Wananchi Jordan waandamana kwa nguvu wakitaka mpaka ufunguliwe waingie Palestina

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,191
10,925
Joto la vita limeanza kupanda ndani ya Jordan ambayo pamoja na Misri ndizo nchi muhimu kwa usalama wa Israel.

Wananchi wa nchi hiyo hawajaridhishwa na namna nchi yao ambayo ina udugu mkubwa na Palestina kwa namna inavyoshughulikia madhila ya wapalestina na vita vya Gaza. Hata walipomuona mfalme wao akishiriki kudondosha vifurushi vya chakula Gaza haikusaidia kupunguza hamasa zao za kutaka kuingia Jerusalem.

Siku ya leo wananchi hao wamefanya maandamano makubwa wakiimba wanataka mpaka ufunguliwe waende kuwasaidia wenzao wa Palestina wanaokandamizwa na Israel.
Baadhi ya waandamanaji hao walibeba bango linalomuonesha msemaji wa Hamas ambaye hujificha uso aitwaye Abu Ubaida ambaye amepata umaarufu mkubwa katika ulimwengu wa kiarabu.Msemaji huyo amekuwa akitoa takwimu za kivita kila siku kutoka maeneo yote ya Gaza hata yale yaliyokatiwa mawasilaino ya simu na intaneti.

Sambamba na maandamano hayo ya aina yake kumetokea urushwaji wa risasi kwenye daraja la mfalme Hussein ambalo ndilo lango kuu la kuingia na kutoka kwa wapalestina wanaotoka nje ya eneo lao.Tukio hilo limepelekea kufungw kwa muda kwa daraja hilo

 
Dalili nzuri hii... let Arabs wafight and then watimuliwe Jordan yote... Ukiichokoza Israel huwezi kuilipa so Ardhi ndio Malipo halali ya kuichokoza Israel... waachiwe wavuke au walianzishie huko huko wafuatwe nao.. Mtoto akililia Wembe mpe umkate.

Muslim kila kitokeacha husema Inshallah Allah ndie anapanga, nadhani Allah ashapanga Jews warudi kwenye ardhi yao asili waliyopewa na Allah from the river to the sea.. includ Part of Iraq Medina yote ni Jews land..

This is Good news mwisho wa Dunia ufike tushachoka na migogoro isiyoisha sababu ya Allah tu
 
Wawaae waebde muisrael aongeze himaya yake ndani ya Jordan.Sababu atawavurumisha hadi maeneo ya ndani ya Jordan na kuyakalia kwa nguvu na hatayarudisha hata umoja wa mataifa upige kelele vipi harudishi

Jordan na Misri ndicho wanaogopa kujiingiza kivita Gaza wanajua ardhi yao itachukuliwa na Israel itanegwa na hairudi ndiyo imetoka hiyo
 
Wananchi wa nchi hiyo hawajaridhishwa na namna nchi yao ambayo ina udugu mkubwa na Palestina kwa namna inavyoshughulikia madhila ya wapalestina na vita vya Gaza.

HISTORIA

Siku Ya Kiza ya Mwezi septemba (Black September), pia inajulikana kama siku ya Vita vya Raia wa Jordan dhidi ya Wakimbizi wa Kipalestina waliokaribishwa Jordan, vita hiyo ya wenyeji dhidi ya wakuja ilikuwa ya silaha na iliyoongozwa na Mfalme Hussein dhidi ya Chama cha Ukombozi wa Palestina -PLO , kililoongozwa na mwenyekiti wa PLO injinia Yasser Arafat.

View: https://m.youtube.com/watch?v=DShud_iyX9s
Vita hivyo vya Jordan mnamo 1970, vilivyojulikana zaidi kama Black September, vilikuja baada ya mafanikio ya idara ya kijasusi ya Usalama wa Taifa la Jordan kubaini njama za wapalestina kutaka kumuua Mfalme Hussein wa Jorda na mkuu wake wa ujasusi. Ilikuwa ni siri kwa miaka mingi hadi ilipofichuliwa katika kumbukumbu ya afisa wa zamani wa CIA aliyekuwa akihudumu katika eneo hilo la Mashariki ya Kati wakati huo.

