Victor Mlaki
JF-Expert Member
- May 1, 2016
- 3,557
- 3,465
Napenda kuipongeza tume kwa kufanya kazi nzuri ya kuhakikisha walimu wanapatiwa huduma kuendana na mahitaji ya kiteknolojia ya sasa. Jambo hili kwa kweli linatia moyo na limeisogeza huduma mikononi mwa walaji.
Masikitiko yangu makubwa ni kuona mfumo huu muhimu wa Taarifa za walimu ukiacha ombwe la utambuzi wa elimu, licha ya uwepo wa hamasa ya kujiendeleza kielimu. Mfumo huu hauna uchaguzi wa kujaza taarifa kama Mwalimu amejiendeleza na kuwa na elimu katika ngazi ya uzamili.
Huwa najiuiliza ni kigezo kipi kinachotumiwa kuhalalisha kuwa ualimu mwisho ni shahada ya kwanza au postgraduate diploma?. Ualimu ndiyo fani inayojihusisha na elimu kwa upana na undani wake hivyo kitendo cha kuweka ukomo fulani ni fedheha.
Ipo wapi haja ya elimu ya watu wazima "lifelong education" ikiwa mifumo yetu inabagaza ngazi za elimu na kuzifanya kama kwamba hazipo?. Elimu katika ngazi yoyote ni uwekezaji wenye mrejesho jamii na binafsi, kupo wapi hata kutambua tu ngazi hizo za elimu katika kada ya ualimu wa shule zinazotoa elimu ya msingi?.
Masikitiko yangu makubwa ni kuona mfumo huu muhimu wa Taarifa za walimu ukiacha ombwe la utambuzi wa elimu, licha ya uwepo wa hamasa ya kujiendeleza kielimu. Mfumo huu hauna uchaguzi wa kujaza taarifa kama Mwalimu amejiendeleza na kuwa na elimu katika ngazi ya uzamili.
Huwa najiuiliza ni kigezo kipi kinachotumiwa kuhalalisha kuwa ualimu mwisho ni shahada ya kwanza au postgraduate diploma?. Ualimu ndiyo fani inayojihusisha na elimu kwa upana na undani wake hivyo kitendo cha kuweka ukomo fulani ni fedheha.
Ipo wapi haja ya elimu ya watu wazima "lifelong education" ikiwa mifumo yetu inabagaza ngazi za elimu na kuzifanya kama kwamba hazipo?. Elimu katika ngazi yoyote ni uwekezaji wenye mrejesho jamii na binafsi, kupo wapi hata kutambua tu ngazi hizo za elimu katika kada ya ualimu wa shule zinazotoa elimu ya msingi?.