Tetesi: Meya Mstaafu Boniface Jacob wa CHADEMA kiongozi mgomo Kariakoo?

Ukiingiza wanasiasa wa upinzani, mizani inaparaganyika.
Nadhan umeelewa nn namaanisha! Haipasw kutafuta mchaw wa tatizo bali ni kutafuta solution ya tatizo!! Kuna kaujinga sana Nchi hii yaan kama kuna changamoto sekta flan bas hapo hutafutwa mchawi wakat ukiangalia walalamikaji wana hoja!!
 
Nadhan umeelewa nn namaanisha! Haipasw kutafuta mchaw wa tatizo bali ni kutafuta solution ya tatizo!! Kuna kaujinga sana Nchi hii yaan kama kuna changamoto sekta flan bas hapo hutafutwa mchawi wakat ukiangalia walalamikaji wana hoja!!
Usijidai huelewi.
Changanya tatizo lako hata kama ni geunine, na siasa hasa ukiwa upinzani, utakuwa umeharibu ushawishi wako.
Na pengine hutofanikiwa.

Sehemu za majimbo chini ya uongozi wa upinzani, Magufuli alikataa kujenga barabara.

Ni ujinga kuingiza siasa za vyama kwenye tatizo la Kariakoo, tatizo linalogusa wengi.
 
Usijidai huelewi.
Changanya tatizo lako hata kama ni geunine, na siasa hasa ukiwa upinzani, utakuwa umeharibu ushawishi wako.
Na pengine hutofanikiwa.

Sehemu za majimbo chini ya uongozi wa upinzani, Magufuli alikataa kujenga barabara.

Ni ujinga kuingiza siasa za vyama kwenye tatizo la Kariakoo, tatizo linalogusa wengi.
Unajua mzee wa bambasi, ni vzr kabla ya kwenda direct kuwalaum upinzani juu ya issue ya kariakoo ungeleta ushahid ni nan yupo nyuma ya hili kwa evidence!!
 
Unajua mzee wa bambasi, ni vzr kabla ya kwenda direct kuwalaum upinzani juu ya issue ya kariakoo ungeleta ushahid ni nan yupo nyuma ya hili kwa evidence!!
Mimi namlaumu huyo Boniface Jacob ambaye ni kiherehere.
Angekaa kimya wafanya biashara waongee.
 
Ukishadai haki yako tayari ni siasa.
Wanasiasa wakishaingilia kati madai huweza kugeuka na kupata mtazamo wa tofauti, hii ni kutokana na "nature" ya siasa zetu.

Hao wagomaji inawezekana kabisa wapo wa CCM, upinzani, na wasio na vyama, hawa wangeachwa wapiganie haki zao kama walivyoanza, lakini hiyo assistance wanayopata toka upinzani, naona kabisa inaweza kusababisha kukomoana mbele ya safari.
 
Wanasiasa wakishaingilia kati madai huweza kugeuka na kupata mtazamo wa tofauti, hii ni kutokana na "nature" ya siasa zetu.

Hao wagomaji inawezekana kabisa wapo wa CCM, upinzani, na wasio na vyama, hawa wangeachwa wapiganie haki zao kama walivyoanza, lakini hiyo assistance wanayopata toka upinzani, naona kabisa inaweza kusababisha kukomoana mbele ya safari.
Naturally watapata assistance ya wapinzani, kwa sababu haya ni madudu yaliyotokea chini ya uongozi wa CCM.

Na CCM nao wanatakiwa kujipanga kusema manifesto yetu haituongozi hivi, kuna changamoto tunazitatua, kitu ambacho Majaliwa kashaanza kukifanya.

Tunaweza kupingana kwa hoja na kufanya siasa zenye tija bila kuendekeza siasa za kukomoana.

Wafanyabiashara walipe kodi halali, wasionewe na kutozwa kodi kandamizi, watawala wajirekebishe na wapinzani wafanye kazi yao ya kukosoa watawala.