Rais Richard Nixon na Mshauri wa Usalama wa Kitaifa Henry Kissinger walichukua sifa kubwa kwa kusimamia mzozo wa Septemba Nyeusi, lakini kwa kweli jukumu lao lilikuwa kidogo kwa matokeo ya tishio kubwa kwa maisha ya Hussein, jeshi la Iraqi mashariki mwa Jordan.

Pia wapalestina waiingiza Lebanon katika vita ya wenyewe kwa wenyewe ambapo PLO kiliamua kuwaunga mkono jamii moja ya Lebanon dhidi ya walebanoni wakristo na wa Druze.

View: https://m.youtube.com/watch?v=q70bGTwk4VM

Lebanon ni nchi mojawapo ya KiArabu yenye wakristo wengine ambao ni wenye ushawishi katika kila nyanja na vitengo nyeti vya nchi hiyo. Wapalestina walipenyeza fitina kwa WaLebanoni wa imani tofauti wazichape vita vya wenyewe kwa wenyewe vya silaha.

Baada ya Waarabu wa mataifa mengine kuona chokochoko za wapalestina wakimbizi mamilioni waliokuwepo Jordan na Lebanon kuingiza nchi wenyeji wa wakimbizi katika vita, mabomu kulipuka mitaani, kutaka kupindua serikali za nchi zilizowakaribisha wakimbizi wa kipalestina, nchi za kiarabu zimesita kuwakaribisha wapelestina kutokana na historia hiyo mbaya.

Tamaa ya Maandamano hayo ya 2024 'wananchi' nchini Jordan ni kichaka cha wapalestina mamilioni ya wakimbizi wa kipalestina walio raia wa Jordan kuleta chokochoko tena nchini Jordan.

Mfalme Abdullah II ambaye alimrithi babaye Mfalme Hussein aliyefariki, naye yupo ktk wakati mgumu akiwachekea wapalestina ambayo ni watu wa vurugu na chokochoko na hakuna mtawala wa kiarabu anayekubali kuwakaribisha wapalestina iwe kwa mamia au maelfu kwa kuwa wanajua hila za wapalestina. Nchi za kiarabu wapo radhi kutoa misaada ya kifedha, chakula na kupaza sauti katika Umoja wa Mataifa lakini siyo kuwakaribisha kama wakimbizi katika nchi zao za kiarabu.

1711666656635.png

Mfalme Abdullah II wa Jordan
 
Baba wa King Abdullah II mfalme Hussein:
Mahojiano ya kuvutia na marehemu mfalme wa Jordani King Hussein. Televisheni ya Thames katika mahojiano ya 'Wiki Hii' ilipewa hisani ya kipekee kutoka Familia ya Kifalme ya Jordan kukubali mahojiano.

Ndani ya kipindi hiki cha televisheni tunapata kumuona Mfalme Hussein na familia yake changa, akiwemo Mfalme wa sasa (King Abdullah) akiwa mtoto. Ilionyeshwa kwa mara ya kwanza kwenye Televisheni ya Uingereza tarehe 10/02/1972

2014 6 August
A fascinating interview with the late king of Jordan. Thames Televisions 'This Week' was granted unique access to the Jordanian Royal Family. We get to see the King and his young family, including the present King (Abdullah) as a child. First shown on British Television on 10/02/1972


View: https://m.youtube.com/watch?v=rCYJchah3kY
 
Dalili nzuri hii... let Arabs wafight and then watimuliwe Jordan yote... Ukiichokoza Israel huwezi kuilipa so Ardhi ndio Malipo halali ya kuichokoza Israel... waachiwe wavuke au walianzishie huko huko wafuatwe nao.. Mtoto akililia Wembe mpe umkate.

Muslim kila kitokeacha husema Inshallah Allah ndie anapanga, nadhani Allah ashapanga Jews warudi kwenye ardhi yao asili waliyopewa na Allah from the river to the sea.. includ Part of Iraq Medina yote ni Jews land..

