Mfalme Abdallah wa Jordan na Rais El Sisi wa Misri waitaka Israel ifungue mpaka haraka

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,192
10,928
Juhudi za kuwafikishia raia wa Palestina misaada kwa haraka zimepata nguvu baada ya washirika wawili muhimu wa Israel kupaza sauti zao kwa pamoja.

Mfalme Abdallah hapo juzi Alkhamis alitua Cairo bila mwaliko akitokea Italia,Uiengereza na Ujerumani kushauriana na viongozi wa nchi hizo kuhusiana na mashambulizi yanayoendelea huko Gaza kutoka jeshi la Israel.

Katika mkutano wao huo wote walikubaliana kutoruhusu wapalestina kufanywa wakimbizi kwa mara nyengine.Badala yake wamesisitiza Israel wafungue mipaka yake na hasa upande wa Misri ili misaada ya chakula na mahitaji mengine iwafikie wapalestina.

Katika nchi ya Misri maandamano yamepigwa marufuku kwa muda mrefu,hata hivyo jana Ijumaa raisi mwenyewe ndiye aliyeyapa kibali.

Katibu mkuu wa umoja wa mataifa naye ameonekana kukemea kwa ukali kitendo cha Israel kukataa kufungua mpaka ili misaada inayosubiri mpakani iweze kuingia Gaza.

Misaada hiyo imeelezwa isipoingia katika kipindi cha masaa 24 yajayo wapalestina wataanza kufa kwa njaa na kiu kwani wamezuilika kujitafutia riziki zao kutokana na kudondoshewa mabomu mfululizo kutoka jeshi la Israel.

Egypt's El Sisi and Jordan's King Abdullah call for 'immediate stop' to Israel-Gaza war

1697864491816.png
 
Nimeona wamisr wengi wameandamana wanataman wavunje geti wanasema wapo tayar kwa vita,,,inasikitisha sana mtu ufungiwe hamna maji,chakula,umeme,etc misaada pia izuiliwe hata kama ni roho ya ushetani hiki kiwango ni chakutishaunyama wanaofanyiwa wa palestina
 
Nimeona wamisr wengi wameandamana wanataman wavunje geti wanasema wapo tayar kwa vita,,,inasikitisha sana mtu ufungiwe hamna maji,chakula,umeme,etc misaada pia izuiliwe hata kama ni roho ya ushetani hiki kiwango ni chakutishaunyama wanaofanyiwa wa palestina
Ndio maana wote wanazunguka halafu wanaishia Misri.Wanajua kipi kitakachotokea pindi Elsisi atakapoingiwa na imani ya hali ya juu akafungua geti.Wataanza askari wake kwanza kuvuka kabla ya wananchi. Kule Jordan geti limewekwa mbali sana na raia kwani nako wakati wowote mambo yakizidi hakuna wa kuwazuia asilimia 80 ya raia hao kukanyaga kwa mguu mpaka Jericho.
1697872773448.png
 
Sasa ule mpaka ktk Mji wa Arafa aliyefunga ni Israel? hapo ndipo unafiki wa Mwarabu unaonekana maana waliambiwa funguwa mpaka wao wakasema hawafungui maana ni janja ya Israel kuwatoa watu Gaza ili wajimilikishe ardhi sasa waanze wao kufunguwa halafu mengine yafwate. Na kosa lingine huyo King kwanza amaekwenda ulaya kuwasiliana na wakubwa halafu ndio anarudi na maigizo ya kutuwa Misri na amri mpya ya Israel wafunguwe mipaka? Narudia kusema hii vita ina mambo mengi sana yapo Nyuma ya Pazia kuyajua ni vigumu sana maana wakubwa wote wamewekeza macho na nguvu hapo wao ndio wanajua, kwa macho ya kawaida ni vigumu kujuwa mpaka uwe mmoja ktk wao.
 
Juhudi za kuwafikishia raia wa Palestina misaada kwa haraka zimepata nguvu baada ya washirika wawili muhimu wa Israel kupaza sauti zao kwa pamoja.