Tusiogope siasa, tukatae siasa chafu.
 
meya Bon mstaaf hata yeye ni mfanyabisahara wa mayayi kariakoo ni wajibu wake kwa hayo ayafanyayo
 
Katika maswala kama hili la kulipa/kutolipa kodi sijui ni nani anakomolewa hasa.
Mimi naona kama pande zote mbili wasipoafikiana watakuwa wamekomoana.

Maswala ya kulipa kodi yanahitaji taratibu nzuri zinazoeleweka tu vizuri na kila upande utimize vyema taratibu hizo kama zilivyopangwa.

Mswala ya siasa kuingia kati ni dalili tosha kwamba taratibu zilizopo siyo nzuri.
Ni wazi, siasa huingia popote panapoonekana pana ombwe linalohitaji kujazwa. Ni fursa kwa upinzani kutumia mianya kama hiyo. Ndiyo maana ya upinzani.
Kwa mtazamo wangu naona hapo anayekomolewa zaidi ni yule aliyeshika makali, nimeona wamezungumziwa machinga wanaoenda kwenye maduka ya wahindi wapewe mzigo wautembeze ili nao wapate kula yao.

Sasa kwa watu kama hawa huu mgomo ukiendelea naona kabisa wakiumia wao zaidi, wana familia zinawategemea, ndugu, na jamaa, hawawezi kuwa sawa na serikali ambayo hata kama ikikosa mapato ya Kariakoo, bado ina vyanzo vingine vya mapato.

Hapa ndio mantiki ya hoja yangu kupinga wapinzani kudandia hii issue, inaonekana wameitazama juu juu bila kuitafakari kwa undani, wanaona raha tu maduka kufungwa bila kujiuliza wale wanaotegemea maduka yafunguliwe ili wapate rizki zao wataishi vipi, suala linalohusisha riziki za wengine lisichukuliwe kama mtaji wa kisiasa, huo utakuwa ni ubinafsi.
 
Naturally watapata assistance ya wapinzani, kwa sababu haya ni madudu yaliyotokea chini ya uongozi wa CCM.

Na CCM nao wanatakiwa kujipanga kusema manifesto yetu haituongozi hivi, kuna changamoto tunazitatua, kitu ambacho Majaliwa kashaanza kukifanya.

Tunaweza kupingana kwa hoja na kufanya siasa zenye tija bila kuendekeza siasa za kukomoana.

Wafanyabiashara walipe kodi halali, wasionewe na kutozwa kodi kandamizi, watawala wajirekebishe na wapinzani wafanye kazi yao ya kukosoa watawala.

Tusiogope siasa, tukatae siasa chafu.
Hapo kwenye suala la siasa safi na chafu ndio tatizo linapoanzia, tumeshaona mara nyingi wakisema hawataki siasa za matusi huku aakigoma kuyataja hayo matusi yenyewe, au ni nani mwenye kipimo cha tusi ni lipi, na lipi sio tusi.

Hapo ndipo nilipopatilia shaka mpaka nikaweka neno "kukomoana" naamini hili jambo lipo tu kwenye vichwa vya watawala, kwao popote anapoingia mpinzani hata kwenye hoja ya msingi lazima watafute vikwazo, kule bungeni kuna hoja nyingi za maana huwa zunapigwa teke na CCM kisa tu zimetolewa na wapinzani.

Hiyo ndio sababu yangu kuhofia madai ya wafanyabiashara nayo kuja kupigwa teke mbele ya safari, kwasababu tu ya msukumo unaotoka upande wa upinzani kwa sasa, japo wengine kwenu mnaliona jambo la kawaida kwasababu athari zake zinaweza zisiwaumize nyie kwa namna yoyote.
 
Hapo kwenye suala la siasa safi na chafu ndio tatizo linapoanzia, tumeshaona mara nyingi wakisema hawataki siasa za matusi huku aakigoma kuyataja hayo matusi yenyewe, au ni nani mwenye kipimo cha tusi ni lipi, na lipi sio tusi.

Hapo ndipo nilipopatilia shaka mpaka nikaweka neno "kukomoana" naamini hili jambo lipo tu kwenye vichwa vya watawala, kwao popote anapoingia mpinzani hata kwenye hoja ya msingi lazima watafute vikwazo, kule bungeni kuna hoja nyingi za maana huwa zunapigwa teke na CCM kisa tu zimetolewa na wapinzani.