This is Good news mwisho wa Dunia ufike tushachoka na migogoro isiyoisha sababu ya Allah tu
We Jamaa bhana! Waache wenzio wamefunga mwezi mtukufu,mchana wanashinda bila kula halafu usiku wanakesha wanakula. Sasa mnataka kuwanyanganya maeneo yao tena mpaka Madina😃😃😃
 
Dalili nzuri hii... let Arabs wafight and then watimuliwe Jordan yote... Ukiichokoza Israel huwezi kuilipa so Ardhi ndio Malipo halali ya kuichokoza Israel... waachiwe wavuke au walianzishie huko huko wafuatwe nao.. Mtoto akililia Wembe mpe umkate.

Muslim kila kitokeacha husema Inshallah Allah ndie anapanga, nadhani Allah ashapanga Jews warudi kwenye ardhi yao asili waliyopewa na Allah from the river to the sea.. includ Part of Iraq Medina yote ni Jews land..

This is Good news mwisho wa Dunia ufike tushachoka na migogoro isiyoisha sababu ya Allah tu
Natamani wangie halafu wakitandikwa tusisikie wanaomba msaada. Waislam wajinga sana
 
Wakiachiwa wapite kisha wapigwe carpet bombing mtasema Israel inaua wananchi, hivi mpaka sasa waarabu mnasubiri nini kuivamia Israel, kazi kuvaa dera/kanzu na kubwatuka bwatuka akbar akbar lakini hamna lolote.
 
Ati kwa mjibu wa torati Jordan Iko ndani ya Israel ya kale (Ancient Israel). Jordan na Lebanon yote ni maeneo ya Israel
 
Sababu na mifano ya nchi za kiarabu kukosa msukumo wa kuungana, na kubakia tu maneno ya matumaini ya mdomoni bila dhati ya moyoni ni nyingi :

KWANINI MUUNGANO WA NCHI EGYPT NA SYRIA KUWA TAIFA MOJA LA JAMHURI YA MUUNGANI WA KIARABU (UAR) ULIFELI NA KUVUNJIKA
1711714060946.png

Jamhuri ya Muungano wa Kiarabu (UAR) ilianzishwa mwaka 1958 kama muungano wa kisiasa kati ya Syria na Misri.

Muungano huo ulionyesha hisia ya utaifa na mshikamano wa Waarabu (Pan-Arabism). Kwa kiasi kikubwa ilisukumwa na hamu ya kushinda migawanyiko ya mipaka iliyotazamwa na wengi kama uumbaji bandia wa nguvu za kikoloni za nchi kikoloni za Uropa.

Hata hivyo, umoja huo hatimaye ulisambaratika mwaka 1961 kutokana na hisia zilizoenea nchini Syria kwamba imekuwa chombo cha kuendeleza utawala wa Misri.

UMOJA WA UARABU / PAN ARABISM
Nguvu kuu ya uundaji wa UAR ilikuwa Pan-Arabism. Hisia za utaifa wa pamoja wa Waarabu tayari ziliibuka katika Mashariki ya Kati mwanzoni mwa karne ya ishirini. Mitazamo hii kwa kiasi kikubwa ilichochewa na nia ya kuondosha utawala mbovu, usio na tija, na ngeni wa Milki ya Ottoman ya Uturuki.

Uzoefu uliowaleta kujongea pamoja katika muungano uliletwa na lugha, filamu, muziki wa wasanii kadhaa maarafu wa kiarabu kama kina Umm Kulthum na utamaduni wa kawaida ulizua hisia za pamoja ambazo zilienea katika Mashariki ya Kati inayozungumza Kiarabu.

Baada ya kuteka Mashariki ya Kati wakati wa Vita vya Kwanza vya Kidunia (1914-1918), serikali za kikoloni ziligawanya Waarabu kwa kuchora mipaka ya kisiasa ambayo hapo awali haikuwapo.

