Mfahamu malkia wa kuzimu

Mfahamu malkia wa kuzimu

Naombeni tofauti kati ya
Shetani,
Ibilisi,
Jini,
Mchawi,
Mwanga,

Na


Malaika.
 
Dunia inateswa na mambo mengi Sana ambayo wengi wetu huwa tunadhani yanatokana na akili zetu na mawazo yetu ama pengine ni uamuzi wetu binafsi.
La hasha, kila jambo linalotokea huwa limepangwa ktk ulimwengu wa roho tusioweza kuuona Kwa macho ya damu na nyama.
Kiongozi mkuu au mfalme wa maovu na shida zote duniani ni shetani ,kuzimu wanamwita Lucifer.
Huyu ni kiongozi mkubwa Sana ambaye makazi yake ni chini ya maji, bahari na maziwa. (kuzimu)
Lucifer huwa hafanyi kazi yoyote ngumu, yeye hupokea Taarifa na kutoa amri Kwa pepo mkuu Belzebur, ambaye naye huwaagiza mapepo wengine watatu ambao nao ni wakuu.
Kwa Sababu maalumu, nitamtaja pepo mmoja tu Kati ya hao watatu wengine na kazi zake hapa duniani.
Kwa kawaida, Lucifer ana serikali yake kuzimu yenye dola kamili, na waziri mkuu wake ni Belzebur.
Lucifer huwapa kazi za kufanya hawa hao mapepo, kila Siku.
Na wote hukaa angani, kila mmoja akikaa pande moja ya dunia ,yaani mashariki, kaskazini, magharibi na kusini, na kazi yao ni moja tu ni kuzuia Maombi ya watu Wa Mungu, Na wote wanakuwa chini ya Belzebur.
Huzuia Maombi, ndo maana unaweza kuomba Mungu miaka kibao bila majibu, Soma Daniel 10:13.
Malkia wao anaitwa Kilenzi, hili ni pepo hatari la kike ambalo ndo limeshikilia anasa na pesa zote za dunia hii.
Kilenzi linavunja ndoa za watu na kuharibu maisha ya vijana na mabinti.
Ni pepo haribifu la maisha ya watu, wote wanaotafuta Mali kishirikina, kilenzi ndo mgawaji wa hizo mali endapo tu utafuata masharti yao.
Kilenzi ndo waziri wa fedha na uchumi huko kuzimu.
Kati ya mapepo makuu yote, ni yeye tu ndo jike peke yake.
Mtu yoyote, akitaka chochote, iwe utajiri, Urais, Umaarufu, hata Kama hana elimu Lucifer humpatia kupitia kilenzi endapo tu, atatimiza masharti yao ambayo ni magumu mno.
Kila Siku saa 8 usiku ktk majira ya nchi zote duniani, mapepo hawa hushuka kutoka angani na kwenda kuzimu Kwa ajili ya kufanya sherehe na mikutano maalumu ya kuiangamiza dunia.
Inapotimia saa9:55 alfajiri, yanakuwa tayari yamemaliza kazi zao kuzimu na kurudi angani.
Watu wengi hawajui kuwa muda mzuri wa kuomba Mungu ni kuanzia saa 8:00 usiku hadi mwisho saa 9:55 alfajiri.
Maana kilenzi na wenzake wanakuwa kuzimu na hivyo kuliacha anga likiwa safi.
Kilenzi ndo pepo aliyeshikilia hadi serikali nyingi duniani. Soma ,Ufunuo wa Yohana. 17:1-8.

Jamani tukaeni jaribu na Mungu, Kwa leo naishia hapa, Siku nyingine nitafafanua zaidi.

