Salaam,
Mwisho wa mwaka ndio huu, Namshukuru MUNGU ametuweka hai hadi sasa, wengi wetu tukiangalia tumefanya mambo kinyume na maagizo, amri, sheria zake huyo aliyetulinda...hebu tujiulize ni jambo gani kubwa zuri ulilotenda unaweza kujitetea kwake kuwa ulimtendea huyu MUNGU aliyekulinda, kukufanikisha hivi?
Kwa wale ambao mwaka huu 2012 ulikuwa wa mafanikio katika elimu, afya, kazi, jamii(familia n.k) Hongera na pongezi kwenu.
Kwa wale mwaka huu ulikuwa na changamoto kubwa, mwaka kuwa mgumu kwao(kielimu, kijamii, kikazi, kutotimiza malengo n.k) Pole...tushukuru kwa yote na tusikate tamaa.
Mwaka mpya(tunaoutarajia) ni malengo gani umeweka, umejiandaaje kukabiliana na changamoto zijazo.
Msamaha kwa wote tuliokoseana kwa kujua na kutokujua.
Naam,
Heri ya mafanikio kwa mwaka 2013 wana-JF wote na wageni(guests) pia.