Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 116,476
- 215,295
Alex Msama anatangaza kila mahali nchini Tanzania kwamba anaanda Tamasha la Pasaka , ambapo inadaiwa Wasanii mbalimbali wa nyimbo za injili watatumbuiza , Hakuishia hapo ameendelea kudai kwamba Mtume na Nabii Boniface Mwamposa atatoa neno .
Kilichonishangaza ni Maelezo kwamba , pamoja na kwamba ni Tamasha la Pasaka lakini pia ni sherehe ya miaka miwili ya Urais wa Samia Suluhu Hassan , na kwamba Mgeni Rasmi wa Tamasha hilo ni Nape Nnauye , ambaye ni Waziri wa Habari
Labda kwa kumbukumbu hasa kwa wale ambao hawamfahamu Alex Msama , ni hivi , huyu Alex Msama ni Kada mtiifu wa ccm anayejificha kwenye matamasha ya Injili , ambapo amekuwa akitumia Taasisi inayoitwa Msama Promotion , aliwahi kuendesha vipindi vya kwaya za Jumapili Clouds FM , huku lengo lake kuu likiwa kujitangaza yeye binafsi , Msama ni mwanaccm aliyejaribu kugombea karibu kila kitu kwenye chama hicho na mara zote ameangukia pua , alifanya hivyo akidhani matamasha ya Kwaya yatambeba .
Kitendo cha kuchanganya Tamasha la Pasaka na sherehe za miaka miwili ya Urais wa Samia Suluhu Hassan , hakieleweki , na ni ishara kwamba huyu ametumia Pasaka kutapeli watu huku lengo lake kuu likiwa ni kusherehekea Miaka miwili ya Samia Madarakani , ili labda huko mbele akumbukwe kwenye teuzi , Lakini kwanini Msama atumie Pasaka kwa ajili ya sherehe za urais wa Samia , mbona angeweza tu kuandaa tamasha la sherehe za miaka miwili ya Samia na angekubaliwa tu ? kingine ni hiki , Nape Nnauye hatujui hata kama aliwahi kupata Kipaimara , sasa mtu kama huyu anawezaje kuwa mgeni rasmi kwenye Tamasha la kidini tena la shughuli nyeti kama ya Pasaka ?
Nachukua nafasi hii kumkumbusha Nabii Mwamposa kuwa Makini na kutumika kwenye matamasha haya ya kisiasa yaliyovikwa majina ya kidini , yeye angebaki Tanganyika Parkers kuendelea kufungua watu , hawa akina Msama watampoteza .
Naomba kuwasilisha .
Kilichonishangaza ni Maelezo kwamba , pamoja na kwamba ni Tamasha la Pasaka lakini pia ni sherehe ya miaka miwili ya Urais wa Samia Suluhu Hassan , na kwamba Mgeni Rasmi wa Tamasha hilo ni Nape Nnauye , ambaye ni Waziri wa Habari
Labda kwa kumbukumbu hasa kwa wale ambao hawamfahamu Alex Msama , ni hivi , huyu Alex Msama ni Kada mtiifu wa ccm anayejificha kwenye matamasha ya Injili , ambapo amekuwa akitumia Taasisi inayoitwa Msama Promotion , aliwahi kuendesha vipindi vya kwaya za Jumapili Clouds FM , huku lengo lake kuu likiwa kujitangaza yeye binafsi , Msama ni mwanaccm aliyejaribu kugombea karibu kila kitu kwenye chama hicho na mara zote ameangukia pua , alifanya hivyo akidhani matamasha ya Kwaya yatambeba .
Kitendo cha kuchanganya Tamasha la Pasaka na sherehe za miaka miwili ya Urais wa Samia Suluhu Hassan , hakieleweki , na ni ishara kwamba huyu ametumia Pasaka kutapeli watu huku lengo lake kuu likiwa ni kusherehekea Miaka miwili ya Samia Madarakani , ili labda huko mbele akumbukwe kwenye teuzi , Lakini kwanini Msama atumie Pasaka kwa ajili ya sherehe za urais wa Samia , mbona angeweza tu kuandaa tamasha la sherehe za miaka miwili ya Samia na angekubaliwa tu ? kingine ni hiki , Nape Nnauye hatujui hata kama aliwahi kupata Kipaimara , sasa mtu kama huyu anawezaje kuwa mgeni rasmi kwenye Tamasha la kidini tena la shughuli nyeti kama ya Pasaka ?
Nachukua nafasi hii kumkumbusha Nabii Mwamposa kuwa Makini na kutumika kwenye matamasha haya ya kisiasa yaliyovikwa majina ya kidini , yeye angebaki Tanganyika Parkers kuendelea kufungua watu , hawa akina Msama watampoteza .
Naomba kuwasilisha .