Hiyo ndio sababu yangu kuhofia madai ya wafanyabiashara nayo kuja kupigwa teke mbele ya safari, kwasababu tu ya msukumo unaotoka upande wa upinzani kwa sasa, japo wengine kwenu mnaliona jambo la kawaida kwasababu athari zake zinaweza zisiwaumize nyie kwa namna yoyote.
Hatuwezi kumaliza tatizo kwa kuliogopa.

Inatakiwa watu waelimishwe na waliondoe, kama watawala watataka kuleta siasa chafu kwenye madai halali ya wananchi, kwa sababu tu madai halali ya wananchi yamepata support ya wapinzani, watawala watakuwa wanawapa mtaji wa kisiasa zaidi wapinzani, wapinzani wajipange kuutumia mtaji huo na kuutafsiri kwenye kura.

Watawala wakijua hilo tu, watashika adabu wenyewe.

Majaliwa alianza kwa kuwaambia wafanyabiashara wamfuate Dodoma, wakakataa na kusema yeye ndiye aje Kariakoo, ikabidi akubali. Watu wanaanza kuamka.
 
Sasa kwa watu kama hawa huu mgomo ukiendelea naona kabisa wakiumia wao zaidi, wana familia zinawategemea, ndugu, na jamaa, hawawezi kuwa sawa na serikali ambayo hata kama ikikosa mapato ya Kariakoo, bado ina vyanzo vingine vya mapato.
Kuna hatari kubwa zaidi inayotokana na serikali kukosa mapato, kiasi kwamba serikali yenyewe inaweza kuondolewa madarakani.
Hapo ndipo sehemu ya wapinzani inapoanzia. Upinzani wowote lengo ni kushika madaraka.
Kwa hiyo, popote palipo na fursa ya kuiondoa serikali iliyopo na kuiingiza nyingine, ni lazima upinzani ujihusishe katika hali hiyo.
Huo utakuwa siyo upinzani kama hauwezi kutumia nafasi za namna hii inayojitokeza hapa.
 
Hatuwezi kumaliza tatizo kwa kuliogopa.

Inatakiwa watu waelimishwe na waliondoe, kama watawala watataka kuleta siasa chafu kwenye madai halali ya wananchi, kwa sababu tu madai halali ya wananchi yamepata support ya wapinzani, watawala watakuwa wanawapa mtaji wa kisiasa zaidi wapinzani, wapinzani wajipange kuutumia mtaji huo na kuutafsiri kwenye kura.

Watawala wakijua hilo tu, watashika adabu wenyewe.

Majaliwa alianza kwa kuwaambia wafanyabiashara wamfuate Dodoma, wakakataa na kusema yeye ndiye aje Kariakoo, ikabidi akubali. Watu wanaanza kuamka.
Hili sidhani kama linahitaji elimu, naona ni utashi tu wa wanasiasa wenyewe.

Watawala wanaona wakitoa haki pale wapinzani wanapopapigia kelele watakuwa wameshindwa, matokeo yake ndio ubabe kila mahalu usio na maana, hata ikibidi kuwanyima wengine haki yao.

Hili la K'koo limeanzia kwa wafanyabiashara wenyewe, napenda kuona lingine litakalokuwa staged na wapinzani au kundi lingine tofauti kama walimu kuanzia mwanzo mpaka mwisho, nione kama litafikia hatua hii lililofikia hili la K'koo, hapo ndio nitajua tumeamka.
 
Hili sidhani kama linahitaji elimu, naona ni utashi tu wa wanasiasa wenyewe.

Watawala wanaona wakitoa haki pale wapinzani wanapopapigia kelele watakuwa wameshindwa, matokeo yake ndio ubabe kila mahalu usio na maana, hata ikibidi kuwanyima wengine haki yao.
Uzuri wa hii issue ni kwamba imeanzishwa na wafanyabiashara wenyewe, hao wapinzani wamedandia tu.

Kwa hivyo watawala wakidindisha, watakuwa wanapingana na wafanyabiashara, si wapinzani.
 