Miongoni mwa mambo mengine, mgawanyiko uliwezesha Wazungu washindi kuwazawadia viongozi marafiki wa Kiarabu hali ambayo wangeweza kutawala. Kwa hivyo, viongozi wa eneo hilo, ambao uungaji mkono wao kwa Wazungu wakati wa vita hapo awali ulisukumwa na kuhusisha Uarabu na hamu ya kujiondoa kutoka kwa utawala wa kigeni wa Ottoman ya Uturuki, sasa walikuwa na motisha ya kuendelea kushirikiana na Wazungu na kuhimiza uaminifu kwa wale wadogo, walioundwa hivi karibuni. majimbo.

Takriban katika kila nchi ya Kiarabu, mipango ya umoja wa kieneo wa Waarabu ilipingwa na juhudi za kuweka hisia ya mshikamano wa kizalendo na kujitambulisha na taifa hilo jipya kupitia uundaji wa bendera ya taifa, wimbo wa taifa na alama nyingine za ndani.

Hata hivyo, teknolojia ya kisasa, sanaa ya muziki, uhamaji, na magazeti na maandishi mengine yaliyochapishwa kutokana na ongezeko la waliojua kusoma na kuandika yaliimarisha hisia ya Uarabu wa pamoja ambao ulivuka mipaka mipya ya kisiasa.

Zaidi ya hayo, tawala hizo mpya ziligundua kwamba kwa kushawishi hisia za Uarabu, zingeweza kuongeza uungwaji mkono wa wenyeji na kuendeleza uhalali wao kama marais au wafalme wa nchi hizo mpya huru.

Majaribio ya kusawazisha mielekeo iliyojaa mivutano ya Pan-Arabism na masilahi ya serikali za nchi mpya tofauti za kiarabu iliendelea kuunda siasa za Waarabu na jamii vizuri katika miongo iliyofuata. Msingi wa UAR na kuvunjika kwake kulitokana na kichocheo cha kujijengea utaifa wa kila nchi ya kiarabu.

WAASISI MUHIMU WA MUUNGANO
Waasisi wakuu nyuma ya muungano UAR walikuwa wanachama wa Ba‘thist (Syria) na Nasserites nchini Misri chini ya rais Gamal Abdel Nasser (1918–1970) wa Misri.

Syria ilipopata kuwa demokrasia mwaka wa 1954, uungwaji mkono mkubwa wa umma kwa taifa jipya la Kiarabu, linalojumuisha yote, uliakisiwa katika majukwaa ya vyama pinzani vya kisiasa. Wakomunisti na Muslim Brotherhood waliunga mkono kuvuka mipaka, ingawa Wakomunisti walipendelea uhusiano wa karibu na Muungano wa Sovieti.

Tabaka la wafanyabiashara linalokua nchini Syria liliona fursa za kiuchumi katika kukomesha mipaka na, kwa hivyo, pia liliona muungano vyema. Mienendo hii ya ndani ilipelekea Chama chenye nguvu cha Ba‘th cha Syria, kilichoongozwa na Michel ‘Aflaq (1910–1989) na Akram Hourani (1912–1996), kupendekeza wazo la jamhuri ya muungano na Misri.

Hasa, Maba‘thi, wakishabikia jukwaa la kiitikadi ambalo liliunganisha utaifa wa Kiarabu, ujamaa, na usekula, walijikuta katika mapambano ya ndani ya mamlaka dhidi ya Wakomunisti wenye kuimarisha. Chama hicho kilitarajia kuwa muungano huo ungesababisha kusambaratika kwa washindani wake wa kisiasa.

Huko Misri, wakati huo huo, "Mapinduzi ya Maafisa wa Kijeshi" mnamo 1952 yalishuhudia Kanali Nasser akinyakua mamlaka kutoka kwa Mfalme Farouk (1920-1965) na kuibuka kama rais mpya wa Misri.

Msimamo thabiti wa Nasser dhidi ya uwepo wa Waingereza katika Suez na kutaifishwa kwa mali ya kigeni ulikuwa umemfanya kuwa kiongozi anayesifika katika ulimwengu wote wa Kiarabu.