Mmoja Wa mabinti aliye chini ya miliki ya kilenzi, Kama upo Kama huyu haha kwenye picha, basi wewe ni wa kilenzi, Nitafafanua zaidi.
Ha ha ha! Shetani awe na ubavu wa kuzuia mawasiliano na Mungu? Labda si mungu tunayemjua, ukweli ni kwamba shetani hana uwezo wa kuingilia mawasiliano na Mungu, maana Mungu anajua hata nia yako tu ya kumwomba na nini utakachoomba hata kabla! Shetani huteseka na kuumia mno na kamwe hawezi kuhimili hata jina la Mungu linapotajwa kwa ibada!
Nakubaliana nawe kwamba ana uwezo na anasa na mali za duniani lakini hili la kukatiza katikati ya Mungu na Binadamu kamwe haliwezi tokea. Anachoweza fanya ni kujaribu kuyahamishia mawazo yako mahala pengine (Distraction) na kukuhimiza ujishughulishe na masuala yasiyo na tija kwa roho yako lakini hufyata mkia utapolitaja (invoke) jina la Yesu maana jina hilo linapotajwa kwa ibada kuzimu hutetemeka na Luciferi na Majeshi yake hutawanyika!
Chezea na kingine lakini si jina la Mungu!
Kwa mtego wa mali na utajiri Luciferi amejitwalia wafuasi wengi kabisa. Utitiri wa dini na madhehebu yanayohubiri na kuahidi utajiri na ukwasi ni miongoni mwa makuwadi wa Luciferi, maana hata Yesu alisema itakuwa rahisi kwa ngamia kupenya kwenye tundu la shindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa mbingu; wewe unayehangaika dhehebu baada ya dhehebu kuusaka ukwasi unautarajia ukupeleke pepo ipi, ya mbinguni au kule aliko mmiliki wa utajiri wa duniani hapa Luciferi?
 
Jamani mazee! Hakuna kiumbe ama roho yoyote inayoweza kuzuia maombi ya mtu kumfikia Mungu. Pia hakuna kiumbe ama roho inayoweza kuzuia msjibu ya mtu kutoka kwa Mungu.
Kitu kinachoweza kuzuia maombi ya mtu ni mtu mwenyewe, pale anapo kiuka kanuni ama taratibu kila kitu kina sheria.
Kwa habari ya Daniel maombi yake kuzuiwa , note Daniel alikua agano la kale na shetani halikua haja pokwa mamlaka yake, but sasa shetani hana mamlaka tena kama wewe ni mtu wa sheria uzima, nyie ombeni popote pale hata ukiwa chooni ama bafuni we omba tu kwa imani na Mungu atakusikia na atakujibu kama umetimiza vigezo na masharti.

Njia nzuri ya kupokea majibu ya maombi ni kuacha dhambi na kuishi msisha ya upendo maana hiyo ndio kanuni. Maombi ya mtu mwenye haki yafaa sana
 
Inawekana anadanganya lkn hadi ujue kuwa anadanganya Manake unaujua ukweli so kwakuwa hapa nikama Darasa kama MTU amedanganya ikiwa unaujua ukweli unaweka watu tunapima.....Wanasema hoja inapingwa kwa Hoja

Mzee! Hii mada cha kwanza inahitaji ushahidi zaidi wa Biblia Takatifu, na sio maelezo matupu. na ukiangalia hili ni jukwaa sio mahala pake, kuna jukwaa na hayo mambo nafikiri ni la dini kama sijakosea ndio ingeenda huko ili ijadiliwe kwa mapana yake kwa msingi wa kiimani zaidi na sio porojo
 
Ni mambo mengi yanayo zuia pia mtu kutokupokea majibu ya maombi yake pindi aombapo na sio hayo mapepo, shetani na majeshi yake hao wote ni powerless katika new covenant. Hakuna kitu kinachoweza kuzuia maombi ya mtu kumfikia Mungu, na hakuna kinacho zuia mtu kupokea majibu ya maombi yake kutoka kwa Mungu katika hili agano jipya kama mtu huyo akifata kanuni za maombi na kuzishika