Kuna hatari kubwa zaidi inayotokana na serikali kukosa mapato, kiasi kwamba serikali yenyewe inaweza kuondolewa madarakani.
Hapo ndipo sehemu ya wapinzani inapoanzia. Upinzani wowote lengo ni kushika madaraka.
Kwa hiyo, popote palipo na fursa ya kuiondoa serikali iliyopo na kuiingiza nyingine, ni lazima upinzani ujihusishe katika hali hiyo.
Huo utakuwa siyo upinzani kama hauwezi kutumia nafasi za namna hii inayojitokeza hapa.
Hii serikali ya CCM inayochezea mapesa mengi kama tunavyoona ripoti za CAG kila mwaka, sidhani kama itayumbishwa na mapato ya K'koo pekee.

Napenda kuona kundi lingine litakaloamka na kudai haki zao kama walivyofanya hao wafanyabiashara, hapo ndio nitaona tumeamka.

Lakini kwa upande mwingine wapinzani kudandia ni sawa na kukiri wameshindwa kuifanya vizuri kazi yao ya ushawishi, kwa mantiki hiyo sioni kama nitakosea nikisema tuna upinzani udhaifu.
 
Kuna hatari kubwa zaidi inayotokana na serikali kukosa mapato, kiasi kwamba serikali yenyewe inaweza kuondolewa madarakani.
Hapo ndipo sehemu ya wapinzani inapoanzia. Upinzani wowote lengo ni kushika madaraka.
Kwa hiyo, popote palipo na fursa ya kuiondoa serikali iliyopo na kuiingiza nyingine, ni lazima upinzani ujihusishe katika hali hiyo.
Huo utakuwa siyo upinzani kama hauwezi kutumia nafasi za namna hii inayojitokeza hapa.
Yaani unataka kutuambia serikali inategemea mapato yake toka Kariakoo tu!! Kwanza ungejua karibu bidhaa zote za Kariakoo zinaletwa na GSM toka Uchina. Utaona watafungua karibuni la sivyo cha mtema kuni watakiona hawawezi wakamtunishia Waziri Mkuu hao!!
 
Yaani unataka kutuambia serikali inategemea mapato yake toka Kariakoo tu!! Kwanza ungejua karibu bidhaa zote za Kariakoo zinaletwa na GSM toka Uchina. Utaona watafungua karibuni la sivyo cha mtema kuni watakiona hawawezi wakamtunishia Waziri Mkuu hao!!
Mkuu 'magu2016', binafsi sijuikiasi cha mchango wa hao watu katika pato la serikali, lakini si hawa ni sehemu ndogo tu ya wafanya biashara wengi ambao maslahi yao wote yanaguswa na serikali hiyo hiyo?
Hawa wanaweza kuwa ni chanzo tu cha jambo kubwa.

Lakini hata bila kujua kiasi wanachochangia, dalili zenyewe zinaonyesha umuhimu walio nao. Wewe huoni Waziri Mkuu anavyohaha? Ni maswala mangapi yanayoiamsha serkali akili kwa haraka kama ilivyofanya hapa?

Hata wakuu wa mikoa ikalazimu wapanguliwe, wewe bado huoni umuhimu wake?
 
Mkuu 'magu2016', binafsi sijuikiasi cha mchango wa hao watu katika pato la serikali, lakini si hawa ni sehemu ndogo tu ya wafanya biashara wengi ambao maslahi yao wote yanaguswa na serikali hiyo hiyo?
Hawa wanaweza kuwa ni chanzo tu cha jambo kubwa.

Lakini hata bila kujua kiasi wanachochangia, dalili zenyewe zinaonyesha umuhimu walio nao. Wewe huoni Waziri Mkuu anavyohaha? Ni maswala mangapi yanayoiamsha serkali akili kwa haraka kama ilivyofanya hapa?

Hata wakuu wa mikoa ikalazimu wapanguliwe, wewe bado huoni umuhimu wake?
Wakuu wa Mikoa hawajapanguliwa kwa sababu ya Kariakoo.
 
1684259916732.png
 
Back
Top Bottom