Baada ya kunusurika katika uvamizi wa Waingereza na Wafaransa na Waisraeli mwaka 1956, Nasser alionyeshwa kama shujaa mkubwa wa siku hizi wa Kiarabu mwenye uwezo wa kutetea maslahi ya ulimwengu wa Kiarabu dhidi ya madola ya kibeberu. Umaarufu wake ulimfanya kuwa mgombea aliyekubalika wa kuongoza umoja huo wa Waarabu, ingawa Nasser mwenyewe mwanzoni hakutaka kuunganisha nchi hizo mbili.

Kanali Gamal Nasser aliogopa matatizo yanayohusiana na kuunganisha mifumo miwili tofauti ya kiuchumi na kuunganisha taasisi za kiraia na kijeshi. Kwa upande mwingine, Waba‘thi katika Syria walikuwa na matumaini. Waliamini Nasser angewakabidhi utawala wa Shamu. Hatimaye, waliweza kumshawishi juu ya uwezekano wa muungano.

KUINUKA NA KUKANGUKA KWA MUUNGANO WA JAMHURI YA KIARABU - UAR

Mnamo Februari 1958 Rais Nasser wa Misri na Rais Shukri al-Kuwatli (1891-1967) wa Syria walitia saini mkataba wa muungano. Kufuatia kura ya maoni iliyofanyika kwa wakati mmoja katika nchi zote mbili, nchi hizo mbili ziliunganishwa na UAR ilizaliwa na katiba mpya ya shirikisho, Cairo ikiwa mji mkuu wake, na Nasser kama rais wake.

Uraia tofauti wa Misri na Syria ulikomeshwa. UAR ilipitisha bendera ya Misri kwa nyongeza ya nyota mbili kuwakilisha wanachama wawili wa umoja huo. Kuzaliwa kwa umoja huo kulipokelewa kwa shauku kubwa katika eneo lote la Mashariki ya Kati hivi kwamba kulifuatiwa na msururu wa majaribio ya Waarabu waunga Muungano wa Waarabu mahali pengine kupindua tawala zilizochukuliwa kuwa zinazounga mkono nchi za Magharibi. Kwa hakika, kufuatia mapinduzi ya mwaka 1958, Iraq ilitangaza nia yake ya kujiunga na UAR. Mwaka huo huo, Umoja wa Mataifa ya Kiarabu, shirikisho huru la UAR na Yemen, pia lilianzishwa.

Ingawa umoja huo hapo awali ulipokelewa kwa bashasha, nderemo na shauku kubwa katika nchi zote mbili wanachama wa UAR, upande wa pili kulikuwapo kukatishwa tamaa ndiyo ulikuwa mitazamo maarufu nchini Syria.

Tofauti ya nguvu za kimamlaka kati ya Misri na Syria ilifanya ile ya zamani kuwa nguvu ya kivita isiyopingika, licha ya muundo rasmi wa kikatiba wa shirikisho la jamhuri mpya kujaribu kuleta uwiano sawa wa mamlaka.

Mamlaka aliyopewa rais yalimfanya Gamal Nasser kuwa na nguvu isiyo ya kawaida na kumruhusu kulazimisha sera zisizopendwa za kiuchumi na kijamii nchini Syria.

Ingawa Ba‘thist Hourani wa Syria alitajwa kuwa mmoja wa makamu wanne wa rais, hakuwa na uwezo wa kufurukuta na alijiuzulu kwa maandamano mapema Desemba 1959. Ukuu wa kisiasa wa Misri uliacha nafasi ndogo sana kwa mchango wa Syria katika kusimamia masuala ya muungano. Viongozi wa serikali ya Syria, haswa wanajeshi maafisa wakuu , walihamishiwa Cairo. Kwa njia hii, Nasser angeweza kuhakikisha kuwa wametengwa na misingi yao ya nguvu. Maafisa na wanajeshi kutoka Misri walipangiwa kazi nyingine hadi Syria, ambako kwa vitendo walichukua udhibiti wa urasimu na vikosi vya usalama vya nchini Syria.