Ndo maana nilitoa angalizo mapema Sana.
kuwa nyie ni wajuaji na hamjui kitu.
Kama ishu ni agano jipya kwanini Yesu alifunga siku 40? alikuwa anataka nguvu gani ya ziada Kama kuna tofauti ya zamani na sasa?
Ujuaji mwingi mbele giza.
Mmekuwa mkidanganya waumini wenu na kuwapotezea muda.
Hamfai kabisa, mmevunja ndoa nyingi za watu, hili nitalieleza Kwa kina Siku nyingine.
Na mnatoa unabii wa uongo, ole wenu Mathayo 22:7
 
Mkuu chukua ujasiri wa mshana jr wakati anaweka mabandiko yake kuna watu walikuwa wakimpinga aidha aliendelea kukomaa Mwisho wa siku watu wamekuwa wakimuomba aweke Topic so kiongoz kama unania yakufundisha lete vitu Wengine sisi hatupitwi na jambo tunasoma kila kinachoandikwa tunachanganya na zetu so mkuu karibu uendelee ulipobakisha
Kama aiwahusu wapite kulee!
 
Haya mastori ya kufikirika haya.. cjui huwa mtu anapata wapi muda wa kuandika mambo kama haya...!
 
Kwenye ulimwengu wa Roho kuna....wa GIZA na NURU nivizuri kuzijua pande zote vzr Humu duniani huwezi kujua kila kitu unaweza kusema unaujua zaidi ulimwengu wa NURU unaweza ukakutana na MTU anajua mengi kuliko ww so maisha hayataki kukariri

Ni bora umemweleza ukweli mkuu, anajifanya kila kitu anajua, wakati mambo ya kiroho yana elimu pana Sana.
 
Asante Sana cipro, mid nmependa mafundisho yako name has a muda wa kuomba,
Uwe Unatoa mafunzo hya mazuri, waelewa tutaelewa na kunufaika, wabishi hawaishi
 
Hatukatazwi kujua, isipokua mleta mada anajuza watu kwa taarifa zisizo sahihi. Yaani namaanisha ni mwongo muanzisha mada

Wewe ndo unajiita mcha Mungu? unawezaje kunizulia kuwa mimi ni muongo?
Wewe ni mhuni Kama wahuni wengine wanaojifanya wanamjua Mungu kumbe hakuna kitu.
Unaniita muongo nimemtapeli Nani kupitia mada yangu?
Kama huamini pita kimya, wanaoamini wanajua ni nini nimeandika.
 
Wewe ndo unajiita mcha Mungu? unawezaje kunizulia kuwa mimi ni muongo?
Wewe ni mhuni Kama wahuni wengine wanaojifanya wanamjua Mungu kumbe hakuna kitu.
Unaniita muongo nimemtapeli Nani kupitia mada yangu?
Kama huamini pita kimya, wanaoamini wanajua ni nini nimeandika.

Mie sio muhuni, wewe ni mpotoshaji wa ukweli. Kumcha Mungu ni chanzo cha maarifa. So, najitahidi kwa neema yake kumcha sana ili maarifa yangu ya kumjua Mungu yaongezeke
 
Ndo maana nilitoa angalizo mapema Sana.
kuwa nyie ni wajuaji na hamjui kitu.
Kama ishu ni agano jipya kwanini Yesu alifunga siku 40? alikuwa anataka nguvu gani ya ziada Kama kuna tofauti ya zamani na sasa?
Ujuaji mwingi mbele giza.
Mmekuwa mkidanganya waumini wenu na kuwapotezea muda.
Hamfai kabisa, mmevunja ndoa nyingi za watu, hili nitalieleza Kwa kina Siku nyingine.
Na mnatoa unabii wa uongo, ole wenu Mathayo 22:7

Yesu Kristo, aliongozwa na Roho kwenda nyikani ( akiwa kajazwa Roho Mtakatiku yaani ujazo wa Roho Mtakatifu ndani ya mtu), na ilikua ni sehemu ya yeye kuomba kwa nguvu na kupitishwa katika majaribu ili aweze kupokea nguvu ya Roho Mtakatifu kwa ajili ya huduma ( yaani Roho Mtakatifu juu yake) na ndipo unapo ona Yesu Kristo anatoka nyikani akiwa na nguvu za Roho Mtakatifu ( Roho Mtakatifu juu yake ) na sio kujazwa Roho Mtakatifu ( sio kujawa na Roho Mtakatifu ), ukitaka kuelewa nenda kasome Luka Mtakatifu kuanzia sura ya tatu na ya nne.
 
