Lole Gwakisa
JF-Expert Member
- Nov 5, 2008
- 4,728
- 2,259
Hii imetokea siku ya mwisho ya mwaka 2009, sehemu fulani mawinguni huko!
Kambarage:Ah! ngoja nikapumzike hapo nje kwenye kibaraza changu hapo
nje, nimechoka kusoma.
Mhhh! nani yule anakuja, kama namfahamu,si Rashidi yule??
Waooo!! Simba wa Vita karibu sana huku kwenye utulivu.
Nilijua utakuja muda si mrefu, maana jana nilidokezwa na
Mkuu wa Kaya huku, kuwa yule mwadilifu mliyekuwa pamoja ndio yuko njiani anakuja
Rashidi : Loh, ahsante sana kaka yangu Julius.
Kumbe safari uliyoipita ilikuwa ngumu kweli kweli, lakini
nashukuru nimefika ingawaje nimechoka kweli kweli
Kambarage: Huku ulikokuja ni kwa watu waadilifu, tena nyumba yako
ilee inayowaka taa, kuna kila kitu unachopenda mle.
Rashidi : Duh! na Sofia yumo mle?
Kambarage: Nilimwona juzi akisafisha safisha sebule, alisikia juu ya
ujio wako!
Rashidi :Niambie kaka yangu Julius, Sokoine yu wapi?
Kambarage: Ngoja kwanza, tulia keti hapo. Nipe habari za huko
nyumbani Tanzania, nasikia kunaitwa bongo siku hizi!
Nilimwacha Mkapa kwenye usukani
Rashidi :Julius, Julius nimefika na moyo mzito sana
Tulichopigania wakati wa uhuru Mkapa ndo kakirudisha kwa
wanyonyaji leo hii.
Kijana yule uliyekataa hata kunywa naye chai leo ndiye
rais.Lakini yeye hana matatizo ila yule kijana mwingine
Lowassa uliyemkataa kwa kupata utajiri wa kutisha ana
msumbua sana Kikwete.
Kambarage:Loh! Loh! Loh! na chama changu je??
Rashidi : Huko ndo usiseme!
Nashindwa kukiita kuwa ni chama cha mapinduzi,bora kinge
badilishwa kuwa chama cha kuwaasi wananchi.Kuna ufisadi
yaani wizi wa kila aina.Unakumbuka lile jengo la Vijana
lililojengwa kwa msaada wa waKorea?,kiwanja kimeuzwa sijui
au kuingia ubia na wanyonyaji. Vile vile ule mradi wa kina mama
pale Morocco mambo yale yale! Nina hofu na Lumumba.
Yule kijana wako Kingunge mkomunisti, leo amekuwa mjasiria
mali mjanja mjanja .
Kambarage: Basi ! basi ! Basi! Rashidi tulia kidogo na kapumzike!
Mimi ngoja nikasali kwa siku nzima ya leo.
Kesho nionane na Mkuu wa Kaya!
Kambarage:Ah! ngoja nikapumzike hapo nje kwenye kibaraza changu hapo
nje, nimechoka kusoma.
Mhhh! nani yule anakuja, kama namfahamu,si Rashidi yule??
Waooo!! Simba wa Vita karibu sana huku kwenye utulivu.
Nilijua utakuja muda si mrefu, maana jana nilidokezwa na
Mkuu wa Kaya huku, kuwa yule mwadilifu mliyekuwa pamoja ndio yuko njiani anakuja
Rashidi : Loh, ahsante sana kaka yangu Julius.
Kumbe safari uliyoipita ilikuwa ngumu kweli kweli, lakini
nashukuru nimefika ingawaje nimechoka kweli kweli
Kambarage: Huku ulikokuja ni kwa watu waadilifu, tena nyumba yako
ilee inayowaka taa, kuna kila kitu unachopenda mle.
Rashidi : Duh! na Sofia yumo mle?
Kambarage: Nilimwona juzi akisafisha safisha sebule, alisikia juu ya
ujio wako!
Rashidi :Niambie kaka yangu Julius, Sokoine yu wapi?
Kambarage: Ngoja kwanza, tulia keti hapo. Nipe habari za huko
nyumbani Tanzania, nasikia kunaitwa bongo siku hizi!
Nilimwacha Mkapa kwenye usukani
Rashidi :Julius, Julius nimefika na moyo mzito sana
Tulichopigania wakati wa uhuru Mkapa ndo kakirudisha kwa
wanyonyaji leo hii.
Kijana yule uliyekataa hata kunywa naye chai leo ndiye
rais.Lakini yeye hana matatizo ila yule kijana mwingine
Lowassa uliyemkataa kwa kupata utajiri wa kutisha ana
msumbua sana Kikwete.
Kambarage:Loh! Loh! Loh! na chama changu je??
Rashidi : Huko ndo usiseme!
Nashindwa kukiita kuwa ni chama cha mapinduzi,bora kinge
badilishwa kuwa chama cha kuwaasi wananchi.Kuna ufisadi
yaani wizi wa kila aina.Unakumbuka lile jengo la Vijana
lililojengwa kwa msaada wa waKorea?,kiwanja kimeuzwa sijui
au kuingia ubia na wanyonyaji. Vile vile ule mradi wa kina mama
pale Morocco mambo yale yale! Nina hofu na Lumumba.
Yule kijana wako Kingunge mkomunisti, leo amekuwa mjasiria
mali mjanja mjanja .
Kambarage: Basi ! basi ! Basi! Rashidi tulia kidogo na kapumzike!
Mimi ngoja nikasali kwa siku nzima ya leo.
Kesho nionane na Mkuu wa Kaya!