Aidha, Chama cha Ba’th Syria kilijivunja kwa kufuata marufuku ya vyama vyote vya kisiasa isipokuwa chama cha (Socialist Union)- Muungano wa Kijamii cha Nasser wa Kiarabu, sharti ambalo Gamal Nasser aliliwasilisha kabla ya kuridhia kuunganishwa na ambalo wanachama wa Ba'thi walilikubali chini ya dhana potofu kwamba Syria ingeweza, kuhifadhi kiwango cha uhuru wa ndani katika mfumo mpya wa kitaasisi. Wakomunisti na Muslim Brotherhood, wakati huo huo, walikandamizwa kikatili huku Wamisri wakizidi kuchimbia mizizi ya mamlaka yao. Vile vile, uhuru wa vyombo vya habari vya Syria vilitekwa na utawala mpya. Zaidi ya hayo, majaribio ya kulazimisha sera za kijamaa za Misri nchini Syria yaliacha tabaka la wafanyabiashara wa Syria sio tu kushindwa kufikia masoko ya Misri lakini pia kukabiliwa na vikwazo vikali vya uwezo wake wa kuendesha ndani ya sehemu ya Syria ya UAR.

Kadhalika, marekebisho ya sera na sheria za ardhi yaliwafanya wamiliki wa ardhi wakubwa Syria wasiwe na furaha. Kwa ufupi, Wasyria wa matabaka yote ya kisiasa na kijamii waliachwa wakiwa wamekata tamaa na kuhisi kana kwamba wanatawaliwa na watu wa nje.

Mapinduzi ya 1961 nchini Syria yalisababisha kujiondoa kwenye muungano UAR na kudai upya uhuru wake. Muda mfupi baadaye, pia Shirikisho la Umoja wa nchi za Kiarabu ( Iraq, Yemen, UAR, Jordan, Libya )- the United Arab Federation ulikomeshwa kufuatia ukosoaji wa Wayemeni wa sera za kijamaa kali za Nasser wa Misri.

Kwa kushuhudia uzoefu wa Syria, utawala wa Iraq pia uliamua kujiondoa kwenye umoja huo, licha ya kiapo chake cha awali cha kujitolea kujiunga. Misri ilihifadhi na kuendelea kutumia jina jina la UAR hadi 1971.

Kufuatia mapinduzi mengine ya mwaka 1963 nchini Syria, mazungumzo ya umoja yalifanyika tena, lakini bila matokeo ya mafanikio. Kushindwa kwa muungano UAR ( Misri na Syria) kuliwaacha viongozi wengi nchini Syria na mataifa mengine ya Kiarabu wakiwa wameamua kutoruhusu nchi yao kusukumwa katika nafasi hiyo ya chini.

Kwa hivyo, licha ya kuendelea kuenea kwa hisia za umoja miongoni mwa nchi za Uarabu, kuangamia kwa muungano wa UAR kulileta mwisho wa nafasi yoyote ya kweli ya kuunganisha nchi za Kiarabu katika nchi moja. Na kufikia mwisho wa miaka ya 1980, dhana ya umoja wa Waarabu wote ilikuwa imetoweka na kufa kabisa.

1711714017444.png
 
13 April 2024

JORDAN YAJIIMARISHA DHIDI YA TISHIO LA IRAN KUCHOCHEA MAPINDUZI

Vyombo vya Usalama na Ulinzi nchini Jordan vipo katika hali ya utayari kukabiliana na njama za watawala wa Iran kumuangusha Mfalme wa Jordan
 
13 April 2024

JORDAN YAJIIMARISHA DHIDI YA TISHIO LA IRAN KUCHOCHEA MAPINDUZI

Vyombo vya Usalama na Ulinzi nchini Jordan vipo katika hali ya utayari kukabiliana na njama za watawala wa Iran kumuangusha Mfalme wa Jordan
Na huenda mwisho wa yote Jordan ikapinduliwa.
Itakuwa ni hatua katika ukombozi wa Palestina
 
Back
Top Bottom