Mkuu prosper nimepitia comments za watu zote, kuna mambo makuu mawili
1) Nguvu za Giza
2) Nguvu za Mungu
Ethical ameelezea vyema kabisa kuhusu agano la kale na agano jipya, rejea kwamba agano la kale watu walikuwa wanaadhibiwa directly kwa dhambi zao ila agano jipya hakuna hilo jambo
Mleta mada anaweza kuwa sahihi au pia asiwe sahihi, dunia ya sasa hivi imeharibiwa sana kwa ujuaji na ndio sababu maandiko yanasema watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Zimezuka stori nyingi zinazohusu kuzimu na kila mtu anajikuta anaijua kuzimu sana jambo ambalo ni nadharia tupu. Pili nasikitika sana ninaposoma comments za mtu anasema kama Mleta mada ni mwongo basi weka wewe tulinganishe nani ni mwongo, hii inaonesha ni kwa kiasi gani watu hawa wameaminishwa na sio wasomaji wazuri wa maandiko hivyo hata wakiletewa ushahidi roho zao zimeshafungwa.
Huwa naonaga watu wengi wanaoandika kuhusu mambo ya kuzimu na sijawahi changia kama kina mshana, jichawi, mzizimkavu na wengineo na masikitiko yangu watu wamesahau maandiko ya Quran na Biblia na kuwa interested na topic za namna hii...akili yako ukiijaza vitu hivi basi utaishia kuamini na kusahau ukweli upo wapi.
By the way siamini swala la sala kuzuiwa angani kama ozone layer inavyozuia miale mikali ya jua kuingia duniani...shetani hana Nguvu ya kuzuia maombi yako Bali Ana Nguvu ya ushawishi, mfano kama ulipanga usali saa saba mchana basi atakutia vishawishi na usisali ila ukishikilia msimamo wako unakuwa umemshinda. Pia tulipoambiwa tusali sana sio kwasababu ya maombi yetu kuzuiwa kama Mleta mada anavyodai la hasha Bali sababu ibilisi Ana Nguvu kubwa ya ushawishi hivyo kwa uwezo wetu hatuwezi kushinda ushawishi wake hivyo tunapaswa kujitakasa kila Mara ili roho mtakatifu atuongoze kushinda vishawishi hivyo. Adamu na Eva ukisoma kwa makini utaona mbinu anayoitumia ibilisi hakumshurutisha Eva ale lile tunda bali alimshawishi na ushawishi wake ukafanikiwa. Sasa tafakari kama Adamu na Eva hakukuwa na dhambi lakini alifanikiwa kumshawishi vizuri tu vipi kuhusu sisi tunaoishi kwenye ulimwengu uliojaa dhambi?!
Hivyo maombi hayazuiwi bali mapepo yana kazi kubwa ya kukushawishi na usipokuwa na imani dhabiti unashawishika na kuangamia kabisa...fact za kuzimu hazina ushahidi kwani kwangu nazifananisha na hadithi za Eric Shigongo kuuza vitabu na magazeti