Mfumo jike ni tiba ya mfumo dume?

Mfumo jike ni tiba ya mfumo dume?

Himidini

JF-Expert Member
Joined
May 8, 2013
Posts
5,534
Reaction score
4,190
++
Ndugu wana JF nimekuwa nikitazama kwa makini mwenendo wa haki za wanawake au haki sawa ktk siasa,uchumi,tamaduni,ndoa na mahusiano mengineyo ya kijamii.
Jambo ambalo lipo wazi ni kuwa harakati hizi ni zinapata mafanikio sana Lakini zipo dalili nyingi kuwa tunajenga mfumo jike taratibu na kwa nia njema.

Hoja yangu ni hii Je,,ni kweli kuwa Mfumo jike ukiimarika ndipo ukombozi kamili wa mwanamke utatimia?
Bila shaka mwanamke ameonewa kwa miaka mingi chini ya mfumo dume Je,mfumo jike ukiwepo mfumo dume utatibika?
++

Kwa kuwa hili ni jukwaa la great thinkers,,naomba tujadiliane.KARIBUNI
++
 
Napita tu wakuu_maake mimi sio mtaalamu wa hii mifumo mkuu
 
Kwa mtazamko wangu mfumo jike ukiimarika bado hauwezi kumsaidia mwanamke kujikomboa . Hii inatokana na kwamba mwanamke aliyeko mbali na mji si rahisi kumfikia kumbuka harakati hizi zina mapungufu mengi. Nakumbuka wakati flani niliona mwanamke ameonewa ie ameumizwa na mumewe hata kusababishiwa ulemavu . Basi taasisi flani ilikwenda kumuona mwanamke yule na ikachukua picha lkn haikufanya chochote zaidi ya taasisi yenyewe kupata mtaji kwa kutumia zile picha .

Sasa hizi harakati za ukombozi wa mwanamke zimezungukwa na waroho so kumfikishia elimu mlengwa itakua kazi sana. Mwaname anaeteseka au anaehitaji ukombozi hasa ni yule aliyeko kijijni mwenye majukumu mengi ikiwemo watoto na wengine kama hao. Mwanamke anayehitaji kuelimishwa ni yule anaeteseka peke yake kuitunza familia baba yuko kwenye ulabu. Mimi bado nina mashaka na hizi harakati za ukombozi wa mwanamke toka kwenye mfumo kandamizi. Unajua kwa sababu gani huyu mwnamke anahitaji kuelimishwa namna mfumo dume unavyomkandamiza na faida za ukombozi . Sasa kama wahusika wanatazama kiendacho kinywani itakua ngumu kuufikia ukombozi na hatimaye utabaki kwenye makaratasi na maofisini bila kusahau safari za ulaya na makongamano mbali mbali.

Nahitimisha kwa kusema itachukua muda mrefu mfumo jike kuimarika na naiona kama nightmare.Pia elimu yoyote inapotolewa inatakiwa ieleze faida na hasara za mfumo dume na mfumo jike. Ni vema walengwa wakapewa elimu juu ya pande zote mbili na mwisho mwanamke na mwanaume afundishwe kuishi kwa kuchanganya mifumo yote miwili kwani ukiishi kwa kufuata mfumo mmoja tu lazima patakua na mapungufu na mwisho tena tutaanza harakati za kumkomboa mwanaume.
 
Kwa mtazamko wangu mfumo jike ukiimarika bado hauwezi kumsaidia mwanamke kujikomboa . Hii inatokana na kwamba mwanamke aliyeko mbali na mji si rahisi kumfikia kumbuka harakati hizi zina mapungufu mengi. Nakumbuka wakati flani niliona mwanamke ameonewa ie ameumizwa na mumewe hata kusababishiwa ulemavu . Basi taasisi flani ilikwenda kumuona mwanamke yule na ikachukua picha lkn haikufanya chochote zaidi ya taasisi yenyewe kupata mtaji kwa kutumia zile picha .

Sasa hizi harakati za ukombozi wa mwanamke zimezungukwa na waroho so kumfikishia elimu mlengwa itakua kazi sana. Mwaname anaeteseka au anaehitaji ukombozi hasa ni yule aliyeko kijijni mwenye majukumu mengi ikiwemo watoto na wengine kama hao. Mwanamke anayehitaji kuelimishwa ni yule anaeteseka peke yake kuitunza familia baba yuko kwenye ulabu. Mimi bado nina mashaka na hizi harakati za ukombozi wa mwanamke toka kwenye mfumo kandamizi. Unajua kwa sababu gani huyu mwnamke anahitaji kuelimishwa namna mfumo dume unavyomkandamiza na faida za ukombozi . Sasa kama wahusika wanatazama kiendacho kinywani itakua ngumu kuufikia ukombozi na hatimaye utabaki kwenye makaratasi na maofisini bila kusahau safari za ulaya na makongamano mbali mbali.

Nahitimisha kwa kusema itachukua muda mrefu mfumo jike kuimarika na naiona kama nightmare.Pia elimu yoyote inapotolewa inatakiwa ieleze faida na hasara za mfumo dume na mfumo jike. Ni vema walengwa wakapewa elimu juu ya pande zote mbili na mwisho mwanamke na mwanaume afundishwe kuishi kwa kuchanganya mifumo yote miwili kwani ukiishi kwa kufuata mfumo mmoja tu lazima patakua na mapungufu na mwisho tena tutaanza harakati za kumkomboa mwanaume.

