Mgao umeanza tena?

Nauliza kama mgao umeanza upya..manake toka jana kijitonyama tanesco wanachukua umeme wao saa kumi na mbili asubuhi na kurudisha kumi na mbili jioni...hii imekaaje?
<br />
<br />
huku arusha tangu j.pili hadi leo asubuhi ndo umeme umeonekana na kwa muda huu wameshachukua mali yao!
 
Sidhani kama kuna mgawo tatizo lenu hamjalipa bili za Tanesco mnazodaiwa mnasingia mgawo !!!
Huu sio uhuru wa mawazo ila ni upumbavu unaofanya.Usidhani JF ni ya watoto wadogo kama hauna cha maana kuandika si uache
 
Ndio ukweli watu wana madeni kibao ya Tanesco, unategemea umeme wapewe bure, hakuna ! ni bora wakatiwe tu

Kwa hiyo na watu wanaotumia umeme wa luku nao wana madeni
Fikiria kabla ya kuongea na usijaze upupu wako hapa bila kufikiri
May be wewe ndo unayedaiwa mpaka unatufanya tunakosa umeme
 
Nauliza kama mgao umeanza upya..manake toka jana kijitonyama tanesco wanachukua umeme wao saa kumi na mbili asubuhi na kurudisha kumi na mbili jioni...hii imekaaje?
Afadhali ninyi wanawapa baada ya masaa 12 kuna maeneo huko kanda ya ziwa wanalia hawajauona leo ni siku ya tatu. Halafu ninyi mnamlaumu Ngeleja wakati mnapata 'baada ya masaa machache tu!'
 
Kuna mwana jf mmoja humu ana signature inasema "mitanzania ndivyo tulivyo" mimi nakubaliana nayo sana hii kwa sababu kila siku tumekuwa wa kudanganywa na sirikali hii hii na hatufanyi lolote kuonyesha tumekasirika!, ebu tazama suala la mafuta yameshushwa wauzaji wakagoma serikali ikatupiga changa la macho kuwa inachukua hatua kali, bajeti imepita bei imepanda kushinda ilivyokuwa awali. Mgao wa umeme ndio kama mnavyouelezea hapa, je si tunafanyiwa kwa sababu ndivyo tulivyo?!

Kitu kingine mnisaidieni jamani ule mchakato wa katiba mpya umefikia wapi?! 2015 iko mlangoni hivi itakamilika ili uchaguzi uwe huru na haki kweli?!

Sio siri naanza kuwa na wasiwasi na makamanda wetu mjengoni naona kama wamenunuliwa vile!! mbona mambo haya nao hawayapigii kelele wanakubali kupigwa changa la macho kama sisi tulioko nje ya mjengo?!!
 
Serikali ya CCM imewadekeza sana nyinyi, hata ninyi wa kijitonyama mnataka umeme? ili mfanyie nini kwa mfano? Haya madai kuna siku watu wa mbagara charambe nao watadai taa za bara barani kama wa magomeni.
<br />
<br />
nduka umetukuka kwa uongo na kuwa na fikira finyu kama waziri wa ulinzi serikali ya sadam hussen Iraq tungekuwa misri mda huu ungenyonywa mdomo.
 
Nyie hamjui mchezo wa Tanesco. Wanapiga mgao mikoa ABC huku wakitoa umeme masaa tele kwa mikoa XYZ, baadaye wanageuza kibao kwa kutoa mgao kwa mikoa XYZ huku wakitoa umeme masaa kibao kwa mikoa ABC. Hii inapunguza kunung'unika, maana wadanganyika ni wasahaulifu sana.
 
Nauliza kama mgao umeanza upya..manake toka jana kijitonyama tanesco wanachukua umeme wao saa kumi na mbili asubuhi na kurudisha kumi na mbili jioni...hii imekaaje?
Nyie hamjui mchezo wa Tanesco. Wanapiga mgao mikoa ABC huku wakitoa umeme masaa tele kwa mikoa XYZ, baadaye wanageuza kibao kwa kutoa mgao kwa mikoa XYZ huku wakitoa umeme masaa kibao kwa mikoa ABC. Hii inapunguza kunung'unika, maana wadanganyika ni wasahaulifu sana!!!
 
<font color="#a52a2a"><b>Huna uhakika umeisha sema unaskia,tafuta ukweli kwanza ! mgawo uliisha isha !</b></font>
<br />
<br />

we geniusbrain una matatzo gani?
Mi nilidhani unaikingia tu CCM kifua, kumbe hadi TANESCN! Hv ninavyoandika hii thread, umeme ndo umekata, nilikuw ninasoma kesho nina mtihan asubuh!
U must be Ant-development, then acha ushamba wa mawazo!
 
Tuliwaonjesha kidogo ili kupoza ishu bajeti ipitishwe kwanza..awamu hii mpaka mjuute kuwafahamu tanesco.!
 
Nauliza kama mgao umeanza upya..manake toka jana kijitonyama tanesco wanachukua umeme wao saa kumi na mbili asubuhi na kurudisha kumi na mbili jioni...hii imekaaje?

Mgawo umeongezeka zaidi ya mara dufu. kwani shida nini wakati bajeti imeshapita? mgawo mpaka masaa 20 kwa siku
 
Huna uhakika umeisha sema unaskia,tafuta ukweli kwanza ! mgawo uliisha isha !
tatizo lako unataka utukanwe. watu masaa 24 majenereta yananguruma we unasema mgawo umeisha. ukitukaniwa mama yako ni haki yako kabisa.
 
Back
Top Bottom