Endelea kujidanganya na siku zinasonga mbele.
Na sijui Kama una usafi wa kumzidi Daniel mtu wa Mungu ambaye majibu ya Maombi yake yalizuiwa Kwa Siku 21,na mkuu wa uajemi (Belzebur). hadi Mungu akamtuma malaika wa Vita Mikael, akapigana na pepo Belzebur na kulishinda na ndipo Daniel akapata majibu yake.
Tatizo lenu ndugu zangu walokole mna ubishi wa ajabu Sana ambao mara nyingi hauwasaidii Daniel 10:13.
Hakukuwa na Roho Mtakatifu na Yesu anasema utukufu wa mwisho utakuwa mkubwa kuliko ule wa mwanzo hivyo kwa sasa Tuna Neema zaidi ya akina Daniel ila kwa Imani ukijiona huna upako wa agano wa jipya utabaki hivyo hivyo
 
Hakukuwa na Roho Mtakatifu na Yesu anasema utukufu wa mwisho utakuwa mkubwa kuliko ule wa mwanzo hivyo kwa sasa Tuna Neema zaidi ya akina Daniel ila kwa Imani ukijiona huna upako wa agano wa jipya utabaki hivyo hivyo

Muambie huyo! anataka kuaminisha watu kua shetani na majeshi kua wana nguvu ya kuzuia maombi hajui kua shetani ni powerless kwa wale walio na Roho Mtakatifu...
 
Yote haya umeyajuaje ndugu.
Na ninakushauri uache kumchukulia Mungu kama binadamu.
 
Hizi Mada Huwa Ni Nzuri Sana, Lakn Kujua Haya Mambo Yahitaji Usiwe Vuguvugu Bali Moto Au Baridi.

Neno Jema Mtoa Mada.
 
Kama hujui mambo usiwe mbishi, ni vema ukaomba ufundishwe.
Sijakurupuka kuandika ujue, kuna mazito ninayoyajua siwezi kuyaweka hapa maana watu wengi ni wabishi halafu hawajui kitu.
Nimeona jinsi wanavyombishia mshana jr.
Usikimbilie kuniita muongo bila kufanya utafiti, ukiwa na akili hiyo, dunia itakupiga chenga Sana.
malaika na mapepo, wote ni roho, ila wana jinsia ktk ulimwengu wa roho.
Kwa mfano. malaika Mikael naye ni roho ila ni dume.
Hii strictly, kuna Mapepo jike na madume na yanaoana na kuzaana, wewe huwezi kuwaona Kwa macho, ni mambo ya kiroho.
Na Lucifer ni roho ila ni dume.
Usipende kuwa mbishi, penda kuwa mdadisi.
Hawa Vijana Walosoma Hizi Siku Za Karibuni Huwa Wanaamini Sana Elimu Zao Kuliko Ukweli Halisi.

Mtoa Uzi Anayajua Haya Lakn Pia Si Vyema Kumuita Mtu Muongo Wakat Hujui Hata Historia Yake.
Ni Vyema Tukajirekebisha.
 
Umeandika kutokana na kitabu chako kilivyokufunza ila Quran haikusema hivyo baadhi ya vitu ni tofauti sana kwa maana hiyo ingekuwa vizuri pia kusoma na upande wa pili ili kuweza kujibu baadhi ya hoja kwani ht nikiijenga hoja nitakuacha badala yke utajibu kutokana na mihemko nawasilisha
Lqkn Ni Vyema Ukaweka Hizo Tofauti Za Maandiko Ya Quran Dhidi Ya Haya Ya Bible Ilikuweka Mjadala Sawa, Nje Ya Hapo Hujui Kama Mtoa Uzi Anaijua Quran Kwa Kiasi Gani.
 
Back
Top Bottom