Mfalme Abdallah hapo juzi Alkhamis alitua Cairo bila mwaliko akitokea Italia,Uiengereza na Ujerumani kushauriana na viongozi wa nchi hizo kuhusiana na mashambulizi yanayoendelea huko Gaza kutoka jeshi la Israel.

Katika mkutano wao huo wote walikubaliana kutoruhusu wapalestina kufanywa wakimbizi kwa mara nyengine.Badala yake wamesisitiza Israel wafungue mipaka yake na hasa upande wa Misri ili misaada ya chakula na mahitaji mengine iwafikie wapalestina.

Katika nchi ya Misri maandamano yamepigwa marufuku kwa muda mrefu,hata hivyo jana Ijumaa raisi mwenyewe ndiye aliyeyapa kibali.

Katibu mkuu wa umoja wa mataifa naye ameonekana kukemea kwa ukali kitendo cha Israel kukataa kufungua mpaka ili misaada inayosubiri mpakani iweze kuingia Gaza.

Misaada hiyo imeelezwa isipoingia katika kipindi cha masaa 24 yajayo wapalestina wataanza kufa kwa njaa na kiu kwani wamezuilika kujitafutia riziki zao kutokana na kudondoshewa mabomu mfululizo kutoka jeshi la Israel.

Egypt's El Sisi and Jordan's King Abdullah call for 'immediate stop' to Israel-Gaza war

View attachment 2787908
Wa Arab na porojo zao, wanajua kupiga kelele na maneno tu, ndugu zenu wanapigwa, nyie mnatoa matamko tu! Russia ilipoivamia Ukraine, si mliona wazungu walichofanya kulinda ndugu zao?
Na nyie tangazeni, "No, fly zone ndani ya anga ya GAZA" Kuzuia ndege za Israel kushambulia,
Mlikaa kimya,wakati Ghadafi wa Libya, anakula kichapo cha mbwa mwizi, kutoka NATO na USA, sasa hv, mnafura hasira, hamfanyi chochote zaidi ya, maneno!
Undeni umoja wa kijeshi wa kiarab, Arab nations, military and defence Force.
Bila hivyo hawa, Judeo Christians, watawachezea Sana.
 
Juhudi za kuwafikishia raia wa Palestina misaada kwa haraka zimepata nguvu baada ya washirika wawili muhimu wa Israel kupaza sauti zao kwa pamoja.

Mfalme Abdallah hapo juzi Alkhamis alitua Cairo bila mwaliko akitokea Italia,Uiengereza na Ujerumani kushauriana na viongozi wa nchi hizo kuhusiana na mashambulizi yanayoendelea huko Gaza kutoka jeshi la Israel.

Katika mkutano wao huo wote walikubaliana kutoruhusu wapalestina kufanywa wakimbizi kwa mara nyengine.Badala yake wamesisitiza Israel wafungue mipaka yake na hasa upande wa Misri ili misaada ya chakula na mahitaji mengine iwafikie wapalestina.

Katika nchi ya Misri maandamano yamepigwa marufuku kwa muda mrefu,hata hivyo jana Ijumaa raisi mwenyewe ndiye aliyeyapa kibali.

Katibu mkuu wa umoja wa mataifa naye ameonekana kukemea kwa ukali kitendo cha Israel kukataa kufungua mpaka ili misaada inayosubiri mpakani iweze kuingia Gaza.

Misaada hiyo imeelezwa isipoingia katika kipindi cha masaa 24 yajayo wapalestina wataanza kufa kwa njaa na kiu kwani wamezuilika kujitafutia riziki zao kutokana na kudondoshewa mabomu mfululizo kutoka jeshi la Israel.

Egypt's El Sisi and Jordan's King Abdullah call for 'immediate stop' to Israel-Gaza war

View attachment 2787908
Kwanini Israel miaka yote anasaidiwa na America, Uk; France na silaha kubwa wanazo. Lkn juzi wametekwa kama anakamatwa kuku ktk kibanda chake?
 
Hao ni mapuppet wa America nchi kama Misri inaweza kuipiga Israel kwa masaa tu , lakini eti wanaomba Israel afungue mpaka pumbafu tu, hawa ndio viongozi Mwenyezi Mungu atawadhibu sana.
 
Back
Top Bottom