Endelea kujidanganya na siku zinasonga mbele.
Na sijui Kama una usafi wa kumzidi Daniel mtu wa Mungu ambaye majibu ya Maombi yake yalizuiwa Kwa Siku 21,na mkuu wa uajemi (Belzebur). hadi Mungu akamtuma malaika wa Vita Mikael, akapigana na pepo Belzebur na kulishinda na ndipo Daniel akapata majibu yake.
Tatizo lenu ndugu zangu walokole mna ubishi wa ajabu Sana ambao mara nyingi hauwasaidii Daniel 10:13.
Mkuu
Siku nilipofunuliwa/kufundishwa haya mafundisho ya Nabii Daniel, nilistaajabu sana.
Imeandikwa, Siku ile Daniel alipopewa ufahamu na kuanza kutia nia yake (kuanza kusali), Mungu alitoa amri (alimtuma Malaika Gabriel aje amletee Daniel majibu yake).
Lakini wafalmu wa uhajemi (mapepo) wakainuka kuja kupigana na Gabriel ili asimpelekee habari Daniel.
Gabriel alipoelemewa ikabidi aombe msaada kutoka juu Mbinguni, ndipo Malaika Mkuu Mikael akashuka kuja kumsaidia kupigana na yale mapepo.
Upenyo ukapatikanika, Gabriel akashuka haraka kumpasha habari Daniel na akarudi tena kupigana vita.
Ni ukweli usiopingika, haya mapepo huwa yanazuia sala zetu, yanazuia majibu yetu na ndio maana tunakuwa tunaishia kukata tamaa, kwa maana unasali weeee, lakini hupati majibu au majibu yanacheleweshwa.
Lakini nilichojifunza, yatupasa tusali mfululizo pasipo kuchoka mapaka tutakapopata majibu yetu.