwa sababu ya kukusaidia wewe rafiki yake tu au anawaonea huruma watoto na mke wako kwamba wanapata shida kutokana na ukata wako wewe.......Kama hana interest yeyote then hicho unachosema kitakuwa hakina sababu ya kutokea....

Lakini assume kama interest yake au msukumo wake ni uchungu alionao juu ya watoto na mke wa rafiki yake wanaopata taabu na lets say na mke wako wewe anajua kabisa huo ndio msukumo wa rafiki yako......sasa kama ugomvi utakuwa umetokea ambapo kwa namna moja au nyingine unahusiana na wewe kufanya maamuzi ambayo kwa namna moja au nyingine bado yanaendelea kuipa taabu familia yako.....kwa mananeo mengine lengo la rafiki yako halitimii....na wewe unatumia ubabe wako wa mamlaka yako katika familia kumkandamiza mama watoto wako, hauoni itakuwa natural kwa baadhi ya watu (na kwa mfano huu mama watoto wako) kuamua kwenda kwa rafiki yako kulalamika ili kuongeza pressure kwa matumaini kwamba atapata haki yake na watoto wake ?

Misaada mingi tunapewa na hawa watu wa Magharibi kwa sababu wanaamini sisi tunaheshimu utawala wa sheria na tunafuata misingi ya kidomkrasia na ndio maana sio nchi zote zinazopewa misaada na hawa watu na viongozi wetu wamekuwa wanatamba kabisa kwamba wao wanakubalika kwa sababu nchi yetu inaongozwa kwa misingi ya kidemokrasia......Sasa wengine wanapokandamizwa na kunyimwa haki zao za kidemokrasia, huoni kwamba ni natural tu baadhi yao watakimbilia kwa hao wafadhali na kulalamika kwamba hawa viongozi wetu hawafuati misingi ya kidemokrasia ili kuongeza pressure ? Mbona hiyo ni common sense tu ?. Wewe unaweza usifanye hivyo (hata mimi ningekuwa huko nisingeandamana), lakini ninakushangaa kuwashangaa hao waliamua kufanya hivyo......ni haki yao kudai haki yao kwa kuongeza pressure kutoka upande huo..............

Yani unadhani haya mataifa ya magharibi yanatusaidia kwa sababu wanatuonea huruma kwa dhiki yetu? Hawa wanafanya hivyo kupata spheres of influence na kutufanya sisi tuwe tegemezi kwao. Na zaidi tunavyojionesha tegemezi ndio wanapotupa masharti mengi zaidi na kupoteza uhuru wetu.

Walifanya hivyo kwa China hizo siku za nyuma lakini China wakaamua kujizatiti wenyewe na kufanya maamuzi yao magumu mpaka sasa wamewapita kiuchumi. Leo hii mataifa ya magharibi wanakwenda kukopa Uchina na wameufyata.

Na sisi ni lazima tuanze kuonesha kuwa tunaweza kujitegemea na kuweza kutoa maamuzi magumu wenyewe. Sasa kama swala la kurudia uchaguzi u tni mpaka tukawalilie Marekani na Uingereza haya kama watu wa vyama tofauti wangechinjana (Mungu apishilie mbali) si ndio tungewaita waje watutawale tena bayana.

Acheni haya mambo jamani.

Tatizo Zanzibar lipo na tunakubali. Lakini naamini tunaweza kulitatua wenyewe.
 
jebibay

Mimi sihitaji ku-google, nilikuwepo katika uchaguzi ule wa Gore na Bush. Kura kadhaa za Gore zilitupiliwa mbali kwa ajili ya technicalities zinazohusu zile voting machines za Florida. Hii ilikuwa mbaya zaidi kuliko ya Jecha kusema kulikuwa na irregularities za uchaguzi na kusema urudiwe.

Marekani wana legal system yao na tunajua ni nani hasa anaeamua nani mshindi - sio wananchi. Hayo tuwaachie wao.

Sisi waMatumbi kweli hatuwezi kukaa chini na kutatua haya matizo wenyewe mpaka tukalielie milangoni mwa ikulu za hizi nchi za magharibi?
 
Last edited by a moderator:
jebibay

Mimi sihitaji ku-google, nilikuwepo katika uchaguzi ule wa Gore na Bush. Kura kadhaa za Gore zilitupiliwa mbali kwa ajili ya technicalities zinazohusu zile voting machines za Florida. Hii ilikuwa mbaya zaidi kuliko ya Jecha kusema kulikuwa na irregularities za uchaguzi na kusema urudiwe.