++
asante Ablessed
Nimeona maana ya Id yako.

++
 
Last edited by a moderator:
Suluhisho ni mifumo yote miwili yaani MFUMO JIKE NA MFUMO DUME Kuungana kutafuta ufumbuzi. Nenda Nyeri nchini Kenya uone MFUMO JIKE unavyotesa waume!
 
Suluhisho ni mifumo yote miwili yaani MFUMO JIKE NA MFUMO DUME Kuungana kutafuta ufumbuzi. Nenda Nyeri nchini Kenya uone MFUMO JIKE unavyotesa waume!

++

asante sana Sasa sijui mfumo huo utazaliwa vipi? Tutauitaje.....

++
 
wanawake mnadai haki kwenye makaratasi
fanyeni kazi muone kama hamtautokomeza mfumo dume kimya kimya.
you are real great thinker. We waache wapigew kelele we wasijishughulishe na kusoma na kufanya kazi waendelee kuwategemea wanaume halafu wategemee kuondokana na mfumo dume
 
ndeyo asante kwa kuona hilo pia
you are real great thinker. We waache wapigew kelele we wasijishughulishe na kusoma na kufanya kazi waendelee kuwategemea wanaume halafu wategemee kuondokana na mfumo dume
 
Last edited by a moderator:
Tatizo nilionalo kwa hao wanaotetea mfumo jike kuwa unakandamizwa hakuna la maana walilolifanya kuhakikisha kuwa kuwa wanatetea kile wanachokisema. hakuna uhalisia wala hakuna mtetezi wa hao wanaosemwa kuwa wanateseka kwa kuwepo mfumo dume ila wanaongelea jukwaani tuu na kwenye makaratasi na semina na warsha na makongamano kibao ila ukweli halisi hakuna wanalofanya kumtetea mwanamke anayenyanyasika tena wa kijijini ambako hizo warsha na semina hazifiki
Yaani imekuwa ni biashara ya kutafuta fedha za wafadhili mbalimbali ila hakuna uhalisia wa kumtetea mwanamke ambaye anahangaika kule kijijini
Na inafikia mpaka unaona kuwa hao watetezi wanamjua mwanamke wa mjini tuu ndo maana wanatumia muda na resources nyingi kumtetea huyo wa mjini na wanasahau wanaonyanyasika kwa wingi wako kijijini ambako hata mawasiliano hakuna
 
you are real great thinker. We waache wapigew kelele we wasijishughulishe na kusoma na kufanya kazi waendelee kuwategemea wanaume halafu wategemee kuondokana na mfumo dume
++Lakini ukikanyagwa lazima useme umeumia Pengine si kelele ni kutaka kusikika?++
 
Tiger ana thread imefanana na hii kwa mbali. Kiranga alichangia constructively kule.
Sina link, ningeiweka
 
Last edited by a moderator:
Tatizo nilionalo kwa hao wanaotetea mfumo jike kuwa unakandamizwa hakuna la maana walilolifanya kuhakikisha kuwa kuwa wanatetea kile wanachokisema. hakuna uhalisia wala hakuna mtetezi wa hao wanaosemwa kuwa wanateseka kwa kuwepo mfumo dume ila wanaongelea jukwaani tuu na kwenye makaratasi na semina na warsha na makongamano kibao ila ukweli halisi hakuna wanalofanya kumtetea mwanamke anayenyanyasika tena wa kijijini ambako hizo warsha na semina hazifikiYaani imekuwa ni biashara ya kutafuta fedha za wafadhili mbalimbali ila hakuna uhalisia wa kumtetea mwanamke ambaye anahangaika kule kijijini Na inafikia mpaka unaona kuwa hao watetezi wanamjua mwanamke wa mjini tuu ndo maana wanatumia muda na resources nyingi kumtetea huyo wa mjini na wanasahau wanaonyanyasika kwa wingi wako kijijini ambako hata mawasiliano hakuna
++Na je jitihada hizi zikifika kijijini Itakuwa mfumo jike unaondoka?++
 
Mfumo jike unaweza fanya kazi endapo tu tutafuata mila na desturi za kimagharibi!

Ni ngumu mfumo jike kuota mizizi katika jamii ambayo ina heshimu mila na desturi tulizozikuta na tukaamua kuzifuata. Ni nadra kumkuta mtoto wa kike analinda sungusungu nyakati za usiku, tumekua na kukuta iko hivyo, mtoto wa kiume ataambiwa kachunge ng'ombe na wa kike kaoshe vyombo. Hivi vitu kwa wana harakati wa kimagharibi wanaita mfumo kandamizi. (Mfumo dume)

Tumekua na kulelewa katika mila na desturi hiyo hapo juu, na hii imefikia hatua hata unapotoka out na girlfriend wako (baadhi) uamini mwanaume ndio atalipia kila kitu. Kwa wenzetu (western countries) mambo ni tofauti, wao wanaamini katika kushare zaidi.

Kwa maoni yangu niseme mfumo jike hautaweza kushika hatamu mpaka tutakapofuata mila zao!
 
Back
Top Bottom