Marekani wana legal system yao na tunajua ni nani hasa anaeamua nani mshindi - sio wananchi. Hayo tuwaachie wao.

Sisi waMatumbi kweli hatuwezi kukaa chini na kutatua haya matizo wenyewe mpaka tukalielie milangoni mwa ikulu za hizi nchi za magharibi?

Turudi kwenye hoja,jecha hana mamlaka ya kufuta uchaguzi,maamuzi ya wananchi yaheshimiwe,zanzibar kwanza.
 
Last edited by a moderator:
Turudi kwenye hoja,jecha hana mamlaka ya kufuta uchaguzi,maamuzi ya wananchi yaheshimiwe,zanzibar kwanza.

Mkuu kwani mini nina ugomvi na wewe kwa hilo?

Sheria/katiba na mimi ni mbali kwa mbali. Lakini hivi sasa wajuvi wa haya mambo wanakutana kutatua haya matatizo yetu yakimjumuisha Maalim na Dr. Shein.

Kwa nini sisi maamuma wa sheria tuko hapa kijiweni kubishana sheria/katiba tusizozijua, au kwenda ikulu ya Marekani kulialia?

Mimi hasa hili la kwenda kulialia kwenye mataifa ya magharibi ndio linalonikera sana.

Sisi watu huru (au HURU? - kama huna uhakika wa uhuru wako) leo hatuwezi kuwaacha wataalamu wetu waliobobea (au niseme BOBWEA?) katika sheria kututatulia hiki kitu ila kila kukicha zogo tuuu?

Wenzangu, tutakuja heshimu/jivunia lini utu wetu?
 
Unadhani Marekani wataifanya nini Tanzania kama imeamua kurudia uchaguzi wa Zanziabar? Yaani hujui maana ya nchi huru? Kila siku kulialia kwenye mataifa ya magharibi kwa vijitatizo vidogo vidogo?

Hapa sio kuwa Zanzibar imepinduliwa. Tume yao wenyewe (ZEC) imefuta uchaguzi na kutaka urudiwe. Marekani wanaambiwa hili ili wafanye nini?

Hivi haya mawazo ya kitumwa jamani bado wengine wanayo tu?
Ni vyema ukasahihisha kauli yako.
Siyo Tume ya uchaguzi ZEC iliyofuta uchaguzi, bali ni mtu mmoja anayeitwa Jecha 'alijikurupukia' na kurikodiwa kwenye mkanda ambao ulisomwa ZBC akidai kuufuta uchaguzi huo, akisema ni kutokana na mamlaka aliyonayo, bila kuquote Ibara yoyote ndani ya Katiba ya Zsnzibar ya mwaka 1984 inayompa mamlaka hayo. Vile vile alishindwa kuquote kifungu chochote cha sheria ndani ya Zanzibar Electoral Commission Act, kinachompa mamlaka hayo ya kuufuta uchaguzi huo.
Nimesema siyo ZEC iliyofuta uchaguzi huo kwa kuwa tunapotamka chombo kinachoitwa ZEC tunamaanisha composition ya wajumbe wanaounda Tume hiyo ya uchaguzi ambao ni Mwenyekiti wa Tume na Makamu wake pamoja na wajumbe wengine ambao ni makamishina wa Tume hiyo, ambapo wajumbe wenzake wa Tume hiyo walilikana tamko hilo la mwenzao Jecha kwa kuwa halikutokana na kikao cha pamoja na kuamuliwa kama ambavyo matakwa ya kisheria ya ZEC yanavyotaka.
Kutokana na watawala wa Zanzibar kutambua kuwa tamko la Jecha lilitokana na shinikizo lao na kutambua kuwa lilikuwa batili, ndiyo maana tokea atamke tamko lake hilo 'wamemficha' mahali pasipojulikana ili wamwepushe na hasira za wananchi ambao walitumia haki yao ya kidemokrasia ya kumchagua kiongozi wanayemtaka halafu akajitokeza mtu huyo anayeitwa Jecha na kuwapora haki yao hiyo!
 
Tume imefuta uchaguzi baada ya jeshi la kivamizi la Tanganyika JWTZ kuzingira kituo cha matangazo na kuondoka na mwenyekiti wa tume ambaye record ya video ya kuufuta uchaguzi ilionyeshwa kwenye tv .

Mpaka wakati huu Mwenyekiti wa Tume yuko chini ya ulinzi wa WAVAMIZI kutoka Tanganyika

Baada ya usalama was taifa kuingilia tume ya uchaguzi
 
Back
Top Bottom